Mkurugenzi NHC: Uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma umesababisha hasara kwa Shirika la Nyumba

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
1691301259330.png

Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Hamad Abdallah amesema uamuzi huo umekuwa na matokeo hasi kwa miradi iliyopo Dar es Salaam zikiwemo nyumba na mali nyingine zilizokuwa zikitumiwa na Serikali na Maafisa wake zimeachwa wazi.

Kati ya Miradi iliyotajwa kuingia hasara ni pamoja na wa Seven-Eleven (711) uliopo katika mzunguko wa Mbezi Beach/Kawe jijini Dar es Salaam wenye thamani ya Tsh. Bilioni 105 ambao ujenzi wake ulisimamishwa kwa miaka Saba.

Hata hivyo, amebainisha kuwa Ujenzi wa Mradi huo utarejea Septemba 2023, Mradi mwingine uliokwama kwa muda mrefu ni Morocco Square uliosimama katika Serikali ya Awamu ya 5, nao unatarajia kukamilika hivi karibuni.

==============

National Housing Corporation NHC director general Hamad Abdallah has said that the decision to relocate government activities, including all ministries and institutions, to Dodoma negatively impacted Dar es Salaam's real estate market.

Speaking to editors, Mr Abdallah said making Dodoma the capital city, which meant shifting Tanzania's administrative duties to the central region, meant that houses and other real estate property occupied by the government and its officials were left vacant.

The relocation led to losses on the side of NHC, which owns the lion's share of real estate property in Dar es Salaam.

"Whereas we are seeing a boom in real estate demand in Dodoma, it was the reverse in Dar es Salaam," said Abdallah.

He, however, noted that the trend is slowly shifting in favor of Dar es Salaam, which remains Tanzania's commercial capital despite losing its administrative role.

"We are witnessing some gains in the real estate market in the commercial capital. There is a gradual rise in demand for property from the private sector," he shared.

In another development, construction the Seven-Eleven (711) located at the Mbezi Beach/Kawe roundabout in Dar es Salaam is set to resume construction after it stalled for Seven years.

The 711 residential real estate project that was meant to be completed within three years was stopped for seven years.

Speaking to editors in Dar es Salaam, National Housing Corporation (NHC) Director General Hamad Abdallah said negotiations are ongoing and construction will resume in September with 85 percent of the apartments already sold to tenants.

He acknowledged that NHC, which is a government institution, and the owners of the real estate project valued it at Sh105 billion and have incurred massive losses since the project was stopped.

THE CITIZEN
 
View attachment 2709788
Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Hamad Abdallah amesema uamuzi huo umekuwa na matokeo hasi kwa miradi iliyopo Dar es Salaam zikiwemo nyumba na mali nyingine zilizokuwa zikitumiwa na Serikali na Maafisa wake zimeachwa wazi.

Kati ya Miradi iliyotajwa kuingia hasara ni pamoja na wa Seven-Eleven (711) uliopo katika mzunguko wa Mbezi Beach/Kawe jijini Dar es Salaam wenye thamani ya Tsh. Bilioni 105 ambao ujenzi wake ulisimamishwa kwa miaka Saba.

Hata hivyo, amebainisha kuwa Ujenzi wa Mradi huo utarejea Septemba 2023, Mradi mwingine uliokwama kwa muda mrefu ni Morocco Square uliosimama katika Serikali ya Awamu ya 5, nao unatarajia kukamilika hivi karibuni.
Mwambieni CEO Hamad Abdallah kuwa anachojuwa na sisi tukijuwa. Amepewa hiyo kazi ili aifanye NHC yenye kupata hasara ianze kutengeza faida. Kama hawezi arudishe mpira golini, kuna wanaoweza kuliko yeye
 
Hapo ndio hao mabosi wa mashirika wanakwama pakubwa kwenye uendeshaji wa mashirika na mentality hii inaisababishia Serikali hasara.

Hoja ya kusema Serikali kuhamia Dodoma imepelekea hasara shirika ni dhaifu sana. Shirika linatakiwa liwe na mikakati ya kukuza shirika Tanzania nzima na sio Dar es salaam pekee. Kuhamia Dodoma ingekuwa ni fursa ya Shirika kukua na kujiimarisha kifedha.

Pia, hoja ya kusema nyumba zilizokuwa zinakaliwa na watumishi waliohamia Dodoma zimebaki wazi ni dhaifa. Hilo ni shirika la nyumba la Taifa na sio shirika la nyumba la watumishi. Wafanye matangazo ili waone kama zitakosa wakazi au vipi. Shirika limefanywa la watu wachache ndio maana linapata hasara.

Ushauri wangu, asitafutwe mtu wa kurushiwa yai bovu na hapo ni kutaka kusema kwamba kushindwa Kwa Shirika Kuna uhusiano wa moja kwa moja na uongozi wa awamu ya Tano.

Binafsi nauona udhaifu mkubwa wa uendeshaji wa shirika. Shirika linatakiwa libadike kulingana na sera za nchi.
 
Hapo ndio hao mabosi wa mashirika wanakwama pakubwa kwenye uendeshaji wa mashirika na mentality hii inaisababishia Serikali hasara.

Hoja ya kusema Serikali kuhamia Dodoma imepelekea hasara shirika ni dhaifu sana. Shirika linatakiwa liwe na mikakati ya kukuza shirika Tanzania nzima na sio Dar es salaam pekee. Kuhamia Dodoma ingekuwa ni fursa ya Shirika kukua na kujiimarisha kifedha.

Pia, hoja ya kusema nyumba zilizokuwa zinakaliwa na watumishi waliohamia Dodoma zimebaki wazi ni dhaifa. Hilo ni shirika la nyumba la Taifa na sio shirika la nyumba la watumishi. Wafanye matangazo ili waone kama zitakosa wakazi au vipi. Shirika limefanywa la watu wachache ndio maana linapata hasara.

Ushauri wangu, asitafutwe mtu wa kurushiwa yai bovu na hapo ni kutaka kusema kwamba kushindwa Kwa Shirika Kuna uhusiano wa moja kwa moja na uongozi wa awamu ya Tano.

Binafsi nauona udhaifu mkubwa wa uendeshaji wa shirika. Shirika linatakiwa libadike kulingana na sera za nchi.
Hoja yake ni kwamba miradi iliyokuwa inaendelea ilisimama,kusimama kwa miradi hiyo kulisababisha hasara kwa shirika.Kuamia kwa serikali Dodoma kulifanya mipango ielekezwe Dodoma.
 
Mkurugenzi wa NHC naona kazi imemshinda, Mama yetu mpendwa Samia, piga chini haraka huyu, kawa mpiga kelele na kuropoka hovyo hovyo, kazi kashindwa, fukuza haraka sana huyu ni shida sana. 😡
 
Mkurugenzi wa NHC naona kazi imemshinda, Mama yetu mpendwa Samia, piga chini haraka huyu, kawa mpiga kelele na kuropoka hovyo hovyo, kazi kashindwa, fukuza haraka sana huyu ni shida sana. 😡
Kwenye huu mradi wa nhs kawe wamejigawanyia apartments wenyewe kwa wenyewe hata kabla haujaisha. Riz1 kajinunulia units 1000 na zimo studios za kutosha. Zingine 4000 zilizobakia vigogo wengine wamejinyakulia.

Mradi ukija kuisha wanaziuza kwa bei ya juu.

Nchi ya hovyo kabisa
Screenshot_20230806-121223.jpg
 
Huyu mkurugenzi mimi sijamuelewa katolea mfano mradi wa kawe mbona bado haujaisha kuhama kwa serikali kumekwamisha vip?

Waweke bei za kawaida waone kama hawatapata wapangaji
 
Kwenye huu mradi wa nhs kawe wamejigawanyia apartments wenyewe kwa wenyewe hata kabla haujaisha. Riz1 kajinunulia units 1000 na zimo studios za kutosha. Zingine 4000 zilizobakia vigogo wengine wamejinyakulia.

Mradi ukija kuisha wanaziuza kwa bei ya juu.

Nchi ya hovyo kabisaView attachment 2709898
Hivi hii picha ya maghorofa na njia nzuri hivi hawa watu wanazitoaga wapi maana hata ukiisha ule mradi pale kuwa kama hivi ni uongo..
Watu wanamipango sana.
 
Mbaazi kakosa maua huyo,lazima lazima lawama alitupie jua.

Hata mawilayani huko nyumba za shirika ni makazi ya popo tu.

Vipi Iyumbu,Dom? Mradi wao unamwelekeo?
 
Back
Top Bottom