It's friday dude....whatchu got goin' on...?
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.
Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?
Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?
Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.
Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?
Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?
Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!
Sasa jamani, hivi kweli huyu ndiye rais wetu mstaafu tutakayeendelea kumlipa hadi mwisho wa maisha yake? Yaani akishastaafu tu anasema mabovu yangu yote msinisakame tena? Yaani anasema kuwa ni haki kwa wanasiasa kufanya mambo aliyofanya ila wakishastaafu basi game over?
Sasa itatusaidia nini kuendela kumlipa kama hata yeye mwenyewe hata hatambui nafasi yake katika jamii yetu ?
Mr Clean Huyo
Mimi naona amnaonesha mfano mzuri, kwamba amestaafu siasa na sasa anashughulikia masuala ya kijamii kama hilo la afya za wananchi. Hao wanaomtuhumu waende mahakamani. Wanashindwa nini? Maana hata akijitetea mbele ya waandishi wa habari wanaomtuhumu bado hawataamini kuwa alichokisema ni sawa. Mzee Mkapa kula pini hivyo hivyo, ulishastaafu, achana na malumbano yasiyo na msingi. Tulia, ule pensheni yako. Mwenye wivu ajinyonge, na yule mwenye suala la msingi la kulalamikiwa aende mahakamani au kwenye vyombo vingine stahili. Watu mnakalia majungu tu. Ovyoo!
Mkapa up for 6.5bn/- leadership prize
THISDAY REPORTER
Dar es Salaam
A spokesman for Mo Ibrahim said the long list of candidates in no particular order includes Mathieu Kerekou (Benin), Azali Assoumani (Comoros), Domitien Ndayizeye (Burundi), Henrique Rosa (Guinea Bissau), Maaouya Ould SidAhmed Taya (Mauritania), Joaquim Chissano (Mozambique) and Sam Nujoma (Namibia).
Others also in the running for the prize are Benjamin Mkapa (Tanzania), Abass Bonfoh (Togo), Gnassingbe Eyadema (Togo), Bakili Muluzi (Malawi), France-Albert Rene (Seychelles) and Abdiqassim Salad Hassan (Somalia).
Mimi naona amnaonesha mfano mzuri, kwamba amestaafu siasa na sasa anashughulikia masuala ya kijamii kama hilo la afya za wananchi. Hao wanaomtuhumu waende mahakamani. Wanashindwa nini? Maana hata akijitetea mbele ya waandishi wa habari wanaomtuhumu bado hawataamini kuwa alichokisema ni sawa. Mzee Mkapa kula pini hivyo hivyo, ulishastaafu, achana na malumbano yasiyo na msingi. Tulia, ule pensheni yako. Mwenye wivu ajinyonge, na yule mwenye suala la msingi la kulalamikiwa aende mahakamani au kwenye vyombo vingine stahili. Watu mnakalia majungu tu. Ovyoo!
Quote: Mtanzania
Mkapa up for 6.5bn/- leadership prize
THISDAY REPORTER
Dar es Salaam
A spokesman for Mo Ibrahim said the 'long list' of candidates in no particular order includes Mathieu Kerekou (Benin), Azali Assoumani (Comoros), Domitien Ndayizeye (Burundi), Henrique Rosa (Guinea Bissau), Maaouya Ould Sid'Ahmed Taya (Mauritania), Joaquim Chissano (Mozambique) and Sam Nujoma (Namibia).
Others also in the running for the prize are Benjamin Mkapa (Tanzania), Abass Bonfoh (Togo), Gnassingbe Eyadema (Togo), Bakili Muluzi (Malawi), France-Albert Rene (Seychelles) and Abdiqassim Salad Hassan (Somalia).
Hapo Mkapa anachuana na Chissano na Nujoma. Wengine wasindikizaji.
8. Kampuni ya shemeji yako Simu 2000 ndiyo ilihusika katika kuwaleta Net Group ili kuiendesha TANESCO. Kama utakumbuka uamuzi huo ulipingwa sana na Watanzania walio wengi wakiwemo viongoz na wafanyakazi wa TANESCO. Je, Simu 2000 walilipwa kiasi gani kwa kuwa wakala wa kuwaleta Net Group Solutions? Na taratibu zipi zilizotumika katika kuichagua Simu 2000 kama wakala?
7. Pia simu 2000 katika mazingira ya kutatanisha ilipewa tenda ya kusimamia uuzwaji wa Asetts zote za TTCL. Je ni taratibu zipi zilizotumika katika kuwapa Simu 2000 tenda hiyo ukitilia maanani kwamba walikuwa hawana uzoefu wowote wa kusimamia uuzaji wa Assets?
Bubu Ataka Kusema, nakupongeza kwa stail yako nzuri ya "KUMTENDEA HAKI" Mkapa, maana umeweka maswali anayoweza kujibu bila shaka yoyote na hayahusiani na "siasa" anazozisema, kwamba ameshastaafu. Anatakiwa kujibu tuhuma zinazomkabili na si SIASA.
Ama baada ya pongezi, naomba kufanya masahihisho muhimu.
1-Kwanza kabisa kwa kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba Simu2000 Limited si kampuni binafsi na si kampuni ya shemeji yake Mkapa. SImu2000 ni kampuni ya serikali iliyoundwa kusimamia mali na madeni ya TTCL baada ya ubinafsishaji. Mkapa alimteua mtoto wa mke wake aitwaye Peter Maro, kijana mdogo kabisa kuongoza shirika hilo. Kuna tuhuma za Mkapa kujibu kwamba je, ni kweli yeye na mkewe wameuziwa na huyo mtoto wa Anna Mkapa (wa nje) nyumba kibao nchi nzima na kwa Dar es Salaam nyingi ziko maeneo nyeti, anatakiwa kujibu kama ni kweli ama la.
2- Pili ni kweli kampuni ya shemeji yake Mkapa ndio iliyoileta Net Group kampuni hiyo inaitwa Wace Technology, ambayo shemeji yake Mkapa aitwaye Joe Maro, anayefanya kazi BoT anaimiliki pamoja na rafiki yake wa BoT aitwaye Maganga. Mkapa alilazimisha Net Group kuingia Tanesco kwa kutumia FFU.
3.Suala la Simu2000 kuwa na uzoefu ama la, halina maana, hapa ni kama Peter Maro ana uwezo ama la si chombo kwa ujumla wake, maana tunaambiwa kijana anazurura tu kazi zinaendeshwa na watu wengine na yeye anachofanya ni kutoa maelekezo pale anapopata maelekezo kutoka katika familia, yaani 'baba' na mama. Inawezekana hata baba yake mzazi, ambaye wana JF munaweza kutusaidia.
Kama mtu aliyewahi kushika madaraka makubwa kabisa nchini, Mkapa ataendelea kuwa kiongozi wa Watanzania hadi mwisho, atake asitake. Hivyo, bado anawajibika kuitekeleza sera yake ya ukweli na uwazi.