Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Mkurugenzi na mkewe wafa maji Mpwapwa

Nimejiuliza hadi nakosa jibu hivi maji yanapita juu ya daraja au chini ya daraja?

Nijuavyo daraja linakuwa limejengewa maji yanapita chini na gari zinapita juu.

Sasa kama ndo hivyo ilikuwaje maji yakapita juu ya daraja gari zinapopita? Au daraja za dodoma zipo tofauti na daraja nyingine?
Kuna wakati mwingine watu wanachanganya kuna tofauti kubwa kati ya bridge, pipe culvert, box culvert, drift n.k lakini watu wengi hua wanaita tuu daraja,
Ila kinachotokea dada angu kwamba kunakua na overflow yaan maji yanapita juu ya hiyo structure na yanakua mengi n speed kubwa,
Maeneo mengi katika nchi yetu ni drift ambazo zinaruhusu maji kupita juu yake sasa yakiwa mengi na speed kubwa shida inaanzia hapo

Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Ina huzunisha sana hasa kwa watoto wa marehemu hao kuachwa yatima. RIP
 
Ukiona maji hata kama ni kidogo yanapita juu ya daraja usithubutu kupita.
 
Wameacha watoto wadogo wa2, Mke alikuwa Dr pia na alikuwa anawahi shift ya usiku ,...very sad indeed
Duh unawahi shift, kumbe unawahi kifo

Humu duniani tuleni bata jamani, unasepa anytime [emoji848]
 
Inasikitisha sana kuona watu waliopata elimu kufanya makosa yaleyale na kupelekea kupoteza maisha kirahisi tu.
R.I.P
Hapo ndiyo unajua Elimu na Maarifa ni vitu viwili tofauti kabisa! Unaweza kua na Elimu na bado ukakosa Maarifa!! RIP kwa Marehemu wote!!
 
Walikua hawalioni au?
Lazima wife wake ndiyo alimshinikiza wapite maana yeye alikua anawaza kuwai kazini tu! Wanaume Mambo ya hatari tuwakatalie hawa Wanawake, maana wengi wao hawajui kuipima hatari kwa mbali kama sisi Wanaume tunavyojua kizipima kwa mbali!!
 
Haya madaraja haya...Juzi tu tumewazika wanne kwa ajali kama hii ya kusombwa na maji...
Sijui huwa hatujifunzi kwa wenzetu!?[emoji848]
Madereva Wengine wanasubiri hadi Serekali iwaambie darajani kumejaa Maji msipite,bila Kuambiwa na Serekali wao shega tu mwendo mdundo liwalo na liwe!!
 
Dah so sad Hilo eneo s mara ya kwanza kusikia linaleta maafa tahadhar ichukuliwe

Ni kweli kabisa tahadhari ichukuliwe, magari yabebe maboya ya kuogelea pamoja na pima maji kucheki kina chini ya daraja kabla ya kupitisha gari, au?
 
Wameacha watoto wadogo wa2, Mke alikuwa Dr pia na alikuwa anawahi shift ya usiku ,...very sad indeed
Jamaa alikuwa poa sana,mwakajana march kunajamaa aliniunganisha nae alinipeleka na hy nissan had kwny Boma la ng'ombe wa mpwapwa breeds nadhani ni njia ya kuelekea jkt.
 
Gari kwenye maji sio la kuamini kabisa,halina nguvu yoyote,Pole kwa wafiwa
Wapi wamesema gari lilijaribu kupita kwenye maji ?

Nchi ya watu ma dunderhead, motorist kakuta daraja liko wazi kavuka, kafa, analaumiwa badala ya msimamizi wa daraja...

Tutaendelea kufa kwa sababu raia hawajui wajibu wa serikali ni nini, kwa hiyo hakuna atakaedai serikali iwajibike, na serikali inajua na inasema inaongoza wanyonge wasio na sauti. Sauti hapo wanamaanisha upeo. Wanyonge wasio na upeo wa akili.

Kama uko Tanzania toka siku umezaliwa huwezi kunielewa!
 
Madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

Wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

Hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe. Ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
Hizi Elimu za Majanga zinatakiwa kufundishwa tangu Watoto wakiwa primary school,hii itasaidia sana watu wengi kua na tahadhari kwenye Majanga yanapotokea!!
 
Dah so sad Hilo eneo s mara ya kwanza kusikia linaleta maafa tahadhar ichukuliwe

Nb Kuna nafas 1 idara ya mifugo na moja idara ya afya serikal itangaze nafas hiz vijana wapo tu mtaan kaz hakuna
ndio unachokiwwza.wapo watakaimu
 
Madereva wengi tunapata leseni bila kupitia mafunzo sahihi..

Wakati nasoma NIT, nakumbuka niliambiwa usipite kwenye maji yanayotembea kabisa mpaka yaishe yasiguse tairi.. sababu tairi ni mpira uliojaa upepo,, yaani ni kama boya kwenye maji.. gari na uzito wake wote wa juu limebebwa na tairi ambalo ni boya kwenye maji.. sasa boya lazima lisombwe na maji tu, bila kujali uzito gani lilobeba,,, uoni hata binadamu kibonge akipewa boya anaelea tu bila kujali uzito wake,,

Hata gari liwe limebeba mzigo mzito kama copper ama kontena la mawe. Ila kwenye maji yanayotembea linasombwa na maji tu sababu matairi ni kama maboya
ajal haina kinga.ila ni kweli usivuke na gar kwenye maji yanaoenda kwa spidi kubwa labda ziwe zile jeep wrangler beast 4X4 niliona jamaa anapanda nayo kwenye korongo la mto
 
Mimi kuna siku nilikua naelekea Choma cha Nkola nikakuta Mto Manonga imefurika nikaweka gari pembeni wakatokea maafisa wa Mamlaka ya Pamba kwenye gari dogo wakiwa wamelewa wakashauriana na kudanganyana kuwa wavuke gari Lao likasombwa Kati yao watatu ni mmoja alikufa Maji wawili tuliowaokoa Kati ya hao tukawaokoa mmoja kumbe alikuwa amenng'atwa na Nyoka akiwa ndani ya Maji nae akafa

Chukua tahadhari kwenye mwendo yanayojulikana kuwa Flash floods au kwenye mito ya misimu
ilikuwa kwenye daraja?
 
Back
Top Bottom