Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Kuna askari Police mmoja alikuwa ni msaidiza wa IGP Mwema kama sijakosea, naye pia alizolewa na maji yeye pamoja na mkewe huko huko Dodoma akiwa anatokea Tarime kuja Dar miaka kama 4 iliyopita.

Maji yana nguvu sana sema watu wanayadharau.
Kuna mzee mmoja aliniambia ukiota ndoto inayohusu maji au moto ni ujumbe kuhusu maisha yako. Maji na moto ndiyo vitu pekee Mwenyezi Mungu alivitumia kuiadhibu dunia. Moto kule Sodoma na maji enzi za Nuhu.
 
madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe.. ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
Traffic wa Tanzania wachukue huu ujumbe wawe wanatumia kutoa elimu.
 
Kaimu mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa mifugo kanda ya kati, Dk Harun Chawala na mkewe, Neema Mwasanganga wamefariki baada ya gari walilokuwa wamepanda kusombwa NA maji wakati wakivuka daraja la Shaaban Robert mjini Mpwapwa, Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti Tanzania, Dk Jonas Kizima amesema leo Jumamosi Machi 6, 2021 kuwa tukio hilo limewasikitisha kutokana na kupoteza nguvu kazi ya Taifa na taasisi ya utafiti Tanzania.

Amesema Dk Chawala alikuwa anampeleka mkewe kazini kwenye hospitali ya wilaya, lakini walipo fika kwenye daraja hilo maji yaliwazidi na kusombwa.

Dk Kizima amesema tukio hilo limetokea jana saa 2 usiku baada ta gari hilo aina ya Nissan lenye namba za usajili T483 BRR kusombwa na maji kwenye daraja hilo lililopo mita chache kutoka ilipo ofisi ya mkuu wa wilaya.

Kutoka gari ilipotumbukia hadi ilikokutwa miili ni umbali wa karibu kilomita 18 na ilikuwa katika maeneo tofauti.

Mashuhuda wanasema mwili wa mwanamke ulikutwa kitongoji cha Kwamshango kilomita 15 kutoka walipotumbukia wakati mwili wa Dk Chawala ulikutwa kitongoji cha Isinghu umbali wa kilomita 18.

Miili yote imepatikana imehifadhiwa katika hospitali ya Mpwapwa ikisubiri taratibu za ndugu na Serikali.

Chanzo: Mwananchi
Poleni ndugu
 
Kaimu mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa mifugo kanda ya kati, Dk Harun Chawala na mkewe, Neema Mwasanganga wamefariki baada ya gari walilokuwa wamepanda kusombwa NA maji wakati wakivuka daraja la Shaaban Robert mjini Mpwapwa, Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti Tanzania, Dk Jonas Kizima amesema leo Jumamosi Machi 6, 2021 kuwa tukio hilo limewasikitisha kutokana na kupoteza nguvu kazi ya Taifa na taasisi ya utafiti Tanzania.

Amesema Dk Chawala alikuwa anampeleka mkewe kazini kwenye hospitali ya wilaya, lakini walipo fika kwenye daraja hilo maji yaliwazidi na kusombwa.

Dk Kizima amesema tukio hilo limetokea jana saa 2 usiku baada ta gari hilo aina ya Nissan lenye namba za usajili T483 BRR kusombwa na maji kwenye daraja hilo lililopo mita chache kutoka ilipo ofisi ya mkuu wa wilaya.

Kutoka gari ilipotumbukia hadi ilikokutwa miili ni umbali wa karibu kilomita 18 na ilikuwa katika maeneo tofauti.

Mashuhuda wanasema mwili wa mwanamke ulikutwa kitongoji cha Kwamshango kilomita 15 kutoka walipotumbukia wakati mwili wa Dk Chawala ulikutwa kitongoji cha Isinghu umbali wa kilomita 18.

Miili yote imepatikana imehifadhiwa katika hospitali ya Mpwapwa ikisubiri taratibu za ndugu na Serikali.

Chanzo: Mwananchi
Wamenunua madege wameshindwa kujenga madaraja...mitano tena
 
madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe.. ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
Asante kwa maelezo ya kina,tujifunze kitu hapa,madereza wa mabasi wameua sana watu kwa kuamini basi limejaa kwahio ni 'zito' kumbe likikanyaga maji Hamna kitu
 
f4c2bd56-3d4b-4a20-95ab-38533f311817.jpg

Hao ndio waliofaliki
 
Back
Top Bottom