Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

nionavyo mimi ni heri kinga ya marais wote duniani ingetolewa ili wawe na adabu maana wanafanya ufisadi kwa kujua wanakinga ya urais


Hana kinga yoyote huyu, ila anajificha ficha tu nyuma ya aliowapa madaraka kwa ubabe, lakini sasa saa imefika hakuna pa kukimbilia, wabunge wa CCM wameanza kazi ya kutafuta ukweli mbele ya sheria na sisi wananchi tupo nyuma yao!
 
Bubu umenigusa hapo heri mara "vijisenti" huo umember wangempa Mzee Kawawa aliyekuwa bega kwa bega na JKN (rip) kudai Uhuru kuliko huyo Fisadi BWM
 
Mtanzania:

Sio kweli kwamba akina Nyerere na akina Kawawa hawakufanya ufisadi kwa utashi tu. Ndio pamoja na utashi na moral standing yao, usisahau hawa bwana walijiwekea vizingiti vizito sana chini ya Azimio la Arusha ambalo hawa jamaa wa CCM mpya wakaja kuisambaratisha. So, there you are; there was a very elaborate and effective system to prevent leaders from falling into the devil's immoral track ambayo sasa hivi hatuna!

Hiyo ya kumdharau nakubaliana na wewe kabisa. Naogopa sana ya kumfikisha mahakamani Mkapa kunaweza kukamsafisha kuliko kumtia hatiani and the consequences will be far reaching maana hata mafisadi wengine watakuwa wamesafishwa kwa njia moja au nyingine. Hii adhabu wanayopata sasa hivi hawa jamaa ya kuzomewa na kudharauliwa na wananchi ni ya maana zaidi kuliko ya kupelekwa mahakamani.


Hata kama kina Kawawa na Warioba walifanya ufisadi but ufisadi wao walikuwa waerevu zaidi,Mkapa kushatakiwa ni lazima.Watazania tutekeleze ile "motto ya awamu ya tatu- UWAZI NA UKWELI" . UWAZI wa Mkapa ni kufanya ufisadi na biashara ndani ya Ikulu??.("IKULU MAHALI PATAKATIFU" sio msemo wangu but nimemnukuu Mwalimu JKN (RIP)aliyasema wakati wa awamu ya pili)Mwl JKN aliweza kukemea maovu yote hakuogopa mtu baada ya kutawaliwa na Mwenyezi Mungu ndipo makucha ya mafisadi yalipo anza kuchomoza tena kwa kasi ya ajabu, tukija upande wa pili wa shilingi "UKWELI" lazima ujulikane na sheria ifuate mkondo wake Watanzania tumechoshwa kuburuzwa. Kumzarau tu haitoshi na wala haisaidi... nisawa na ule msemo usemao "Kelele za chura...."
 
Mkuu Nyangumi,

Heshima mbele, kuna time and season ya kila kitu, as a nation politically na legally it is not in our interest kurekebisha kifaa, ambayo inapaswa kuwa a longterm national project with a lot of research na hela, sasa hivi tuna an-emergency and very urgent ishu ambayo inahitaji kuwa tackled now, nayo ni kuwakamata mafisadi wote na kuwafikisha kwenye mkondo wa sheria zetu za jamhuri as a starting point ya kuelekea kwenye kukitengeneza kifaa chetu kwa the longterm au permanently,


Mkuu FMES, Nimecheka sana hapa. Nakubaliana nawe kabisa kuwa ni lazima hawa jamaa wafikishwe mahala kunapostahili huko mahakamani. Wasiwasi ni kwamba

i) bila kuweka sawa mfumo unawazaa hao mafisadi hatutawamaliza kama unavyosema maana wataendelea kuzaliwa na mfumo huo unaowazaa utaendelea kuji-adapt ili kuhakikisha kwamba hawakamatiki kirahisi. Cha kuelewa hapa ni kwamba haya yanayotokea leo yanatokea kwa sababu ya, pengine kwa bahati nzuri, JK ameshindwa kudhibiti utokaji wa habari. Hawa mafisadi ni hawahawa waliokuwepo wakati wa Mkapa lakini wakati huo Mkapa hakuwapa nafasi akina Slaa kupata habari zao na kwenda pale Mwembe Yanga na kuwataja. Leo hii isingekuwa Dr Slaa kuwataja haya majamaa pale Mwembe Yanga, na thanks to Speaker kumzuia Slaa kuweka hoja yake bungeni, Rostam Azizi angekuwa bado maarufu na angeendelea kuwa kipenzi cha wazi cha Rais wetu.

ii) Huko mahakamani ni sawa kabisa. Lakini tunachosahau hapa ni kwamba we are dealing with corrupt but very intelligent people, sometimes more intelligent than most of us here in the forum and elsewhere. Mtu kama Chenge is a Havard trained lawyer, amekuwa mwanasheria mkuu for 10 years. Hii maanake ni kwamba sio tu kwamba anazijua sheria zetu vizuri bali pia yeye ndiye aliye-archtect sheria nyingi tulizo nazo leo. Kama Chenge ni fisadi ni rahisi kuelewa hapa kwamba atakuwa aliweka mazingira katika sheria zetu hizohizo kuhakikisha kwamba zinalinda ufisadi na mafisadi. Hii maanake ni kwamba Chenge anajua tutakapofika mahakamani ndiyo utakuwa mwisho wa sisi na tutabaki na hasira zetu tukijiuma vidole. Sio vigumu kujua kitakachotokea nacho ni kuwabambikizia majaji wetu ufisadi bila kuelewa kwamba majaji hawatungi sheria bali wanaamua kesi kwa mujibu wa sheria zilizopo wala sio kwa uchungu walio nao kwa nchi au busara zao! Basi ni rahisi kuelewa kwa nini hawa mafisadi wananasisitiza kupelekwa mahakamani.

Kwa hiyo ndugu yangu FMES, mataifa yote yaliyoamua kupambana na rushwa walianza kwa kupambana na mazalisho ya rushwa. Walihakikisha kwamba sheria zote zinazolinda ufisadi zinatupiliwa mbali. Ndivyo walivyofanya huko China ambapo huwa unatupa mifano yake kila siku. Muhimu zaidi huwezi kusema unapambana na ufisadi bila kuhakikisha kwamba the institutions entrusted with the duty to curb corruption such as the likes of TAKURU are independent, impartial and professional.

Kwa hiyo, nakuunga mkono tuendelee kuwaswaga hawa jamaa kwenda mahakamani, lakini tuhakikishe kuwa zoezi hili linaenda sambamba na kurekibisha mfumo wetu wa utawala na sheria. Unanishangaza sana unaposema hili la kurekebisha sheria zetu unasema linahitaji research na ni long term goal. Yaani JK ana wabunge zaidi ya 90% ambao wote ni loyal hakuna hata rebel moja anashindwa nini, kwa mfano, kupeleka mswada wa sheria haraka unaokataza viongozi wa serikali kununua hisa na kwenye mashirika ya umma yanayobinafsishwa? Hapana ndipo mimi ninanusa harufu ya political calculation kwenye hiki tunachoita vita dhihi ya ufisadi badala ya vita yenyewe!

Anyway, furaha yangu kwenye hii saga ni kwamba political verdict hahitaji kusubiri court verdict. Wananchi wameshapitisha verdict yao kwamba chama kinachotawala Tanzania cha CCM kimejaa viongozi mafisadi na hivyo kinachosubiriwa ni hiyo political verdict ambayo itatolewa wakati wa uchaguzi.
 
Mkapa can be taken to court, say lawyers

2008-04-30 09:25:03
By Gadiosa Lamtey

Prominent scholars have said immediate former president Benjamin Mkapa could be taken to court if there is enough evidence linking him to abuses of office.

The scholars, among them reputable lawyers, said in interviews yesterday that the abuses would include fishy transactions in the public service entered into during his ten-year administration.

The retired third-phase president is one of the most high-profile targets of rapidly circulating reports relating to grand corruption allegations.

One is that he and Daniel Yona, once Energy and Minerals minister under him, bought the 4bn/- state-run Kiwira coal mine at a paltry 700m/- but ultimately paid a mere 70m/- for it.

Tanzania`s constitution stipulates that the country`s sitting president enjoys immunity from criminal and civil proceedings in respect of anything done or not done in his or her personal capacity as an ordinary citizen.

The law also prohibits people from instituting criminal or civil proceedings for anything done or not done in his or her capacity as president even after he or she is no longer in power.

But some Dar es Salaam-based lawyers contacted for comment on the issue yesterday said, the provisions of the constitution notwithstanding, the government is still obliged to take legal action against any former president using his or her office for personal gain.

The legal experts interviewed observed that, in accordance with the Presidential Affairs Act, Mkapa`s immunity may be waived if he would be proven to have deliberately abused his office.

Legal and Human Rights Centre (LHRC) Executive Director Hellen Kijo-Bisimba said the Act can only protect a president executing his or her official duties at the State House ``but the law provides for the president to be taken to task when it is proved that he or she used the public office to do private business``.

Kijo-Bisimba expressed hope that the ongoing investigations into the allegations relating to the coal mine�s controversial purchase would come up with the best decision on how to deal with the former president.

She pointed out that the National Assembly has the legal mandate to waive president`s immunity when necessary and allow the law to take its course.

``What happened to former Zambian president Frederick Chiluba could happen in Tanzania as well. Just as the Zambian legislature waived Chiluba`s presidential immunity and allowed the government to file a case against him, there could be a similar development here.``

Chiluba is facing a pending criminal case for alleged involvement in the gross misappropriation of public funds when he was president of Zambia.

Human rights activist and legal counsel Tundu Lissu observed that the International Criminal Court had categorically stated that the law should not be used to protect presidents or anybody violating human rights or otherwise breaking the law.

He recommended that Tanzania`s constitution similarly stipulate that even the president could face legal action once found use his or her (public) office to further personal interests.

``Mkapa has no excuse on this; the government should take him to court and make him respond to the allegations levelled against him,`` he said.

Another legal expert, Twaha Tasilima, said: ``It is not always and at all costs that a sitting or former president can be protected by the law. There are situations where the immunity can be revoked if it is believed that he or she misused his or her presidential powers.``

He expressed full support for the decision by the Jakaya Kikwete government to investigate the allegations against the former president ``so that the facts can be known and appropriate legal and other measures can be taken.

``It is a laudable development and the people are eagerly waiting for the outcome of the investigations. Should it mean finally taking the former president to court, then that will serve as a lesson to other prominent public figures to act likewise,`` Lissu pointed out.

Prof Mwesiga Baregu, a long-serving don with the University of Dar es Salaam, noted that it was ``prime time for President Kikwete to allow the law to take its course unimpeded by personal interests``.

He said the country`s constitution does not allow anyone to break the law and get away with it and agreed with those insisting that the former president should be taken to court to answer the allegations levelled against him.

Dr Edmund Sengondo Mvungi, Dean of the university`s Department of Constitutional and Administrative Law, stated that the law actually provided for the impeachment of a retired president.

``The Constitution protects the President when he or she executes his or her official duties at the State House but the law is clear that he or she should be taken to task for conducting private business in contravention of the laws of the land,`` he explained.

Dr Mvungi elaborated that the Constitution offered protection to the president only in the course of performing legitimate public duties he is entrusted by the citizenry to perform, ``the duties including inspecting guards of honour but not illegal undertakings``.

``I would strongly recommend that President Jakaya Kikwete decide fast on the next step to take in view of prevailing murky circumstances,`` he said.

Prime Minister Mizengo Pinda told the National Assembly late last week that the government had begun working on allegations of abuse of office and other charges levelled against some third-phase government leaders.

He said the government was still following up and evaluating the allegations so as to know what exactly happened and that any relevant information would be made public after completion of the investigations.

Despite the swelling wave of the allegations and persistent efforts by the media to have him respond to them, the former president has remained unshakably tight-lipped.

SOURCE: Guardian
 
Zanaki,

..ulizia historia ya nyumba ya msasani utagundua kwamba na yenyewe ni zawadi ya Watanzania. JKT na JWTZ ni vyombo vya serikali. kwa msingi huo ukweli unabaki kwamba serikali/Watanzania wamemzawadia Mwalimu nyumba 3.

..Kuhusu makumbusho hilo ni suala la kitaifa. Huu unaweza kuwa mzozo kama ule wa hotuba alizokuwa akitoa Mwalimu akiwa Raisi wa Jamhuri. Je, hotuba zile ni mali ya serikali/Watanzania, au ni mali ya Mwalimu na familia yake?

..Ushindi wa Makongoro arusha haukuwa wa haki. Mahakama iliamua hivyo na yeye hakukata rufaa. Tena kama mahakama ilikuwa imemuonea alikuwa na nafasi ya kugombea tena.

..Sina matatizo na dada yake Makongoro kuchaguliwa[kwa kura] kupitia viti maalum.

..Kila Mtanzania anajua kwamba bila Mwalimu Mkapa asingekuwa Raisi wa Tanzania. Kuonyesha shukurani zake na kuzingatia kwamba Baba yao amewatoka, Mkapa akamteua Makongoro kuwa mbunge.

..unaposema kwamba Mama Maria yuko 'bitter' hainiingii akilini. nasema hivyo kwasababu familia ya Baba wa Taifa imeenziwa kuliko familia za wanasiasa wote waandamizi. Pia hata Baba wa Taifa hakuwahudumia kwa namna yoyote ile watumishi mbalimbali waliofanya naye kazi.

..wako watendaji wengi waliofanya kazi na Mwalimu ambao walitelekezwa na serikali. nimekutajia waziri anayeishi jirani na kwa Mwalimu ambaye nyumba yake ilikuwa haina hata madirisha. Mwalimu hakumsaidia kwa namna yoyote ile. Nyumba hiyo ilikamilika watoto wa waziri huyo walipomaliza shule!! Mwalimu aliliona hilo, Mama Maria analifahamu. Sasa ni vipi leo hii awe bitter kwa kutokujengewa ukuta tu??
 
Hao vingunge wote wameshaipima serikali ya Kikwete na wanajua haiwezi kufanya lolote ,ndio maana hawataki hata kujishughulisha na haya mauzauza ya serikali inayolegalega ,si umiona kule Butiama ni vigogo wangapi hawakuhudhuria ,ivi kama ni wakati wa mwalimu akina Mwinyi na Mkapa na hao wengine wangelisubutu kutohuzuria ,hivi jamani hamna macho maana mwenye macho haambiwi tazama ,hivi karume angesubutu kusema kama mnataka kuwashirikisha wapinzani basi turudishieni ASP na nyie mchukue TANU yenu ,kama maneno ya busara yapo ila CCMZanzibar hawana wala hawayajui maneno ya busara ambayo wangeweza kuyatumia zaidi ya huu ufezuli ambao wameuonyesha mbele ya Mwenyekiti wa Chama chao na Raisi wa Jamhuri ya Tanzania haya maneno au ni heshima gani hii,hivi hamuoni hapo kama kitu heshima hakuna tena na Kikwete ameshaonekana kuwezwa au tuseme wanamblekimeli na inabidi akunje mkia ukali na ari na nguvu zote amekuwa ni kama ile mesali ya debe bovu na mwisho hao mafisadi watamuita Mr Debebovu wakati ndio utakaotueleza.Sisi tunamuelekeza Kikwete afunge mkaja na sasa avae miwani meusi kabisa yaani hata macho asionekane ili aweze kuchukua hatua bila ya kuangalia uso ni wa nani la si hivyo itakuwa tayari wameshamfunga kengele.
 
...Yote niliyosema hapa ni fact,na ukitaka ukweli nimetaja mtu wa kwenda kumuuliza

Zanaki, hizo 'facts' ni Butiku kakwambia? Wengine hatuna access na Butiku, ndio maana watu wanakuswalisha.

Hata hivyo, mimi binafsi naamini mengi uliyo yasema kwa sababu umeshusha nondo fulani nyeti, ambazo hata kina Issa Shivji na Ally Mazrui hawazijui. Ulipotaja uhusiana wa Adam Marwa na Ben Mkapa zile ni nondo za ki-shushushu. Na unajua kwa nini nasema hivyo!

Lakini watu ambao hawaelewi hizo nyeti wana haki ya kuto zichukulia kama 'facts' kwa sababu wewe umesema.

Anyway, ahsante kwa zile details za mazingira ya uchaguzi wa 1995 na jinsi kina Butiku walivyo mtaka Mkapa. Kwenye vitabu vya historia zile nondo hakuna. Kuna mtu kauliza humu Kikwete ana watoto wangapi, akaambiwa tokelea kule na ishu irrelevant. Wengine wakampa link za kwenda kutafuta hizo data. Wengine wakamwambia JK amejaza fomu kwamba ana watoto 8. Kwa maneno mengine wqatu hawana uhakika rasmi, na wala hawataki kujua, Rais wetu ana watoto wangapi. Wenzetu wanafanya utafiti kujua John Adams na Thomas Jefferson walifanya ngono na mtumwa gani miaka mia mbili iliyo pita! Details za historia, ambazo zinaweza kusaidia kumwelewa zaidi Rais wako. Sisi bado kweli!
 
Yaani katika vitu muhimu vinavyoikabili Tanzania sasa hivi tupange msururu wa kuuliza Rais ana watoto wangapi? Halafu tukishajua?

Isipokuwa kama alituhumiwa kubaka au kufanya kitendo kinyume na sheria katika kupata watoto hao au kutumia nafasi yake (mambo ya kina John Adams na TJ).

Kuna madai ya aina hiyo kuhusu Rais?
 
Yaani katika vitu muhimu vinavyoikabili Tanzania sasa hivi tupange msururu wa kuuliza Rais ana watoto wangapi? Halafu tukishajua?

Mwnkj, sikutegemea utasema hivyo. Duuh!

Kwani hapa tunajadili Siasa na vitu vya maana tu? Mbona wewe huwa unaleta funnies na vikatuni vya Wabunge tunasoma tunacheka na ndio mwisho wake. Na mashairi yako na Pundit tunasoma tunafurahi. Na salamu zenu za kutembeleana na kupikiana Ugali na Mwafrika wa Kike ambazo hamuwezi kuziacha kwenye PM. Na mengine mengi tu ya ajabu ajabu.

Itakuwa mtu kuuliza Biography ya Rais? Ni histori tu ndugu yangu. Au unanipinga tu kwa sababu huwa nakupa mzeta mzeta nisipokubaliana na wewe?
 
Mwanakijiji,

Watanzania wana haki ya kumjua rais wao na familia yake kwa sababu nyingi tu.Kuna wengine ni historians wanataka ku document facts.Historians wanapotaka ku document facts mara nyingine wanaweza wasijue umuhimu wa facts zile kwa muda ule, bali mbeleni facts hizo zinaweza kuwa muhimu.

Lakini pia katika context yako ya kwamba kama hamna wrongdoings it is not worth it kutafuta hizi facts, vipi kama mtu atasema ni muhimu kuwajua watoto wa Kikwete ili kesho keshokutwa yasije kujirudia yaliyotokea ya Peter Mkapa/Mramba NetGroup na TTCL?

Vipi kama mtu anasema inabidi tuwajue watoto wa rais ili kusudi mi milioni anayoweza kuiiiba Kikwete isiende kuwekwa kwa jina la Miraji au mtoto mwingine ambaye hajulikani?

Tukiijua familia ya rais vizuri tunaweza kusema kuwa itasaidia hata kwenye vita ya ufisadi. Tushaona mambo ya Kiwira yalivyoenda hapo kina Mkapa, from Ben and Anna to Nico, bado tunafikiri kuijua familia ya rais si muhimu tu?
 
Mwnkj, sikutegemea utasema hivyo. Duuh!

Kwani hapa tunajadili Siasa na vitu vya maana tu? Mbona wewe huwa unaleta funnies na vikatuni vya Wabunge tunasoma tunacheka na ndio mwisho wake. Na mashairi yako na Pundit tunasoma tunafurahi. Na salamu zenu za kutembeleana na kupikiana Ugali na Mwafrika wa Kike ambazo hamuwezi kuziacha kwenye PM. Na mengine mengi tu ya ajabu ajabu. Nianze kuanzia leo ku point vitu ambavyo unavileta hapa ambavyo havina miguu wala kichwa?

Itakuwa mtu kuuliza Biography ya Rais? Ni histori tu ndugu yangu. Au unanipinga tu kwa sababu huwa nakupa mzeta mzeta nisipokubaliana na wewe?

Kwi kwi kwi,

inaonekana salamu zile zinakutoa moyo kabisaaa!
naona inabidi nitafute muda kuniambia nani alikuwa the real first wife wa Kawawa maana naona hiyo itasaidia kuleta umeme kule Kigoma!
 
Kwa kuwa mnauliza familia na mimi ningependa kuuliza swali moja tu. Nikiwa nje ya nchi rafiki yangu mmoja kutoka Namibia alisema kuwa Nyerere ni kiongozi shupavu sana, alihamua kuachana na mkewe Mama Maria hili apiganie vizuri uhuru wa nchi za kiafrika na maendeleo ya nchi yake.

Nilimuamini jamaa kwa sababu wakati fulani, Baba wa taifa alikuwa pekee yake. Na ziara za nje alikuwa anapiga bila ya kuwa na first lady.

Je kuna ukweli uwana mapinduzi ulifanya Baba wa taifa asahau familia kwa muda fulani?

Wenu

BM.
 
Kwi kwi kwi,

inaonekana salamu zile zinakutoa moyo kabisaaa!

Nisife moyo eeeeenh? Kwa hiyo ni poa Mwafrika wa Kike? Mradi usiwe Mwafrika wa Kiume tu, kama yule mfukuzwa alivyo dai. Maana jamaa alikuwa mkimjibu tofauti tofauti yeye anawajumlisha wote kama mtu mmoja. Halafu ana mi confidence ile mbaya. Anadai mmekutana wapi, Russia? Yani sina mbavu!
 
Kwa kuwa mnauliza familia na mimi ningependa kuuliza swali moja tu. Nikiwa nje ya nchi rafiki yangu mmoja kutoka Namibia alisema kuwa Nyerere ni kiongozi shupavu sana, alihamua kuachana na mkewe Mama Maria hili apiganie vizuri uhuru wa nchi za kiafrika na maendeleo ya nchi yake.

Nilimuamini jamaa kwa sababu wakati fulani, Baba wa taifa alikuwa pekee yake. Na ziara za nje alikuwa anapiga bila ya kuwa na first lady.

Je kuna ukweli uwana mapinduzi ulifanya Baba wa taifa asahau familia kwa muda fulani?

Ahsante ewe Bin Maryam, uliye itwa Mbarikiwa, ukazaliwa na Bikira, kwa interest yako ya Historia na Biography ya viongozi wetu. Sijui kuhusu Nyerere kumuacha Maria, lakini kwenye neglect ya familia kwa upande wa watoto ni kweli.

Nyerere ali neglect watoto wake. Mahitaji kama karo yalikuwa yanapitia kwa Butiku. Wakina Anna wamewaambia marafiki zao, ambao nimewasikia. Unaweza kusema Nyerere alikuwa ametingwa na ilimlazimu a delegate hizo kazi, lakini kuna mambo ambayo watoto walikuwa hawawezi kumwambia Butiku. Sio baba yao.

Unakumbuka kuna deputy mmoja wa Saddam Hussein, Abid Hamid Mahmud al-Tikriti, alikuwa kila Sadam akitaka kukaa chini yeye anamvutia kiti. Yule mtu hata kina Uday na Qusay hawamwoni baba yao bila kupitia kwake. Ndio Butiku, Nyerere na kina Anna na kina Mokongoro!

Haya mambo kuhusu Baba wa Taifa hakuna anae yaandika Bongo. Ni kufuru. Wana historia pale UDSM wapo kama hawapo. Wabongo tunasema kujua nani mke wa kweli wa Kawawa hakuta saidia kuleta maji Kigoma. Bahati mbaya, hatumjui mke wa Kawawa na maji hayaji. Bora tumjue, tupige gumzo la Historia tukiganga kiu. Watu wasipo piga gumzo wakati wana kiu na njaa wata riot. Iulize Serikali!

Kuna nadharia moja ya Kaisari na Juvenal inasema ukitaka kutawala watu wape vitu viwili: mkate na sarakasi. Wakisikia njaa wape mkate, wakiwa bored wape maonyesho ya sarakasi kuwatumbuiza. Vinginevyo wata revolt. Sasa Bongo hatupati hayo maji wala hadithi za wake wa Kawawa na idadi ya watoto wa Kikwete, tukapiga gumzo. Ni hatari!

Ahsante ndugu yangu.
 
Mkuu Zanaki,

Heshima mbele, dataz zako ni nzito sana isipokuwa tu marekebisho kidogo,

1.
Na wale wanaosema Mkapa alikuwa ni chaguo la Nyerere,pia hio sio sawa! Chaguo lake lilikuwa Salim,na Salim aligoma akitoa sababu kuwa anataka kumalizia kazi zake OAU kwanza,na atagombea baada ya hapo,ofcoz yeye akijua Nyerere angekuwa bado yuko hai.

Mwalimu alijaribu kumpitisha Salim, wajumbe wa Visiwani wakamgomea kata kata, akaamua kutumia plan B yaani Mkapa!

2.
Waliomshinikiza Mkapa agombee ni Warioba,Salim,Butiku na jamaa mmoja anaitwa Adam Marwa,na hao ndio waliomfuata Nyerere ili amuendorse Mkapa.

Nyerere asingeweza kumu-endorse kiongozi yoyote asiyemtaka yeye, na siku zote alikuwa akimdharau sana Butiku, kiasi kwamba asingeweza kumsikilza, Warioba alikuwa anagombea ni yeye Mwalimu aliyemtoa na kumuweka kwenye kuhesabu kura za urais, siku Mkapa anatangaza kuchukua fomu, alikuwa na Salim na Warioba pembeni kwenye meza na waandishi wa habari, wakitegemea mkapa kuwapa unga, na he did kwa kutumia hela nyingi sana za taifa kumsaidia Salim kushinda tena OAU, na kumpa Warioba ile tume na pia kumsaidia kwenye kupata uhakimu wa law of the sea wa dunia, kote huku mkapa alitumia hela zetu walipa kodi kuwapitisha marafikiza ke, Warioba na Salim, ikiwa ni pamoja na shinikizo la Mwalimu, ambaye alikuwepo!

Ni Mwalimu aliyehangaika usiku kucha kwenye guest house za wajumbe wa CCM ili wampitishe Mkapa, na ni mwalimu aliyekata deal na Salmin la kumpitisha Mkapa, kwa kuwashinikiza wajumbe wote wa Visiwani kumpigia Mkapa, baada ya Mkapa kushindwa na Kikwete mara mbili za kwanza, in return Salmini aliruhusiwa kuiba uchaguzi wa kule Visiwani, na ndio maana alijiamini sana kutaka term ya tatu na kumpitisha mtu wake Bilali, ni maadui wa mkapa ndio walimkata panga Salmin, ambaye aliamini kuwa mkapa hawezi kumzuia, na pia alimshawishi sana mkapa naye adai term ya tatu, kitu ambacho mkapa alijaribu kwenye kikao kimoja cha mawaziri lakini Sumaye na Mwandosya wakam-shut down, akasingizia kuwa ana simu ya Bush na kukimbia kikao, hakurudia tena, lakini akaja kuwalipa Sumaye na Mwandosya kwenye urais!

3.
Ndio maana Salim mpaka leo amesema hawezi kamwe kumsamehe Mkapa kwa vitendo alivyofanyia Dodoma siku ya uchaguzi wa kutafuta mgombea wa CCM.Hana kinyongo na JK kabisa.

Salim hakuwa malaika kwenye ule uchaguzi na yeye alihusika sana kujaribu kuwachafua wenziwe, lakini alizidiwa kete na Muungwana, Mkapa alikuwa hamtaki period kwa sababu ya uarabu wake na kulikuwa na wajumbe wengi sana ndani ya CCm waliokuwa na hiyo thinking, ndio maana mkapa alikuwa amemuonya Ndejembi mapema kuwa aache kumpigia debe Salim, alisema "..mwarabu hawezi kutawala nchi hiii..."

Yes, Salim anamchukia sana Mkapa kuliko anything, lakini pia ana the same chuki na muungwana, the matter of fact kama sio JM kumtuliza, Salim alitaka kufanya mambo mengi ya ajabu baada ya kujifungia wiki nzima ndani analia, yeye na mkewe, aliamua kususia CCM ikiwa ni pamoja na kujitoa kila nafasi aliyokuwa nayo, na aliapa kuwa hatazungumza nao tena na kutojihusisha tena na siasa za bongo, lakini ni JM ndiye aliyewa-calm down yeye na Sumaye, ambao hawakuamini what Mkapa did to them,

Mkapa na Mugandas, wana uhusiano wa siku nyingi unaotokana na Mkapa kujikomba sana zamani kwa Butiku na Mwalimu, na pia watoto wa mkapa wametunzwa na kusomeshwa maisha yao yote na mke wa zamani wa Butiku kule NY infact yule mama ni mzazi zaidi kwa watoto wa mkapa kuliko hata mkapa na mkewe, lakini mkapa alipopata urais tu akamtelekeza yule mama, lakini ni mama Anna tu ambaye amekuwa akimkumbuka mara kwa mara,

Butiku alikuwa na tabia moja nzuri sana akiwa kwenye power, nayo ni kusaidia watu wengi mahali pa kukaa, nyumba yake siku zote ilikuwa imejaa watu, mmoja wapo alikuwa Museveni, maisha yake yote Dar, mpaka akiwa anasoma Mlimani, alikuwa akikaa kwa Butiku na hata kusaidiwa hela na mahitaji yake yote na Butiku, Museveni ndiye peke yake anayemhifadhi sasa hivi ama sivyo Butiku, angeshakuwa kichekesho mjini!

Otherwsie Mkulu Zanaki, dataz zako bado ni nzito!
 
Nisife moyo eeeeenh? Kwa hiyo ni poa Mwafrika wa Kike? Mradi usiwe Mwafrika wa Kiume tu, kama yule mfukuzwa alivyo dai. Maana jamaa alikuwa mkimjibu tofauti tofauti yeye anawajumlisha wote kama mtu mmoja. Halafu ana mi confidence ile mbaya. Anadai mmekutana wapi, Russia? Yani sina mbavu!

Unaweza tu ukabadili jina ukajiita moja ya majina yake na kisha ukaanza paranoia rants kama yeye. Kumbuka tu kama kawaida yangu nitakuwa hapa kukukamua vizuri na kukuanika mbele ya hadhara ya waheshimiwa wa JF!

Fair enough?
 
Si Kweli Kuwa Mkapa Alitaka 3rd Term Mkuu Wa Medani,hapo Umeleta Jipya Ktk Agenda Unayoifahamu Wewe Mwenyewe. Tumuulize Jenerali Ngwilizi Au Mark Mwenyewe Utaufahamu Ukweli Mkuu. Mkapa Alimtuma Dr.omary Kumpiga Chini Salmini 2000 Akiwa Mwanza Alipothubutu Kuwaonya Wakuu Waondoke Madarakani Bado Wakiwa Wana Nuru Wasisubiri Kupigwa Mawe, Mwinyi Akaenda Zenj Kumalizia Kazi Ambayo Ben Alimpa Dkt.omary,unakumbuka Askari Wa Miavuli? Nakukumbusha Tena Akiwa Ikulu Bustanini Baada Ya Kuapishwa 2000 Aliulizwa Na Mwandishi Yule Tvt Je Anafikiria Kujiongezea Muda Madarakani Baada Ya 2005,na Alilijibu Hilo Kwa Uso Mkakamavu Kamwe Haitotokea Kwangu,nitajikita Na Uandishi Na Mambo Ya Nje Ya Nchi Hii,sasa Haya Aliyatamka Kabla Hajateua Waziri Mkuu Wala Baraza Jipya Lake Alilobatiza Siku Hiyohiyo Jina Askari Wa Miavuli. Nahofia Kuhoji Sana Ktk Hili Ila Ni Vema Mkuu Na Sisi Tutambue Kuwa Mark Hakuwa Waziri Kabla Ya Mahojiano Ya Mkapa Na Tvt Yaliyozaa Askari Wa Miavuli,frederick Hakuwa Na Uhakika Na U-pm Wake Na Ninyi Ndio Mliotabiri Kuwa Mark Ndiye.
Aliyemtaka Mkapa Aendelee Kuwa Rais Baada Ya 2005 Anapatikana Ktk Hansard Za Bunge La Mzee Wa Ukerewe,rejea Kumbukumbu Hizo Na Si Vinginevyo. Baraza Limenoga Kwa Soga
 
Back
Top Bottom