Mkandarasi anatulipisha Tsh 50,000 kwa nyumba kila mwezi kuzoa taka Masaki (Dar) lakini huduma ni mbovu

Anonymous

Senior Member
Feb 3, 2006
125
321
Mimi ni mkazi wa Masaki nimeona ripoti ya gharama za utoaji taka kuwa kubwa mitaa ya Mbezi Beach B (maarufu kwa jina la Mbezi Beachi ya Chini) nikaona nami nipaze sauti yangu kwa upende wetu wa Masaki ndani ya Jiji letu hili la Chalamila.

Huku Masaki gharama ni mara mbili ya Mbezi, Mkandarasi hutoza kuanzia kiasi cha Tsh. 40,000 mpaka Tsh. 50,000 kwa nyumba, ajabu ni kuwa kwa mwezi gari la kukusanya taka hupita mara moja tu likijitahidi saana litapita mara mbili kwa mwezi.

Kuna wakati baadhi ya maeneo hufika mpaka miezi miwili hadi mitatu hatujapata huduma wakati Mkandarasi anakuletea invoice na unalipishwa kinguvu, ukikataa unapelekwa kwenye Vyombo vya Sheria, vinakuhukumu ilipe hata kama hujapata huduma, mbaya zaidi ukimhoji Mkandarasi unajibiwa Halmashauri zinataka mapato lazima tu ulipe.

Jamani kama sio uonevu ni nini? Tunaonewa naombeni Vyomba vya Habari mtusaidie kufikisha malalamiko yetu kwenye mamlaka husika tafadhali.

Pia soma:

 
Hapo kinachotakiwa ni muende nao bampa to bampa.... Yani kubalini mtoe hiyo pesa na wao kila wiki wanatakiwa wapite kuzoa... Wasipozoa mnawaamshia popo au mnagoma.... Cha msingi ni ushirikiano, walazimisheni kila wiki wapite ili nao hiyo pesa waifanyie kazi
 
Samahani kama nitakukwaza.

Kama unaona 50K ni kubwa kwa mwezi ni kwamba hustahili kuishi masaki ina maana masaki sio level yako.

Kwani lazima uishi huko mkuu? Waache wenye uwezo wao waishi huko. Kulalamika hakutasaidia chochote.
Hata ingekuwa unaishi new York huwezi lipia Hela hata 100tsh kwa kitu ambacho huduma ni mbovu hebu fikiria unalipa 50000 kalwa mwezi wanakuja mara Moja hizo takataka za siku 29 utakaa nazo ndani? Hapo lazima utumie gharama zingine kutupa taka
 
Alafu mwisho wa mwezi siku ya usafi hakuna kufungua maduka.
Pesa yako na mwisho wa mwezi unafanya usafi
 
🤣🤣 njoo huku kwetu hatuna hizo huduma, huko waachie wenye pesa zao.
 
Ungesema tu, masaki huduma ya kuzoa taka ni mbovu japo mnachangia gharama stahili.
 
Mimi ni mkazi wa Masaki nimeona ripoti ya gharama za utoaji taka kuwa kubwa mitaa ya Mbezi Beach B (maarufu kwa jina la Mbezi Beachi ya Chini) nikaona nami nipaze sauti yangu kwa upende wetu wa Masaki ndani ya Jiji letu hili la Chalamila.

Huku Masaki gharama ni mara mbili ya Mbezi, Mkandarasi hutoza kuanzia kiasi cha Tsh. 40,000 mpaka Tsh. 50,000 kwa nyumba, ajabu ni kuwa kwa mwezi gari la kukusanya taka hupita mara moja tu likijitahidi saana litapita mara mbili kwa mwezi.

Kuna wakati baadhi ya maeneo hufika mpaka miezi miwili hadi mitatu hatujapata huduma wakati Mkandarasi anakuletea invoice na unalipishwa kinguvu, ukikataa unapelekwa kwenye Vyombo vya Sheria, vinakuhukumu ilipe hata kama hujapata huduma, mbaya zaidi ukimhoji Mkandarasi unajibiwa Halmashauri zinataka mapato lazima tu ulipe.

Jamani kama sio uonevu ni nini? Tunaonewa naombeni Vyomba vya Habari mtusaidie kufikisha malalamiko yetu kwenye mamlaka husika tafadhali.

Pia soma:

Wewe sio mkazi wa Masaki bhana watu huko awawezi lalamikia sh 40000 kwa mwezi wewe ludi manzese
 
Mimi ni mkazi wa Masaki nimeona ripoti ya gharama za utoaji taka kuwa kubwa mitaa ya Mbezi Beach B (maarufu kwa jina la Mbezi Beachi ya Chini) nikaona nami nipaze sauti yangu kwa upende wetu wa Masaki ndani ya Jiji letu hili la Chalamila.

Huku Masaki gharama ni mara mbili ya Mbezi, Mkandarasi hutoza kuanzia kiasi cha Tsh. 40,000 mpaka Tsh. 50,000 kwa nyumba, ajabu ni kuwa kwa mwezi gari la kukusanya taka hupita mara moja tu likijitahidi saana litapita mara mbili kwa mwezi.

Kuna wakati baadhi ya maeneo hufika mpaka miezi miwili hadi mitatu hatujapata huduma wakati Mkandarasi anakuletea invoice na unalipishwa kinguvu, ukikataa unapelekwa kwenye Vyombo vya Sheria, vinakuhukumu ilipe hata kama hujapata huduma, mbaya zaidi ukimhoji Mkandarasi unajibiwa Halmashauri zinataka mapato lazima tu ulipe.

Jamani kama sio uonevu ni nini? Tunaonewa naombeni Vyomba vya Habari mtusaidie kufikisha malalamiko yetu kwenye mamlaka husika tafadhali.

Pia soma:

Nimeenda serikali za mitaa kupta ufumbuzi ,wanazingua tu
 
Back
Top Bottom