Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Nimejiuliza hadi nakosa jibu hivi maji yanapita juu ya daraja su chini ya daraja?

Nijuavyo daraja linakuwa limejengewa maji yanapita chini na gari zinapita juu.

Sasa kama ndo hivyo ilikuwaje maji yakapita juu ya daraja gari zinapopita? Au daraja za dodoma zipo tofauti na daraja nyingine?
... huo ndio unaitwa ujenzi chini ya viwango! Ulishawahi kufika Dar-es-Salaam? Kama bado, nenda pale maeneo ya Jangwani ukajionee kituko; daraja na yard ya magari makubwa iliyojengwa "baharini" kwa mabilioni ya shilingi! Huo ni mfano mmoja tu; imejaa kila mahali katika sekta ya ujenzi.
 
Kuna askari Police mmoja alikuwa ni msaidiza wa IGP Mwema kama sijakosea, naye pia alizolewa na maji yeye pamoja na mkewe huko huko Dodoma akiwa anatokea Tarime kuja Dar miaka kama 4 iliyopita.

Maji yana nguvu sana sema watu wanayadharau.
ila tairi ya low profile haielei
 
Madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

Wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

Hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe. Ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
Point yako ni muhimu sana hasa kwa madereva [emoji736]
 
... huo ndio unaitwa ujenzi chini ya viwango! Ulishawahi kufika Dar-es-Salaam? Kama bado, nenda pale maeneo ya Jangwani ukajionee kituko; daraja na yard ya magari makubwa iliyojengwa "baharini" kwa mabilioni ya shilingi! Huo ni mfano mmoja tu; imejaa kila mahali katika sekta ya ujenzi.
Aiseeee
 
Na vipi nikitoa upepo wote naweza kupita na rimu tu? Alafu ntajua mbele kwa mbele
 
Watu hawataki kujifunza kabisa
 
Mimi kuna siku nilikua naelekea Choma cha Nkola nikakuta Mto Manonga umefurika nikaweka gari pembeni wakatokea maafisa wa Mamlaka ya Pamba kwenye gari dogo wakiwa wamelewa wakashauriana na kudanganyana kuwa wavuke gari Lao likasombwa Kati yao watatu mmoja alikufa Maji wawili tuliowaokoa Kati ya hao tukawaokoa mmoja kumbe alikuwa amenng'atwa na Nyoka akiwa ndani ya Maji nae akafa

Chukua tahadhari kwenye maeneo yanayojulikana kuwa naFlash floods au kwenye mito ya misimu
 
Kuna mzee mmoja aliniambia ukiota ndoto inayohusu maji au moto ni ujumbe kuhusu maisha yako. Maji na moto ndiyo vitu pekee Mwenyezi Mungu alivitumia kuiadhibu dunia. Moto kule Sodoma na maji enzi za Nuhu.
Usipende kuamini kila utopolo. Maji ni ishara ya Roho Mtakatifu na moto ni udhihirisho wa nguvu za Mungu dhidi ya maadui zako. Narudia, usipende kuamini kila utopolo unaousikia.
 
Mimi kuna siku nilikua naelekea Choma cha Nkola nikakuta Manonga imefurika nikaweka gari pembeni wakatokea maafisa wa Mamlaka ya Pamba kwenye gari dogo wakiwa wamelewa wakashauriana na kudanganyana kuwa wavuke gari Lao likasombwa Kati yao watatu ni mmoja alikufa Maji wawili tuliowaokoa Kati ya hao tukawaokoa mmoja kumbe alikuwa amenng'atwa na Nyoka akiwa ndani ya Maji nae akafa

Chukua tahadhari kwenye mwendo yanayojulikana kuwa Flash floods au kwenye mito ya misimu
Choma cha Nkola ni wapi huko? Jitahidi unapoeleza kitu toa ufafanuzi unaoeleweka.
 
Kaimu mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa mifugo kanda ya kati, Dk Harun Chawala na mkewe, Neema Mwasanganga wamefariki baada ya gari walilokuwa wamepanda kusombwa na maji wakati wakivuka daraja la Shaaban Robert mjini Mpwapwa, Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti Tanzania, Dk Jonas Kizima amesema leo Jumamosi Machi 6, 2021 kuwa tukio hilo limewasikitisha kutokana na kupoteza nguvu kazi ya Taifa na taasisi ya utafiti Tanzania.

Amesema Dk Chawala alikuwa anampeleka mkewe kazini kwenye hospitali ya wilaya, lakini walipo fika kwenye daraja hilo maji yaliwazidi na kusombwa.

Dk Kizima amesema tukio hilo limetokea jana saa 2 usiku baada ta gari hilo aina ya Nissan lenye namba za usajili T483 BRR kusombwa na maji kwenye daraja hilo lililopo mita chache kutoka ilipo ofisi ya mkuu wa wilaya.

Kutoka gari ilipotumbukia hadi ilikokutwa miili ni umbali wa karibu kilomita 18 na ilikuwa katika maeneo tofauti.

Mashuhuda wanasema mwili wa mwanamke ulikutwa kitongoji cha Kwamshango kilomita 15 kutoka walipotumbukia wakati mwili wa Dk Chawala ulikutwa kitongoji cha Isinghu umbali wa kilomita 18.

Miili yote imepatikana imehifadhiwa katika hospitali ya Mpwapwa ikisubiri taratibu za ndugu na Serikali.

Chanzo: Mwananchi
Watu wengine watasema CORONA maana wanalao jambo.
 
Ahsante sana
Madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

Wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

Hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe. Ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
 
Back
Top Bottom