Mkapa above the law?: Allegations

FMES, heshima mbele.

Nimetaabishwa kidogo madongo uliyo mtupia Butiku hapa. Nilitegemea busara yako iliyotuongoza kwenye mjadala mwingine unao husiana na kuwakejeli viongozo wanao dhaniwa 'wamechoka.'

Nisaidie kuoanisha mawazo yako hapa:
...Butiku alikuwa na tabia moja nzuri sana akiwa kwenye power, nayo ni kusaidia watu wengi mahali pa kukaa, nyumba yake siku zote ilikuwa imejaa watu, mmoja wapo alikuwa Museveni, maisha yake yote Dar, mpaka akiwa anasoma Mlimani, alikuwa akikaa kwa Butiku na hata kusaidiwa hela na mahitaji yake yote na Butiku, Museveni ndiye peke yake anayemhifadhi sasa hivi ama sivyo Butiku, angeshakuwa kichekesho mjini...

Na uongozi ulio uonyesha hapa:

Huenda kwa sasa [Luhigo, Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa THA] physically amechoka kwa umri, sasa subiri huko mbele ya haki ndio utaelewa nani kati ya mkapa na huyu Luhigo atakayekuwa amechoka kwenye kila kiungo cha mwili, maana huko mkapa atapewa mihela yenye moto aibebe kichwani yeye si greedy na mingine aitafune huku ikiwa inawaka moto!

Bravo Mzee Luhigo, wazee hebu mtafuteni mawasiliano yake tuweze kujua anvyoendelea na ikiwezekana kumsaidia kwa chochote maana viongozi kama yeye ni adimu sana Tanzania!

Halafu, ukimaliza kunisaidia kuoanisha hayo mawazo, baadae tutajadili ukweli wa hili:
Nyerere... siku zote alikuwa akimdharau sana Butiku, kiasi kwamba asingeweza kumsikilza...

Kwa wanafunzi wa Nyerere, details za closest deputy wa Rais tumezifuatilia. Na sio rahisi 'kumiliki' facts kuhusu mtu kama Butiku. Kwa mfano, maisha pale kwa Butiku sio kweli kama picha uliyo ileta. Nyumba ya Butiku haiku jaa watu zaidi ya familia ya kawaida ya Kitanzania ambapo tuna familia kubwa zaidi ya Baba na Mama na watoto. Tena kwa kipindi kirefu kwa Butiku kulikuwa empty kwa sababu mji ulikuwa hauja kamilika. Mke wake na mtoto walitimua. Mke mwingine nae baadae wakatimuana kabla familia haijawa kubwa. Mara nyingi pale palikuwa empty. OK?

Kwa hiyo, tutakapo kuja kujadili hili la Nyerere kumdharau Butiku kumbuka humiliki hizi facts peke yako. Na kwamba japo mambo binafsi yanayo zunguka maisha ya Rais hakuna anae yajali Bongo kwa sababu aidha Wanahistoria wapo kama hawapo, au kwa sababu 'mwanamme mzima huwezi kuuliza mwanamme mwenzako Kikwete ana watoto wangapi' na 'kujua nani mke wa Kawawa hakuleti maji Kigoma' bado tupo wanafunzi wa Historia tunao fuatilia maisha ya hawa viongozi wetu.

Hata hivyo, nakushukuru kwa kujali hizi details. Hatuwezi kukaa tunashutumu Mkapa fisadi wakati hatutaki kujua anafanya nini na anaishi vipi nje ya ofisi. Madili ya kifisadi mara nyingi yanapikwa taa zikizimwa. Mchana wanatoa spichi kupinga wanayo yafanya kwenye kona usiku. Ni muhimu kujua hawa ma Rais wanaamkia wapi na wana lala kwa nani. Tupo tunao fuatilia haya.
 
BMW hakuonesha kuwa na wapambe wengi hadharani, ama kweli ukistaajabu ya Mussa ... kumbe mkuu alikuwa na wapambe wachache lakini makini katika kufuja na kuhujumu mali za watanzania.

Mwanamapinduzi hata akifa, anadumu
 
Kwa wanafunzi wa Nyerere, details za closest deputy wa Rais tumezifuatilia. Na sio rahisi 'kumiliki' facts kuhusu mtu kama Butiku. Kwa mfano, maisha pale kwa Butiku sio kweli kama picha uliyo ileta. Nyumba ya Butiku haiku jaa watu zaidi ya familia ya kawaida ya Kitanzania ambapo tuna familia kubwa zaidi ya Baba na Mama na watoto. Tena kwa kipindi kirefu kwa Butiku kulikuwa empty kwa sababu mji ulikuwa hauja kamilika. Mke wake na mtoto walitimua. Mke mwingine nae baadae wakatimuana kabla familia haijawa kubwa. Mara nyingi pale palikuwa empty. OK?

1.
Kwa hiyo, tutakapo kuja kujadili hili la Nyerere kumdharau Butiku kumbuka humiliki hizi facts peke yako.

Mkuu mbona kila kukicha una mambo mapya ya kutafuta confrontation na watu hapa bila sababu, hakuna anyemiliki any facts hapa ila ukweli hujisema wenyewe, wewe ni kusema tu ukweli wa ishu na wananchi hapa JF wana akili sana ya kujua ukweli na uongo ulipo, haya maneno ya kumiliki facts unayatoa wapi? Hivi kuna mahali kwenye post yangu nimesema ninamiliki fatcs are you out of your mind bro?

Na kwamba japo mambo binafsi yanayo zunguka maisha ya Rais hakuna anae yajali Bongo kwa sababu aidha Wanahistoria wapo kama hawapo, au kwa sababu 'mwanamme mzima huwezi kuuliza mwanamme mwenzako Kikwete ana watoto wangapi' na 'kujua nani mke wa Kawawa hakuleti maji Kigoma' bado tupo wanafunzi wa Historia tunao fuatilia maisha ya hawa viongozi wetu.

There you go na matatizo yako, ni wapi nimeuliza habari za watoto wa Kikwete? Man are you okay au?

Kwa wanafunzi wa Nyerere, details za closest deputy wa Rais tumezifuatilia. Na sio rahisi 'kumiliki' facts kuhusu mtu kama Butiku. Kwa mfano, maisha pale kwa Butiku sio kweli kama picha uliyo ileta. Nyumba ya Butiku haiku jaa watu zaidi ya familia ya kawaida ya Kitanzania ambapo tuna familia kubwa zaidi ya Baba na Mama na watoto.


Butiku alikuwa na mke wa kwanza aliyezaa naye mtoto mmoja wa kike, lakini pia alikuwa na watoto wawili wa ku-adopt mmoja wa kike na kiume ambao baadaye wote waliwapelekea US kwa mke wa kwanza, nyumbani kwa Butiku kulikuwa alyways na watu aliokuwa akiwasiadia, Museveni akiwa mmojawapo wakati akisoma Mlimani, pia kulikuwa na mtu mwingine ambaye baadaye alikuja kuwa one of the big kwenye uwt, ambaye alikuwa ndio kwanza amemaliza Mlimani, familia nzima ya Mwalimu kutoka Butiama, walikuwa wakifikia kwa nani mkuu wanapokuja Dar? Ilikuwa ni kwa Butiku, mpaka baadaye Madaraka alipohamia kwake ndio walipoanza kugawanyika betweeen Steve Wanzangi na Madaraka, lakini siku zote walikuwa wakiishi kwa Butiku, kwa sababu Msasani kulikuwa kumejaa bro watu bro! na ndio hasa siku zote ilyokuwa kazi ya Butiku na mpaka leo, Butiku ndiye anyehusika na all family ishus za Nyerere, mkuu similiki any facts lakini hawa ni watu nimeishi nao mjini maisha yangu yote labda useme mengine!

Tena kwa kipindi kirefu kwa Butiku kulikuwa empty kwa sababu mji ulikuwa hauja kamilika. Mke wake na mtoto walitimua. Mke mwingine nae baadae wakatimuana kabla familia haijawa kubwa. Mara nyingi pale palikuwa empty. OK?

Baada ya ku-separate na mke wa kwanza Butiku, alikuwa akiishi na mama mwingine, lakini at the same time alikuwa akitembea pia na mama kate kamba, kwa hiyo nyumba yake haikuwahi kuwa empty kama unavyosema, lakini one thing ni kwamba baada ya Gladis na mama yake kuhamia US na wale watoto wawili, ndipo ikabidi sasa watu waanze kuutimua, kwa hiyo mkuu sio ishu ya kumiliki facts isipokuwa ni kuweka facts kama unazo, ila kwenye hili huna facts, lakini Zanaki anazo nilichofanya ni kuongezea kidogo na yeye mwenyewe amekubali,

Next time kabla huja-pick a fight hakikisha unajua unachokisema, kwenye siasa huwa tuna-pick a fight ambayo ni winnable na unaijua, maisha yangu nimekuwa na the Butikus na nyereres na pia the mugandas, nimeingia nyumba zoa in and out ni watu ninaowajua vizuri mpaka kule kwao musoma nimeingia sana Ku-Ng'ombe mpaka Butiama, kwenye hili huna facts bro ila una hadithi, sasa kaaa pembeni ule dataz!

Ahsante Mkuu!
 
1.
Si Kweli Kuwa Mkapa Alitaka 3rd Term Mkuu Wa Medani,hapo Umeleta Jipya Ktk Agenda Unayoifahamu Wewe Mwenyewe. Tumuulize Jenerali Ngwilizi Au Mark Mwenyewe Utaufahamu Ukweli Mkuu.

Mkuu wangu mtetezi wa Mkapa, karibu tena, hii ishu niliisema kwa mara ya kwanza mwaka 2005 kule BCS, kwa hiyo sio agenda mpya kama unavyosema, mkapa akishinikizwa na mkewe baada ya ule moto wa Ikulu, alijaribu ku-test upepo kwenye kikao cha cabinet, Sumaye na Mwandosya, wakam-shut down, akasingizia kuwa kuna simu kutoka kwa Bush, akakimbia kikao hakurudi tena na wala hakusema tena, na ndipo sasa uwizi wake mkubwa ulipokolea na akawalipa vizuri Sumaye na Mwandosya kwenye uchaguzi wa rais.


2.
Mkapa Alimtuma Dr.omary Kumpiga Chini Salmini 2000 Akiwa Mwanza Alipothubutu Kuwaonya Wakuu Waondoke Madarakani Bado Wakiwa Wana Nuru Wasisubiri Kupigwa Mawe, Mwinyi Akaenda Zenj Kumalizia Kazi Ambayo Ben Alimpa Dkt.omary,

Mkuu nenda katafute tena facts maana hizi umedanganywa, Salmini alitolewa knockout kwenye kikao cha kamati kuu, White house Dodoma, ujeuri owte wa Salmin alikuwa akitegemea mkapa ataamunga mkono kwa sababu ya deal aliyoifanya na Mwalimu, kumpitisha 1995 wajumbe wote wa cc walikuwa wanajua hilo ndio maana siku ya kikao walipomwita Salimin walimoumba mkapa atoke nje ya kikao, na ni Natepe aliyemuuliza Salmin kuwa anataka nini hasa? The final blow alikuja pewa na JM, na ndipo kwa mara ya kwanza alipoambiwa rasmi kuwa hata mtu wake Bilali hatapewa nafasi ya kugombea urais wa visiwani, ni kutokana na kiburi chake Salmin cha kutaka term ya tatu, na kutokuwa na nidhamu kwa rais, katika kipindi kizima cha urais wa Salmin na mkapa, Salmin hakuwahi kushudhuria hata kikao kimoja cha baraza la mawaziri la muungano, ikiwa ni kutomheshimu mkapa, Dr. Omary na Salimn were too close ni infact wote walikuwa hawamtaki kabisa Mwalimu na sera zake on Zanzibar kwa hiyo no way mkapa angeeweza kumtuma Omar kwa salmin, only one person could get ot Salmin naye ni JM, hivi karibuni Salmin alioa mke mpya mdogo hebu tafuta habari alimualika nani ktuoka serikali ya bara, JM peke yake!

3.
unakumbuka Askari Wa Miavuli? Nakukumbusha Tena Akiwa Ikulu Bustanini Baada Ya Kuapishwa 2000 Aliulizwa Na Mwandishi Yule Tvt Je Anafikiria Kujiongezea Muda Madarakani Baada Ya 2005,na Alilijibu Hilo Kwa Uso Mkakamavu Kamwe Haitotokea Kwangu,nitajikita Na Uandishi Na Mambo Ya Nje Ya Nchi Hii,sasa Haya Aliyatamka Kabla Hajateua Waziri Mkuu Wala Baraza Jipya Lake Alilobatiza Siku Hiyohiyo Jina Askari Wa Miavuli.

Neno la askari wa miavuli, alilisema wakati akifungua project ya maji kule Chalinze, ambayo ilikuwa imesiamiwa na Kikwete na Lowassa, wakiwa mawaziri wa maji na nje, kwa msaaada wa China, ndipo waandishi walipomuuliza swali la makusudi kuhusiana na tetesi then kuwa mawaziri hao wana mpango wa kugombea urais na yeye akawasifu kuwa they are doing a great job, na kwamba ni askari wake wa miavuli, na kesho yake ikawa a big deal kwenye magazeti kuwa amewafagilia urais hayo mengine ni yako siyajui kabisaa mkuu!

4.
Nahofia Kuhoji Sana Ktk Hili Ila Ni Vema Mkuu Na Sisi Tutambue Kuwa Mark Hakuwa Waziri Kabla Ya Mahojiano Ya Mkapa Na Tvt Yaliyozaa Askari Wa Miavuli,frederick Hakuwa Na Uhakika Na U-pm Wake Na Ninyi Ndio Mliotabiri Kuwa Mark Ndiye.
Aliyemtaka Mkapa Aendelee Kuwa Rais Baada Ya 2005 Anapatikana Ktk Hansard Za Bunge La Mzee Wa Ukerewe,rejea Kumbukumbu Hizo Na Si Vinginevyo. Baraza Limenoga Kwa Soga

Mkuu haya yote ni yako, Mwandosya na Sumaye wamekuwa mawaziri kipindi chote cha utawala wa mkapa, sasa sijui exactly unaongelea nini? Na hakuna wakati wowote uwaziri wao ulikuwa kwenye matatizo, ingawa kuna wakati kidogo muungwana awe waziri wa vijana, lakini muungwana akamsubiri mkapa kwenye kikao cha cc kule Zanzibar na kumtwanga kama mtoto, kwamba amehusika na kuwatumia usalama wa taifa kumuibia kura za ujumbe wa NEC,

Shinikizo la kutaka term ya tatu ilianzia kwa mkewe, baaada ya kuunguliwa na mali nyingi sana kwenye ule moto, according to the dataz mama alipoteza mali nyingi sana tena sana kwenye ule moto bro! Hayo ya Hansard sijawahi kuyasikia, lakini leo ukweiza kuingia BSC ya then utakuwa haya maneno yangu ya mwaka 2005, kama nilivyoyaandika hapa kile kipindi cha uchaguzi.

Ahsante Mkuu!
 
Mzee... Rostam anadai kuwa yeye ndiye aliyeongoza kundi la Wabunge kupinga Salmin kujiongezea muda wa kutawala...
 
Rostam hawezi fungua mdomo mbele ya Raza, ambaye ndiye aliyekuwa msari wa mbele kudai Salimn aendelee, halafu kumbuka kuwa then Rostam was no body, na hakuwa mjumbe wa CC kwa hiyo mkuu maneno yake kama ni kweli ni 100% uongo mtupu!
 
Nina mashaka makubwa sana kama taarifa hizi ni za kweli.

Kuna haja ya wana JF kuwa na utaratibu wa kufuatilia taarifa mbali mbali zinazoletwa humu ndani kabla ya kuanza kuzichangia.
 
Jamani Just To The Least, Huyu Mkapa Ni Mtu Mwenye Dharau Sana Kwa Watanzania, Kinachoshangaza Ni Kwamba Yeye Marafiki Zake Wana Akina Yona, Basil Mramba, Ruhunda, Waletr Bgoya Na Wengine Wengi Wanafikiri Kuwa They Own This Country. They Even Have Guts To This They Cannot Face The Mighty Arm Of Law. Wote Hawa Tunawajua Wamejinufaisha Sana Wakati Wa Huyu Mkapa Akiwa Ikulu.

Mimi Naomba Wana Jf Mlio Hapo Dar Es Salaam Mjaribu Kumfuatilia Huyu Bwana Walter Bgoya, Maana Tetesi Zinasema Presure Haziishi Kupanda Hadi Sasa Wana Private Doctor Anayewatibu Wakiwa Nyumbani Kwao.

Mkapa And His Friends Need To Remember That He Can Run But Not Hide, He Is Now Very Naked In The Eyes Of Tanzanians.
 
FMES;

...Unakosa context ya vitu ninavyo visema. Ninaposema humiliki facts nina maana kuna vitu unavisema kana kwamba ni siri unazozijua wewe mwenyewe na hivyo unazipinda unavyo taka. Unaposema Nyerere alikuwa anamdharau confidant wake usidhani kitu kama hicho kitapita bila kuwa challenged. Huyo aide ambae mwenyewe umesema sasa hivi ndio anaangalia familia ya Nyerere, halafu huyo huyo Nyerere awe anamdharau. Siwezi kuamini mpindo kama huo kwa sababu tu wewe unasema umefika Butiama, au umeingia na kutoka nyumba za Mugandas.

Sina ugomvi na wewe. Nime point out contradiction uliyo ionyesha kwa kumdharau Butiku kwamba angekuwa ana aibika mjini kama sio Museveni kumsaidia, wakati hapo hapo uli purport kuwakemea wanao dhihaki watu waadilifu kwamba wamechoka. Hiyo contradiction hujaieleza umeanza kuwakia vitu vingine.

You are not entitled to your own facts.
 
Ninaposema humiliki facts nina maana kuna vitu unavisema kana kwamba ni siri unazozijua wewe mwenyewe na hivyo unazipinda unavyo taka.

Mkuu Kuhani,

Ninakujibu hivi kazi moja kubwa na mhimu ya Butiku, ilikuwa ni kuangalia familia ya Nyerere, kwa sababu Butiku hakuwa msadizi tu bali alikuwa ni ndugu wa Mwalimu, sikumbuki wakati wowote wa utawala wa Mwalimu, Butiku aliwahi kusikika kwenye policy making, au kama mshauri wa rais, yaani Mwalimu, najua for a fact kuwa matatizo yote yanayohusu familia ya Nyerere yalikuwa yanasimamiwa na Butiku, sasa naomba useme kuwa huu ni uongo halafu uweke ukweli?

Lakini I know for sure kuwa Butiku, alihusika sana na kuwa-promote baadhi ya viongozi kwa Mwalimu, na mkapa ni mmojawapo, lakini kumshauri utawala hata siku moja sijawahi kusikia, labda wewe unafahamu sasa unachotakiwa ni kuweka hizo facts bila kujaribu kutafuta confrontation, kwa sababu kama una ukweli huna sababu ya kutafuta ugomvi ni kuweka ukweli tu, sasa kubali kuwa huna ukweli lakini kunitafuta mimi hunipati maana huna facts,

Nimekuambia hivi Museveni, ameishi kwa Butiku na ndiye anyemsaidia sana sasa hivi financially, ndio maana hata wakati mmoja Butiku aliamua kupeleka sherehe za kum-celebrate Mwalimu, kwenye bunge la Uganda, na alifanya hivyo ili kumtishia nyau mkapa, lakini mkapa akamkatia msaada wa hela kule foundation, sasa kama wewe una ukweli tofauti uweke hapa bro, tusiandikie mate!

2.
wakati hapo hapo uli purport kuwakemea wanao dhihaki watu waadilifu kwamba wamechoka. Hiyo contradiction hujaieleza umeanza kuwakia vitu vingine.

Again hii point haihusinai kabisa na the ishu at hand, lakini nitaijibu anyways, nimesema yoyote anayemcheka Luhigo kwa kuchoka kimaisha ambaye wengi hapa tunaamini alikuwa kiongozi safi haelewi siri ya maisha, kwa sababu mkapa ambaye sasa hajachoka, hana thamani mbele ya mungu kama Luhigo, ambaye alikataa wizi hapa duniani na amechoka lakini sio mbele ya mungu, sasa what is your problem na hii kauli? Exactly usichoelewa ni nini mkuu mpaka unataka kuanzisha mabishano yasiyokuwa na kichwa wala miguu?

Kuchoka kwa Butiku ni sawa kwa sababu hakuwa msafi, huko Nyerere Foundation amefanya mangapi ya faulo na hela? Akiwa Ikulu amefanya mengi sana ya ufisadi na kwenye hilo sijawahi kuficha sasa huyu akichoka na maisha kwangu sio tatizo kwa sababu sio muaminifu kama Luhigo, now usichoelewa hapa ni nini?

Mkuu JF, unaweza kuji-establish kwa facts, naona unahangaika sana kuonekana kuwa bingwa which is okay lakini tafuta facts kwenye ishus, kurukia watu hapa kama mimi hakutakusaidia kitu zaidi tu kuwavuta those wenye akili finyu kama zako, naona umejaribu sana na Mwafrika Wa Kike yamekushinda, sasa unahangaika hoja huna wala facts huna, angalau hata dataz huna, wewe unalilia logic tu, mkuu logic ina ishu zake hii sio mojawapo, hakuna anaye-own facts hapa ila watu hutoa facts au hoja, ili kupingana na facts na hoja, lakini sio kama wewe maneno tu na ugomvi lakini hoja hakuna, tumewaona wengi hapa kama wewe bro, lakini walishia kubadili majina kama sio kukimbia, sasa in the future jaribu kutafuta hoja na facts otherwise utachekesha hapa!

Ahsante Mkuu!
 
FMES;
Kwanza nashukuru hatimaye kunifahamisha “hakuna anaye-own facts hapa.” Unaporudia kitu kwa mtu aliye kutamkia hicho kitu maana yake umeanza kukielewa. Naona tunaanza kusogea mbele taratibu. We’ll get around the innuendos, the few-letter words and all the jazz. We’ll get there!

Facts ambazo nasema huzimiliki, kwa hiyo huwezi kuzipinda ni kama hizi:

"Kuchoka kwa Butiku ni sawa kwa sababu hakuwa msafi, huko Nyerere Foundation amefanya mangapi ya faulo na hela? Akiwa Ikulu amefanya mengi sana ya ufisadi na kwenye hilo sijawahi kuficha."


Hilo wewe hujawahi kuficha? Ha ha ha haaaa. You didn’t get it all, did you? Unaongea kana kwamba uko entitled to these bent facts. Wewe una uhakika gani na hilo? Una access gani ya hizo data ambazo wengine hawana? Yani nacheka ile mbaya.

Kuhusu mimi kuchekesha hapa JF najivunia uhuru unaoniwezesha kuto taka kukumbatiwa wala kukumbatia lolote bila kulipima mwenyewe. Nataka uhuru wa fikra, kwa sababu nimeapa mbele ya madhabahu ya Mwenye Enzi Mungu kupigana na kila aina ya unduli dhidi ya mawazo ya Bin Adam. Kwa hiyo, unapo niita nina mawazo finyu, hilo kwangu mara nyingi ni dhihirisho, ni vindication, ya kwamba niko njia sahihi, kwamba kuna uchache wa mawazo kama yangu kwa hiyo labda ni mawazo asili. Ki ufupi ndio hiyo falsafa inayonifanya niswalishe lolote, la yeyote, ninalo liona limepinda. Wewe hujazoea kupingwa, inaonekana, na unadhani nakutafuta.

Hilo la deputy wa Nyerere kufanya ufisadi Ikulu nalikataa kata kata bila wewe ku substantiate. Na kithibitisho ambacho naki foreclose kabla hujahangaika kukileta ni kwamba wewe unajua kwa sababu wewe ni FMES, na umefika Butiama na ukaingia na kutoka kwa the Mugandas toka siku za utoto wao.

La mwisho, nimesema si vibaya, na una unayo haki - tena labda wajibu – wa kuni characterize unavyotaka, lakini kumbuka ukisema ‘kuwavuta those wenye akili finyu kama zako’ unatukana wasio husika. Sio vizuri kutukana watu ki jumla jumla hivyo. Ahsante.
 
FMES;
Kwanza nashukuru hatimaye kunifahamisha “hakuna anaye-own facts hapa.” Unaporudia kitu kwa mtu aliye kutamkia hicho kitu maana yake umeanza kukielewa. Naona tunaanza kusogea mbele taratibu. We’ll get around the innuendos, the few-letter words and all the jazz. We’ll get there! Facts ambazo nasema huzimiliki, kwa hiyo huwezi kuzipinda ni kama hizi: "Kuchoka kwa Butiku ni sawa kwa sababu hakuwa msafi, huko Nyerere Foundation amefanya mangapi ya faulo na hela? Akiwa Ikulu amefanya mengi sana ya ufisadi na kwenye hilo sijawahi kuficha." Hilo wewe hujawahi kuficha? Ha ha ha haaaa. You didn’t get it all, did you? Unaongea kana kwamba uko entitled to these bent facts. Wewe una uhakika gani na hilo? Una access gani ya hizo data ambazo wengine hawana? Yani nacheka ile mbaya.

Mkuu ninakuomba ukatafute thread inayosema Butiku, na kupinga Lowassa kutopewa nafasi ya kujitetea kabla ya kujiuzulu nimeyasema yote, tena kwa kubishana na mkulu Kalamu, besides habari za Butiku kumuandikia barua Mkapa, baada ya uchaguzi wa Dodoma, nilikuwa mtu wa kwanza kuzileta BCS, na hata barua nilikuwa nayo lakini upepo haukuwa sawa ndio maana sikuiweka, upepo ulipokaa sawa nilimpa mtu hapa akaiweka, nafikiri hili linaweza kujibu maswali yako yote ya facts na access, kama wewe huna kama unavyoonekana sio wote hapa hatuna, unajua hata mimi unanichekesha sana unapojaribu kujibu dataz ambazo huna kwa kutumia logic, ambazo nazo pia hata huelewi mahali pake zinapotakiwa kuwa applied, mimi ninakuona ni kichekesho kwa sababu ukweli ni kwamba huna facts za nay ishu kama nilivyokushauri dawa ni wewe kukaa pembeni na subiri uletewe dataz!
Kuhusu mimi kuchekesha hapa JF najivunia uhuru unaoniwezesha kuto taka kukumbatiwa wala kukumbatia lolote bila kulipima mwenyewe. Nataka uhuru wa fikra, kwa sababu nimeapa mbele ya madhabahu ya Mwenye Enzi Mungu kupigana na kila aina ya unduli dhidi ya mawazo ya Bin Adam. Kwa hiyo, unapo niita nina mawazo finyu, hilo kwangu mara nyingi ni dhihirisho, ni vindication, ya kwamba niko njia sahihi, kwamba kuna uchache wa mawazo kama yangu kwa hiyo labda ni mawazo asili. Ki ufupi ndio hiyo falsafa inayonifanya niswalishe lolote, la yeyote, ninalo liona limepinda. Wewe hujazoea kupingwa, inaonekana, na unadhani nakutafuta.

Tatizo lako ni kwamba huelewi kuwa kila mtu hapa JF anao huo uhuru, lakini sio kila mmoja ana dataz na facts, ingawa kila mtu hapa anazo logic na maswali ya kitoto kama yako na kujiita una akili sana hilo hakuna anayekuzuia, ila one thing huwezi tisha mtu hapa wala bila ya kuwa na facts za ishu, mimi nimezitoa facts kama unazo tofauti ziweke hapa wananchi hapa sio wajinga, hapa sio CUF huko ambako mnamsikiliza Seif tu, No hapa unachambuliwa na ujinga wako unawekwa hadharani, si uanona kwenye hii ishu jinsi unavyoanikwa waziii kuwa wewe ni mtupu wa akili!

Hilo la deputy wa Nyerere kufanya ufisadi Ikulu nalikataa kata kata bila wewe ku substantiate. Na kithibitisho ambacho naki foreclose kabla hujahangaika kukileta ni kwamba wewe unajua kwa sababu wewe ni FMES, na umefika Butiama na ukaingia na kutoka kwa the Mugandas toka siku za utoto wao.

Unajua ninarudia kuwa akili zako ni finyu sana, toka BCS niemsema mara nyingi sana jinsi Butiku,alivyoshirki sana kwenye kuifilisi Gapex, kwa kumtumia rafiki yake Kyoma, na nikasema hata jinsi muandishi mmoja wa habari ambaye alikuwa akiandika sana kuhusu ukweli wa Butiku na Gapex, jinsi Butiku alivyomahimishia ubalozi wetu London, sasa wewe hukuwepo kwenye hizi forum, na sina mpango wa kurudia habari hizo kial wakati maana kuna mengi sana sasa ya mafisadi, yes mimi ni Field Marshall Super Emergency System, ninaweka ishu facts pamoja na dataz tena very clear, zako ziko wapi mkuu?

Hebu tueleze ni kwa nini Warioba alishindwa kule Nyerere Foundation, kama sio Butiku kutotaka kuingiliwa kwenye ulaji? Acha filimbi mkuu kama huna hoja!

La mwisho, nimesema si vibaya, na una unayo haki - tena labda wajibu – wa kuni characterize unavyotaka, lakini kumbuka ukisema ‘kuwavuta those wenye akili finyu kama zako’ unatukana wasio husika. Sio vizuri kutukana watu ki jumla jumla hivyo. Ahsante.

Hapa unajaribu kulia wolf! wolf! ili usaidiwe na wengine, nafikiri unazo akili timamu za kujua kuwa kama kawaida yako uko on your own, maana watu hapa hawapendi maneno mengi bila dataz wala facts, au logic zisizokuwa na miguu wala kichwa, ninasema hivi uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana na unaonyehswa wazi na hizi pumba unazozirusha kila kona, kila mahali unarukia rukia watu hapa, ukweli wala hoja huna, ndio maana ninasema kuwa uwezo wako wa kufikiri ni finyu sana, na you can only attract wale walio sawa na wewe,

Mkuu huna hoja, ni vyema uka kaaa pembeni!
 
Nina mashaka makubwa sana kama taarifa hizi ni za kweli.

Kuna haja ya wana JF kuwa na utaratibu wa kufuatilia taarifa mbali mbali zinazoletwa humu ndani kabla ya kuanza kuzichangia.

....where in particular?..........otherwise tumekusikia Mkuu
 
Nina mashaka makubwa sana kama taarifa hizi ni za kweli.

Kama unaweza kuweka habari za uongo Jf hebu jaribu mkuu uone yatakayo kukuta, wewe kutokuwa na habari fulani haina maana kuwa hazipo, ila wewe tu huna, halafu kuna one thing huelewi vizuri ni kwamba ndani ya hii forum kuna ndugu wa kweli wa Butiku, pamoja na Mwalimu mwenyewe, na wametulia kimyaa na wanasoma kila kitu, Zanaki angebisha hizi dataz ningeeelewa maana yeye ndie hasa wa huko ndani,

Sisi tunaposema habari fulani sio kweli au ina mashaka, huwa tunahakikisha kuwa tunauweka ukweli tulionao wa ile habari na kuwaachia wananchi waamue, ila huwa hatukurupuki hata siku moja, maana we have been here for a very long long time, tunajua nini faida ya kuandika uongo hapa JF, na hasa kuandika bila ukweli wala hoja, utaishia kuwa kichekesho na kushuka hadhi!

Otherwise, tunaendelea kumkoma nyani giladi hapa mpaka kieleweke!
 
...ndani ya hii forum kuna ndugu wa kweli wa Butiku, pamoja na Mwalimu mwenyewe, na wametulia kimyaa na wanasoma kila kitu, Zanaki angebisha hizi dataz ningeeelewa maana yeye ndie hasa wa huko ndani,

FMES,

Swali dogo tu nahakika utalielewa.

Data zako ni kweli au ziko subject to vouching ya huyo insider Zanaki?
 
Mkuu maswali yako yote nimeyajibu, vipi mbona unashindwa kujibu yangu? Nafikiri unapenda ujiko tu wa kuendeleza hii topic,

For once vipi ukijibu maswali yangu niliyokuuliza, maana yako yote nimeyajibu, haya ya Zanaki sio ya kumiliki facts kama ulivyoanza, ila unaweza kumiliki facts kama anaye-kuchallenge anakuwa kama wewe hana facts on the ishu,

Now Zanaki has nothing to do with this bro! Tizama toka ulikoanzia mapka sasa ulipofikia mkuu, hivi huoni aibu?
 
... Zanaki angebisha hizi dataz ningeeelewa maana yeye ndie hasa wa huko ndani,
FMES,

Swali dogo tu nahakika utalielewa.

Data zako ni kweli au ziko subject to vouching ya huyo insider Zanaki?
 
Mkuu acha upuuzi na kupoteza nafasi hapa, jibu maswali yangu nimetoa dataz sasa zako ziko wapi? Tizama ulikoanzia na ulipofika sasa hivi huoni aibu mtu mzima? Hili swali lako halihusiani na topic mkuu, sasa ni wakati wa wewe kujibu maswali yangu vipi ukiyajibu?

Hii tu ndio dawa yenu watu wa kuja, sasa nenda kule basement mkaanze tena na mambo ya CUF, huku mchana kweupee hukuwezi mkuu! Hapa huwa hatudanganyani kama huko basement, halafu mkija nje kazi kujikomba kwa viongozi wa CCM, usiku mnakuwa CUF huko mabesement,

hapa hatufanyi hayo mkuu, ni fimbo kwa fimbo, yaani facts na dataz huna kaaa pembeni! Utabadili majina hapa mpaka uchoke sisi huwa tunakwenda na jina moja tu, fimbo tu!
 
Quote: Kuhani Mkuu
Hilo la deputy wa Nyerere kufanya ufisadi Ikulu nalikataa kata kata bila wewe ku substantiate. Na kithibitisho ambacho naki foreclose kabla hujahangaika kukileta ni kwamba wewe unajua kwa sababu wewe ni FMES, na umefika Butiama na ukaingia na kutoka kwa the Mugandas toka siku za utoto wao.

Mkuu Kuhani, hili ndilo swali lako la msingi, na majbu nimekupa hapa chini:-

Quote:- FMES

Unajua ninarudia kuwa akili zako ni finyu sana, toka BCS niemsema mara nyingi sana jinsi Butiku,alivyoshirki sana kwenye kuifilisi Gapex, kwa kumtumia rafiki yake Nyakyoma, na nikasema hata jinsi muandishi mmoja wa habari ambaye alikuwa akiandika sana kuhusu ukweli wa Butiku na Gapex, jinsi Butiku alivyomahimishia ubalozi wetu London, sasa wewe hukuwepo kwenye hizi forum, na sina mpango wa kurudia habari hizo kial wakati maana kuna mengi sana sasa ya mafisadi, yes mimi ni Field Marshall Super Emergency System, ninaweka ishu facts pamoja na dataz tena very clear, zako ziko wapi mkuu?

Hebu tueleze ni kwa nini Warioba alishindwa kule Nyerere Foundation, kama sio Butiku kutotaka kuingiliwa kwenye ulaji? Acha filimbi mkuu kama huna hoja!

Sasa nilitegemea utakuja na majibu, ili niongeze fimbo, badala yake umerukia Zanaki na nonesense, vipi ukitoa hoja au facts hapa au ukakubali kuwa huna ulikuwa unataka kutishia nyau tu?

Unajua unasumbua sana watu hapa bila ukweli wala hoja, this time ninataka ujifunze adabu, uache filimbi bro!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom