Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Suala hapa siyo hawa Maaskofu kujua eti kama Mkapa alishiriki katika haya mabo ya kifisadi ama la!They are not their to judge!
Mkapa ndiyo anayoyakujibu ila tusiwabebeshe misalaba isiyo yao hawa maaskofu wanakila sababu ya kuamini wanayotaka kuamini na Mkapa na porojo zake zote ana haki ya kuamini na kusema analotaka!

Kanisani ni sehemu ya kujumuika kumuomba Mungu na kutubu.Na kueleza yaliyo mema kwa jamii

Kanisani hasa Katoliki hatuna mahakama ya SHARIA wala kitu kinachofanana na hicho.

Katoliki una uhuru wa kwenda mbele ya padre na kutubu kua NILIUA ,NILIFISADI fedha ,NILIZINI na MKEE wa jamaa fulani ,LAKINI pamoja na matamshi hayo mazito mbele ya PADRE,PADRE kamwe hatokuzunguka na kwenda kwa POLISI kutoa taarifa ya kwamba huyu jamaa ni ndiye aliyeua mtu fulani.

Ila KAMA uliua mbele ya PADRE na padre kutakiwa na polisi ama mahakama na ATASEMA alichokiona.

WATU wanachojaribu kufanya hapa ni kuyafanya makanisa kama MAHAKAMA ya SHARIA,Ndg zangu linapokuja suala la KIROHO kwa upande wa KATOLIK hua wanamuachia YEYE MWEZA wa YOTE.Ndio hiyo tofauti kati ya hasa wa kristu na dini zingine.Maana dini zingine zimepewa mamlaka ya kuhukumu.
 
Kanisani hasa Katoliki hatuna mahakama ya SHARIA wala kitu kinachofanana na hicho.
Taratibu za kutubu nim pamoja na malipizi. Na ukiiba au kuchukua kitu nje ya taratibu malipizi yake ni pamoja na kurejesha ulichokichukua!!! Kuna mali alizochukua Mkapa nje ya utaratibu.
Ukweli domo peke yakee halitavunja ufisadi dawa yake ni kuwashitaki.
 
Amani inajengwa na msingi wa HAKI. Watanzania tumechoka na neno "amani" wakati hakuna haki. Watu wachache wanajichotea mapesa yetu na ku-control uchumi wetu huku wananchi walio wengi wanaishi maisha duni sana. Kwa msingi huo Mkapa na wenzake wasitufanye sisi tuendelee kuwa wajinga kwa kutumia neno Amani. Tutafute HAKI kwanza ndipo tutakuwa na AMANI.
 
Taratibu za kutubu nim pamoja na malipizi. Na ukiiba au kuchukua kitu nje ya taratibu malipizi yake ni pamoja na kurejesha ulichokichukua!!! Kuna mali alizochukua Mkapa nje ya utaratibu.
Ukweli domo peke yakee halitavunja ufisadi dawa yake ni kuwashitaki.

Mkuu nakupata.
Mimi ninalopinga hapa ni ya kwamba watu humu wanataka mfano Mkapa akienda kutubu kwa PADRE na PADRE akamwambia nenda kauze mali zako ugawie masikini,Na Mkapa ikatokea akakataa maelezo hayo,Watu humu wanataka PADRE amchukulia hatua za kesheria.NONSENSE
Hiyo si kazi ya watumishi wa Mungu ktk maadili ya KIKRISTU,Yesu MWENEWE mbona hakumchukulia hatua za kinidhamu yule jamaa aliyemwambia kauze mali zako na unifuate?Na badala yake alisema ni vigumu kwa tajiri kuingia kuliko ngamia---------

Ndio maana tukawa na vyombo vya ki KAIZAR yani MAHAKAMA kama huku tumeshindwa tusiwape mzigo watumishi wasiyohusika na huko.

LEO hii hata kama PADRE,ASKOFU akiwa anamuona kila siku changudoa fulani na huyo changudoa akatokea kanisani Padre hatomfukuza badala yake atampiga sala.

KAnisa linahitaji watu waovu ili lipate kuwaokoa, KAnisa ni kama mvuvi apandaye mashua kwenda kuvua samaki bahari,mvuvi hawezi vua samaki waliokwisha vuliwa.
Hii ndio tofauti ya kanisa hasa la kikristu na utawala wa Kaizar ya kwamba KANISA wateja wake ni kutafuta waovu ili lipate kuwaokoa.Utawala wa serikali wao ni kua EXPEL waovu

Kama watu wangekua wema wala YESU asingalikuja .
 
Nimependezwa na namna thread hii inavyokwenda.Specifically ni ktk wachangiaji kuepuka kujibizana na wale wenye nia ya kusafisha(kujisafisha?).
 
Acheni kupiga domo

Big up Mkapa,natamani ungelikuwa Rais hadi leo hii,upuuzi unaoendelea sasa,laiti ungakikuwepo hayangekuwa hivi.

God bless Mkapa.
huu upuuzi unaouona sasa ulifanyika enzi za mkapa. Angalia EPA, rada, chenge na mengineo mengi. awamu hii yameibuka tu. Mkapa alaaniwe na kizazi chake chote
 
Kwakuwa inasadikika kuwa baadhi ya mabilioni yaliyochotwa awamu ya tatu yalitumika ktk kampen za awamu ya nne(by chama tawala?),then kwa ujumla wake ni kwamba uchafu n uchafu tu..Tucangalie nan kachafuka zaidi...Wooote waliohucka ni maadui wa taifa hili,na hawaitakii nchi yetu mema.
 
Kila mtu aliyezaliwa na mwanamke ana mapungufu yake, na wote tukubali kwa kusema AMEN. Mapungufu hayo yanatofautiana kati ya mtu na mtu, na ndipo tunaweza kusema fulani bwana amekithiri kwa hili na lile. Nafurahia nilivyo sasa kwa sababu nilisomeshwa na taifa langu tena niseme Nyerere maana alikuwa anajua maana ya Elimu na sasa naishi maisha mazuri hapa mjini japo si fisadi kabisa. Jameni jamii inateseka sasa, funga macho tizama hali halisi ya maisha ya mtu wa kawaida Tanzania kwa sasa anavyoteseka malazi, chakula, huduma za afya, n.k. Huyu anasema tuache kupiga domo kwa sababu alishachota na hataki watu waseme. Ingewezekana kukata rufaa ya kifo basi ningekata Julius Nyerere afufuke, turejeshe Azimio la Arusha, Tuimbe kwa mantiki ule wimbo wa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote.........Ila sasa pengine wimbo huo umeleta hasara kwani unakaribisha wageni na wageni wameshatujulia kuwa viongozi wetu ni watu wa 10% na kila kitu unapata bila jasho. Wahindi usiseme, ukitaka kama una ndugu yako anafanya kazi kwa mhindi muulize akuhadithie songombingo la huko,. Yaani watanzania tunejeuzwa tambara bovu ndani ya nchi yetu. Hata mhindi akiwa ni jirani yako akisababisha any externalities ukimuuliza anakuambia mimi nafaimu ile diwani na nkuu ya wilaya pale. Akiimaanisha hajalishwi na wewe. System imewalea na kuwaona ni bora ndiyo maana tunadharaulika ndani ya nchi yetu. Achilia mbali Makaburu na wawekezaji wengine, wameshajua watanzania ni wa kukanyaga migongo tuu na hakuna kiongozi anayewatetea kwani kiongozi wanawaza 10% tuu kila kukicha. Hawakumbuki kabisa ahadi zao kwa wananchi wakati wa uchaguzi. Si wanasema eti usipopiga kura hujatumia demokrasia, sasa mimi nilipiga kura ya kwanza 1995 tu na baada ya kuona mchezo mbaya wa wizi wa kura then nimekataa kabisa sipigi kura mimi. Sijawahi kushawishiwa na kiongozi yeyote labda atokee sasa. Sasa wewe BEN tuache tupige domo nina imani siku moja kelele zetu zitazaa matunda. Jameni hii ni awareness tosha. Ui Ui NUi mama we twafa jamani.
 
Nakubaliana moja kwa moja kwamba badala ya kupiga DOMO mafisadi wakamatwe...Either domo hilo linapigwa na wananchi ama Viongozi walioko serikalini ama jf....Bado nakubali kuwa kweli dawa ya DOMO NI VITENDO.
 
MKAPA NI MTU SAFI?

ninaona kizunguzungu.

ni kweli amefanya mengi mazuri lakini MABAYA aliyoyafanya ni zaidi ya hayo mengi na lazima awajibike.

hiyo ni sawa sawa na kazi yote aliyoifanya ina thamani ya Tsh. 100,000 lakini yeye ameiba Tsh. 100,000,000. mtu wa aina hii utasema ni safi? ndiyo kaliingizia taifa sumthing lakini ameliibia zaidi.

Hudson Kazonta, Singida
Daily News; Sunday,August 17, 2008 @18:01

Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, amewataka Watanzania kuacha kupiga domo badala yake watafute vipaji ili kulinda umoja na amani nchini.Amesema hayo jumapili wakati akizungumza kwenye sherehe ya Jubilei ya miaka 100 ya Ukristo Jimbo Katoliki la Singida zilizofanyika katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu.

Alisema pamoja na amani na utulivu uliopo hapa nchini, lakini bado kuna watu ambao wanatafuta mambo mabaya kwa lengo la kuwagawa Watanzania. Alisema Watanzania wana imani, dini na makabila mbalimbali, lakini ni vyema kila mtu akatumia kitu hicho kuwa pamoja na kudumisha amani na utulivu.

Alikemea tabia ya baadhi ya watu kuwa na utamaduni wa kushabikia maneno ya vijiweni badala yake akawataka kuonyesha upendo na staha ili kuleta umoja miongoni mwa Watanzania. Awali Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu Dar es Salaam, Polcarp Kardinali Pengo aliwataka Watanzania kupeleka ujumbe wa amani kwa wanaotumia silaha kwa lengo la kuvuruga amani. Alisisitiza kuwa kazi hiyo itaendelea mpaka mwisho wa dahari na kwamba miaka 100 ya Jimbo la Singida ni mwanzo wa kazi iliyopo mbele ya Kanisa la Singida na Kanisa la Ulimwengu mzima.
 
Mkapa jibu tuhuma - Lipumba

2008-08-20 13:08:45
Na Simon Mhina

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahimu Lipumba, amemuonya Rais mstaafu Bw. Benjamin Mkapa kuwa ataendelea kusakamwa na kulaumiwa hadi atakapoingia kaburini, iwapo hatojibu tuhuma za rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma wakati wa utawala wake.

Aidha kiongozi huyo amesisitiza kwamba watanzania wanapotoa shutuma dhidi yake, hawapigi domo kama alivyodai, kwani machungu wanayopata kutokana na ufisadi hayavumiliki.

Liwake jua, ije mvua hakuna atakayesahau dhuluma anayodaiwa kuwafanyia watanzania, alisema
Profesa Lipumba alikuwa anajibu kauli iliyotolewa Jumapili iliyopita mjini Singida na Bw. Mkapa akiwaonya watanzania waache kupiga domo, huku akiwashutumu baadhi ya watu kuzungumzia mabaya ya \'wenzao\' na kusahau yale mazuri.

``Kwanza kabisa amenishangaza. Ameonyesha jinsi alivyo wa ajabu. Shutuma dhidi yake si kupiga domo, watanzania wanayo haki ya kupata majibu ya tuhuma hizo kutoka kwake.

Suala la mazuri aliyofanya si ajabu maana ndiyo kazi aliyowaomba watanzania. Aliwaomba kura awe Rais, afanye mambo mazuri. Wanachokitaka sasa ni juu ya mabaya aliyofanya. Wanataka ufafanuzi na hii ni haki yao,`` alisema.

Mwenyekiti huyo alisema shutuma dhidi ya Mkapa na miguno yote, itakoma mara moja, iwapo kiongozi huyo atayatolea tamko mambo anayoshutumiwa nayo.

Alisema, kwa mfano, haelewi ni kwa vipi Bw. Mkapa alipoingia madarakani alitaja mali zake, lakini alipotoka akageuka bubu.

``Suala la kutaja mali aliamua mwenyewe na akafanya hivyo, sasa watanzania wanataka wajue mali gani ametoka nazo? Ni zile zile au zimeongezeka? Watanzania wanapotoa madai hayo hawapigi domo, awajibu,`` alisema.

Alisema wakati wote wa utawala wake alikuwa aking\'aka kwa nguvu zote kuwa atapambana na rushwa na ufisadi, hivyo ili malalamiko dhidi yake yafikie kikomo, anatakiwa kutoa maelezo kama vile ya manunuzi ya rada na uanzishwaji wa kampuni ya Meremeta.

``Wakati tunatoa shutuma za rushwa enzi za utawala wake, alikuwa anatutisha na kutufokea kuwa eti tupeleke ushahidi.

Sasa ushahidi tumepata kwamba yeye ndiye mmiliki wa Kiwira, muasisi wa rada na ndiye aliyemlinda Chenge. Ajitokeze ajibu tuhuma,`` alidai Profesa Lipumba.

Mwenyekiti huyo alisema ni wakati wake ambapo fedha ziliporwa Benki Kuu kupitia akaunti ya malipo ya nje (EPA) na kukifanya chombo hicho cha fedha kisiaminike tena ndani na nje ya nchini.

Alisema BoT imeaibika mno kimataifa kutokana na kashfa ya EPA, hivyo Bw. Mkapa anatakiwa atoe maelezo.

Alisema kuweweseka kwa Bw. Mkapa kila mara kuhusu tuhuma dhidi yake, huku akijaribu kuzijibu kwa njia za panya, kunaashiria kwamba yeye ni sawa na mtoto aliyepata uchizi baada ya kukiuka miiko ya baba na mama yake iliyomfanya akue.

Akifafanua, Profesa Lipumba alisema Bw. Mkapa aliaminiwa sana na Mwalimu Julius Nyerere katika suala la rushwa na uaminifu huo wa kinafiki ndio uliomfanya Baba wa Taifa ampigie debe kwa vile hakumgundua.

Alisema kwa vile Bw. Mkapa baadaye aligeuka, akawa kiongozi na mlinzi namba moja wa mafisadi, ndio maana anashindwa kuzungumza hoja inayoeleweka.

Mwenyekiti huyo alisema labda Bw. Mkapa amesahau maswali anayoulizwa kila mara; ``Naomba nimkumbushe. Je, ni kweli alinunua mgodi wa Kiwira na marafiki zake kwa bei chee? Kama sio aseme hapana, anaweweseka nini?`` Alihoji.

Alisema haelewi kwa nini Bw. Mkapa hakutumia muda huo kujibu tuhuma, badala yake analalamika kwamba kuna watu hawasemi mema ya wenzao.

``Kwa hiyo mtu akifanya mema, akiiba hana kosa? Anataka kwa vile kafanya mema tunyamaze. Kwani waliopo magerezani wao hawakuwahi kufanya mema mitaani kwao?`` Alihoji.

SOURCE: Nipashe
 
BUbu,Si ameshasema acheni mdomo?Hiyo ndiyo njia yake ya kujibu tuhuma otherwise hana jibu zaidi la hilo!Anataka tumwache ale alichochuma kiungwana taratibu!
 
BUbu,Si ameshasema acheni mdomo?Hiyo ndiyo njia yake ya kujibu tuhuma otherwise hana jibu zaidi la hilo!Anataka tumwache ale alichochuma kiungwana taratibu!

Na sisi tunamwambia arudishe mali zetu alizokupua ndiyo tutaacha kumsakama fisadi huyu.
 
Na sisi tunamwambia arudishe mali zetu alizokupua ndiyo tutaacha kumsakama fisadi huyu.

Haya Mkuu!Mimi nimeamua kupunguza domo langu sasa msakameni muone kama atakonda ama kupungua kitu zaidi ya kwamba choreni chini mjue mmeumia!Hatoi kitu!
Kwisha Habari!
 
Huyu Mkapa wetu!
Tuamini tu kwamba ni mmoja kati ya watu waliozaliwa wajinga, wakapa bahati ya kubebwa, na wakafika juu ktk madaraka.

Ni Viongozi wachache ambao wana nguvu za kutukana waliowachagua eti "Pumbavu", tena ktk TV na kila mtu akamuona. Nadhani pia ni aibu ndogo aliyozaliwa nayo kama mnyama.
 
Yes, kuna mabaya amabayo Mkapa ameyafanya ktk kipindi cha miaka 10 akiwa ikulu: (1) mikataba mibaya hususani madini (ambayo hata hivyo ni mwanasheria mkuu ndiye anapaswa kulaumiwa);(2) kumuachia mke wake a—dictate badhi ya shughuli za kiserikali ( one of his weakness). (3) kujihusisha na bishara akiwa ikulu (which is a minor thing)....

Couple of months ago, niliandika kuwa mwanasheia mkuu wa zamani, Andrew Chenge, ambaye ndiye aliyeshiriki kusaini mikataba mibovu kuwa ndiye anayepaswa kulaumiwa na sio mzee Ben; well, watu wakasema, "yeah..., yeah..., yeah...," Now, read this [it's from ALASIRI]—coz I kinda feel like vindicated/validated.


Na Mwandishi Wetu, Jijini
Taarifa ya jana ya Waziri Mkuu, Bwana Mizengo Pinda juu ya utekelezaji wa mapendekezo 23 ya Bunge, kuhusu mkataba tata wa Richmond, imezua vuguvugu kubwa miongoni mwa wananchi, ambapo hivi sasa, watu wanataka kila aliyeliingizia losi taifa , aburuzwe kortini.

Wakiongea na gazeti hili leo asubuhi, wananchi kadhaa wamedai kuwa Serikali imeingia mikataba kibao ya hasara wakati kuna watalaam wazuri wa sheria ambao wangeweza kuzuia hali hiyo.

Wamesema mtu wa kwanza anayepaswa kulaumiwa kwa suala hilo, ni aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Andrew Chenge ambaye wanadai alijua fika mikataba kadhaa inayosainiwa haina maslahi kwa taifa.

``Chenge ni mwanasheria mzuri tu na alijua yote hayo lakini hakuzuia...anapaswa kuchukuliwa hatua,`` amesema
Bw. Mahenge Fanuel na kuungwa mkono na Bi. Halima Salehe ambao wote ni wanafunzi wa chuo kimoja cha elimu ya juu Jijini.

Wakazi wengine wamesema kinachotakiwa kufanywa hivi sasa ni Serikali kuchukua hatua dhidi ya watalaam wote waliohusika na mikataba yote feki.

``Sio huo wa Richmond tu, ipo mikataba mingi ambayo watalaam wameliingiza taifa kwenye matatizo...wote hao waangaliwe na kuchukuliwa hatua,`` amesema Bi. Jamillah Shaaban.

Akizungumzia sakata hilo, Mwenyekiti wa chama cha TLP,
Bw. Augustine Mrema naye amemshikia bango Bw. Chenge.
akitaka afunguliwe mashtaka ya jinai kuhusiana na mkataba wa IPTL.

Amesema Bw. Chenge alifahamu vema kuwa mkataba huo ni mbovu lakini akashindwa kuishauri vema Serikali.

``Inabidi ashitakiwe kwa mashtaka ya jinai ya kuisababishia nchi hasara kubwa wakati alikuwa akifahamu kinachoendelea katika mchakato mzima wa uingiaji mkataba huo,`` akasema Bw. Mrema.

Amesema jana alimshangaa Waziri Mkuu alipoliambia Bunge kuwa miongoni mwa wanasheria waliompa ushauri na maoni juu ya majadiliano ya mikataba ni Bw. Chenge.

``Haiwezekani mtu aliyehusika kulibebesha taifa hasara kubwa kutokana na kuishauri vibaya Serikali, akatoa ushauri mzuri,`` akasema.

Jana akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo 23 yaliyotolewa Februari mwaka huu, Waziri Mkuu alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wanasheria watatu.

Alisema ofisi yake ilipata maoni kutoka kwa Bw. Chenge, Mbunge wa Musoma Vijijini, CCM, Namrod Mkono na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa sasa, Bw. Johnson Mwanyika.

``Maoni yao yataisaidia sana Serikali katika kuimarisha mfumo wetu wa majadiliano ya mikataba. Naomba nitumie nafasi hii kuwashukuru waheshimiwa wabunge kwa maoni na ushauri wao mzuri sana,``alisema Bw. Pinda.

SOURCE: Alasiri ).
 
ALASIRI????
Kama kumbukumbu yangu itakuwa iko vizuri,ni wiki kadhaa tu zilizopita huyuhuyu anayedai usemi wake umekuwa validated alianzisha thread akisema kuwa gazeti hilo lilikuwa likiandka vchwa vya habari ambapo ndani yake habari hazikuwa na lolote(anayeikumbuka ile thread ntaomba anisaidie).Leo hii.....Very same person.....Analikumbatia gazet hilo ktk kujenga hoja.Hii ni "wabongo zaidi ya tuwajuavyo!".
 
Mkapa ni fisi. Mlafi wa kutupa ametutia umaskini wa karne mia tano. mali alizoiba unataka nikuonyeshe ziko wapi.kaulize barrick hela zake wanampa nani.
 
Note: - means minus, + means plus lets see this simple mathematics here below

-Kikwete na ubaya wake + (-Kikwete na kampeni za kuwa tuwe tunamzungumzia Mkapa)= - X. below zero
Mkapa na mazuri aliyoyafanya+ (-mkapa na mabaya alyoyafanya)=0

Mwinyi na aliyoyafanya + (-kutokukusanya kodi,kushindwa, rushwa,kila mtu afanye kivyake)=0

Nyerere na aliyoyafanya +( aliyoshindwa kufanya, but was meant for good)=+X (far above zero)

Kikwete bado anashika mkia kwani yuko below line zero, Mkapa na Mwinyi walifanya zero.Nyerere bado anaongoza.

Waberoya
 
Hili Bunge uchwara la CCM halikuona umuhimu wa kuzungumzia wizi uliofanywa na fisadi Mkapa wa mgodi wetu wa Kiwira na kuhakikisha mgodi ho unarudi chini ya miliki ya Watanzania. Ngeleja inadaiwa alikuwa anasubiri 'ruhusa' kutoka kwa Spika ili azungumzie jinsi serikali itakavyoyafanyia kazi mapendekezo ya kamati ya madini. Kwa mara nyingine tena maslahi ya mafisadi na chama chao yamepewa kipaumbele kuliko yale ya Tanzania.

Date::9/1/2008
Bunge laisha suala la Kiwira kimya

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

SERIKALI imeshindwa kutimiza ahadi yake ya kutoa kauli kuhusu utata wa umiliki wa Mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira unaomhusisha Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kama ilivyokuwa imeahidi wakati wa kuanza kwa mkutano wa 12 wa Bunge.

Hatua hiyo ya serikali kushindwa kutoa kauli, imekuja wakati bado kukiwa na giza nene lililogubika mgodi huo wenye thamani ya Sh 4 bilioni, lakini ukadaiwa kuuzwa kwa Kampuni ya Tan Power Resources Limited, kwa thamani ya Sh 700 milioni mwaka 2005.

Awali, katika mkutano wa 12 wa Bunge la Bajeti, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliahidi kwamba serikali ingetoa kauli kuhusu mgodi huo kabla ya kumalizika kwa mkutano huo, hata hivyo, ahadi hiyo haikutimizwa.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja, alipoulizwa jana afafanue kuhusu serikali kushindwa kutoa kauli kama alivyoahidi Waziri Mkuu Pinda, alikiri ahadi hiyo, lakini akafafanua kwamba, tatizo ni ratiba.

Ngeleja aliweka bayana kwamba, mambo mengi ikiwemo mjadala wa Richmond na mengine yalishindwa kujadiliwa kutokana na ratiba na kuongeza kwamba, serikali itatoa kauli kuhusu Kiwira iwapo itapangiwa ratiba katika mkutano ujao wa Bunge.

"Kweli tulipaswa kutoa kauli, si kwamba tumeshindwa suala ni ratiba, kulikuwa na mambo mengi ndiyo maana umeona hata mambo kama Richmond na mengine hayakujadiliwa, lakini tunategemea Bunge lijalo tukipangiwa ratiba tutatoa kauli," alisisitiza Ngeleja.

Alisema ratiba za mambo kama hayo si mamlaka ya waziri, kwani pia kuna Kamati ya Uongozi inahusishwa ili suala liwekwe kwenye ratiba na hivyo akasisitiza kwamba, wakati wa Bunge lijalo ikipangiwa ratiba ataweza kutoa kauli.

Naibu Spika Anna Makinda alipoulizwa jana kuhusu Bunge linachukuliaje ahadi ya serikali iliyotolewa na Waziri Mkuu kisha ikashindwa kutimizwa, alisema hadi sasa hati hiyo ya serikali kutoa kauli ipo.

Makinda alifafanua kwamba, kwa kuwa hati ya serikali ipo basi itakuwa ni kazi yao kupanga ratiba katika Bunge lijalo ili jambo hilo liweze kutolewa tamko.

"Hadi sasa hati ya serikali kuhusu hilo ipo, kwa kuwa bado ipo itakuwa ni kazi yetu kupanga ratiba ili iweze kufanyika hivyo katika mkutano ujao," alijibu Makinda.

Alipoulizwa zaidi, kauli ya Waziri Mkuu Pinda iliweka bayana kwamba serikali ingetoa kauli kabla ya kumalizika mkutano wa 12 (uliokwisha), anahisi tatizo ni ratiba au serikali haikuwa tayari, alijibu: "Both (vyote wili), inawezekana."

"Inawezekana ikawa ni ratiba imebana na vinginevyo pia, wewe mwenyewe si umeona ratiba ilivyobana safari hii?" alihoji.

Makinda alipoulizwa kama tatizo ni ratiba vipi Bunge lilitaka kujadili hotuba ya Rais ambayo ilikuja baadaye wakati Kiwira ni jambo lilioibuliwa tangu mwanzoni mwa Bunge: alijibu, " Jambo la msingi hati ipo, hivyo ni suala la ratiba tu."

Matarajio ya umma ni kwamba, kauli ya Waziri Mkuu bungeni inapaswa kutekelezwa kwani ndiye mkuu wa shughuli za serikali katika mhimili huo.

Hivyo, iwapo kauli ya Waziri Mkuu Pinda ambaye alisema Waziri wa Nishati na Madini (William Ngeleja) angeweza kutoa kauli ya serikali lakini ikashindikana, alipaswa kuueleza umma sababu hasa za kushindikana hilo.

Kushindwa kutoa kauli hiyo, kunaweza kutafsiriwa kwamba suala la mgodi wa Kiwira ni zito kwa serikali na kuna mkono wa watu wazito kama wanaotuhumiwa akiwemo Mkapa na Yona, ambao huenda wamepata mradi huo kinyume cha taratibu.

Tuhuma hizo nzito dhidi ya Mkapa ziliibuliwa na Mbunge wa Vunjo (CCM) Aloyce Kimaro, katika mkutano wa 11 wa Bunge la mwezi Aprili.

Kimaro aliibua tuhuma hizo akisema Mkapa akiwa madarakani kwa ushirikiano na Yona kwa kutumia Kampuni ya Tan Power Limited, walitumia madaraka kujibinafsishia mradi huo kwa bei ya Sh 700 milioni kisha wakalipa Sh 70 milioni katika mradi wenye thamani ya Sh 4 bilioni.

Mbunge huyo ambaye amejipatia umaarufu katika siku za karibuni baada ya kuibua sakata la nyumba, pia alimshutumu Mkapa kulihujumu Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupitia kampuni hiyo ya Tan Power ambayo inapaswa kulipwa Sh 146 milioni, kama Capacity Charge kwa siku.

Ingawa uongozi wa mgodi huo umejaribu kumsafisha Mkapa, lakini hadi sasa hakuna kauli rasmi ya serikali kuhusu ama kutohusika au kuhusika kwa mkuu huyo wa nchi mstaafu pamoja na Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona.
 
Back
Top Bottom