Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa amekanusha matumizi mabaya ya ofisi yake na kuanzisha biashara akiwa madarakani. Akihutubia wananchi katika Kijiji alichozaliwa cha Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkapa alisema wanaomtuhumu wanamchukia kwa kutowapendelea wakati wa utawala wake.


Na yeye ameenda kuseme a jimboni kwake kama Lowassa na Chenge? Wallahi hayawi hayawi sasa yamekuwa! Ukiona kunafuka moshi ujue chini kuna moto,

Haya ndugu wa mke kaeni chonjo sasa, mmetajirika kupindukia kipindi cha miaka mitano tu ya term yake ya pili, mkuu wangu Joe Maro wewe tulikuwa washikaji wote tumechacha hatuna kitu, leo mkuu unaendesha Range Rover ya kuletwa kwa ndege kutoka UK, hata wazungu wenyewe walimuandikia rais wetu wa sasa kuwa hawajawahi kuona gari likisafirishwa kwa ndege, ambayo gaharama yake ni sawa na kununua magari mengine mawili kama moja inyoletwa kwa ndege, wakamuuliza rais wetu kuwa hivi kweli taifa lako lina wananchi wenye mapesa kiasi hiki ya halali?

Hakuna masika yasiyokuwa na mvua, inaonekana mvua inaanza kukaribia kunyesha, maana sasa tunajionea bubu akitaka kusema, tunazo dataz zaidi za EPA na Mkapa na mkuu wa idara mstaafu, jinsi hata baada ya kugundulika kuwa huko BOT kuna utata na ishu ya EPA, bado accounts za EPA ziliendelea kuruhusiwa kutoa mapesa ya wananchi, wakati sheria za taifa za usalama zinataka zile accounts kuwa zimefungwa as soon ilipogundulika kuwa zina utata, zisingeruhusiwa tena kutoa mapesa, lakini kwa amri ya kutoka kwa mstaafu wa idara zikaendelea kururhusiwa tu, lakini cha ajabu zikasimamishwa pale tu accounts zote zilipokaukiwa na mapesa ya wananchi ambayo kina Chenge na Mramba, na hasa Mkapa, walikuwa tayari wamemaliza kuzichota na kuzihamisha, eti ndio mkuu wa usalama akaamuru zisimamishwe kutoa hela, too late hela za wananchi zimekwisha tayari,

Sasa Mkapa unayalilia magazeti kuwa hayana maana, eti Redio yetu haina maana, ulipokuwa unampa muungwana urais hakukuwa na tatizo na media zetu na redio zetu, lakini sasa kwa sababu unaulizwa maswali ya ufisadi wako unaanza kulia huko jimboni ambako kwa kawaida huwa hukujali hata mara moja, leo kuna wananchi huko eti wamekushangilia, what a shame? Mbona hayo maneno usiyasemee Dar?

Kuhusu ustaafu wako kwa nini usitum,ie mfano wa Mwalimu, kuwa umestaafu na unakula pension kama Mwalimu alipostaafu? Tuone kama kuna mwananchi hata mmoja angekushangilia, hakuna masika yasiyokuwa na mvua mkuu, masika tayari sasa subiri mvua inakujia mkuu tena very soon, kama huamini sasa subiri kikao kijacho cha bajeti, maana sasa tunazo dataz kuwa wabunge wote wa CCM, wamepewa kibali maalum cha maandishi na rais kutosumbuliwa tena na viongozi wa serilali na CCM, wanapotaka kumkoma nyani bungeni!

Mkuu wangu Muungwana, ulifanya kosa moja kubwa, nalo lilikuwa kuendekeza ushikaji, sasa wakati umefika wa kuwatema bila ya kuwaangalia usoni, according to the dataz ni kwamba mawaziri wengi zaidi kutemwa kwenye next bajeti.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Fisadi Mkapa kapata nguvu baada ya kifo cha Ballali, lakini hajui kwamba kubwabwaja kwake hakusaidii lolote maana anahusika katika ufisadi wa rada, ununuzi wa ndege ya rais uliofanyika akiwa amebakisha miezi miwili tu kumaliza muda wake, ununuzi wa magari ya jeshi na helicopters za jeshi, kujimilikisha yeye na Yona KCM katika mazingira ya kifisadi na kisha kuishinikiza TANESCO chini ya uongozi wa makaburu aliowaleta fisadi Mkapa kusaini mkataba wa kumlipa Mkapa shilingi 146 millioni kwa siku, kuchota mabilioni ya pesa kupitia account ya EPA pale BoT na kuyaingiza kwenye bank accounts za makampuni ya kifisadi na chama cha kifisadi na hatimaye kuishia mifukoni mwa mafisadi akiwamo Mkapa.

Fisadi Mkapa wacha kujidanganya, Watanzania tutaendelea kuuliza maswali mpaka kieleweke kwa ufisadi wako, mshahara na marupurpu yako uliyostahili kulipwa na Watanzania ni makubwa mno na hukustahili kufanya ufisadi sasa tamaa ya fisi imekuponza.
 
Tatizo ni kwamba JK bado amelikalia tawi hilo na kuegemea mti huo, kwa hiyo hathubutu kukata tawi wala mti! Na hana ujasiri kama wa Bingu wa Mutharika, na hata kama nafsi yake ikimtuma hivyo, hathubutu kwa kuwa athari za bifu kati ya Bingu na Bakili hapo jirani anaziona, pengine anaamini "bora nusu shari kuliko shari kamili". Lakini bahati mbaya labda bado hajaweza kutofautisha katika mazingira yake ya kibongo ya sasa, ipi nusu shari na ipi shari kamili! Na wahenga wa kwetu wanasema "Uthinyehe mumbango mbula yethinasha" maana yake "Usinye pangoni kabla mvua haijaisha" maana utaendelea kukaa pangoni humo, hivyo harufu hiyo itakutesa mwenyewe! Kwa mwungwana JK mvua haijaisha bado, analihitaji bado "pango" lake hathubutu "kulichafua"!
 
Fisadi Mkapa alikuwa Bubu kimya miezi yote hii, hata wiki moja haijaisha tangu Ballali kufariki na kuzikwa kapata nguvu ya kusema!!! Kama anataka kuongea kweli kwanini asiite news conference na kuwaruhusu waandishi wa babari wamuulize swali lolote na bila kujali news conference hiyo itachukua muda gani ajibu bila matusi wala vitisho kama alivyozoea kufanya. Kaamua kwenda kuongelea kijijini bila haya hata aibu. Ama kweli fisadi ni fisadi tu!!!
 
Hata ukiwauliza kina Kasusura na Ken Lay walisema not guilty kuhusu kashifa zao za wizi. Huwezi kuwa guilty kabla ya kufikishwa mahakamani, ngoja tukupeleke mahakamani kisha utajibu kwamba uliiba au laa.

Kwa nini usiende pale habari maelezo ukajibu hizo shutuma, kwa nini usije kwenye hadhira ya watu ukasema kwamba huusiki kujiuzia Kiwira, hujui kuhusu IPTL na hufahamu chochote kuhusu M bank.

Time is ticking, muda wako unakaribia. Hatutalala mpaka na wewe ushwe na karandinga pale Kisutu.
 
atasema tu! rais kuitwa fisadi barabarani kwanini asiseme! atasema na bado hasa!

yeye kila akinyamaza ndo the more we pile up the pressure, mwisho wake ndo kama hivi anaanza kusema kidogo kidogo!
 
Mzee Mkapa hiyo style ya kukana mbona ni kawaida tu? Sijashawishika kabisa jinsi ulivyochukua muda mrefu kusema "Huo (uvumi) ni uongo …uongo ….uongo ….uongo …uongo….uongo….uongo," Umejibu so general. Hata mtoto angeambiwa kaiba mboga angejibu "Huo (uvumi) ni uongo …uongo ….uongo ….uongo …uongo….uongo….uongo," huku akichuruzikwa michuzi.
Tunakusubiri utujibu KIWIRA COAL MINE NI YENU?
 
Kwanini Chinga azungumzie kijijini KWAO wakati alikuwa na dhamana ya kuongoza nchi hii kwa miaka 10?Atokeze tu mbele ya kamera ili dunia yote imwone hapo ndipo itafikia safari ya kwenda kuonana na Zombe huko.
 
Naanza Kupata Wasi Wasi Na Hao Wapakwa Mafuta...maana Ndio Jukwaa La Kujisafisha?hili La Bwm Ni La Pili Ukiachia Lile La El Alipompandisha....askofu Laizer...amsafishe
 
Sidhani kama kuna action (ya kisheria) yeyote itafanya dhidi yake,maana JK anaprotect ile mbaya, chukua mfano halisi wa Balali, JK kazungusha mpaka "kafa"
 
Kwahiyo Kanisa bado linapokea misaada kutoka kwa Mkapa pamoja na scandals zote alizonazo? Mafundisho ya Dini niliyopewa primary school yaliwahi toa maelezo yanayokingana na matendo yanayofanywa na kanisa leo hii. Vilevile, biblia inakemea waziwazi uungaji mkono wa mambo ya dizaini hii. Ama kweli njaa mbaya.... Duh!!!!!

Kanisa Katoliki lilitakiwa kuonyesha mfano mzuri kwa kukataa msaada kutoka kwa muumini fisadi anayefahamika kuwaongezea umaskini Wadanganyika kwa kiasi kikubwa; na muumini huyo kwa kiburi chake mpaka leo hii hajatoa maelezo in details kupinga DHAMBI alizowatendea Wadanganyika. Nitawaheshimu viongozi wa kanisa waliopokea msaada huu wakija tangaza siku za karibuni kwamba wametafakari na kuona kwamba walipokea kimakosa msaada huo ambao unaenda kinyume na mafundisho ya Biblia.


Msaada aliokabidhi Mkapa umetolewa na shirika moja la canada na si msaada kutoka mfukoni mwake. naomba kuweka rekodi sahihi wakati tukiendelea kuchangia hoja iliyopo mbele yetu.Tatizo labda ni fisadi kupewa dhamana ya kupeleka msaada kanisani!
 
Kumbe "Mr.Clean" kasingiziwa na wale ambao hakuwapendelea alipokuwa madarakani?! Nani hao akina Dr. Slaa au?
 
Naamini hapa ni mwanzo, walimtumia Balali kukidhi tamaa zao binafsi ila mzuka wake hautawaacha, mengi yatatokea na hapo alipoanzia ni mwanzo wa kiwewe na kuweweseka.
 
kwa nn kaongelea kwa wanakijiji wasio jua kuhoji maswali???na kwa nn ajibu tuhuma akiwa BUsh.........
 
umefika wakati waliokuwa wanusubiri ufike wajisafishe, Balali ameshakufa hakuna mtu wa kuwashitaki ndo maana wameanza kuibuka na kusema wanamsingizia, aje asemee maeklezo watu wamalize hasira zao kwa maswali uone kama hata hakuna alimgusa ataweza kusimama na kuondoka maana hayo maswali atayoulizwa hataweza kuyajibu na ataongeza maswali zaidi kwa uongo atakaousema.
 
Lakini si muungwana alishasema "mwacheni mzee apumzike", whether Ballali yuko hai au la! Hivyo hashitakiwi huyo!
 
Lakini si muungwana alishasema "mwacheni mzee apumzike", whether Ballali yuko hai au la! Hivyo hashitakiwi huyo!

"Mzee anayepumzika" alikubali kuchota pesa EPA ili muungwana azitumie katika kampeni na hatimaye kukalia usukani, lazima amlinde.

Ila pumziko lake halina amani yoyote japo utajiri unatiririka kila kona. Na kwa vile amekiri kuwa anajua wanasoma na kusikia meni, basi hata yeye nakala za makala za magazeti huwa anazichungulia na anajua hatumpendi, tunamchukia kwa wizi wa fedha zetu na siku serikali ya JK ikianguka, na wasongo wakatawala kabla hajafa, atawajibika. Pole zake chinga!
 
Back
Top Bottom