DOKEZO Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangaliwe, ananyanyasa Wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangalizwe, ananyanyasa Wanafunzi

Shule ya Msingi Mungu Maji iliyopo Tarafa ya Mungu Maji, Kata Unyamikumbi, Wilaya ya Singida Mjini, kuna changamoto, Wanafunzi wa Darasa la Kwanza lina Watoto 180 wanaosoma darasa moja.

Wanafunzi wanabanana, hawapo katika mazingira rafiki ya kusoma kwa kuwa pia kuna Walimu wawili tu wanaofundisha darasa hilo.

Nashauri Serikali iangalie juu ya hilo, changamoto nyingine ni kuhusu Mwalimu mmoja kati ya hao wawili anaitwa Kiwale amekuwa akiwanyanyasa Wanafunzi kiasi kwamba baadhi ya Watoto wamekuwa wakigoma kwenda shule kutokana na kumhofia Mwalimu huyo.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mungumaji, Charles Kirimba, sisi wazazi tumekulisha mara kadha akuhusu tabia za mtumishi mwenzako ambaye yupo chini yako, ukaahidi kushughulikia lakini bado mambo yamekuwa ni yaleyale.

Hatujui nini hasa ambacho kinamfanya Mwalimu huyo kuwa na jeuri licha ya sisi wazazi kumlalamika mara kadhaa.

Imefikia hatua baadhi ya Wanafunzi wanakimbia au wanatoroka pindi wanapojua kuwa ni zamu ya Mwalimu kiwale kuingia darasani.

===== ===

MAJIBU YA MKURUGENZI WA MANISPAA
JamiiForums.com ilipomtafuta Mkurugenzi wa Manispaa, Jeshi Godfrey Lupembe kwa ajili ya ufafanuzi wa madai hayo amesema “Siwezi kulizungumzi hilo suala, Andika barua leta malalamiko yako, pia sina kibali cha kuzungumza, muulize Mkuu wa Mkoa au Katibu Tawala ili watoe ruhusa.

“Kazi za Serikali huwezi kutoa majibu bila kuwa na maandishi.”

MAJIBU YA AFISA ELIMU
Akijibu hoja hizo, Afisa Elimu Msingi, Omari Maje amesema “Kwanza Wanafunzi waliopo ni 130 na sio 180 kama alivyosema, tuhuma sio za kweli, mtoa mada anatumia mtandao vibaya, Serikali ipo kazini, aje ofisini kwangu aone mamlaka husika, kama suala lake ni la kweli tulifanyie kazi mara moja.”
 
We mzazi nani kakuambia walimu wako chini ya walimu wakuu? Mwalimu mkuu ni sawa na walimu wenzake tu na hana mamlaka kubwa kumuwajibisha mwalimu mwenzake. Walimu wako chini ya mkurugenzi wa halmashauri na halmashauri ina idara ya elimu ambayo inaongozwa na ofisa elimu. Ofisa elimu wa halmashauri ndiyo kiongozi mkuu wa walimu na yeye ana maofisa wa idara zake zinazoweza kumuwajibisha huyo mwalimu kama anaenda kinyume na maadili ya ualimu. Mwalimu mkuu ni kiranja tu shuleni wa kupeleka taarifa za shuleni wilayani/halmashauri.
 
Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangalizwe, ananyanyasa Wanafunzi

Shule ya Msingi Mungu Maji iliyopo Tarafa ya Mungu Maji, Kata Unyamikumbi, Wilaya ya Singida Mjini, kuna changamoto, Wanafunzi wa Darasa la Kwanza lina Watoto 180 wanaosoma darasa moja.

Wanafunzi wanabanana, hawapo katika mazingira rafiki ya kusoma kwa kuwa pia kuna Walimu wawili tu wanaofundisha darasa hilo.

Nashauri Serikali iangalie juu ya hilo, changamoto nyingine ni kuhusu Mwalimu mmoja kati ya hao wawili anaitwa Kiwale amekuwa akiwanyanyasa Wanafunzi kiasi kwamba baadhi ya Watoto wamekuwa wakigoma kwenda shule kutokana na kumhofia Mwalimu huyo.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mungumaji, Charles Kirimba, sisi wazazi tumekulisha mara kadha akuhusu tabia za mtumishi mwenzako ambaye yupo chini yako, ukaahidi kushughulikia lakini bado mambo yamekuwa ni yaleyale.

Hatujui nini hasa ambacho kinamfanya Mwalimu huyo kuwa na jeuri licha ya sisi wazazi kumlalamika mara kadhaa.

Imefikia hatua baadhi ya Wanafunzi wanakimbia au wanatoroka pindi wanapojua kuwa ni zamu ya Mwalimu kiwale kuingia darasani.
Nendeni kwa afisa elimu na barua ya malalamiko pamoja na sahihi zenu.
 
Andika barua ya malalamiko nà mashtaka ipeleke kwa mamlaka ya nidhamu inayoitwa TEACHERS SERVICE COMMISSION.

Ambatanisha vielelezo vyote vya ukatili na manyanyaso dhidi ya watoto.

Kisha copy ya barua ipeleke kwa mkurugenzi wa mànispaa, afisa elimu wa wilaya, ustawi wa jamii na kituo kikuu cha polisi.
 
Tatizo la sisi wazazi tunawasikiliza watoto sana.. ila ushauri wangu kama unaweza mtafutie shule nyingine ambapo unahisi mtoto wako atasoma bila kusumbuliwa..
 
Chumba kimoja kinakaa wanafunzi 180 badala ya wazazi kutatua hiyo changamoto kwa kujenga angalau vyumba vingine vitatu mnaleta majungu huku. Kumbe Singida mabumunda mko wengi.
 
Title ni unyanyasaji,kwenye andiko sijaona namna hao wanafunzi wananyanyaswa,are you serious?
 
Kweli watanzania wengi wajinga wajinga tu!

Mzazi kalalamikia tatizo, watoto wadogo darasa la kwanza, wanakemewa na kunyanyaswa! Hawa ni watoto wadogo, wanahitaji mazingira rafiki waweze kuipenda shule na kusoma kwa raha! Badala mkaangalie jinsi ya kutatua tatizo watoto wasome kwa raha, mnaleta majibu ya ovyo ovyo tu!

Na nyie viongozi, kama si wajibu wenu, si mkamwelekeze kunanohusika? Na nyie mnaotaka aandike barua ailete na kopi sijui wapi, akishajulikana, mtoto wake atakuwa salama?

Kweli nchi hii imejaa vilaza tu na viongozi waliopewa kazi bila kuwa na uwezo bali labda kwa kujuana au kuhonga!

Shame on you all!
 
We mzazi nani kakuambia walimu wako chini ya walimu wakuu? Mwalimu mkuu ni sawa na walimu wenzake tu na hana mamlaka kubwa kumuwajibisha mwalimu mwenzake. Walimu wako chini ya mkurugenzi wa halmashauri na halmashauri ina idara ya elimu ambayo inaongozwa na ofisa elimu. Ofisa elimu wa halmashauri ndiyo kiongozi mkuu wa walimu na yeye ana maofisa wa idara zake zinazoweza kumuwajibisha huyo mwalimu kama anaenda kinyume na maadili ya ualimu. Mwalimu mkuu ni kiranja tu shuleni wa kupeleka taarifa za shuleni wilayani/halmashauri.
Wakiambiwa tu,shule hii ni yenu Wazazi hahahah,aisee wanapata nguvu kubwa sana.
CCM WAJANJA SANA
 
Mizazi mingi ni mipumbavu sana ikiongozwa na madiwani wao. Inapenda majungu sana.

Inashadadia mambo ya kikuda hadwaaasas.

Walimu wanafanya kazi kubwa sana. Wapewe maua yao
 
Back
Top Bottom