Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

1.
Bubu, hizi stories za kumshtaki Mkapa ni porojo tu. Bahati mbaya sana hata wasomi hawagundui kuwa ni porojo. Kwa Rais wa nchi ile yetu, hakuna anayefanana na Mkapa so far.

- One point uko right ni kwamba hakuna anayefanana na Mkapa kwa uporaji wa mali za wananchi bila aibu, baada ya Yona, Mramba na Mgonja kwenda Kisutu, hakuna porojo tena mkuu sasa ni kazi tu, na wote mpaka watafika huko hili kwa sasa halina ubishi na Mkapa analijua wazi sana.

2.
Watu wote wanaangalia kwenye ANBEN, KIWIRA na source ya UFISADI ila hawaangalii kuhusu uchuni ya nchi yetu na mabadiliko ya haraka sana Tanzania kipindi chake. Binafsi, so far sijamuona rais kama Mkapa kwa Tanzania. Mkapa was the best president of TZ and and will remain so in records for many years. Hakuna kuchekacheka na very serious person.

- What a point, kwamba kwa sababu Mkapa aliinua uchumi, kitu ambacho kilikuwa ni kazi yake anyways as rais, basi asiguswe na sheria mkuu basi tubadili katiba ya Jamhuri, mwananchi yoyote aliyewahi kulifanyia mema taifa letu akivunja sheria asiguswe. Hizo records ziko wapi na ni nani anyeziandika na kuzitunza kwamba Mkapa was the best ever president sasa kama anaamini hayo kwa nini asijitokeze na kuweka record straight kwamba yeye ameiba lakini alikuwa ni the best! Huyu ni mwzi tu mkuu ametuibia wananchi wa Tanzania anastahjili kutinga Kisutu na it is coming hana ujanja!

3.
Of course bila kuwa kama vile tusingeweza hata kuc-chat hapa kwenye JF. Ali-open up kila kitu, vingine vinawafanya watu wajichanganye kwa vile wao wanataka. Mimi nashauri kuwa alitakiwa apewa another 10 years watu wajue uchumi imara maana ni nini!.

- Hapana labda miaka 10 jela na arudishe mali za umma, ya ku-open ni ya Mwinyi yeye alijaribu kutumia maguvu kuzima freedom of speech, unasema aliyoyafanya Pemba ndio ku-open up? I mean ni haki yako kumtetea Mkapa lakini tafuta hoja nzito basi sio hizi za ku-open up maana huwezi kufanya openup kwa kuua wananchi wasio na hatia eti kwa sababu hawakubali hoja zako tu!

3.
Zaidi ya hiyo, hizi politics za bei ya vitu kwa investors, by the way sijui kama watu wamewahi kujiuliza watu kama Abrahamovich na na mwenzake mwenye kampuni ya Yukos walinunua kwa bei gani zile kampuni kule Russia na kwanini?! How do we compare with Tanzania? Russia ni mfano mmoja, iko kibao, lakini Russia tunafanana kwa na uchumi wa aina moja (state controlled) kabla ya collapse ya USSR.

- Tunataka Mkapa akajibu tuhuma zake kwenye sheria ya Russia hayana ushusiano wowote na wizi wake Mkapa kwa mali zetu wananchi wa Tanzania, kama unayosema ni legally utetezi wa Mkapa, basi msaidie kujipanga lakini ya Russia hayatuhusu kabisaaa na wala hayafanani.


4.
Mambo ya mafisadi, hata Kikwete akiondoka tutawaona wengi tu. Mbona enzi za mwinyi kulikuwa kuchafu zaidi lakini kwa kuwa press freedom ilikuwa ndogo hatukuweza kujua na kufanya kama sasa. Unakumbuka ambushi ya Mrema airport na yake majina? Umewahi uliza whose names were they? Mimi nadhani tusiwe na jazba tu kuwa Mkapa aende mahakamani. Tujumuishe mambo kadhaa ambayo ni mazuri. Vinginevyo tunaweza jikuta tunashangilia tu kama soccer fans ambao kila wakati wanategemea team yao ishinde. Ikishindwa unafukuza coach!

- Mwinyi kama ana makosa yachunguzwe na yasemwe wazi na aende Kisutu pia, never before uhuru wa habari kama kipindi cha Mwinyi maana kile ni kipindi tulijua hata amri zilizokuwa zikitolewa na mkewe Mama Sitti, lakini sio siri hata Mama Anna kuna wakati alikua akitoa amri kwa taifa huko nyuma lakini hatukujua, lakini ya Mama Sitti hata Mwalimu alituambia wazi, sasa Mwinyi ndiye hasa aliyekua baba wa demokrasia na hana mfano.

- Sheria ni lazima ichukue mkondo wake, Mkapa ni lazima afike huko kama kweli tunataka kusafisha ufisadi, maana yeye ndiye baba wa ufisadi wa high level ambao Tanzania hatukuwahi kuwa nao before na naomba kurudia kwamba ni waste of time kuwafikisha kina yona, Mramba na Mgonja kwenye sheria bila kiongozi wao Mkapa, sasa kama kudai sheria ichukue mkondo wake ni kuwa na jazba so be it!.


Mungu Aibariki Tanzania.
 
- Mwinyi kama ana makosa yachunguzwe na yasemwe wazi na aende Kisutu pia, never before uhuru wa habari kama kipindi cha Mwinyi maana kile ni kipindi tulijua hata amri zilizokuwa zikitolewa na mkewe Mama Sitti, lakini sio siri hata Mama Anna kuna wakati alikua akitoa amri kwa taifa huko nyuma lakini hatukujua, lakini ya Mama Sitti hata Mwalimu alituambia wazi, sasa Mwinyi ndiye hasa aliyekua baba wa demokrasia na hana mfano.

- Sheria ni lazima ichukue mkondo wake, Mkapa ni lazima afike huko kama kweli tunataka kusafisha ufisadi, maana yeye ndiye baba wa ufisadi wa high level ambao Tanzania hatukuwahi kuwa nao before na naomba kurudia kwamba ni waste of time kuwafikisha kina yona, Mramba na Mgonja kwenye sheria bila kiongozi wao Mkapa, sasa kama kudai sheria ichukue mkondo wake ni kuwa na jazba so be it!.


Mungu Aibariki Tanzania.

Naam hakuna yeyote anayestahili kuwa juu ya sheria ndani ya nchi yetu. Wote wailofanya madudu ya kuiangamiza nchi yetu wachunguzwe na kama kuna ushahidi tosha dhidi yao basi wafunguliwe mashtaka haraka sana. Hii itasaidia kuleta maendeleo ya kweli ndani ya nchi yetu na viongozi kuwa na maadili mema ya uongozi badala ya kukimbilia uongozi ili wakajitajirishe kwa kuwafisadi Watanzania. Tunapata mikopo na misaada chungu nzima toka nchi mbali mbali, tuna rasilimali chungu nzima ndani ya nchi yetu lakini mwaka wa 47 sasa bado Watanzania walio wengi wanaishi maisha ya ufukara wakati mafisadi wachache the so called viongozi wanakuwa na utajiri wa kupindukia bila woga wala hata aibu. Enzi za kuwaabudu viongozi wezi na mafisadi kama wafalme zimeshapitwa na wakati.
 
Waheshimiwa ashakum simatusi, kwawale wenye huruma nadhani hata mama Tereza wa kalkata angekuwapo leo basi angeshindwa kumsamehe mtu aliekamilisha matendo ya Kijambazi kama ya Mkapa. Kuaminiwa na taifa pekee ni hadhi tosha ya kukutia unyenyekevu na kukujengea busara. ukakabidhiwa wadhifa wa Rais ; Hadhi,heshima,taadhima pamoja na mengine mengi POWER ya kuwa Alfa na Omega wa Taifa ukamua KUIABUZ bila woga wala huruma. pamoja na hayo ukilipwa mshahara na marupurupu chungu,sasa hatujui alitaka nini? ndio mana tunamhitaji mahkamani akajieleze ,kama hoja zake zitaitosheleza sheria tutamalizana nae, nakama hakuitosheleza awajibishwe.
Nakumbusha: tuna utamaduni wa kumtunza afanyae mazuri na kumuadhibu afanyae mabaya na anaeomba radhi au alietenda bila kukusudia huweza kusamehewea. Na pia kuna mizani kati ya mazuri na mabaya uliyotenda na hilo hata mbele ya Mungu, kuna thawabu na dhambi. Orodha ya dhambi za Mkapa kwa taifa zinaelekea kuwa wazi. Orodha ya thawabu imesimama katika uchumi ambao baada ya kuujenga, kama aliujenga, akaishia kuukwapua yeye mwenyewe na wapambe wake. baadhi ya wapambe wembe unasogea vichwani Mkapa ataarishe kichwa kwa kutia maji. kumbukeni hatuzungumzii kumpiga mawe au kumfunga tairi na kumtia moto kama mwizi wa mitaani La ,tunampa haki yake ya katiba, kumfikisha mbele ya sheria
 
Heri ya X-mas na mwaka mpya wadau.


Pamoja na kwamba nakubaliana kabisa na Dr. Slaa kwamba Mh. Mkapa hana kinga... kulingana na kipengele cha katiba kwenye mambo aliyofanya binafsi...

Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...

Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...

Over and Out

Mimi pia sina mengi ya kuandika mkuu!Lakini niweke angalizo tu.Wakuu nyinyi endeleeni na mchakato wa kumburuza mkapa mahakamani na endeleeni kumshawishi Kikwete ili abadili msimamo wake.Lakini yote hayo yakikamilika basi mjiandae na kusambaratika kwa taifa la tanzania.



Nina imani kuwa tutajenga taifa imara sana kama tukianza na kumshitaki Mkapa, kwa vile tutarudi kwenye msingi wa sheria mama kuwa "NO ONE IS ABOVE THE LAW"



Kusema taifa litasambaratika ni sawa na kusema kuwa kuna watu wengi wanasapoti aliyofanya mkapa. Sidhani kama hiyo ni kweli, kwa vile Mkapa hakujenga utaifa wa nchi bali aliubomoa; ni tofauti kidogo kama ingekuwa ni Nyerere anashitakiwa kwa sababu alitaifisha shule za watu binafsi kwa ajili ya manufaa ya Taifa zima.
 
Mwanjelwa,
Utanisamehe mkuu lakini nadhani hufahamu nini maendeleo!..Kwani kila nchi zote duniani zimepiga hatua fulani hata Haiti ambayo ilikuwa ya mwisho.. Na ktk maendelo hayo Tanzania imekuwa ikirudi nyuma kila mwaka ukilinganisha na nchi nyingine..
Unachotazama wewe kama maendeleo ni kukua kwa umri wa nchi yetu. Ni sawa na kumwona mtoto uliyemwona miaka kumi iliyopita ukitegemea angebakia ktk urefu ule ule..
 
Rev. Kishoka,
Kwa hiyo hakuna uwazi kwa wananchi ktk kuziona hizo kanuni na maadili ya viongozi!..damn, hata hivyo namshukuru sana Dr. Slaa kwa kunielewa kwamba kazi hii sio ya Kikwete wala Hosea ni kazi yao kisheria kwani kinachohitajika ni sahihi 12 kisha 2/3 ya Wabunge kuafiki.
Hata kama tutashindwa, hao wabunge watakaopinga maombi ya wananchi walio wengi watapata malipo yao halali uchaguzi wa 2010..Changamoto ni huo uwezo wa kumjadili rais Mstaafu bungeni kwa makosa ya utumiaji vibaya madaraka yake inatosha kuwa somo kwa viongozi wengine!..
 
Heri ya X-mas na mwaka mpya wadau.


Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...

Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...

Over and Out


Huu ni upuuzi ambao tunaupiga vita. kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa my foot!!!
 
Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Nasema mie simo na tuendelee kumuombea Dr. Slaa!
 
Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Nani anatumiwa na nani? Naamini hakuna wajinga humu.


Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Hii ni theory kutoka wapi? Prove it.
 
Heri ya X-mas na mwaka mpya wadau.


Pamoja na kwamba nakubaliana kabisa na Dr. Slaa kwamba Mh. Mkapa hana kinga... kulingana na kipengele cha katiba kwenye mambo aliyofanya binafsi...

Sikubaliani na Mtanzania yeyote yule ambaye anadhani kumshitaki Mkapa ni sawa na kumshitaki kiongozi mwingine...

Angalieni mbali wakuu... kwa ajili ya usalama na utengamano wa Taifa... naomba Mkapa asipelekwe Mahakamani hata kama ametenda makosa...

Over and Out

Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Nasema mie simo na tuendelee kumuombea Dr. Slaa!


......................b/s&^%$%$!^$()@#&(*)$@_)$@)$%^&&*^T&*&^*&&*$#$$$%#$#@$@#@$#
 
Mwanzoni nilipokuwa nikiwasoma akina Mukandara, FMES, Bubu ataka kusema na wengine kwa kweli nilivutiwa sana na michango yao. Kwa nini nilivutiwa ni kwa sababu ilikuwa inalenga kuukosoa mfumo wa utawala uliopo katika nchi yetu ili kujenga mfumo wa utawala bora. Lakini muda unavyozidi kwenda naona na wao wametumbukia kule kule kwenye msimamo kwamba yule ambaye hatumpendi lazima tumsishikie bango mpaka akome. Kwa mfano Mkapa alikuwemo kwenye ile orodha ya watu wa aibu katika Tanzania. Na mtu mwingine aliyekuwepo kwenye orodha ni Kikwete. Lakini bado watu wanataka Kikwete huyo huyo amshike mwenzie hiyo inachekesha sana.

Kuna usemi usemao mwizi akiibiwa huwa mkali sana. Sasa kama mnataka kuwa na mfumo bora na sheria zifuate mkondo wake kwa nini akina Slaa wasiwafikishe wale wote waliowataja pale Mwembe Yanga. Vinginevyo kumshikia bango Mkapa ni kuonekana kama Mkapa haters basi.

Tukienda mbli zaidi ni kwamba CCM imeichukulia nchi kama shamba la bibi. Haitaki katiba mpya ambayo itahakikisha kuwa kuna utawala bora na rasilimali za nchi zinatumika ipasavyo. Watu wamejirundikia madaraka matokeo yake kila mtu ana anajipendekeza kwa mwenye madaraka. Akiondoka ndiyo tunaanza kudeal na aliyeondoka. Hivi kwa nini nchi iwe ya watu wanaodeal na post mortem cases tu. Hivi tumeshakaa chini na kuangalia kwa mfano viongozi wa sasa hivi wamekula shilingi ngapi za nchi?. Hatuangaliii kwa sababu hatutaki kuwaharibia kwa kuwa tunawapenda sana. Njia nzuri ni kuhamishia kwa wale tusiowapenda. Mimi ushauri wangu ni kwamba kama Slaa anataka kudeal na hii issue squarely deal na ile list yako of shame.

Kwa wachangiaji wengine mimi naona tuache kuwapa nafasi wanasiasa walioko madarakani watulize vizuri. Wakati wa Mwinyi tuliangalia ukandamizaji wa Nyerere kumbe Mwinyi anaharibu nchi mpaka ikashindwa kukusanya kodi. Wakati wa Mkapa tuliangalia udhaifu wa Mwinyi kumbe Mkapa na washikaji zake wakawa wanakomba mali. Wakati wa Kikwete tunaangalia ushenzi wa Mkapa kumbe akina Kikwete na wenzie wanakula hela kwa trip zisizo macho wala masikio. Tutasubiri raisi mwingine ili tuanze kudeal na Kikwete. Hapa kweli mara nyingine inauma sana. Let's be people of today. Viongozi wetu wawajibike sasa siyo masuala ya historia.
 
Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Nasema mie simo na tuendelee kumuombea Dr. Slaa!

Mkuu Gembe.. hayo mawazo ya mwaka 47 hayafai kwa 2009!!! Watanzania wa enzi hizo wa kudanganywa kwamba bila CCM taifa litayumba si waleo ndugu, Watanzania wa leo si wale wa kutishiwa kwamba Mwizi Mkapa akishitakiwa kwa wizi wake nchi itayumba, Kwa taaarifa yako ni kwamba Mkapa akishitakiwa, watanzania watazidi kushikama kwa furaha kubwa watachapa kazi kwa uaminifu na Taifa litasonga mbele. Tena hata wale ambao walikuwa na ka mpango ka kufanya madudu kama Ya mkapa wataacha maramoja kwa kuogopa sheria kuwa juu yao.

Kwa mtaji huu nahimiza sheria ichukue Mkondo wake maramoja! bila kuleta longo longo la Mungu watu.. eti wakishitakiwa Taifa halipo. Hatutaki U Mugabe hapa wacha wakinywee kikombe chao.
 
Nani anatumiwa na nani? Naamini hakuna wajinga humu.

Dr. Slaa,
anatumiwa na wanasiasa uchwara,yeye pia mwenyewe anaendeleaza siasa za kuachafuana na kutafuta nani mchawi badala tya kueleza sera za CHADEMa ni zipi.Mie nashangaa siasa za nchi hizi masikini watu wanakuwa washabiki wa mtu anayesahbikia kutoa mafisadi bila hata kujua ana mbinu zipi za maendeleo!

Siyo vyema kuanza kupelekena mahakamani kwa makosa ambayo walifanya viongozi wetu wakubwa ambao wana heshima kubwa mbele ya jamii.Na hata Jk alisema Msumbuji.

mie nawashangaa watu wa aina ya kichuguu,wanakuwa washabiki wamambo ambayo hayana faida kwao.If you know how nchi hii inavyoongozwa utajiona wewe unakosea sana.Kuna watu wamepandikizwa kwenye vyama vya upinzani na kwa taarifa yako saiasa nchini mwetu ni usanii mtupu

Hii ni theory kutoka wapi? Prove it.



Mwalimu nyerere alishasema Bila CCM madhubuti nchi itayumba!
 
Kwa mtaji huu nahimiza sheria ichukue Mkondo wake maramoja! bila kuleta longo longo la Mungu watu.. eti wakishitakiwa Taifa halipo. Hatutaki U Mugabe hapa wacha wakinywee kikombe chao.

Sheria ipi?Mie nashangaa hoja ya slaa,sheria ya kinga ya rais ipo kikatiba so mpaka katiba ibadilishwe na hata ikibadilishwa itaanza kutumika kwa mwaka huo hivyo hautaweza kumshtaki Mkapa Tena na ninavyoijua CCM ya sasa watakubali kubadilisha hicho kipengele ili kuwaridhisha na Mkapa hatashtakiwa!
 
Lakini muda unavyozidi kwenda naona na wao wametumbukia kule kule kwenye msimamo kwamba yule ambaye hatumpendi lazima tumsishikie bango mpaka akome. Kwa mfano Mkapa alikuwemo kwenye ile orodha ya watu wa aibu katika Tanzania. Na mtu mwingine aliyekuwepo kwenye orodha ni Kikwete. Lakini bado watu wanataka Kikwete huyo huyo amshike mwenzie hiyo inachekesha sana.

(a) Sidhani kama hapa ni swala la kumpenda au kutompenda Mkapa; kinachoongelewa hapa ni sheria za nchi. Afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomwandama, halafu mahakama itatoa haki. Kama tutawafunga wale tusiowapenda tu na kuwaacha tunaowapenda bila kujali makosa yao, basi hatuna haja ya kuwa na vyombo vya sheria kabisa. Ni kiasi cha kuwawekea alama watu wote tusiowapenda na kuwambia watangulie kwenda jela bila hata kuwafikisha mahakamani.

(b) Katika taratibu za kusimamia sheria, inapotokea wawili wametenda kosa, lakini hakuna ushahidi wa kutosha kuwatia hatiani, basi mwendesha mashitaka anaweza kumsamehe mmoja wa waharifu hao kusudi atoe ushahidi thabiti dhidi ya yule mwingine (plea bargain).
 
Mwalimu nyerere alishasema Bila CCM madhubuti nchi itayumba![/size]
It was the same Nyerere who said CCM siyo baba au mama yake. And for your info CCM madhubuti no longer exists. Ask Makamba.
 
Hii hapa inakandamizia mawazo yangu niliyoyatoa

Njia ya kupambana na ufisadi ni kuweka mifumo sahihi

Juvenalis Ngowi





HIVI majuzi rafiki yangu mmoja aliniuliza ni yapi maoni yangu kuhusu kufikishwa mahakamani kwa baadhi ya vigogo na wafanyabiashara kuhusiana na tuhuma za ufisadi.

Nilimwambia siwezi kutoa jibu sasa hadi nione mwisho wa kesi hizo lakini pia cha muhimu zaidi nataka kuona nini dhamira ya serikali kuchukua hatua hii kwa wakati huu.

Lengo la kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa ufisadi ni muhimu kwa kuwa inawezekana ikawa hakuna nia thabiti ya kupambana na ufisadi.

Kwa kuzingatia hili ndiyo maana nasema hatuwezi kukurupuka na kusema hatua iliyochukuliwa ni stahiki au la.

Itakumbukwa kwamba umaarufu wa Rais Jakaya Kikwete ulianza kushuka kwa kasi kubwa.

Wale wanaompenda sana rais wakaanza kutushawishi kwamba Rais Kikwete kama yeye ni maarufu ila serikali yake ndiyo imepoteza umaarufu.

Haya ni maajabu ya Musa. Iwezekaneje tawi ulilokalia lianguke lakini wewe usianguke?

Kelele dhidi ya wezi wa fedha za EPA zilikuwa nyingi kupita kipimo.

Je, kuwapeleka watuhumiwa mahakamani kulikuwa na lengo la kunyamazisha kelele zile?

Au kulikuwa kujaribu kurudisha umaarufu na heshima ya rais na serikali yake? Hapa hoja yangu ni moja, tunaweza kufurahi ikiwa lengo la serikali ni kupambana na ufisadi katika mapambano endelevu.

Ndiyo maana tunapomsikia katibu mkuu wa chama tawala akitutaka tufunge midomo linapokuja suala la EPA tunashindwa kuona kama kuna dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Tatizo moja la wanasiasa ni kusema wasichokiamini na kuamini katika wasichokipenda.

Naona ugumu mkubwa wa kupambana na ufisadi na sioni matumaini mbele. Siasa za sasa ni fedha. Ni rushwa.

Tutakuwa wanafiki kama hatutakubali kwamba fedha ndizo zimewaweka madarakani wengi wa wanaopigia kelele suala la rushwa.

Wanakosa uhalali wa kimaadili wa kukemea ufisadi kwa kuwa wao ni sehemu hiyo ya ufisadi.

Wapo waliopata nafasi ndani ya chama kwa kutumia fedha za rushwa. Wapo waliopata ubunge kwa kutoa rushwa. Niliwahi kuhoji uwezo wa baba aliyekutwa akidokoa mboga kuwakemea wanae wanapokosa adabu.

Tuna chama ambacho chaguzi zake zinafahamika kwamba zimetawaliwa na mlungula. Ilifika mahali hadi TAKUKURU wakaingilia kati na kufungua kesi ambazo sijui zimeishia wapi na vipi.

Yale yale ya EPA tunayoyaogopa. Isije ikawa ni kile kinachoitwa nguvu za soda. Kelele zimekuwa nyingi hivyo zizimwe kwa njia itakayoonekana na wengi kwamba ni njia sahihi.

Mwalimu wangu mmoja wa somo la Utawala wa Taasisi alikuwa akisisitiza kila mara kwamba njia sahihi ya kupambana na ufisadi si kutumia AK47.

Hapa alimaanisha kwamba ufisadi unaweza kushindwa kwa kutumia mfumo maalumu wa kiuongozi.

Hata ukikamata na kuwafunga watu 20 au 100 kama hujabadili mfumo wako kuzuia ufisadi, basi hautakwisha kamwe.

Kwa mfano tuna mfumo gani wa kuteua watendaji wetu? Tunasikia jinsia ikipewa nafasi ya kwanza katika uteuzi. Hii ni hatari sana. Tumewahi kuhisi pia uteuzi unaofanywa ili kuleta uwiano wa kikanda au udini. Hii ni hatari mno.

Tunahitaji mfumo ambao hautaruhusu wasiostahili kustahilishwa. Nafasi yoyote inapaswa apewe mtu anayestahili bila kujali jinsia, anatoka kanda gani au dini yake. Wigo wa uteuzi unapaswa kwenda mbali zaidi ya wale mliofahamiana shuleni, kazini au kwenye kampeni. Tunahitaji mfumo utakaoruhusu uteuzi wa nafasi bila kuzingatia mambo hayo, bali uwezo na uadilifu wa anayeteuliwa.

Wale waliokuwa wakisema kwamba umaarufu wa serikali umepungua lakini wa rais bado uko juu walikataa kutupa nadharia kwamba baadhi ya watendaji aliowateua bwana rais wameshindwa kutimiza wajibu wao.

Hawawezi. Lakini kama hivyo ndivyo, sisi tulio chini tunalazimika kumlaumu aliyeteua.

Yeye ndiye mwenye uwezo wa kuweka na kuondoa. Nakumbuka wakati wa mabadiliko ya baraza la mawaziri, baadhi ya watu walihoji kwa nini Andrew Chenge amerudishwa katika baraza la mawaziri, yeye mwenyewe akajibu akisema aulizwe aliyemteua. Hivi karibuni Yusuf Makamba alipotuhumiwa na wenzake kwamba ana mambo mengi, hivyo anashindwa kutumikia vema nafasi yake ya ukatibu mkuu, naye alitoa jibu linalokaribiana na Chenge, kwamba yeye amepewa hivyo vyeo na akamuuliza mwandishi yule, ‘ukipewa uhariri utakataa?’

Majibu ya watu hawa wawili yanatufanya tumlalamikie rais pale mambo yanapokwenda kombo kutokana na utendaji wa wateule wake. Yeye ndiye aliyewaweka na ndiye anayeweza kuwaondoa.

Lakini kama wengi wanavyosema, kuna haja ya kuwa na katiba mpya. Katiba hii inampa rais madaraka makubwa mno katika maeneo mengi.

Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba kama angetaka kuwa dikteta angekuwa hivyo kwani katiba inampa nguvu za ajabu. Tunapozungumzia mabadiliko ya katiba si kwa ajili tu ya kuwa na uchaguzi huru na wa haki kama wanavyolalamikia wapinzani, ila ni pamoja na kupambana na ufisadi. Kama kweli serikali ya sasa inataka kupambana na ufisadi na sisi tukubaliane nao kwamba kuna dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi, kuna ulazima wa kubadili katiba ili kuweka mfumo utakaodhibiti ufisadi.

Narudia tena, hatuwezi kupambana na ufisadi kwa kutumia mahakama na magereza.

Isitoshe hata mahakama na magereza vinaweza vikawa sehemu ya huo ufisadi. Tunaweza kupambana na ufisadi kwa kutumia mfumo (systems). Na hilo tulione katika marekebisho ya sheria na hasa katiba.

Nguvu ya kweli ya mbunge leo iko wapi? Wabunge wanapaswa kuidhibiti serikali lakini ukweli wanaweza kufanya hivyo? Gazeti la serikali liliandika kuhusu baadhi ya wabunge waliodaiwa kutofautiana na rais kuhusu namna anavyoshughulikia masuala ya EPA.

Tulishuhudia wabunge waking’aka na kudai wanachonganishwa na serikali yao. Tuna mfumo gani ambao utaondoa ufisadi ikiwa anayeidhibiti serikali anaogopa kuonekana anatofautiana na serikali?

Kazi ya Bunge inakuwa ipi? Angalia wanavyochangia bajeti bungeni. Wabunge wanaongea kwa uchungu mkubwa lakini mwisho wa yote wanasema wanaunga mkono mia kwa mia.

Tunahitaji mfumo tofauti, ambapo Bunge likigundua kasoro serikali inabanwa. Usishangae sasa wabunge wanaanza hata kukimbia wajibu wao wa kwanza wa kuibana serikali na badala yake wanataka wapewe fuko la fedha wakapeleke maendeleo wenyewe kwa wananchi wao. Huu ni uharibifu wa mfumo ambao kwanza tayari ni dhaifu katika kupambana na ufisadi badala ya kuuimarisha.

Lakini pia ni mfumo utakaotoa nafasi kubwa zaidi ya ufisadi. Hiki kitu kinachoitwa mfuko wa maendeleo wa jimbo unaacha maswali mengi kuliko majibu, lakini pia unaweka ugumu wa kudhibiti ufisadi, kwani aliyepaswa kuwa mchungaji naye anahitaji kuchungwa. Mbunge anapopewa mfuko wa fedha nani atamwajibisha?

Tunapoyatazama haya yote ndipo tunapoona wazi kwamba bado ni vigumu kushinda kesi ishirini na ushei hivi zilizofunguliwa zinazoweza kuonyesha dira ya mapambano dhidi ya ufisadi.

Hata pale ambapo sheria inatoa mwanya wa wabunge kuidhibiti serikali, bado naona Bunge halijafanya hivyo kwa kiwango kinachostahili.

Nimetoa mfano mmoja tu wa uchangiaji bajeti ambapo wabunge wanaeleza mapungufu mengi lakini mwisho wa yote wanaipitisha bajeti.

Hivi kuna haja gani ya kuwa na mjadala mrefu ambao kimsingi unatumia kodi za wananchi ikiwa katika mjadala huo hautaweza kubadili kile ambacho serikali ilishapanga kukifanya?

Lakini mfano mwingine unaoonyesha namna wabunge wetu wasivyotumia vema nafasi yao kama mfumo kudhibiti serikali na hasa ufisadi, ni pale wanapotumia nafasi yao ya kikatiba kuthibitisha uteuzi wa waziri mkuu anayekuwa ameteuliwa na rais. Ukweli ni kwamba kinachotokea pale ni tofauti na dhamira ya kifungu kile cha katiba.

Kila anayesimama anafanya kazi ya kumsifu, kumpamba na kumkweza aliyeteuliwa na kuomba wabunge wapige kura ya kuthibitisha.

Wanaosimama na kuchangia wanakuwa kama wana wajibu wa kumwombea mteule kura.

Kimsingi wale walipaswa wachokonoe, wajue udhaifu wake uko wapi. Upeo wake wa uelewa wa mambo, uwezo wake kiuongozi na kadhalika. Sicho tunachokiona katika jimbo letu.

Lazima tutengeneze na kuimarisha mifumo yetu ili iweze kupambana na ufisadi. Haina maana kusubiri watu wafisidi nchi yetu kisha tukimbie kuwalundika Keko.

Wanigeria kutoka kabila la Ibo wana msemo wao kwamba usihangaike kufunga mlango wa zizi wakati ng’ombe wameshaibwa.

Tuamke sasa tufunge milango ya zizi letu kabla ng’ombe wote hawajaisha zizini. Inawezekana tuna baadhi ya mifumo ya kudhibiti ufisadi lakini na yenyewe inaufisadi au inashindwa kutumia vizuri madaraka yake.

Sijabahatika kuangalia kwa kina mfumo wa utendaji wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Lakini hii ni kati ya ofisi nyeti na zenye uwezo mkubwa wa kupambana na ufisadi kimfumo kuliko kutumia PCCB, Idara ya Upelelezi wa Jinai na Mahakama.

Kama huyu akifanya kazi yake mapema tayari kutakuwa na mifumo ambayo udhibiti wa jinai ya rushwa itanaswa haraka hata bila kuunda timu na tume mbali mbali. Tutakapokuwa na mfumo unaozuia viongozi na watumishi kufisidi nchi, ndipo nitakapoanza kuona pambazuko katika vita ya ufisadi.

Chanzo cha habari: Tanzania Daima 28/12/2008
 
1. Mwanzoni nilipokuwa nikiwasoma akina Mukandara, FMES, Bubu ataka kusema na wengine kwa kweli nilivutiwa sana na michango yao.

2. Kwa nini nilivutiwa ni kwa sababu ilikuwa inalenga kuukosoa mfumo wa utawala uliopo katika nchi yetu ili kujenga mfumo wa utawala bora.

3. Lakini muda unavyozidi kwenda naona na wao wametumbukia kule kule kwenye msimamo kwamba yule ambaye hatumpendi lazima tumsishikie bango mpaka akome.

- Mkuu unapoteza muda bure tu na hizi rangi zako nakuona kwenye hii thread unavyojichanganya, huko nyuma ulisema Mama Kilango ndiye mwenye matatizo na Mkapa kwa sababu ya kukosa urais, na since then unabadilika rangi tu maneno yako ni yale yale ukadai hivi ni vita vya kifamilia,

- Sasa umefika huku, kwamba kuna tunaodai utawala bora lakini tuna chuki na Mkapa, kwa kudai sheria ichukue mkondo wake unadiriki kusema kwamba eti kwa sababu Mkapa amefanya mazuri kwa taifa akivunja sheria aachiwe tu, mkuu tunajua kua siku zote kwenye msafara wa Mamba sio ajabu kukuta makenge nao pia wamo.

Mkapa hajipendi mwenyewe maana angekua anajipenda asingepora mali za taifa akiwa Ikulu, sheria lazima ifuate mkondo wake kwenye hili hakuna suluhu.
 
Rev. Kishoka,
Kwa hiyo hakuna uwazi kwa wananchi ktk kuziona hizo kanuni na maadili ya viongozi!..damn, hata hivyo namshukuru sana Dr. Slaa kwa kunielewa kwamba kazi hii sio ya Kikwete wala Hosea ni kazi yao kisheria kwani kinachohitajika ni sahihi 12 kisha 2/3 ya Wabunge kuafiki. Hata kama tutashindwa, hao wabunge watakaopinga maombi ya wananchi walio wengi watapata malipo yao halali uchaguzi wa 2010..Changamoto ni huo uwezo wa kumjadili rais Mstaafu bungeni kwa makosa ya utumiaji vibaya madaraka yake inatosha kuwa somo kwa viongozi wengine!..

Labda wakisema ipigwe kura ya wazi hapo nahofia itashindikana. Lakini kama itakuwa kura ya siri Walah nakuambieni theruthi 2 zitafika. Naamini wabunge wengi wa CCM wamechukizwa na wizi huo, sema wasemee wapi wakati zimwi la nidhamu ya chama lime wakalia kooni? Ni wachache tu wenye kujitoa kama kina Kilango, mwakyembe wano weza kuhimili zimwi hilo na kusimamia wanacho kiamini
 
......................Hata kama alileta mabadiliko ya haraka sana, kitu ambacho mimi sikubaliani nacho, Tanzania hatuna sheria inayosema kwamba kiongozi wa nchi anayeleta 'mabadiliko ya haraka sana' atasemehewa maovu yake yote ya kuwafisadi na kuwaibia Watanzania


Sipingani na mawazo yako kwani kila mtu ana wazo na anatakiwa asikilizwe. Lakini nchi haiwezi kuendeshwa dreams za kila mmoja. Haiwezi kuwa nchi. Hata hivyo kurudi kwenye point yako hapo juu ....nadhani ndiyo maana sheria ya kwamba alichotenda Rais akiwa madarakani hakiwezi mpeleka mahakamani. Kipengere nadhani hakichatofuatisha issues za biashara, kampuni au hata kuua. Ila kinasema akiwa madarakani (I stand to be corrected here with a strong augument). Kwani wewe Bubu unadhani kwanini waliweka hii kipengere?!
 
Back
Top Bottom