Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Nimeachwa hoi na story hii!

Wana JF, nionavyo mimi tatizo si kufanya biashara.
Tatizo ni kufanyabiashara wakiwa ndani ya Ikulu.

Kumbe ndiyo maana mbio za kukimbilia Ikulu wakati wa uchaguzi huwa kali.

Inanikumbusha maneno ya Mwalimu Nyerere kwa wagombea urais; Mnakimbilia kwenda Ikulu, kwani kuna biashara gani?

Mwalimu angekuwa hai angejua sababu ya mbio za kukimbilia Ikulu!
 
Ibrah,
Mwalimu alizijua sababu za kukimbilia Ikulu. Ndio maana alitutahadharisha Watanzania tuwe makini tunapochagua viongozi. Tusiangalie tu sura na haiba ya mtu, lakini uwezo, mtazamo na vision ya kuwasaidia Watanzania, vitu ambavyo havipo leo miongoni mwa viongozi wetu.
 
Uwozo wa viongozi wetu kweli huwa unanitia kichefuchefu sana mpaka natamani nikimbie nchi ili nisiwe nasoma uwozo kama huu tena. Hata kwa mabepari wenyewe marekani, ukishakuwa kiongozi wa nchi unaachana kabisa na mambo biashara kuondoa conflict of interest. Kwetu sis watu wanatumia nafasi zao za uongozi kufungua biashara na kupata mikopo kutoka kwenye taasisi za serikali ambako wanajua kabisa kuwa hawatanyimwa kulingana na nafasi zao za uongozi; tabu kabisa hii.

Mwaka 1995, Nyerere alikuwa akimunadi Mkapa na kusema mtu huyu ni safi. Sijui kama kweli Nyerere alikuwa anamjua Mkapa.
 
Yebo Yebo,
Kinachoshangaza hata vyama vya upinzani havikupiga kelele wakati wizi wa nyumba za serikali unaendelea. Nyumba zile ziko katika prime areas. Bei yake ktk soko ni kubwa zaidi ya bei ambayo viongozi walijitwalia.

Ndiyo maana Mzee BWM akahakiksha hizo nyumba zauzwa na akajichagulia hiyo. Yawezekana pia alikuwa akiitamani siku nying kwa hiyo wakajitafutia sababu ya kuuza hizo nyumba kwa kuwatumia walala hoi wafanyakazi!

Kiranja wa uuzaji Mhe. JP Magu akashikia bango kwelikweli kutetea upuzi ili apate sababu ya kumnunulia hawara yake Sundi nyumba ya serikali na mdogo wake apate nyumba pale Bagamoyo Rd!

Tumombe Mungu ili JK naye wakati anaondoka asije na lwake.
 
Mie sishangai watu wanaomtetea Ben, nae ana wapambe wake, na pengine nae yumo humu kajisajili. sheria au sio sheria, hatuhitaji kwenda shule kujua kuwa raisi wa nchi kuomba mkopo na kununua mali akiwa bado katika ofisi yake ya uraisi huko ni kutumia madaraka yake vibaya: aa; wanaotoa mikopo wanapitisha document zake bila hata kuuliza swali kwa kuwa ni raisi; bee; yeye kulipwa mshahara mkubwa, na mkewe kulipwa mshahara wa ufirst lady ni ili kuwafanya wasiangalie pembeni: chee; hata kama kapata kihalali, tujiulize, kwanini mzee kifimbo hakuwa na hata kibanda cha maana hadi akajengewa na serikali wakati kastaafu? ye ndo hakuviona? tena alikuwa na nafasi nzuri sana maana enzi zake hata tulikuwa twapishana na almasi/dhahabu/tanzanite bila kujua thamani yake; mzee wa watu aliweka maslahi ya wananchi mbele hadi kifo kikamfika kwa mapenzi yake mema,; hawa wezi alowaachia nchi ndo wanaifilisi kwa kasi na ari mpya; Ben anamiliki mali ambazo hata hawezi kuzitumia, huyo bibie Anna na tamaa yake ya mzee fisi ndo kanunua kila kitu, bora alirudisha zile nyumba za serikali alizo nunua(or so am told), kabakiza nyingine hata kazisahau, mama mwizi yule!
 
Pinokyo,

What? Alirudisha?

Tena nasikia Mama Anna hata yale maghorofa yaliyokuwa ya TTCL pale Ilala Boma aliyanunua yeye. Na yale amayerudisha?
 
Hivi hawa This Day hawajipendi? Rais Kikwete si ameshasema "mwacheni mzee wetu apumzike!".... ndio maana hatuwezi kumuuliza kuhusu Rada? sasa leo mkamuulize kuhusu kampuni...
 
Pinokyo,

What? Alirudisha?

Tena nasikia Mama Anna hata yale maghorofa yaliyokuwa ya TTCL pale Ilala Boma aliyanunua yeye. Na yale amayerudisha

Niliambiwa wakati sakata la kampeni ya kurudisha nyumba za serikali lilipopamba moto alishauriwa kurudisha nyumba; akarudisha baadhi, zile ambao 'wanoko' walizijua; ila ziko nyingi hadi mikoani bado kashikilia; alidiriki hata kuchukua share ya mfanyakazi halali wa serikali huko kusini; mwivi mkubwa!
 
Cha kushangaza hapa ni watu wanaoona kuwa huku ni kumwandama Mkapa.Asingekuwa rais unadhani angeweza kupata mkopo wa milioni 750,kwa kutumia kampuni ambayo haina history ya kuafanya biashara kubwa kiasi hicho? Nenda leo,uone jengo linauzwa,na lina wapangaji ndani,uone kama utapewa mkopo! Mkapa aliwafukuza wapangaji waliokuwemo mule,nadhani ilikuwa ni NORCONSULT.Hii ni dhambi,na yeye alikuwa hana haja ya kufanya biashara kama hio,kwani kamwe asingekufa maskini,na watoto wake wote ni wakubwa,hana majukumu yeyote.Serikali inamtunza mpka kufa.
 
Kusema kwamba hizo objectives ni za kawaida katika doc zozote za makampuni pale BRELA sina maana ya kuunga mkono wala kupinga. Hoja inabaki pale pale, je, ni halali basi kwa rais aliye madarakani kuanzisha kampuni na kufuata "kawaida" kama wewe na mimi?

Suala la sheria inawezekana kukawa hakuna sheria japo inaelekezwa kuwapo kwa Code of Conduct ya viongozi. Sina hakika kama Tanzania ipo, sina hakika ya kuwapo kwa miiko ya viongozi, sina hakika kuwapo kwa mwongozo wa maadili ya viongozi, sina hakika kuwapo kwa AIBU kwa viongozi wetu wa CCM (isomeke Chukua Chako mapema). Na hii inatokana na kutokuwapo kwa VYOMBO VYA HABARI VINAVYOWEZA KUTHUBUTU (Leo THISDAY WANATHUBUTU TUNAWASHAMBULIA, eti WANAMTANDAO). Pia hali hii inatokana na kutokuwapo kwa Wapinzani wa dhati, wenye kuwa na vitengo vya kufanya utafiti, na sio wanaosubiri hoja zinazotengenezwa na makachero na kuzidandia, ama zile ambazo wana maslahi nazo. Kwanini Wapinzani wasifanya uchunguzi na kuibuka na hoja na ikibidi kwenda mahakamani kuwashitaki viongozi wezi? Ingekua hivyo sote TUNGEFAIDI KEKO yetu ya UHURU
 
Halisi,

Mtikila mbona anafanya? Tatizo ni sisi wananchi, hatuwaungi mkono watu wanaokuwa tayari kuumbua uozo serikalini. Badala yake tunazua visingizio mbalimbali mara wana mtandao, mara mchungaji naye kazidi na case nk.

Siku ambapo umma wa Watanzania utaamka na kuwa tayari kuelewa pale panapokuwa na ushahidi kwamba viongozi wao ni majambazi, basi hapo ndipo
magazeti zaidi yatajitokeza, Upinzani watapata nguvu na ari ya kuchambua uozo nk.
 
Mie sishangai watu wanaomtetea Ben, nae ana wapambe wake, na pengine nae yumo humu kajisajili. sheria au sio sheria, hatuhitaji kwenda shule kujua kuwa raisi wa nchi kuomba mkopo na kununua mali akiwa bado katika ofisi yake ya uraisi huko ni kutumia madaraka yake vibaya: aa; wanaotoa mikopo wanapitisha document zake bila hata kuuliza swali kwa kuwa ni raisi; bee; yeye kulipwa mshahara mkubwa, na mkewe kulipwa mshahara wa ufirst lady ni ili kuwafanya wasiangalie pembeni: chee; hata kama kapata kihalali, tujiulize, kwanini mzee kifimbo hakuwa na hata kibanda cha maana hadi akajengewa na serikali wakati kastaafu? ye ndo hakuviona? tena alikuwa na nafasi nzuri sana maana enzi zake hata tulikuwa twapishana na almasi/dhahabu/tanzanite bila kujua thamani yake; mzee wa watu aliweka maslahi ya wananchi mbele hadi kifo kikamfika kwa mapenzi yake mema,; hawa wezi alowaachia nchi ndo wanaifilisi kwa kasi na ari mpya; Ben anamiliki mali ambazo hata hawezi kuzitumia, huyo bibie Anna na tamaa yake ya mzee fisi ndo kanunua kila kitu, bora alirudisha zile nyumba za serikali alizo nunua(or so am told), kabakiza nyingine hata kazisahau, mama mwizi yule!

Off topic kidogo Mwalimu (RIP) ile nyumba ya Msasani alikopa THB wakati ule kwa ufahamu wangu na ile ya Butiama alijengewa na marehemu Samora Machel (RIP)na Musumbiji kama shukrani yao ninavyofahamu mimi. Pengine nakosea?
 
Kuna mtu hapa kakumbusha kwamba Kampuni ilianzishwa wakati mwalimu akiwa hoi taaban London, hii ni hatari na mara baada ya kufa ndio NBC hiyoooooooooooo ikaenda zake kwa bei ambayo humu ndani kuna wanaojua zaidi yangu. Haya Tupeni uhondo
 
Tanzania ni lazima tuanzishe kitu kama SOCA (http://www.soca.gov.uk/) ya UK ambayo kazi yake kubwa ni kuzuia wizi wa mali ya umma na uhujumu (proceed of crime). BMW aonyeshe kiasi cha kodi alicholipa kwa utitiri wa utajiri wake akishindwa afilisiwe kama wafanyavyo SOCA hapa UK. Ni jukumu lako (anayeshutumiwa) ku-prove beyond reasonable doubt kwamba amelipa kodi kihalali. Hili litawakumba vile vile wenzetu ambao kila siku wanabadili magari ya kifahari bila kulipa kodi. (Organised crime covers a very wide range of activity and individuals involved in a number of crime sectors). The syndicate should be investigated fully na tuanze kuweka list ya Rich people in Tanzania.

Iwe ni jambo la kujisifia kuwa tajiri nambari moja Tanzania na uonyeshe unalipa kodi kiasi gani katika biashara zako, sio kwenda kuliibia taifa na kuchanja mbuga wakati hulipi kodi. NI AIBU KWA WTZ.
 
Jamani tuache terminologies za sheria pembeni! Was it fair Kiongozi wa nchi kuanzisha kampuni akiwa madarakani? jamani..kwa kweli this is unfari to our voters who are more than 80% peasants. Honestly hawa viongozi hawatendi haki kabisa. And Iam sure hata wao wanalijua hili! Where are we going? ukiona watu wenye EVERYTHING THEY WANT IN THE COUNTRY wakianza kuiba kwa kutumia loopholes za sheria? After all sheria zinatengenezwa na wao wenyewe! Its sad and very sad for our country. Maana hawa viongozi they control everything from our souls to our pockets. Sasa hebu niambieni....eti tunasema kisheria hawana makosa. Perhaps hawana, but is this the ethical way of running a country? just like a limited company? This day hawana makosa wanareport kilichokwenye public record, lakini kwa sababu ya unyonge wetu hatujazoea kuona watawala wetu wakiwa exposed na mambo wanayoyafanya!
 
Thanka Dua...nimeipenda sana post hasa kuhusu uhalifu wa kupangwa sio kuuza madawa ya kulevya tu, bali hata kuwa na kipato ambacho huwezi kukielezea.
 
Ole,
Mwalimu alikopa kujenga pale msasani. Baadaye akawauzia serikali, na ambayo ilimaliza malipo ya mkopo. Halafu serikali "ikamzawadia" nyumba hiyo alipostaafu!!

Hivi huu ujanja wa kufanya biashara Mkapa ameupata baada ya kuingia Ikulu? Manaake kwa miaka yote alipokuwa Waziri hatukusikia akijishughulisha na chochote zaidi ya daladala aliyokuwa nayo. Mkewe alikuwa sekretari UNHCR miaka nenda rudi.
 
Hapa JF iliwahi kuwepo thread ya mali za viongozi, sijui iliishaje. Mi naona bora ifufuliwa tuanze kuanika hizi mali zao; tunaweza kuwa tunazungumzia BM hapa kumbe waliopo sasa, EL na wenzake wako busy kujikusanyia; miaka mitao ijayo tutakuwa bado tunashangaa hapa na mali zao, by then watakuwa wamemaliza walalahoi kwa ulafi wao.
 
Back
Top Bottom