Mkurugenzi Rombo: Shule iliyoandikisha Wanafunzi Watatu hakuna imani za kishirikina ni maamuzi ya wazazi tu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Capture.JPG



Baada ya kuripotiwa Shule ya Msingi ya Mlembea inayomilikiwa na Serikali katika Tarafa ya Mashati, Halmashauri ya Rombo Mkoani Kilimanjaro kuandikisha Wanafunzi watatu pekee kwa ajili ya Mwaka wa Masomo 2024, uffanuzi umetolewa.

Awali imeelezwa kuwa baadhi ya sababu za na uhaba wa Wanafunzi ni imani za kishirikina na Vijana wengi kudaiwa kujiingiza kwenye ulevi na kushindwa kuendeleza familia na wengine kukimbilia Mjini kutafuta maisha, zaidi soma hapa - Kilimanjaro: Shule ya Msingi ya Serikali yaandikisha Wanafunzi watatu (3) kuanza Darasa la Kwanza


MAJIBU YA SERIKALI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rombo, Godwin Chacha ameelezea kinachoendelea kwa kusema:

Ni kweli Wanafunzi waliokuwa wameandikishwa ni Watatu na wameongezeka kufikia nane lakini matarajio ya Shule ni kuwa wanaweza kuongezeka lakini hawatazidi kumi na moja (11).

Sababu zipo kadhaa, baadhi ni Wazazi wengi kuwapeleka Watoto wao kwenye Shule za binafsi, pia maeneo ya mipakani kuna Wazazi wanapeleka Watoto wao kwenda kusoma Kenya.

Kwa kuwa tuna ujirani mwema kuna magari yanayokuja kubeba Wanafunzi wanaenda huko kusoma kisha jioni wanawarudisha.

Sababu nyingine ni kuwa ‘population’ sio kubwa sana hapa na Watu wengi wamesambaa na wanasambaa hivyo kusababisha baadhi kuwahamisha Watoto wao pia.

Kingine ni kuwa Kilimanjaro watu wamesoma sana na hivyo suala la kuzaa Watoto wengi sio jambo linalopendelewa sana kama ilivyo maeneo mengine, watu wengi wana Watoto chini ya watatu au wawili.

Hivyo, niweke wazi kuwa hakuna imani za kishirikina kama baadhi wanavyodai (kwamba siku za nyuma Wanafunzi walikuwa wakianguka wenyewe shuleni hapo), ni haki ya mzazi kuamua mtoto wake akasome anapotaka.

Hali hiyo ya uchache wa Wanafunzi hauwezi kuathiri Wanafunzi au Walimu, wakiwa wachache wanaweza kupewa elimu bora zaidi kuliko wale ambao wangekuwa wengi kwenye darasa moja, japo hatusemi kuwa tunafurahia kuwa na idadi ndogo ya Wanafunzi.

Tunakaribisha wadau ikiwemo mbalimbali ikiwemo Wanahabari waje waone mazingira na inawezekana ikachangia kuongeza uwekezaji pia.
 



Baada ya kuripotiwa Shule ya Msingi ya Mlembea inayomilikiwa na Serikali katika Tarafa ya Mashati, Halmashauri ya Rombo Mkoani Kilimanjaro kuandikisha Wanafunzi watatu pekee kwa ajili ya Mwaka wa Masomo 2024, uffanuzi umetolewa.

Awali imeelezwa kuwa baadhi ya sababu za na uhaba wa Wanafunzi ni imani za kishirikina na Vijana wengi kudaiwa kujiingiza kwenye ulevi na kushindwa kuendeleza familia na wengine kukimbilia Mjini kutafuta maisha, zaidi soma hapa - Kilimanjaro: Shule ya Msingi ya Serikali yaandikisha Wanafunzi watatu (3) kuanza Darasa la Kwanza


MAJIBU YA SERIKALI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rombo, Godwin Chacha ameelezea kinachoendelea kwa kusema:

Ni kweli Wanafunzi waliokuwa wameandikishwa ni Watatu na wameongezeka kufikia nane lakini matarajio yao ni kuwa wanaweza kuongezeka lakini hawatazidi kumi na moja (11).

Sababu zipo kadhaa, baadhi ni Wazazi wengi kuwapeleka Watoto wao kwenye Shule za binafsi, pia maeneo ya mipakani kuna Wazazi wanapeleka Watoto wao kwenda kusoma Kenya.

Kwa kuwa tuna ujirani mwema kuna magari yanayokuja kubeb wanafunzi wanaenda kusoma jioni wanawarudisha.

Sababu nyingine ni kuwa ‘population’ sio kubwa sana hapa na watu wengi wamesambaa na wanasambaa hivyo kusababisha baadhi kuwahamisha Watoto wao pia.

Kingine ni kuwa Kilimnjaro watu wamesoma sana na hivyo suala la kuzaa watoto wengi sio jambo linalopendelewa sana kama ilivyo maeneo mengine, watu wengi wana watoto chini ya watatu au wawili.

Hivyo, hakuna imani za kishirikina kama baadhi wanavyodai, ni haki ya mzazi kuamkua mtoto wake akasome anapotaka.

Hali hiyo ya uchache wa Wanafunzi haiwezi kuathiri Wanafunzi au Walimu, wakiwa wachache wanaweza kupewa elimu bora zaidi kuliko wale ambao wangekuwa wengi kwenye darasa moja, japo hatusemi kuwa tunafurahia kuwa na idadi ndogo ya Wanafunzi.

Tunakaribisha wadau ikiwemo mbalimbali ikiwemo Wanahabari waje waone mazingira na inawezekana ikachangia kuongeza uwekezaji pia.
Moja Kati ya DED viazi waliyopo nchi hii ni huyu Chacha. Na amedumu sana hapo Rombo.

Mambo ni zig zag.
 
Rombo mbona inajulikana watoto wake wamesambaa nchi nzima, asilimia kubwa ya familia za Rombo zinaishi mijini wakiongozwa na Dar es Salaam, na kutokana na wengi kuwa wafanya biashara wa kuanzia kipato cha chini , , watoto wao wanapendelea kupelekwa private wakiamini ndio kuna elimu Bora, na population ya huko wengi ni wazee waliostaafu, na vijana mashamba boy kutoka mikoa mingine, serikali ingezifanya shule za huko ziwe za boarding zipokee hata watoto kutoka zanzibar na Kanda ya ziwa maana huko kuna upungufu wa shule na watoto wanarundikana mashuleni.
 
Rombo mbona inajulikana watoto wake wamesambaa nchi nzima, asilimia kubwa ya familia za Rombo zinaishi mijini wakiongozwa na Dar es Salaam, na kutokana na wengi kuwa wafanya biashara wa kuanzia kipato cha chini , , watoto wao wanapendelea kupelekwa private wakiamini ndio kuna elimu Bora, na population ya huko wengi ni wazee waliostaafu, na vijana mashamba boy kutoka mikoa mingine, serikali ingezifanya shule za huko ziwe za boarding zipokee hata watoto kutoka zanzibar na Kanda ya ziwa maana huko kuna upungufu wa shule na watoto wanarundikana mashuleni.
Wanawake wa Rombo walishawahi kulalamika wanalazimika kwenda kufata wanaume kenya baada ya vijana wa Rombo kuwa walevi kupindukia
 
Rombo mbona inajulikana watoto wake wamesambaa nchi nzima, asilimia kubwa ya familia za Rombo zinaishi mijini wakiongozwa na Dar es Salaam, na kutokana na wengi kuwa wafanya biashara wa kuanzia kipato cha chini , , watoto wao wanapendelea kupelekwa private wakiamini ndio kuna elimu Bora, na population ya huko wengi ni wazee waliostaafu, na vijana mashamba boy kutoka mikoa mingine, serikali ingezifanya shule za huko ziwe za boarding zipokee hata watoto kutoka zanzibar na Kanda ya ziwa maana huko kuna upungufu wa shule na watoto wanarundikana mashuleni.
Sema Rombo ulevi umezidi aisee...ni Wilaya Fulani hiv isiyo na future yoyote
 
Rombo mbona inajulikana watoto wake wamesambaa nchi nzima, asilimia kubwa ya familia za Rombo zinaishi mijini wakiongozwa na Dar es Salaam, na kutokana na wengi kuwa wafanya biashara wa kuanzia kipato cha chini , , watoto wao wanapendelea kupelekwa private wakiamini ndio kuna elimu Bora, na population ya huko wengi ni wazee waliostaafu, na vijana mashamba boy kutoka mikoa mingine, serikali ingezifanya shule za huko ziwe za boarding zipokee hata watoto kutoka zanzibar na Kanda ya ziwa maana huko kuna upungufu wa shule na watoto wanarundikana mashuleni.
Ushauri Mujarabu kabisa ...

Nadhani Serikali ichukue huu ushauri
 
Rombo mbona inajulikana watoto wake wamesambaa nchi nzima, asilimia kubwa ya familia za Rombo zinaishi mijini wakiongozwa na Dar es Salaam, na kutokana na wengi kuwa wafanya biashara wa kuanzia kipato cha chini , , watoto wao wanapendelea kupelekwa private wakiamini ndio kuna elimu Bora, na population ya huko wengi ni wazee waliostaafu, na vijana mashamba boy kutoka mikoa mingine, serikali ingezifanya shule za huko ziwe za boarding zipokee hata watoto kutoka zanzibar na Kanda ya ziwa maana huko kuna upungufu wa shule na watoto wanarundikana mashuleni.
Huo ndio ukweli.


Rombo hapakaliki, kila anaueweza anakimbilia sehemu nyingine kutafuta.

Huku wanabaki wazee na rejects.

Hata wanafunzi waliopo mostly utakuta wanakaa na mabibi zao.

Na kwasababu pia shulenni nyingi na watu hakuna.

Bora hata hiyo shule imepata watoto 3, Kuna shule nyingine inaitwa Mseta tarafa hiyo hiyo ya Mashati tena ilijengwa kwa msaada wa Kilimanjaro National Park, ilishafungwa muda kwa kukosa wanafunzi.

Huyo kilaza Chacha sidhani Kama hata anajua chocchote
 
Kwani waziri wa elimu si anatokea huko Rombo?. Serikali ifikirie zaidi kuhusu elimu ya Tanzania. Zipo shule nyingi wanafunzi hawazidi kumi, kinachoonekana hapa wazazi wengi wameanua kuwapeleka watoto wao shule za binafsi kwa ajili ya ubora wa elimu.
 
Sasa hiyo shule siyo hasara kwa serikali? Inadahili chini ya kiwango kinachotakiwa!
Sio hiyo peke yake.
Mimi nimesoma Moshi Vijijini Miaka hiyo ya 95.
Kwanza Darasani tulikuwa 30 tu.
Shule nzima Idadi yetu hatukuwahi kufika 250.
Kata niliyokuwepo ina vijiji 5. Shule za Msingi 6, za Umma.
Nafikiri Mkurugenzi ana hoja.
Na pia siku hizi watu wa Kilimanjaro wanahama na familia kuja mjini, tofauti na hapo nyuma. Baba anaenda kutafuta, Mama na watoto wanabaki kijijini.
 
Back
Top Bottom