Mkapa above the law?: Allegations

Mkuu acha upuuzi na kupoteza nafasi hapa, jibu maswali yangu nimetoa dataz sasa zako ziko wapi? Tizama ulikoanzia na ulipofika sasa hivi huoni aibu mtu mzima? Hili swali lako halihusiani na topic mkuu, sasa ni wakati wa wewe kujibu maswali yangu vipi ukiyajibu?

Hii tu ndio dawa yenu watu wa kuja, sasa nenda kule basement mkaanze tena na mambo ya CUF, huku mchana kweupee hukuwezi mkuu! Hapa huwa hatudanganyani kama huko basement, halafu mkija nje kazi kujikomba kwa viongozi wa CCM, usiku mnakuwa CUF huko mabesement,

hapa hatufanyi hayo mkuu, ni fimbo kwa fimbo, yaani facts na dataz huna kaaa pembeni! Utabadili majina hapa mpaka uchoke sisi huwa tunakwenda na jina moja tu, fimbo tu!

mpe dawa huyo...
 
Mkapa alipe kodi

2008-05-04 10:46:21
Na Simon Mhinda, Cynthia Mwilolezi, PST, Arusha

Mbunge wa Jimbo la Karatu, (CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa, amesema Rais wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, anatakiwa kulipa kodi ya pango kwa serikali kwa sababu aliitumia Ikulu kama ofisi yake ya kufanyia biashara.

``Nasema hivi sababu nina ushahidi, na siropoki tu kwa sababu za kisiasa, hivyo Mkapa anatakiwa kulipa pango la ofisi ya serikali, kutokana na kufanya Ikulu kama ofisi yake ya biashara`` alisema Dk. Slaa.

Aliyasema hayo jana wakati akitoa mada kuhusu nafasi ya mbunge, wananchi na ushirikiano kitutendaji, kwenye mdahalo wa Ulingo wa Maendeleo Mkoani Arusha, ulioandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la ANGONETI lililoko Mkoani hapa.

Alisema kuwa Mkapa aliandika barua akiwa madarakani kuomba fedha kwa anuani ya Ikulu kama mjasiliamali na sio Rais.

Dk. Slaa alisema kuwa hali hiyo ni hatari kwa uchumi wa nchi, kwani viongozi wa wanafanya kazi kwa manufaa binafsi.

``Halafu wanatudanganya wananchi kuwa nchi ya Tanzania maskini, si kweli, kama maskini wawekezaji wasingekuja kuwekeza... hiki ni kiini macho ili wananchi wasiwe na ufahamu`` alisisitiza Dk. Slaa.

Aidha, aliwataka wananchi kuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, ili kuepuka kuchagua Marais wajasiliamali ambao watatumia madaraka yao kujinufaisha.

Aidha, alizitaka taasisi na mashirika ya watu binafsi kuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuhoji maendeleo yao, bila kuogopa mtu yoyote kwani kwa kufanya hivyo itasaidia nchi kuondokana na ufisadi.

Pia alisema wananchi wengi hawajui wajibu wa wabunge wao na wengine huishia kuwaomba fedha za matumizi.

Dk.Slaa pia alisema uchumi wa nchi sasa upo kwenye mifuko iliyotoboka kwani viongozi wachache wamekuwa watumia vibaya madaraka na kujilimbikizia mali isivyo halali.

``Ili tuondokane na tatizo hili tushirikiane kuwafichua mafisadi kwa kutafuta nyaraka muhimu ili tukiwaeleza watu isiwe majungu`` alisema Dk. Slaa.

Naye Ofisa Mifugo Mkoa wa Arusha, Bw.Hargeney Chitukulo akisoma hotuba ya ufunguzi mdahalo huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Arusha, Bw. Isidore Shirima alisema kinachosababisha maendeleo ya nchi kurudi nyuma ni pamoja na kutegemea zaidi wafadhili.

Wakati huo huo, Mwandishi Simon Mhina anaripoti kwamba Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salamaa Mhashamu Methodius Kilaini, amemtaka Rais Benjamin Mkapa, na mkewe Anna kujibu tuhuma za ufisadi bila kusita kwa vile Watanzania wengi wana shauku ya kusikia neo kutoka kwao.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, kiongozi huyo alisema ni kweli usiopingika kwamba Rais mstaafu hawezi kujibu kila tuhuma inayotolewa barabarani au kwenye mikutano ya hadhara, lakini akasema kwa vile tuhuma hizo zimetolewa kwenye chombo muhimu kama Bunge haitakuwa vyema iwapo Bw. Mkapa atakaa kimya bila kutoa maelezo.

Askofu Kilaini alisema huenda taarifa iliyotangazwa na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda kuwa Serikali inachunguza tuhuma hizo, ndizo zimemfanya Bw. Mkapa kukaa kimya hadi sasa.

Hata hivyo, alisema Watanzania wana shauku ya kusikia neno kutoka kwake.

``Nimesikia kwamba Waziri Mkuu amesema tuhuma hizo zitashughulikiwa, itakuwa jambo la busara mno iwapo atatumia fursa hiyo kutoa maelezo yake kwa nia ya kujisafisha,`` alisema.

Askofu Kilaini alisema kwa vile hizo ni tuhuma zinaweza kuwa za kweli au uongo, hivyo ni vema zikatolewa ufafanuzi, ili Watanzania waweze kuchuja pumba na mchele.

Alionya kuwa tuhuma hata kama ni za uongo zisipokanushwa katika utaratibu unaotakiwa, zinaweza kuhesabika kuwa ni za kweli.

Askofu Kilaini amewamwagia sifa wabunge wa CCM kwa kuanza kujadili hoja za kitaifa, bila kujali maslahi ya kisiasa kama ilivyozoeleka.

``Kwa kweli sasa siasa ni tamu, kitendo cha Mbunge wa CCM kumshutumu waziwazi Mwenyekiti wa zamani wa Chama chake, tena aliyekuwa Rais kinaashiria kuwa sasa Bunge halitaki mchezo,`` alisema na kuongeza ``Hivi ndivyo inavyotakiwa iwe.

Wabunge wawe huru kujadili mambo ya kitaifa, bila kufungwa kamba na mizengwe ya vyama vyao,��
Katika Kikao cha Bunge kilichopita, Mbunge wa Vunjo (CCM) Bw. Aloyce Kimaro, alimshutumu Bw. Mkapa na mkewe pamoja na Bw. Yona kwa kujiuzia kwa bei ya kutupa mgodi wa Kiwira.

Mgodi huo unakadiriwa kuwa na thamani ya Sh. bilioni nne lakini Bw. Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Daniel Yona, walijiuzia kwa Sh. milioni 70.

Askofu Kilaini alisema Kanisa linapenda watu wanaosema ukweli na daima tabia hiyo ikiendelezwa taifa litasimamama mahali pazuri.

Alisema utamaduni huo mpya ulioanzishwa na wabunge wa CCM, utakiletea heshima kubwa chama chao.

Alisema Watanzania walishaanza kukata tamaa, kwamba wabunge wa CCM wanakwamisha mambo mengi yenye maslahi kwa Taifa kwa sababu za kiitikadi, lakini sasa wamejivua aibu hiyo.

Aliwataka wabunge hao kuendelea kujikakamua kwa vile mwenendo mpya waliouonyesha katika kujadili mambo mbalimbali utawanufaisha Watanzania na CCM pia.

Kiongozi huyo alisema ukiachilia mbali Bw. Mkapa, wengine waliotajwa kama Bw. Yona hawana sababu yoyote ya msingi ya kuendelea kukaa kimya.

``Kwa upande wa Mkapa wanaweza kuzungumzia mambo ya itifaki, labda. Lakini hawa wengine nao wanakaa kimya kwa sababu gani?`` alihoji.

SOURCE: Nipashe
 
MKUU FM mchango wako is really educative and infomative..BUTIKU ANAYE BINTI ANAITWA ..BHOKE!??

PIA WATU WANASEMA WATOTO WA MWALIMU KAMA ANDREW,EMIL ,JOHN ,ANNA..mbali ya MADA,MAKO, NA ROSE amabao wanasikika..Kuwa discouraged na kuchnganyikiwa na maisha blame ipo kwa BUTIKU ambaye aliaminiwa na mwalimu ku play role ya fatherhood kwa watoto wake..lakini akawa hana muda nao...kwani hata mama maria akisikika akilalamika siku moja kuwa watoto hao wote ni graduates tangu miaka hiyo...lakini wakawa hawataki ajira !!..wapo tu butiama au msasani..what was the problem ..na hawa ..basing ya ukaribu wa kukua na hii familia..
 
Unajua mkuu it is very sad, jinsi hii familia ilivyo-turn out to be after all the promising future iliyokuwa in their hands, lakini inasikitisha sana walipofikia sasa hivi, na pia cha kushangaza zaidi ni jinsi Mwalimu, alivyokuwa akimpenda zaidi mtoto wa Butiku, yaani gladis kuliko watoto wake mwenyewe, ambao alimuachia Butiku, ambaye aliwatia sana ndani masilahi yao huku akimdanganya Mwalimu, kuwa kila kitu kiko sawa,

Unajua nilikuwa ninaamini watu kama Milton na Matare, kuja kuwakomboa wengine na hasa Milton, kwa sababu Magige ambaye ni msomi aliyebobea naye alipoamua kurudi Butiama, nikakata tamaa kabisa, lakini Mungu atawasaidia,

Na ninaamini kuwa Butiku, analipwa na Mungu anayostahili.
 
Unajua mkuu it is very sad, jinsi hii familia ilivyo-turn out to be after all the promising future iliyokuwa in their hands, lakini inasikitisha sana walipofikia sasa hivi, na pia cha kushangaza zaidi ni jinsi Mwalimu, alivyokuwa akimpenda zaidi mtoto wa Butiku, yaani gladis kuliko watoto wake mwenyewe, ambao alimuachia Butiku, ambaye aliwatia sana ndani masilahi yao huku akimdanganya Mwalimu, kuwa kila kitu kiko sawa,

Unajua nilikuwa ninaamini watu kama Milton na Matare, kuja kuwakomboa wengine na hasa Milton, kwa sababu Magige ambaye ni msomi aliyebobea naye alipoamua kurudi Butiama, nikakata tamaa kabisa, lakini Mungu atawasaidia,

Na ninaamini kuwa Butiku, analipwa na Mungu anayostahili.

......strong point mkuu ...mamlaka yote kuhusu mustakabali wa familia alikuwa amemuachia BUTIKU..lakini hawa kina emil..walikuwa wanakuwa discouraged namna watoto wa butiku na mawaziri wa mwalimu walivyokuwa wakiishi maisha tofauti..huku wao wakibanwa!...nafikiri matatizo mengine ni pschological..lets hope kati ya wajukuu wa mwalimu atatokea tu..wa kuja kubeba jina lake..

ehee yule PAULETA nasikia ni adopted ..siku hizi yupo wapi!!?
 
*Kiwanda chasusa makaa yake, ni kutokana na hofu ya ufisadi

Na, Rashid Mkwinda, Kyela

WIKI chache baada ya Mbunge wa Vunjo,Bw. Aloyce Kimaro (CCM) kupinga bungeni ununuzi na umiliki wa mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira uliowahusisha Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa na Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Bw. Daniel Yona, Kampuni ya Saruji ya Mbeya imesusa kununua nishati hiyo kwa hofu ya kuhusishwa na hujuma na ufisadi dhidi ya mali Watanzania.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili hivi karibuni ndani ya mgodi huo, umebaini zaidi ya tani 4,000 za makaa ya mawe zinazozalishwa kwa mwezi sasa zimedoda kutokana na hatua ya Kiwanda cha Saruji cha Tembo kilichopo Songwe, kuacha kununua makaa hayo.

"Tunaamini wananchi ndio wanaohitajika kunufaika na uwekezaji...lakini tunaposikia viongozi waliopata kuongoza serikali wakitajwa kuhusika na ununuzi wenye utata wa mgodi wa Kiwira, tunachelea kuonekana tunaendelea kuunga mkono ufisadi na hujuma dhidi ya mali za walipa kodi", alidai mmoja wa viongozi wa kampuni hiyo.

Alisema baada ya kiwanda hicho kuacha kununua nishati hiyo Kiwira, sasa kimelazimika kuagiza makaa hayo kutoka Afrika Kusini ili kuendesha shughuli za uzalishaji kiwandani hapo.

Alidai awali Kiwanda cha Saruji ambacho kilikuwa mali ya serikali na baadaye kupewa mwekezaji, kililazimika kununua makaa ya mawe kutoka katika mgodi huo kwa kile kilichodaiwa, shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi hali iliyochangia kuchangia kupanda mara kwa mara kwa bei ya saruji kutokana na malighafi hafifu za makaa ya mawe yanayozalishwa na mgodi wa Kiwira.

Katika hoja yake binafsi aliyoitoa hivi karibuni bungeni, Bw. Kimaro, alisema mgodi wa Kiwira ulijengwa na Serikali ya China kwa kwa dola bilioni 4 na kukabidhiwa kwa Serikali ya Tanzania mwaka 1988 na baadaye kuuziwa Bw. Mkapa na Bw. Yona kwa sh. milioni 700. Hadi sasa wamelipa sh. milioni 70.

Wamiliki wa mgodi huo ambao gazeti hili limepata orodha yake ni pamoja na Kampuni ya ANBEN Limited ambayo wamiliki wake wamebainishwa kuwa ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu Bw. Mkapa na mkewe Mama Anna ,Kampuni ya DEVCONSULT Limited ambayo imeoneshwa kuwa ni ya Bw. Daniel Yona mwenye hisa ya asilimia 90 na mtoto wake Danny Yona mwenye hisa asilimia 10.

Wanahisa wengine ni Kampuni ya Universal Technologies Limited ambayo imeoneshwa mmiliki wake kuwa ni Bw. Evans Mapundi na Bw. Wilfred Malekia,Kampuni ya Choice Industries Limited iliyooneshwa kuwa ni ya Bw.Joseph Mbuna na Kampuni ya Fosnik Entreprise Limited ya Bw.Nicholas Mkapa na Bi. Foster Mkapa ambao wana hisa ya asilimia 50 kila moja.

Bodi ya Wakurugenzi wa awali wa mgodi huo ilivyooneshwa kwa gazeti hili mwaka 2004 iliongozwa na Mama Anna kama Mwenyekiti na mwaka 2005, Mwenyekiti alikuwa Bw. Evans Mapundi.

Majira limedokezwa kwamba mbali na uzalishaji wa mgodi huo kudorora, wafanyakazi wapatao 515 wamekuwa wakipunjwa mishahara yao tangu ulipobinafsishwa kutoka serikalini Julai 2005.

Vyanzo vyetu ndani ya mgodi huo vilisema hivi sasa mfanyakazi mmoja hulipwa kima cha chini cha sh. 60,000 bila kujali muda wa ziada na mazingira magumu na ya hatari ya kazi ambapo baada ya makato hujikuta akiambulia sh 49,000 tu.

Pia vilieleza kuwa mgodi huo unakabiliwa na tatizo la uchakavu wa mitambo ya uzalishaji umeme ambao ulikuwa umeunganishwa katika gridi ya Taifa kwa matumizi mengine ya wananchi, hivyo kusababisha kutoa megawati 1 hadi 2 kutoka megawati sita zilizokuwa zikizalishwa kabla ya kubinafsishwa.

Mgodi huo ambao hapo awali ulikuwa una maeneo ya uvunaji wa makaa ya mawe kwa sehemu tatu, hivi sasa maeneo hayo yamesimamishwa na kubakiwa na uvunaji na uchimbaji wa eneo moja ambalo linatarajiwa kumalizika Desemba mwaka huu jambo linaloashiri kufa kwa mgodi huo kutokana na kile kinachodaiwa kutokuwa na maandalizi ya kuwepo maeneo mengine ya uvunaji.

Majira limedokezwa kuwa tangu kubinafsishwa kwa mgodi huo hakuna vifaa vipya vilivyofungwa kiwandani hapo ilhali mashine zilizokuwepo awali kama zile za kubangulia makaa na viberenge vimeanza kuuzwa kama vyuma chakavu. Kulikuwa na viberenge 12 vya tani saba na tani mbili na nusu ambavyo vimeuzwa na kubaki vinne.

Vile vile mashine za kubangulia makaa ambazo awali zilikuwa sita nazo zimeuzwa kama vyuma chakavu na kubakiza moja ambayo utendaji wake umekuwa hafifu kutokana na uchakavu, pia mashine zinazotumika kuzolea makaa mgodini zilikuwa nane, sita kati yake zimeuzwa kama vyuma chakavu na kubakiwa mbili ambazo nazo ziko katika hali duni ya utendaji kutokana na uchakavu wake.

Kulingana na rekodi ambazo gazeti hili inazo ni kwamba mgodi huo kabla ya kubinafsishwa ulikuwa ukizalisha tani 300 kwa siku na sasa unazalisha tani 30 hadi 50 kwa siku kutokana na uchakavu wa mitambo.
 
mkuu Wa Medani, Askari Wa Miavuli Ni Neno Aliloibuka Nalo Siku Moja Baada Kuapishwa 2000,nasisitiza Wasiliana Na Tbc Watakupa Hiyo Clip Na Day One Yake Maana Nakumbuka Project Ya Maji Wami Ni Baada Ya 2000 Mkuu. Kuhusu Hilo La 3rd Term Bado Nasisitiza Kuheshimu Kauli Yake Iliyomo Ktk Mahojiano Hayo Ambayo Umma Mzima Uliyaona,ni Kabla Ya Sumaye Hajafahamu Kuwa Anarejea Ktk Nafasi Yake, Magazeti Yalimnukuu Ktk Hilo Na Kuelekeza Ubashiri Wake Juu Ya Ujio Wa Mark Mwandosya Especially Rai Na Dada Zake. Mwandosya Ameingia Barazani 2000 Kama Waziri Wa Mawasiliano Na Uchukuzi Baada Kuupata Ubunge Bila Kupingwa Kule Kwa Mwambulukutu Na Ukumbuke Rungwe Iligawanywa Majimbo Mawili Mwaka 2000 Baada Kasheshe Ya Mwaikambo Vs Mwambulukutu, Zaidi Ukumbuke Mbunge Wa Rungwe 1995-2000 Ni Emmanuel Mwambulukutu.sibishani Kwa Kumtetea Bm Bali Nafurahia Ukweli Zaidi Kuliko Hisia, Ninafurahi Sana Nionapo Mrindimo Wa Hoja Zako Juu Ya Ufisadi,hasira Yako Ni Kali Kuliko Ncha Ya Upanga,najivunia Kuwaona Watu Wa Aina Yako Ktk Harakati Za Kujenga Uzalendo Ktk Dunia Ya Kweli,keep It Up Mkuu,we're Still Learning Kwani Sisi Ni Vijana; Kwa Leo Habari Ndio Hiyo Ila Huo Ndio Ukweli Mkuu
 
BWM anajua kuwa hana cha kuwaambia wa-tz deal zake zimebumburuka lazima auwe soo kwa kukaa kimya. Na wala sioni haja ya kupiga kelele kila siku kuwa ajitokeze asema mnataka aseme nini sasa wakati kila kitu kiko wazi???...suala hapa kama kweli sheria ni msumeno kama wanavyodai basi awekwe kolokoloni sio kila siku kurudia mambo yale yale....Kelele za chura hizo hazimzuiii ng'ombe kunywa maji...Ni muda wa action sio longolongo
 
Mkapa era in the spotlight: Dubious payments made in twilight of presidency

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

A SIGNIFICANT number of dubious official payments amounting to hundreds of billions of shillings are believed to have been made during the final few months and even weeks of former president Benjamin Mkapa’s tenure in 2005, it has been learnt.

And according to one well-placed source: ’’These payments may not necessarily have been diverted to finance the 2005 general elections, as widely believed.’’

’’It now appears that a huge chunk of these particular monies was actually deposited in private bank accounts controlled by some top government officials�ostensibly to guarantee them a comfortable retirement,’’ said the source.

The revelation is the latest pointer to an emerging pattern of serial corruption and abuse of public office by various public officials, especially linked to the winding�up period of the Mkapa presidency.

Some of the questionable payments include the well-documented embezzlement of more than 133bn/- from the Bank of Tanzania’s external payment arrears (EPA) account, which was systematically carried out during 2005/06.

One particular shell company - Kagoda Agriculture Limited - was paid a staggering $30.8m (approx. 40bn/-) out of the EPA account, with auditors uncovering massive fraud and collusion with senior central bank officials in the scandal.

The payments to the Kagoda company were reportedly made with the blessings of highly authoritative people in the Mkapa government. The mysterious beneficiaries of the funds paid to Kagoda are yet to be made public.

Apart from the EPA funds, a cumulative total of more than 500bn/- was paid out in the twilight of the third phase government towards the overly-inflated costs of the BoT Twin Towers project.

The state-run Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) has been investigating allegations that the Twin Towers were overpriced by at least four times the value of similar buildings in some of the world’s most expensive cities such as London, New York and Tokyo.

In the same period, the Controller and Auditor-General uncovered dubious payments of up to 8bn/- made by the BoT to a local law firm, Mkono and Company Advocates.

The CAG’s report also discovered questionable payments of a similar magnitude made by the central bank to Mwananchi Gold Company Limited.

Also in the same year, the central bank bought a 155bn/- treasury bond and later exchanged the amount into US dollar currency to finance the bankruptcy of Meremeta gold mine, which was a joint venture company owned on a 50-50 basis by the government and a South African firm, Trinnex (Pty) Limited.

After the liquidation of Meremeta, a supposedly government-owned firm registered as an offshore company in Mauritius, TANGOLD, inherited the assets and liabilities of Meremeta.

Following the bankruptcy of Meremeta, the BoT deposited close to $13m (approx. 15bn/-) into TANGOLD’s bank account.

THISDAY investigations have also established that more payments of billions of shillings were made by BoT to TANGOLD and another related company, Deep Green Finance Company Limited, towards the end of 2005.

Official government records show the following pattern of payments made by the central bank to Meremeta/TANGOLD and Deep Green Finance in the year under review:

On August 1, 2005, the BoT paid $1,354,167.26 (approx. 1.6bn/-) to Deep Green Finance through cheque number 241740. The funds were withdrawn on the same day by special clearance.

Exactly a month later, the BoT, through cheque number 015558, paid another $1,827,137.44 (approx. 2bn/-) to Deep Green Finance. The funds were again withdrawn by special clearance on the same day.

There are also bank records showing transfers of billions of shillings between accounts owned by Meremeta/TANGOLD and Deep Green Finance.

On October 4, 2005 the BoT deposited another $1,789,075.89 (approx. 2.2bn/-) again to Deep Green Finance company.

In the same month (October 31), the Ministry of Finance paid more than 2bn/- to Deep Green Finance company.

On November 30, 2005, BoT again deposited more than 2bn/- into an account owned by Deep Green Finance, with the funds withdrawn the following day.

Other dubious payments amounting to 70bn/- were also made to Alex Stewart Asseyers, on the basis of a controversial gold mine auditing contract with the government.

Apart from all these dubious payments, a number of controversial contracts were also signed by the government in 2005 in the mining and privatisation sectors.

They include the 15-year extension of the contract of the Tanzania International Container Terminal Services (TICTS), personally ordered by then-president Mkapa in late 2005.

Both the CAG’s office and the National Assembly have declared this contract extension illegal, and have advised the government of incumbent President Jakaya Kikwete to terminate the agreement.

In 2005, Mkapa and his senior cabinet minister, Daniel Yona, were also involved in the dubious privatisation of the previously state-run Kiwira Coal Mine Limited.

Investigations by THISDAY revealed that Mkapa and Yona (then energy and minerals minister) used their powerful positions in public office to fast-track the privatisation of Kiwira coal mine and hand over control of the lucrative mine to a private company, Tanpower Resources, which they jointly formed in 2004 while both were still in government.

Tanpower Resources currently holds 85 per cent shares in Kiwira Coal and Power Limited, which in March 2006 entered into a controversial, $271.8m (approx. 340bn/-) contract with the state-run Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) for the supply of 200 megawatts of electricity to the national power grid.

Our investigations further revealed that Mkapa and the then first lady, Anna Mkapa, jointly formed ANBEM Limited company in 1999, through which they actively engaged in private business dealings while they were still at State House.

Operating from within the official State House walls, ANBEM Limited went on to acquire loans of up to 750m/- from the National Bank of Commerce and CRDB Bank.
 
Kulingana na rekodi ambazo gazeti hili inazo ni kwamba mgodi huo kabla ya kubinafsishwa ulikuwa ukizalisha tani 300 kwa siku na sasa unazalisha tani 30 hadi 50 kwa siku kutokana na uchakavu wa mitambo.

Hii sentensi inachanganya sana inaonekana mwandishi hakwenda shule. Haeleweki atauambia ni sababu gani iliyofanya mgodi upunguze uzalishaji. Ubinafsishaji au mitambo michakavu?
 
Tanzania kweli inahitaji uvumilivu. Hizi transanction zote zilifanyika na watu bado wanaendelea kupeta tu.

watoto wanasomea kwenye miti, madawati hakuna, shule zenyewe kuna sehemu bado ni za udongo. Hospital ndio usiseme, kabajeti asilimia kubwa wahisani.

Kwa nini tusidai pesa zetu kwa hao mafisadi? Nafikiri viongozi wameisha sema wao hawawezi kuwadai mafisadi lakini hivi na wananchi hatuwezi kuwadai?
 
1.
BWM anajua kuwa hana cha kuwaambia wa-tz deal zake zimebumburuka lazima auwe soo kwa kukaa kimya. Na wala sioni haja ya kupiga kelele kila siku kuwa ajitokeze asema mnataka aseme nini sasa wakati kila kitu kiko wazi???...suala hapa kama kweli sheria ni msumeno kama wanavyodai basi awekwe kolokoloni sio kila siku kurudia mambo yale yale....Kelele za chura hizo hazimzuiii ng'ombe kunywa maji...Ni muda wa action sio longolongo

Mkuu Kipanga,

Heshima mbele na ubaikiwe tu!


2.
naogopa hata kuchangia,ila mkuu FMES nakuvulia kofia.U would know why

Unajua mkuu Zanaki, heshima mbele kwanza, ninajua kuwa una akili sana, ninakukumbuka toka BCS jinsi siku moja ulivyosema kuwa Mungai ndiye waziri mkuu mpya,

now hapa ninajua for a fact all your games, lakini nilikuwa ninakusogeza pole pole ujivike kitanzi mwenyewe, you almost fooled me, lakini unajua nina kinga moja nzito sana nayo ni ninatumia jina moja tu!

Tuendelee kukata ishus mkuu!
 
A SIGNIFICANT number of dubious official payments amounting to hundreds of billions of shillings are believed to have been made during the final few months and even weeks of former president Benjamin Mkapa’s tenure in 2005, it has been learnt.

Mungu Aibariki Tanzania tu!
 
Kwa kifupi hizi hela zimeingia mifukoni mwa watu na sio zote zilifinance campaign za CCM kama tulivyokuwa tunaamini hapo nyuma?
 
Hahahaaaaaaaaa,kazi kwelikweli wakubwa mnapotanuana mbavu zenu.
Hapa ni shuleni ipo siku watu tafauru paper kwa nguvu ya maono ya JF
 
Kwahiyo tuiombe msamaha kwanza CCM kisha tuwatoe roho walio kula .Ndio hekima hiyo wakubwa
 
Unajua mkuu Zanaki, heshima mbele kwanza, ninajua kuwa una akili sana, ninakukumbuka toka BCS jinsi siku moja ulivyosema kuwa Mungai ndiye waziri mkuu mpya

Hapo kwa kweli a big NO! Sijawahi kuwa mchangiaji BCS na mara ya kwanza nimeisikia BCS ni humu,kama kulikuwa na mtu mwingine anaitwa Zanaki huko,well its just a coincidence.Pili,sikuwahi hata siku moja kudhani kuwa Mungai angekuwa PM.Ni mtu ambaye hajui siasa za nchi hii.Hata wakati huo,kati ya majina yaliyokuwa yanatajwa,la Mungai sikuwahi kulisikia,na sio mtu aliyekuwa karibu na JK.Mimi na wengine wengi tulijua PM angekuwa Sitta,kwa sababu kabla ya wote hawa,sijui Rostam,Lowassa n.k,aliyembeba toka enzi hizo ni Sitta.

now hapa ninajua for a fact all your games, lakini nilikuwa ninakusogeza pole pole ujivike kitanzi mwenyewe, you almost fooled me, lakini unajua nina kinga moja nzito sana nayo ni ninatumia jina moja tu!

Sijajifunga kitanzi hata kidogo,infact the comment i made earlier on,was meant as a compliment! Jamboforums ni forum ya kwanza kwa mimi kujiandikisha na kutoa maoni,huko BCS sio mimi na sina haja kukataa kama kweli nilikuwa mimi huko BCS.And trust me brother,i'm not here to fool anybody,i'm here to share what i know that maybe many people would not,na pia kujifunza yale ambayo nilikuwa siyajui..na kwa kweli i have learnt a lot.In short,with all due respect,you do not know me and neither do i know you,having said that,i feel priviledged to exchange views with you na members wengine wote humu....i trully respect your inputs hapa and i feel maybe we should stick to issues.Au sio brother?
 
Hapo kwa kweli a big NO! Sijawahi kuwa mchangiaji BCS na mara ya kwanza nimeisikia BCS ni humu,kama kulikuwa na mtu mwingine anaitwa Zanaki huko,well its just a coincidence.

There you go, ni kweli mkuu kulikuwa na mtu alikuwa na jina kama lako Zanaki, aliyesema kuwa Mungai ndiye next pm, anyways unajua fumbo huwa tunafumbia mjinga maana werevu hunga'mua,

Heshima mbele kwa elimu yako nzito, tuendelee kukata ishus mkuu, taifa liko njia panda!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom