Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

na wakala wa manunuzi haya alikuwa ni yule yule muhindi wakala wa Rada aliyejipatia shilingi bilioni 12 na kuanza kuzisambaza kwenye bank accounts mbali mbali za vingunge akiwemo mzee wa vijisenti...sasa CAG anashauri ndege hiyo iuzwe

CAG: Ndege ya Rais iuzwe

na Tamali Vullu
Tanzania Daima

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh, amesema iwapo ofisi yake ingeombwa kuifanyia ukaguzi ndege ya rais, wangeshauri iuzwe.

Utouh, alisema hayo mwishoni mwa wiki katika semina iliyoandaliwa na ofisi yake kwa wahariri wa vyombo vya habari, iliyofanyika mjini Bagamoyo ili kufahamu majukumu ya ofisi hiyo.

Kauli hiyo ya CAG, inatokana na swali la mmoja wa wahariri aliyetaka kujua kama ofisi hiyo ingepewa jukumu la kuifanyika ukaguzi ndege hiyo, ingetoa ushauri gani kwa serikali.

Alisema hivi sasa hakuna sababu ya msingi ya kuifanyia ukaguzi ndege hiyo kwa kuwa gharama zilizotumika kununulia ni halisi na ni uamuzi wa rais kuamua kuitumia anapokwenda safari za nje ya nchi au la.

"Kwa sasa hakuna msingi wa kuifanyia ukaguzi, kwani gharama iliyotumika kununua ni sahihi na hapa suala la thamani ya pesa halipo, kwa sababu ni uamuzi wake kuitumia ama la," alisema.

Wiki iliyopita, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa (CCM), alidai ndege hiyo haina faida kwa taifa na kutaka iuzwe.

Mbunge huyo alitoa kauli hiyo bungeni wakati akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi kwa mwaka wa fedha 2008/20009.

Alisema matumizi ya ndege hiyo kwa sasa, ambayo hivi karibuni iligongwa na gari la maofisa usalama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, hayakidhi mahitaji ya rais, kwani haitumiki anaposafiri nje ya nchi.

Alisema uwezo wa ndege hiyo iliyonunuliwa kwa bei kubwa hata kuibua malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na wabunge, ni kubeba watu 12 wakati rais anapokuwa na safari, huwa na ujumbe wa zaidi ya watu 18, hivyo haifai kwa matumizi yaliyolengwa licha ya kununuliwa kwa bei kubwa.

Katika hatua nyingine, Utouh, alisema wamekuwa wakikumbana na vitisho vya aina mbalimbali kwa kuwa kazi wanayofanya inaingilia masilahi binafsi ya watu.

"Kazi yetu haina tofauti na ya uandishi wa habari, ingawa tunafanya hivyo kwa masilahi ya taasisi husika na taifa kwa ujumla, lakini tunagusa masilahi ya watu, hivyo vitisho vipo, lakini wanasema ukishayavulia nguo maji, sharti uyaoge," alisema.

Aidha, alisema ofisi yake ipo katika mchakato wa kuandaa ripoti nne ambazo wanatarajia kuzikamilisha kabla ya Desemba mwaka huu.

Alizitaja ripoti hizo kuwa ni za ukaguzi kwa shule za sekondari katika masomo ya hesabu na sayansi, afya ya msingi kwa wananchi, taka ngumu na viwango vya barabara.

Alisema baada ya kukamilisha ripoti hiyo, huikabidhi kwa rais na baadaye kupelekwa bungeni.

Awali, akiwasilisha mada kuhusu ukaguzi wa mashirika ya umma, Jumaa Mshihiri, alisema ofisi hiyo inakabiliwa na upungufu wa wakaguzi katika mashirika hayo.

Alisema kutokana na hali hiyo, wakati mwingine wanalazimika kutafuta wakaguzi binafsi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo na wakaguzi hao hupatikana baada ya kutangaza zabuni.
 
kuuza ndege ya rais? sawa itauzwa shilingi ngapi? isje ikauzwa kwa tenda kwa milioni moja
 
Kwahiyo viongozi wetu wanataka kutuambia kwamba Bunge linaweza allocate 4 unproductive hours za porojo na kuacha kupanga ratiba kwa mambo muhimu yanayomgusa kila Mdanganyika? I don't believe me eyes........

Kifupi ni kwamba Ndugu Waziri hakutoa majibu ya swali aliloulizwa. Alichokua anajaribu kukifanya ni kuwayeyusha waliomwuliza maswali akiwa na uhakika kwamba hawatafikiri haraka haraka na kumpatia supplemental questions za kumbana kwenye suala hili.

Mungu tubariki Wadanganyika.
 
Blaa blaa hizo zote unazoziongea tunazijua.Lakini hata kwa akili yangu ndogo tuu, najua kwamba hakuna mtu aliye msaafi,narudia hakuna.Sasa unacho-ongea wewe ni cha ajabu! Kinachozungumziwa kumbuka ni degree of ujinga.Wala sina aibu kusema kwamba Kikwete ni mjinga zaidi kuliko Mkapa.Kwa kweli kinacho-onekana kwa viongozi wetu hawa ni ujinga,period.
 
Unajua unachokiongea wewe au unatumia uhuru wako wa kuongea?

Biashara Ikulu ni minor thing? Kikwete ndio anamchafua Mkapa au ndio anamlinda?

You are almost ridiculous!

Very ridiculous ??????????????????????
 
Mtikila dume,ulikuwa unatafuta wanasheria wa Milosevich wasaidie kuangalia jinsi ya kumpeleka Mkapa The Hague sijui umefikia wapi mkuu? Immunity yake imekuwa tatizo au vipi?huko ndiko anakoweza kufanyiwa usafi akatakata.
 
Hata Uganda leo wapo watu ukiwahoji watakuambia Idd Amin alikuwa mtu safi. Ni mtazamo wa mtu, lakini ukweli Mkapa ni Mchafu sana!
 
Historia inam hukumu Pres Mkapa kwa uongozi wake uliotukuka na mema mengi aliyoyafanya katika ujenzi wa uchumi imara. Hii haina maana kuwa hakuwa na mapungufu, kama binadamu kuna mahala amekosea yeye binafsi, wasaidizi wake nk. Lakini overall the Man is living Legend!
 
Mtikila dume,ulikuwa unatafuta wanasheria wa Milosevich wasaidie kuangalia jinsi ya kumpeleka Mkapa The Hague sijui umefikia wapi mkuu? Immunity yake imekuwa tatizo au vipi?huko ndiko anakoweza kufanyiwa usafi akatakata.

Really? Mtikila who?
 
Historia inam hukumu Pres Mkapa kwa uongozi wake uliotukuka na mema mengi aliyoyafanya katika ujenzi wa uchumi imara. Hii haina maana kuwa hakuwa na mapungufu, kama binadamu kuna mahala amekosea yeye binafsi, wasaidizi wake nk. Lakini overall the Man is living Legend!

Unachosema ni kweli ndugu. Mimi binafsi naona utawala wa Mkapa ni best we had, aliweza kuprovide leadership na kurekebisha uchumi. Kwa sasa hatuwezi kumlinganisha na JK hata kidogo ni sawa na kumfananisha mwanafunzi wa kidato cha sita na wa shule ya msingi.
LAKINI LAKINI ni lazima tuseme kweli, Mkapa yeye ndio maesimamia wizi mkubwa kabisa uliowahi kutokea kwenye nchi yetu, labda unaweza ukaniambia ni kutukuka kupi huko mtu unaoversee EPA, Radar nad kindege kibovu cha Rais, yeye kama mkuu wa nchi kwanini alisimamia ujinga huu, unaeza kumtetea kwa hili?
 
Unachosema ni kweli ndugu. Mimi binafsi naona utawala wa Mkapa ni best we had, aliweza kuprovide leadership na kurekebisha uchumi. Kwa sasa hatuwezi kumlinganisha na JK hata kidogo ni sawa na kumfananisha mwanafunzi wa kidato cha sita na wa shule ya msingi.
LAKINI LAKINI ni lazima tuseme kweli, Mkapa yeye ndio maesimamia wizi mkubwa kabisa uliowahi kutokea kwenye nchi yetu, labda unaweza ukaniambia ni kutukuka kupi huko mtu unaoversee EPA, Radar nad kindege kibovu cha Rais, yeye kama mkuu wa nchi kwanini alisimamia ujinga huu, unaeza kumtetea kwa hili?

Huenda ni kweli Mkapa was a good president. Lakini nasikitika kuwataarifu kuwa when all is said and done Mkapa hatakumbukwa kwa mema aliyoifanyia Tanzania, bali kwa kuweka kono lake katika kukwapua mali na hazina ya Watanzania.
 
Mkapa: Mimi sasa na dini

Na George Boniphace, Mwanza
Majira

RAIS mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa amesema amefumba midomo katika masuala yanayohusu siasa na badala yake kwa sasa anajihusisha zaidi na mambo ya dini.

Rais Mkapa alisema hayo Jumapili iliyopita baada ya ibada ya misa katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Fransisco Exaveri lililopo Nyakahoja jijini hapa.

Alisema kwa sasa anatumia muda mwingi akisali na kuwataka waumini wa dini mbali mbali nchini kusali zaidi na kuwataka Watanzania kujenga moyo wa upendo miongoni mwao.

Aliongeza kuwa waumini wa kweli mara kwa mara huwaombea wenzao amani na upendo na kwamba amani hiyo huanzia baina ya mtu na mtu, majirani, jamii hadi nchi na nchi.

Alisema kwa sasa anaona ni afadhali aendelee kumwomba Mungu na kueneza jina lake kwa njia ya Biblia, jambo ambalo aliwataka Watanzania kufanya hivyo na kwamba watapata neema zaidi iwapo watafuata mahubiri yake na kuhudhuria ibada za misa mara kwa mara na kuwasamehe
waliowakosea.

"Enzi za mimi kujihusisha na mambo ya siasa zilikoma pale nilipokabidhi madaraka kwa Serikali ya Awamu ya Nne mwaka 2005," alisema Rais Mkapa.

Aidha, alisema hata katika ibada hiyo, hakutarajia kupewa nafasi ya kuwaeleza wananchi jambo lolote na kuongeza kuwa alihudhuria ibada hiyo kama muumini wa kawaida.

Aliwaeleza waumini katika Kanisa hilo huku akitoa mifano ya vifungu katika Biblia, ambavyo vilikuwa vikigusia masuala ya upendo miongoni mwa jamii. Misa hiyo ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Alex
Msekela.

Rais Mkapa alifika hapa Septemba 6 mwaka huu, akitokea wilayani Chato, Kagera, kuhudhuria hitma ya marehemu baba wa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Bw. John Magufuli ambayo pia ilihudhuriwa na Waziri Mkuu wa Kenya, Bw. Raila Odinga.
 
Rudisha kwanza mgodi wetu uliofisadi na sala za fisadi kamwe hazipokelewi. Umewadhulumu Watanzania milioni 40 kwa uroho wako wa kutaka utajiri wa haraka haraka halafu leo unajifanya mcha mungu! Uwongo wako tumeshaugundua.
 
May be anaabudu dini ya Shetani. Lakini dini ya Mungu wa kweli haiwezi kuwa chaka la mafisadi. Rudisha kwanza mali za watanzania ulizokwiba fisadi mkuu ktk Tanzania.
 
Uumini wa kweli ama si wakweli ni kati ya mungu na yeye , siyo bubu au mimi tunaoweza kumtenganisha na mungu
 
Makanisa na Misikiti vinatuangusha sana kwenye suala la ufisadi na rushwa. Ukatoliki wa siku hizi hata muumini wa kawaida anapewa nafasi kuhutubia kanisani kwenye ibada!!
 
Back
Top Bottom