Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Waheshimiwa naona tunakwenda vizuri wote tujipongeze. Inaelekea kuwa wengi wetu, hata wabunge na wanasiasa wakuu ukweli unawafunukia kuwa mh: Mkapa ana muda wa kukimbia tu, siwakujificha. na hii imesababishwa na kuelekeza dira yetu ktk tatizo lenyewe: KATIBA tuiangalie katiba, Mkapa hana endapo mweke kiporo kwanza. ibara 46 (1) na(2) ziko wazi juu ya rais ALIYEPO MADARAKANI kuwa hawezi kushtakiwa hata kwa makosa ya kabla ya kutwaa kwake wadhifa wa Urais.(ie alikosea alipokua mitaani ukachelewa kufungua mashtaka nae akaingia ikulu, 46 (2) inamlinda) na matatizo yale ya nyuma.akaendelea kututumikia katikati ya njia akaamua kukipaka, akajikinga kwa nguvu za dola alizopewa, akamaliza kipindi chake bado46(2)itamlinda. Tuhuma zikajitokeza (kumbuka amemaliza kipindi cha urais hakuachishwa as a result of 46A(10) ). natuhuma hizo hazipoi bali zinapamba moto. je nini cha kufanya? tuirudie katiba palepale 46(2) inayosema: Wakati wote rais atakaokua ameshika madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye kama raia wa kawaida ama kabla au baada ya kushika madaraka ya rais. (mpaka hapo tupo clear)inaendelea: ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani,rais atapewa au ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujiba wa sheria iliyotungwa na bunge, inamalizia kuwa iwe na maelezo kamili juu ya tuhuma na madai yanayokusudiwa.
Hebu tuiangalie 46 (3) ili tuione hii vema inafaa tuanzie 46A(10) inasema:endapo bunge litathibitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha rais, spika atawafahamishrais na mwenyekiti tume ya uchaguzi juu ya azimio la bunge, na hapo rais atawajibika kujiuzulu ndani ya siku tatu baada ya baada ya bunge kupitisha azimio hilo. ikiwa 46A (10)imetokea then rais anaondolewa madarakani na 46 (3) inamhakikishia kinga. kwa hiyo kunaonekana upungufu wa lugha katika 46(2) haimtaji rais mstaafu kuwa anaweza akapewa taarifa ya siku30 na mujibu wa sheria ukamwandama. pamoja na upungufu huo naona bado ibara hiyo inaweza kumsukumia mh:Mkapa siku 30 za mataarisho to face the PEOPLE.
 
Kafara,
Nilvyosikia mimi enzi hizooo. kuwa aliyemuua Karume ni shemeji yake au mtu katika familia ambaye alikuwa analipa kisasi..Hakuuawa on the spot kama sikosei, na Kisiasa mauaji yale yalifikiriwa yamepangwa na kundi la Umma party kina Abraham babu..ndio maana walikuwa wanted Zanzibar.

mkuu mkandara, nachelea kutoka nje ya mada lakini huyu jamaa (muuaji wa karume) alifika makao makuu na kutoa salute kisha kummiminia risasi karume kwani naamini alitaka kuhakikisha haponi. baada ya hapo wakati anaondoka ndio akapigwa risasi na walinzi wa karume akafa hapohapo. marehemu thabiti kombo alikuwepo kwenye tukio yeye aliparazwa na risasi makalioni (kama si kosei). kama ulivyosema huyu jamaa inasemekana alikuwa analipa kisasi cha mzazi wake kuuawa na utawala wa karume.
naomba kuishia hapa.
 
Kafara,
Shukran mkuu kwa taarifa hiyo, nimekusikia.. unajua tena habari za kusikia na usiri nchini ni vigumu kuwa na taarifa kamili..

Rev Kishoka,
Mkuu nadhani siku za nyuma tuliwahi kufikia hapo kuwa ni jukumu la Bunge letu kumsimamisha Mkapa badala ya kuwasubiri Hosea au Kikwete wapitishe uchunguzi, kulingana na Katiba...Lakini mpira umekuwa ukipigwa danadana muda wote hata hizi sahihi 20 za wabunge inakuwa kazi kuzipata.
Kila mtu akiogopa kurusha jiwe la kwanza na hata baadhi wabunge wa Upinzani wamekuwa Upande wa pili hivyo kufanya sheria hii kuwa ngumu kutumika kupitia Bunge kwa sababu nafikiri inatakiwa kitu kama 2/3 ya Wabunge kuelekea ushindi..
Na kibaya zaidi kuna watu wanaendeleza kampeni za kumwekea Kikwete na Hosea jukumu hili wakati ukweli umesimama kuwa hawa wawakilishi wetu ndio wenye matatizo. kwa mara ya kwanza nao wanasimamia maslahiu yao binafsi ndani ya Bunge...
Mwisho wakuu zangu ningeomba mwenye Kanuni za Uongozi na Maadili ya viongozi Kitaifa anirushie..
 
Dk Slaa kulia na Mkapa bungeni
Date: 12/28/2008
Mussa Juma, Karatu
Mwananchi

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbrod Slaa amesema anajiandaa kuzungumzia suala la Rais mstaafu, Benjamin Mkapa kushtakiwa kwa makosa anayodaiwa kufanya akiwa Ikulu katika bunge lijalo.

Dk Slaa aliiambia Mwananchi Jumapili jana kuwa atafanya hiyo ili kuondoa upotoshaji wa suala hilo ambayo imeanza kufanywa na baadhi ya wasomi nchini.

Alisema baadhi ya wasomi nchini wameanza kupotosha jamii kuwa Mkapa hawezi kushtakiwa mpaka bunge limwondolee kinga.

Dk Slaa alisema Mkapa anaweza kushtakiwa bila ya kuondolewa kinga yake.

Alisema anashangaa wasomi nchini kuendelea kuipotosha jamii juu ya suala la kufunguliwa mashitaka Rais mstahafu, na anakusudia kuliweka bayana suala hilo tena katika bunge lijalo.

"Katika bunge lililopita katika hotuba ya Waziri Mkuu, niliwahi kulisema hili kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria na lazima tutofautishe mamlaka ya rais na mtu binafsi na hili nitalieleza tena bunge,"alisema Dk Slaa ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

Alisema matendo ambayo Rais hawezi kufunguliwa kesi mpaka aondolewe kinga ni yale tu ambayo aliyafanyaka kama Rais, katika madaraka yake kisheria kama kuwaachia huru wafungwa, kuidhinisha sheria na masuala mengine yaliyoanishwa kwenye katiba ya nchi.

Dk Slaa alisema masuala kama ya Rais Mkapa kufanya biashara akiwa Ikulu hayahitaji kuwa na kinga ili ashitakiwe kwani ameyafanya nje ya mamlaka ya rais aliyopewa.

"Watu wengi hawapendi kusoma, ni wavivu. Jambo hili lipo wazi kabisa na nashangaa wasomi wetu ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) kudai eti kumshitaki mkapa ni kuvunja katiba,"alisema Dk Slaa.


Alisema kinachoendelea hivi sasa hapa nchini ni kukosekana kwa usimamizi mzuri wa sheria na viongozi wenye kauli ya mwisho juu ya masuala yenye maslahi ya Taifa.

"Ni aibu Waziri Mkuu anazungumza kuwa hakuna aliye juu ya sheria, Takukuru wanadai hawamchunguzi Mkapa kwani mpaka aondolewe kinga, haya ni mambo ya ajabu,"alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye ndiye alikuwa wa kwanza kutoa hadharani tuhuma nzito dhidi ya Mkapa kwa kuanzisha kampuni akiwa Ikulu na kujiingiza katika biashara mbalimbali, alisema umefika wakati sheria kufuatwa bila kujali nafasi za wahusika.


Akizungumzia vita dhidi ya ufisadi, alisema Chadema itaendelea kushinikiza watuhumiwa wote kufikishwa mahakamani hadi wamalizike.

"Sisi ndio tumeanzisha huu mjadala hakuna wa kuufunga sio Makamba (Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf) wala Chiligati (Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, John) na tutapiga kelele hadi watuhumiwa wote wakamatwe,"alisema Dk Slaa.

Dk Slaa aliwataka Watanzania kwa ujumla wao kusimama kidete na kuliombea Taifa lao kwani wasipoamka na kutetea rasilimali zao nchi yao itamalizwa na mafisadi na siku zijazo hali itakuwa mbaya zaidi.

"Tukiendelea hivi taifa linaporomoka ni lazima tuungane tuwaondoe mafisadi na tunakwenda kwenye uchaguzi Mbeya Vijijini mshikamano wetu ni muhimu kuing’oa serikali ya CCM,"alisema Dk Slaa.

Akizungumzia kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda hivi karibuni kuhusu kuzuia magari ya kifahari, alisema jambo hili ni kuwadanyanga wananchi kwani serikali haina nia ya dhati kuacha kutumia magari hayo.

"Anasema wanazuia wakati kuna magari 700 wamenunua kweli hapa kuna umakini na thamani ya gari moja ni zaidi ya Sh100 milioni na tunaendelea kudai nchi ni masikini,"alisema Dk Slaa.

 
Dr. Slaa,
Mkuu kama utasimama imara ktk hili basi kura yangu umeipata..yaani nahitaji nini zaidi kutoka kwako!.hata sioni, labda hilo Azimio la Zanzibar..
-Dr. Slaa for President!
 
1. Alisema baadhi ya wasomi nchini wameanza kupotosha jamii kuwa Mkapa hawezi kushtakiwa mpaka bunge limwondolee kinga. Dk Slaa alisema Mkapa anaweza kushtakiwa bila ya kuondolewa kinga yake.

2. Alisema anashangaa wasomi nchini kuendelea kuipotosha jamii juu ya suala la kufunguliwa mashitaka Rais mstahafu, na anakusudia kuliweka bayana suala hilo tena katika bunge lijalo.

3. "Katika bunge lililopita katika hotuba ya Waziri Mkuu, niliwahi kulisema hili kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria na lazima tutofautishe mamlaka ya rais na mtu binafsi na hili nitalieleza tena bunge,"alisema Dk Slaa ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

4. Alisema matendo ambayo Rais hawezi kufunguliwa kesi mpaka aondolewe kinga ni yale tu ambayo aliyafanyaka kama Rais, katika madaraka yake kisheria kama kuwaachia huru wafungwa, kuidhinisha sheria na masuala mengine yaliyoanishwa kwenye katiba ya nchi. Dk Slaa alisema masuala kama ya Rais Mkapa kufanya biashara akiwa Ikulu hayahitaji kuwa na kinga ili ashitakiwe kwani ameyafanya nje ya mamlaka ya rais aliyopewa.

5. "Watu wengi hawapendi kusoma, ni wavivu. Jambo hili lipo wazi kabisa na nashangaa wasomi wetu ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) kudai eti kumshitaki mkapa ni kuvunja katiba,"alisema Dk Slaa.

6. Alisema kinachoendelea hivi sasa hapa nchini ni kukosekana kwa usimamizi mzuri wa sheria na viongozi wenye kauli ya mwisho juu ya masuala yenye maslahi ya Taifa. "Ni aibu Waziri Mkuu anazungumza kuwa hakuna aliye juu ya sheria, Takukuru wanadai hawamchunguzi Mkapa kwani mpaka aondolewe kinga, haya ni mambo ya ajabu,"alisema Dk Slaa. Akizungumzia vita dhidi ya ufisadi, alisema Chadema itaendelea kushinikiza watuhumiwa wote kufikishwa mahakamani hadi wamalizike.

7. "Sisi ndio tumeanzisha huu mjadala hakuna wa kuufunga sio Makamba (Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf) wala Chiligati (Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, John) na tutapiga kelele hadi watuhumiwa wote wakamatwe,"alisema Dk Slaa. Dk Slaa aliwataka Watanzania kwa ujumla wao kusimama kidete na kuliombea Taifa lao kwani wasipoamka na kutetea rasilimali zao nchi yao itamalizwa na mafisadi na siku zijazo hali itakuwa mbaya zaidi.

8. Akizungumzia kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda hivi karibuni kuhusu kuzuia magari ya kifahari, alisema jambo hili ni kuwadanyanga wananchi kwani serikali haina nia ya dhati kuacha kutumia magari hayo. "Anasema wanazuia wakati kuna magari 700 wamenunua kweli hapa kuna umakini na thamani ya gari moja ni zaidi ya Sh100 milioni na tunaendelea kudai nchi ni masikini,"alisema Dk Slaa.

- Ndio maana nilisema kwamba huyu Shujaa wangu Dr. Slaaa apewe nafasi ya kugombea urais huko Chadema, hata asiposhinda ataaamsha sana wanachi walioko usingizini,

Dr. Slaaa heshima mbelee shujaaa, hapa tupo ukurasa mmoja.
 
Nimeanza kufarijika kusikia Dr. Slaa amelisemea hilo la Rais Mstaafu Mkapa kutohitajika kuondolewa kinga ili ashtakiwe. Ugumu unakuja, jee kuandikisha biashara ni kosa kisheria kwa Mkapa akiwa Ikulu. Hili halikuelezwa popote. Kuna baadhi ya makosa ni moral wrongs lakini sio legal wrongs.
Kama itathibitika hakuvunja sheria yoyote kusajili AnnBen, then kitendo cha kujiuzia Kiwira kimevunja sheria yoyote?. Hii inamaana mchakato wa uuzwaji wa Kiwira was it tranparency?. Ikithibitika nothing illegal, then he is off the hook.

Hata kama he is off the hook, amini usiamini dhamira yake inamsuta (if he has conscious) kwa baadhi ya madudu aliyoyafanya ikiwemo Radar na JetStrem. Wenye akili timamu wote tunajua kulikuwa na mkono wake tukijua haijui pesa, yaani ni Mr. Clean. Sasa baada ya kuthibitika kumbe kuoa Mchagga, kabadili na kabila sasa anaijua pesa vilivyo, them kwenye deal ya Rada na Ndege yake sii bure, vijisenti vyake vipo tena Uswisi, huko hakuna majina ni codes tu na password. No way to prove anything.
 
- Ndio maana nilisema kwamba huyu Shujaa wangu Dr. Slaaa apewe nafasi ya kugombea urais huko Chadema, hata asiposhinda ataaamsha sana wanachi walioko usingizini,

Dr. Slaaa heshima mbelee shujaaa, hapa tupo ukurasa mmoja.

FMES Kwa kweli Dk Slaa anastahili kupewa nafasi ya kugombea Urais huko CHADEMA amekuwa ni mwiba mkali dhidi ya mafisadi wote ndani ya chama na serikali pamoja na vitisho mbali vya kumfungulia mashtaka hata kuchukua uhai wake, lakini wakati mwingine nahofia kama hakupata nafasi hiyo basi Watanzania tutapoteza mtu muhimu sana ndani ya bunge letu. Kama kampeni zake zikiandaliwa vizuri katika kila kona ya nchi yetu na CCM haitatumia vyombo vya dola kumshinikiza na kumzuia kufanya kampeni zake basi ataibuka mshindi wa Urais.
 
Pasco, wizi wa Mkapa asilaumiwe mkewe mchaga, Mkapa ni mwizi by nature alikuwa tu hajapata opportunity ya kuonyesha makucha yake kabla hajawa raisi. Huwezi kushawishiwa kiasi hicho, kama huyo anna maro alim-influence labda lakini hakumhipnitise useme it's all her fault. Stop hating on the Chagas and women kama Adam, eti excuse ni ".....ni huyu mwanamke uliyenipa".
 
Nimeanza kufarijika kusikia Dr. Slaa amelisemea hilo la Rais Mstaafu Mkapa kutohitajika kuondolewa kinga ili ashtakiwe. Ugumu unakuja, jee kuandikisha biashara ni kosa kisheria kwa Mkapa akiwa Ikulu. Hili halikuelezwa popote. Kuna baadhi ya makosa ni moral wrongs lakini sio legal wrongs.
Kama itathibitika hakuvunja sheria yoyote kusajili AnnBen, then kitendo cha kujiuzia Kiwira kimevunja sheria yoyote?. Hii inamaana mchakato wa uuzwaji wa Kiwira was it tranparency?. Ikithibitika nothing illegal, then he is off the hook.

Hata kama he is off the hook, amini usiamini dhamira yake inamsuta (if he has conscious) kwa baadhi ya madudu aliyoyafanya ikiwemo Radar na JetStrem. Wenye akili timamu wote tunajua kulikuwa na mkono wake tukijua haijui pesa, yaani ni Mr. Clean. Sasa baada ya kuthibitika kumbe kuoa Mchagga, kabadili na kabila sasa anaijua pesa vilivyo, them kwenye deal ya Rada na Ndege yake sii bure, vijisenti vyake vipo tena Uswisi, huko hakuna majina ni codes tu na password. No way to prove anything.

Mkapa ni mjuvi wa mambo anajua fika kwamba katiba ya Tanzania haikmuruhusu kufanya biashara akiwa Ikulu ndiyo maana alifanya siri kubwa biashara aliyoifanya akiwa Ikulu. Pia kujimilikisha mgodi wa Kiwira kulijaa utata mwingi ambao unaonekana ulikuwa ni wizi wa mchana kweupe. Maswali ya kujiuliza:

1. Ni nani ndani ya serikali aliyeamua mgodi wa Kiwira uuzwe na kwa vigezo vipi?

2. Je uamuzi wa kuuza Kiwira ulitangazwa hadharani kupitia magazeti yetu na kukaribisha zabuni kwa wale ambao wangependa kununua mgodi huo? au ilikuwa ni siri ya Mkapa na Yona?

2. Nani waliokuwa katika kamati ya kupitia zabuni mbali mbali za waliotaka kununua mgodi huo?

3. Nani ndani ya serikali aliyeamua mgodi huo uuzwe kwa shilingi 700 millioni badala ya thamani yake ya shilingi bilioni 4.

4. Je Mkapa alitumia wadhifa wake kuwashinikiza viongozi wa juu wa TANESCO, wakati huo walikuwa ni makaburu wa Net Group ambao waliletwa nchini na Mkapa na kuingizwa TANESCO kwa mtutu wa bundki maana asilimia kubwa hatukukubaliana na Mkapa kuhusu TANESCO kuendeshwa na Net Group.

5. Kwenye ununuzi wa rada, ndege ya Rais, magari ya jeshi na helicopters Mkapa alihusika kwa karibu mno na wakala ni yule yule mhindi yule yule Vithlani ambaye ameikimbia nchi. Pia kwenye mikataba ya uchimbaji dhahabu Mkapa alihusika kwa karimu na lifanya kila njia kuhakikisha mikataba ili haiwekwi hadharani au hata kupelekwa bungeni kujadiliwa kama ilikuwa na maslahi kwa nchi. Kwente uuzwaji wa nyumba za serikali pia ambapo mpaka sasa inasemekana serikali imepata hasara ya $200 millioni, Mkapa alihusika kwa karibu.

Kwa kifupi alikuwa anajua anafanya nini ili kuficha madhambi yake ya ufisadi ndiyo maana kuna umuhimu mkubwa wa kumchunguza na kama kuna ushahidi wa kutosha dhidi yake basi hakuna jinsi nyingine bali ni kumfungulia mashtaka.

Katiba ya Tanzania haimlindi Rais kwa maovu aliyoyafanya kama mtu binafsi akiwa Ikulu.
 
Heri ya X-mas na mwaka mpya wadau.


Pamoja na kwamba nakubaliana kabisa na Dr. Slaa kwamba Mh. Mkapa hana kinga... kulingana na kipengele cha katiba kwenye mambo aliyofanya binafsi...

Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...

Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...

Over and Out
 
Heri ya X-mas na mwaka mpya wadau.


Pamoja na kwamba nakubaliana kabisa na Dr. Slaa kwamba Mh. Mkapa hana kinga... kulingana na kipengele cha katiba kwenye mambo aliyofanya binafsi...

Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...

Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...

Over and Out

Kama huna cha kuandika si bora ukae kimya!
 
Kama huna cha kuandika si bora ukae kimya!

Mimi pia sina mengi ya kuandika mkuu!Lakini niweke angalizo tu.Wakuu nyinyi endeleeni na mchakato wa kumburuza mkapa mahakamani na endeleeni kumshawishi Kikwete ili abadili msimamo wake.Lakini yote hayo yakikamilika basi mjiandae na kusambaratika kwa taifa la tanzania.
 
Kafara,
Shukran mkuu kwa taarifa hiyo, nimekusikia.. unajua tena habari za kusikia na usiri nchini ni vigumu kuwa na taarifa kamili..

Rev Kishoka,
Mkuu nadhani siku za nyuma tuliwahi kufikia hapo kuwa ni jukumu la Bunge letu kumsimamisha Mkapa badala ya kuwasubiri Hosea au Kikwete wapitishe uchunguzi, kulingana na Katiba...Lakini mpira umekuwa ukipigwa danadana muda wote hata hizi sahihi 20 za wabunge inakuwa kazi kuzipata.
Kila mtu akiogopa kurusha jiwe la kwanza na hata baadhi wabunge wa Upinzani wamekuwa Upande wa pili hivyo kufanya sheria hii kuwa ngumu kutumika kupitia Bunge kwa sababu nafikiri inatakiwa kitu kama 2/3 ya Wabunge kuelekea ushindi..
Na kibaya zaidi kuna watu wanaendeleza kampeni za kumwekea Kikwete na Hosea jukumu hili wakati ukweli umesimama kuwa hawa wawakilishi wetu ndio wenye matatizo. kwa mara ya kwanza nao wanasimamia maslahiu yao binafsi ndani ya Bunge...
Mwisho wakuu zangu ningeomba mwenye Kanuni za Uongozi na Maadili ya viongozi Kitaifa anirushie..


Mkandara,

Miongozo na kanuni za maadili ziko kule tume ya maadili ambako kina Lipumba wlaipoenda kuomba kuona madaftari yaliyosajili mali za viongozi walikataliwa!
 
Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...Over and Out

- Mkuu Kasheshe, sometimes huwa sikuelewi sana, tunasema hivi Mkapa afikishwe Kisutu tena haraka sana, halafu in the process kama kuna rais mwingine wa zamani naye alipora mali za wananchi naye pia aburuzwe, kama hayupo basi familia yake iburuzwe, I mean taifa gani linasambaratishwa na wezi kufikishwa kwenye sheria?

- Hivi hivi vitisho mnavitoa wapi kwamba huyu Mkapa is so big kwamba akienda kwenye sheria kwa wizi wake wa kupora mali za taifa, basi taifa zima litasarambatika what a nonesense? Taifa linatakiwa kuwa imara kwa kusimamia sheria, sasa ukiona taifa linasambaratika kwa kusimamia sheria, maana yake ni moja tu halikuwa taifa anyways form the begining, sitaki kuamini kuwa that is the case na taifa letu!

Kuwapeleka Yona, Mramba, na Mgonja Kisutu, bila Mkapa ni waste of our national time na hasa our taxpayers money, Mkapa ni lazima aburuzwe Kisutu kama ni kusambaratika so be it itakuwa on our bloods!
 
FMES Kwa kweli Dk Slaa anastahili kupewa nafasi ya kugombea Urais huko CHADEMA amekuwa ni mwiba mkali dhidi ya mafisadi wote ndani ya chama na serikali pamoja na vitisho mbali vya kumfungulia mashtaka hata kuchukua uhai wake, lakini wakati mwingine nahofia kama hakupata nafasi hiyo basi Watanzania tutapoteza mtu muhimu sana ndani ya bunge letu. Kama kampeni zake zikiandaliwa vizuri katika kila kona ya nchi yetu na CCM haitatumia vyombo vya dola kumshinikiza na kumzuia kufanya kampeni zake basi ataibuka mshindi wa Urais.

Bubu, hizi stories za kumshtaki Mkapa ni porojo tu. Bahati mbaya sana hata wasomi hawagundui kuwa ni porojo. Kwa Rais wa nchi ile yetu, hakuna anayefanana na Mkapa so far. Watu wote wanaangalia kwenye ANBEN, KIWIRA na source ya UFISADI ila hawaangalii kuhusu uchuni ya nchi yetu na mabadiliko ya haraka sana Tanzania kipindi chake.

Binafsi, so far sijamuona rais kama Mkapa kwa Tanzania. Mkapa was the best president of TZ and and will remain so in records for many years. Hakuna kuchekacheka na very serious person. Of course bila kuwa kama vile tusingeweza hata kuc-chat hapa kwenye JF. Ali-open up kila kitu, vingine vinawafanya watu wajichanganye kwa vile wao wanataka. Mimi nashauri kuwa alitakiwa apewa another 10 years watu wajue uchumi imara maana ni nini!.


Zaidi ya hiyo, hizi politics za bei ya vitu kwa investors, by the way sijui kama watu wamewahi kujiuliza watu kama Abrahamovich na na mwenzake mwenye kampuni ya Yukos walinunua kwa bei gani zile kampuni kule Russia na kwanini?! How do we compare with Tanzania? Russia ni mfano mmoja, iko kibao, lakini Russia tunafanana kwa na uchumi wa aina moja (state controlled) kabla ya collapse ya USSR.


Mambo ya mafisadi, hata Kikwete akiondoka tutawaona wengi tu. Mbona enzi za mwinyi kulikuwa kuchafu zaidi lakini kwa kuwa press freedom ilikuwa ndogo hatukuweza kujua na kufanya kama sasa. Unakumbuka ambushi ya Mrema airport na yake majina? Umewahi uliza whose names were they?

Mimi nadhani tusiwe na jazba tu kuwa Mkapa aende mahakamani. Tujumuishe mambo kadhaa ambayo ni mazuri. Vinginevyo tunaweza jikuta tunashangilia tu kama soccer fans ambao kila wakati wanategemea team yao ishinde. Ikishindwa unafukuza coach!
 
- Mkuu Kasheshe, sometimes huwa sikuelewi sana, tunasema hivi Mkapa afikishwe Kisutu tena haraka sana, halafu in the process kama kuna rais mwingine wa zamani naye alipora mali za wananchi naye pia aburuzwe, kama hayupo basi familia yake iburuzwe, I mean taifa gani linasambaratishwa na wezi kufikishwa kwenye sheria?

- Hivi hivi vitisho mnavitoa wapi kwamba huyu Mkapa is so big kwamba akienda kwenye sheria kwa wizi wake wa kupora mali za taifa, basi taifa zima litasarambatika what a nonesense? Taifa linatakiwa kuwa imara kwa kusimamia sheria, sasa ukiona taifa linasambaratika kwa kusimamia sheria, maana yake ni moja tu halikuwa taifa anyways form the begining, sitaki kuamini kuwa that is the case na taifa letu!

Kuwapeleka Yona, Mramba, na Mgonja Kisutu, bila Mkapa ni waste of our national time na hasa our taxpayers money, Mkapa ni lazima aburuzwe Kisutu kama ni kusambaratika so be it itakuwa on our bloods!


Mkuu hapa umenena. Ukweli ni kwamba mimi ni-admirer wa Ben, nampa credit nyingi sana kwa jinsi alivyoendesha utawala kwa kipindi chake, hasa miaka mitano ya kwanza na miaka michache ya kipindi chake cha pili, ni fact kuwa alibadilisha mambo ambayo kwa muda mrefu tuliendesha ki-komunisti na kiswahili. Lakini hii haina maana kuwa aachwe eti kwa sababu alikuwa rais. Mkapa akifikishwa mahamani kwa kusimamia EPA na ujinga mwingine wote kama kujiuzia Kiwira, kuuza nyumba kwa bei ya kutupa, kuua watu Zanzibar na mengine mengi, kwanza atakuwa amepata anachostahili, na pili itakuwa ni precedence nzuri, na kwa wengine watakaokuwa marais watajua kuwa Urais sio kinga ya kufanya maovu na kuwaona wengine wajinga. Kumfikisha Mkapa mahakamani hakutasababisha kusambaratika kwa taifa, ila kutawasambaratisha mafisadi maana yeye kwa sasa ndio kigogo wao, kama yeye akifikishwa tu hakutakuwa na sababu ya wengine kushindwa kuwafikisha huko.
 
Bubu, hizi stories za kumshtaki Mkapa ni porojo tu. Bahati mbaya sana hata wasomi hawagundui kuwa ni porojo. Kwa Rais wa nchi ile yetu, hakuna anayefanana na Mkapa so far. Watu wote wanaangalia kwenye ANBEN, KIWIRA na source ya UFISADI ila hawaangalii kuhusu uchuni ya nchi yetu na mabadiliko ya haraka sana Tanzania kipindi chake.

Binafsi, so far sijamuona rais kama Mkapa kwa Tanzania. Mkapa was the best president of TZ and and will remain so in records for many years. Hakuna kuchekacheka na very serious person. Of course bila kuwa kama vile tusingeweza hata kuc-chat hapa kwenye JF. Ali-open up kila kitu, vingine vinawafanya watu wajichanganye kwa vile wao wanataka. Mimi nashauri kuwa alitakiwa apewa another 10 years watu wajue uchumi imara maana ni nini!.


Zaidi ya hiyo, hizi politics za bei ya vitu kwa investors, by the way sijui kama watu wamewahi kujiuliza watu kama Abrahamovich na na mwenzake mwenye kampuni ya Yukos walinunua kwa bei gani zile kampuni kule Russia na kwanini?! How do we compare with Tanzania? Russia ni mfano mmoja, iko kibao, lakini Russia tunafanana kwa na uchumi wa aina moja (state controlled) kabla ya collapse ya USSR.


Mambo ya mafisadi, hata Kikwete akiondoka tutawaona wengi tu. Mbona enzi za mwinyi kulikuwa kuchafu zaidi lakini kwa kuwa press freedom ilikuwa ndogo hatukuweza kujua na kufanya kama sasa. Unakumbuka ambushi ya Mrema airport na yake majina? Umewahi uliza whose names were they?

Mimi nadhani tusiwe na jazba tu kuwa Mkapa aende mahakamani. Tujumuishe mambo kadhaa ambayo ni mazuri. Vinginevyo tunaweza jikuta tunashangilia tu kama soccer fans ambao kila wakati wanategemea team yao ishinde. Ikishindwa unafukuza coach!

Mimi ni yule ambaye naona Mkapa hakufanya lolote kuleta maendeleo kwa Watanzania walio wengi kama alivyojitajirisha yeye mwenyewe, mafisadi wachache na wageni waliojifanya 'wawekezaji'. Kamwe fisadi Mkapa hawezi kuwa the best president of Tanzania hizi ni alinacha tu, itakuwaje fisadi aliyekuwa busy kutuibia na kutufisadi, kuwaona wazungu ni bora kuliko Watanzania kumbuka kasheshe la Net Group, kusaini mikataba isiyo na maslahi kwa nchi yetu awe ni the best president wa Tanzania. Mwizi kamwe hastahili kupewa sifa kama hizo.

Nadhani niko na Watanzania wengi katika hili. Alitumia uhuni wa kututukana Watanzania kwamba tuna wivu kuona mtu kajipatia vijisenti vyake tunadhani ni mwizi na pia ni wavivu kumbe wakati huo huo yeye na mafisadi wenzie akina Mramba, Yona, Chenge, Magufuli walikuwa busy kutupora nyumba zetu, kusaini mikataba ya uchimbaji wa dhahabu ambayo haikuwa na maslahi kwa nchi yetu na kuhakikisha mikataba hiyo ni siri, kukupua mabilioni ya pesa pale BoT, kusaini mikataba ya kifisadi ya kununua rada, ndege ya Rais, kujimilikisha Kiwira pamoja na kufanya biashara akiwa Ikulu.

Tuliambiwa na WB na IMF kwamba 'data' zilionyesha kwamba uchumi wa Tanzania wakati wa Mkapa ulikuwa kati ya 5% mpaka 7%. Uchumi hata wa Tanzania ukikuwa kwa asilimia hizo basi wananchi wataona ongezeko kubwa la ajira na mishahara kuongezeka kwa kasi lakini haikuwa hivyo bali IMF na WB pamoja na kummwagia sifa kem kem Watanzania wengi waliendelea kuishi maisha ya ufukara wa kutisha. Hata kama alileta mabadiliko ya haraka sana, kitu ambacho mimi sikubaliani nacho, Tanzania hatuna sheria inayosema kwamban kiongozi wa nchi anayeleta 'mabadiliko ya haraka sana' atasemehewa maovu yake yote ya kuwafisadi na kuwaibia Watanzania

Miezi michache iliyopita tuliambiwa na Pinda, Mwanyika na Mkuu wa polisi watu ambao wana nyadhifa za juu katika serikali na JK, kwamba mafisadi wa EPA ni matajiri wakubwa haiwezekani kabisa kuwafungulia mashtaka maana nchi ingewaka moto na kushindwa kuiongoza. Naam kwa kutumia maneno yako, kelele za Watanzania kuwafikisha mafisadi wa EPA nazo zilikuwa ni porojo tu ambazo hazikuwakosesha mafisadi usingizi. Lakini Watanzania hatukuchoka, kwa kupitia vyombo vyetu vya habari ikiwa ni pamoja na TV, Redio, magazeti na mitandao kelele zetu zikazidi kupamba moto siku hadi siku na hatimaye mafisadi wa EPA mmoja baada ya mwingine wameanza kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao.

Hivyo basi na hizi porojo za kumfungulia mashtaka fisadi Mkapa zinaweza kabisa kuzaa matunda ikiwa Watanzania tutaendelea na kelele zetu kila kukicha kuhakikisha kwamba katika nchi yetu hakuna yeyote yule aliye juu ya sheria. Kama keba, kafanya ufisadi dhidi ya Watanzania basi ushahidi dhidi yake ukusanywe na afunguliwe mashtaka na hapo sheria iachwe ifuate mkondo wake. Naam sheria ni msumeno huwaathiri wakubwa na wadogo bila kujali nyadhifa zao za sasa au zilizopita.

FISADI NI ADUI WA MAENDELEO YA TANZANIA. KAMWE TUSIMUONEE AIBU FISADI WALA KUMUOGOPA~BAK
 
Haya ni baadhi ya mambo yaliyofanywa na Mkapa kuifisadi nchi yetu ambaye wewe unamuona ni best president in Tanzania na alileta 'mabadiliko ya haraka' sijui ni mabadiliko gani maana hayakugusa maisha ya kila siku ya Watanzania walio wengi.

Revealed: Tanzania`s shocking vast wealth

2008-08-31 09:07:51
By Staff Writer

As massive poverty continues to rock the majority of Tanzanians, the latest data reveal that Tanzania`s wealth in terms of the top five metals out of eleven provable mineral deposits amounting to millions of tonnes.

It is hard to believe it, but that is the reality in a country where 38million plus population lives in abject poverty, below a dollar per day, while 89percent of the total population survive on a single meal per day.

According to a geological survey conducted last year by the ministry of energy and minerals, Tanzania has huge reserves in eleven key minerals which include gold, Nickel, Tanzanite, Diamonds, copper, Iron ore, coal, Limestone, soda ash, gypsum and phosphate.

The five key minerals and their provable amounts in brackets is Gold (2,222tones), Nickel (209million tones), Diamonds (Carat 50.9million), Copper (13.65million tones), and Iron ore (103million tones).

However since this was just a geological survey undertaken by experts last year, its actual result is approximated to be accurate by up to 70 percent.

So far, only three types of minerals - gold, diamonds, Tanzanite - are being fully mined by multinational companies which at the end of the day take 97percent, leaving only peanut to the original Tanzanian owners.

If well managed through sound, people-centered mining policies, the mining sector can catapult Tanzanians to the proverbial promised land in decades and generations to come.

Comparing these huge deposits and the actual situation of poverty in the country, the message that comes across one`s mind is that Tanzania is in what experts describe as `resource curse`.

The term `resource curse` refers to the observation that nations with rich endowments of natural resources (oil, metals, timber) often dramatically under-perform economically relative to what one would expect.

Common sense and simple economics suggest that countries blessed with an abundance of natural resources should live long and prosper.

Yet over many years, it has been observed that nations rich in oil, gas, or mineral resources have been disadvantaged in the drive for economic progress.

Why are we poor?

Perhaps the biggest question that begs an urgent answer is; why are we so poor despite having all these huge minerals deposits?

It is a question that policy makers and politicians have been avoiding to seek answers for.

Tanzania like many other African countries is highly blessed with rich natural resources, but its people are swimming in the deep sea of massive poverty.

But the appalling truth is that instead of financing people`s development, Africa's huge mineral resources were used to fund the brutal civil wars that ravaged millions of people during the past four decades.

Today in Africa only a few countries like Botswana, Ghana and South Africa have managed to use their natural resources, especially minerals, to facilitate development and welfare to their people.

This example is vividly manifested in the Democratic Republic of Congo, Sierra Leone, Ivory Coast, Nigeria, Sudan and Angola whereby masters of the wars used natural resources to finance their deadly power struggle.

However in Tanzania, there wasn`t any civil war apart from the role played by the founding President, (the late) Dr Julius Nyerere, in liberating Southern African countries during the nationalist struggle.

While it is an undeniable truth that the move to allow the private sector to participate in the mining industry was brilliant one, the truth is that due to poor policies introduced by the third phase government, the whole idea has become a disaster to Tanzanians.

This is well echoed in the lucrative mining industry which has been mainly benefiting multinational companies, while paying the government a small slice of the cake.

Last year, for instance, the Minister for Energy and Minerals, William Ngeleja, told the parliament that during the period between 2001 and 2006, Tanzania produced gold worth $2.6 billion (Tshs3.38 trillion), but the government earned only $78 million.

In simple arithmetic, this is just 3 percent of the total revenues generated from thousands of tonnes of gold produced in the Lake Victoria gold belt. It also shows that the government earned an average of $13 million annually during that period from the multibillion industry whose real investments currently is valued at $2.5 billion.

According to the available statistics from the mining industry, from June 2000 to December 2006, the two biggest gold mines in the country produced a total of 5,686,710 ounces of gold, which at the current gold price of $600 per ounce is valued at Tshs 4.3 trillion ($ 3.3 billion), but what the nation earned is frightening and a shame.

While mineral production has increased in Tanzania in the past few years with export per year estimated to be nearly $900 million (Tshs1.17 trillion), the contribution of the mining sector to the Gross Domestic Product (GDP) remains very minimal, accounting to 3 percent.


According to the National Economic Survey report released in 2006, the growth rate of mining and quarrying sector increased from 15.4 percent in 2004 to 15.7 percent in 2005, whereby the increment was attributed to new investments in Tulawaka gold mines in Biharamulo District, Kagera Region.

The report further states that, the contribution of the sector to GDP, which is the total value of goods and services produced in a country during a year, increased from 3.2 percent in 2004 to 3.5 percent in 2007.

We would like to hear from you about this story; what you think the problem is, and what needs to be done. Send your comments through sundayguardian@guardian.co.tz

 
Back
Top Bottom