Mkakati wa Kuingiza Nchi Kwenye Machafuko

Mkakati wa Kuingiza Nchi Kwenye Machafuko

Leo kanisani asubuhi Dr Mpango kakabidhi shilingi milioni 20 kule Bagamoyo kwa ajili ya mafuta ya gari la Baba Askofu Msomba.

Ni pesa aliyotumwa na Dr Samia aikabidhi kwa kanisa. Serikali yenye mbinu za hadharani pia inazo chafu za gizani.
Bila shaka hao maaskofu walifurahi sana na vigelegele chungu nzima juu yake mkuu 'Steven'.

Hata hivyo inashangaza kidogo kwamba unasahau kuwa hongo hii siyo ya kwanza kwa hawa viongozi wa dini, au hukumbuki?

Lakini hilo tuliache pembeni, mkuu wangu. Lakini nashangaa sana kwa mtu kama wewe kuandika hayo hapo juu. Yaani hilo limekugusa sana hadi ukaona ni muhimu ulilete humu? Hiyo milioni 20 inaweza kufuta maumivu ya aliyeumizwa. Hiyo milioni 20 unaamini ndiyo bei halisi ya hawa watu kuwanyamazisha?

Sikumbuki kilitolewa kiasi gani kule kwa Marehemu Mzee Kibao. umepata mrejesho wowote kuwa kiasi hicho ndicho kimewafuta machozi ya uchungu waliompoteza mzee wao?
Lakini hata huwezi kutambua 'implications' za maswala kama haya kwa taifa zima! Yaani nyinyi mmekuwa ni viongozi wa kununua utu wa waTanzania, kweli? Mna hakika hii ndiyo njia sahihi na ya kibinaadam ya kumaliza matatizo makubwa yanayolikabiri taifa hili kwa sasa? Huu ndio uongozi mnaoujuwa?

Haya, nasubiri kusikia kule kwa Mdude Nyagali kitatolewa kiasi gani; na kwa hao wengine wote wanaoendelea kuvunjiwa HAKI zao zitanunuliwa kwa kiasi gani.
Hizi hela zinatoka wapi, ni za walipa kodi, au ni zile toka kwa wajomba Oman na kwingineko?

Mkuu 'Stene', ulipo anza humu JF kidogo ulikuwa tofauti, sasa naona hali imekuwa nyingine kabisa!
 
Leo kanisani asubuhi Dr Mpango kakabidhi shilingi milioni 20 kule Bagamoyo kwa ajili ya mafuta ya gari la Baba Askofu Msomba.

Ni pesa aliyotumwa na Dr Samia aikabidhi kwa kanisa. Serikali yenye mbinu za hadharani pia inazo chafu za gizani.
Huu ni mchango wa maneno ya kusikitisha sana. Nimeusoma na kuandika nilichoandika mwanzo; lakini najikuta bado siwezi kuyatoa maneno haya kwenye akili zangu, yanaendela tu kujirudia rudia kichwani kama mwangwi vile.

Hii ndiyo njia mtakayo endelea nayo kuwatawala waTanzania?
 
Samia ndiye atakayeleta machafuko katika hili taifa. Na ameshaleta tayari.
Kabisa, kuuza, misitu, Bandari, Ngorongoro kuwaondoa Wamasai ili waarabu wawinde na kuua Simba, Twiga Pundamilia ni kuleta machafuko.

Kutaka kumuua Padre Kitima ni kuleta machafuko.
 
Jambo hili sio jepesi kulisema lakini hakuna budi lisemwe bila kupindisha maneno. Viongozi wa CHADEMA wanataka vurugu na machafuko yaliyotokea Kenya na maeneo mengine duniani yatokee nchini kwetu kama njia ya kuzuia au kuvuruga uchaguzi.

Baada ya Fr Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu (TEC) kujeruhiwa, jana Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Ndugu Godbless Lema, ameandika kuwataka Maaskofu watoe tamko ili waumini wao wasusie uchaguzi.

Pia, Ndugu Godlisen Malisa ambaye ni mwanachama wa CHADEMA ameandika kwenye ukurasa wake wa instagram akimtaka Askofu Mkuu wa KKKT atoe tamko. Wafuasi wake wamemshambulia sana Askofu Malasusa kwa kila aina ya matusi bila yeye kuchukua hatua zozote.

Naye Bi. Maria Sarungi, shabiki na mshirika wa karibu wa Tundu Lissu aliyeko nchini Kenya akiratibu na kuhamasisha matukio haya kwa msaada wa mataifa ambayo hayana nia njema na nchi yetu, ameandika kwamba aliyekamatwa na Polisi hausiki!! Amejuaje hausiki? Aliyepigwa yuko hospitalini. Je anamjua aliyempiga? Alimuona na kumtambua usiku saa nne?

Maria anasema aliyekamatwa alikuwa anakula tu Kanteen ya TEC. Sasa mtu akiwa anakula hawezi kuwa mshirika wa tukio? Maria anajuaje mtu huyo hakuwa anakula kama sehemu ya mpango wa kutekeleza uhalifu? Anajuaje hakuwa pale akiwaambia aliopanga nao muda Fr Kitima akinyanyuka wakae tayari kumshambulia?

Hii sio bahati mbaya hata kidogo. Ni mkakati maalumu wa kuchochea vurugu za kisiasa kwa kutumia dini.

Suala la kupigwa na kujeruhiwa kwa Fr Kitima ni muendelezo wa mpango wa makusudi kuigombanisha Serikali na wananchi, haswa wa dini ya kikristo.

Ni lazima watanzania tuwe makini sana. Amani na utulivu wa nchi yetu ni lazima tuvilinde. Niwahakikishie, hapa kinachotafutwa na CHADEMA ni ‘trigger point’ (jambo litakalosababisha chuki isiyomithilika kwa kundi fulani aidha vijana au waumini wa dini) ili kuanzisha vurugu na machafuko kuzuia uchaguzi.

Viongozi wa CHADEMA wanatafuta kila namna nchi yetu ionekane inakiuka haki za binadamu iwekewe vikwazo! Wanawaaminisha wafuasi wao kwamba wanakubalika ila wanaonewa na sasa wanaumizwa!

Hii ndio nia yao! Hakuna namna wataweza kushinda uchaguzi sasa wameamua kutekeleza mkakati huu ovu. Wanachi wenzangu, tusikubali kuingizwa mtegoni. TUSIKUBALI. Tuilinde nchi yetu. Tuelimishane. Tuhimizane upendo na kuthaminiana. Tupingane kwa hoja. Tuhakikishe hakugawanyiki 🙏🏿
Umeandika uongo na utumbo
 
Huu ni mchango wa maneno ya kusikitisha sana. Nimeusoma na kuandika nilichoandika mwanzo; lakini najikuta bado siwezi kuyatoa maneno haya kwenye akili zangu, yanaendela tu kujirudia rudia kichwani kama mwangwi vile.

Hii ndiyo njia mtakayo endelea nayo kuwatawala waTanzania?
Miradi mikubwa inayoendelea kuzinduliwa nchi nzima ndio njia sahihi inayotumiwa na serikali katika kuwavuta wananchi.

Hizi kelele za JF na uanaharakati huanzia na humalizikia mitandaoni, watanzania wenyewe wapo huko mikoani na wanayaona yote yanayofanywa na serikali yao.
 
Miradi mikubwa inayoendelea kuzinduliwa nchi nzima ndio njia sahihi inayotumiwa na serikali katika kuwavuta wananchi.

Hizi kelele za JF na uanaharakati huanzia na humalizikia mitandaoni, watanzania wenyewe wapo huko mikoani na wanayaona yote yanayofanywa na serikali yao.
Hawa watanzania mnaowafuga kama mifugo; na hasa kama mbwa wa kuwatupia mifupa ili wafurahi na kuwashukuru kwa kutingisha mikia sijui mmewatoa wapi nyinyi; kama siyo fikra za kijinga kabisa.

Muwanyime HAKI ya kuchagua viongozi wanaowataka wao; halafu waje kwenu kutoa shukrani za kuwapa Tsh20 milioni, baada ya kuwaumiza!. Hawa watu mliowaondoa uwezo wa kufikiri, nyinyi mmewaokota wapi?

Kama hizi ni kelele za JF kama unavyo sema wewe; na unajuwa mnapendwa sana kwa sababu ya miradi hiyo; nini kinacho watia hofu ya kufanyika uchaguzi HURU na wa HAKI utakao wachagua nyinyi mnaopendwa sana na waTanzania?

hayo maneno hapo juu, umeyarudia rudia sana kuyaandika humu kama ilivyo kawaida yako. Kama hizi kelele za huku JF hazina lolote, mbona unarudi rudi humu; pamoja na kwamba huna mchango wowote wa maana tokea uingie humu kwa kazi ya kutetea maovu!

Sasa tunaelekea ukingoni. Oktoba haipo mbali. Msipo stuka wakati huu na kufanya marekebisho ili msiendelee kulazimisha watu muwatawale; mtaingia kwenye historia mpya kwa yote yatakayotokea.
 
Hawa watanzania mnaowafuga kama mifugo; na hasa kama mbwa wa kuwatupia mifupa ili wafurahi na kuwashukuru kwa kutingisha mikia sijui mmewatoa wapi nyinyi; kama siyo fikra za kijinga kabisa.

Muwanyime HAKI ya kuchagua viongozi wanaowataka wao; halafu waje kwenu kutoa shukrani za kuwapa Tsh20 milioni, baada ya kuwaumiza!. Hawa watu mliowaondoa uwezo wa kufikiri, nyinyi mmewaokota wapi?

Kama hizi ni kelele za JF kama unavyo sema wewe; na unajuwa mnapendwa sana kwa sababu ya miradi hiyo; nini kinacho watia hofu ya kufanyika uchaguzi HURU na wa HAKI utakao wachagua nyinyi mnaopendwa sana na waTanzania?

hayo maneno hapo juu, umeyarudia rudia sana kuyaandika humu kama ilivyo kawaida yako. Kama hizi kelele za huku JF hazina lolote, mbona unarudi rudi humu; pamoja na kwamba huna mchango wowote wa maana tokea uingie humu kwa kazi ya kutetea maovu!

Sasa tunaelekea ukingoni. Oktoba haipo mbali. Msipo stuka wakati huu na kufanya marekebisho ili msiendelee kulazimisha watu muwatawale; mtaingia kwenye historia mpya kwa yote yatakayotokea.
Wenye akili timamu wanajua kuwa uchaguzi mkuu ni mchakato wa kuja na kuondoka, huwa wanatazama kitu gani chenye kutazamika na kushikika kinachoachwa na huo uchaguzi.

SGR inakamalika muda huu limebakia eneo dogo tu kuelekea Mwanza.

Viwanja vya ndege vinakamilika muda huu nchi nzima.

Maji yanapatikana karibu kila mahali Tanzania. Umeme umesambazwa mikoa karibu yote.

Hayo ni masuala yenye kuwapa heshima CCM mbele ya mpiga kura. Hizi siasa za kina Lissu na uanaharakati huwa ni habari ya muda mfupi inayokuwepo haswa miaka hii ya uchaguzi.
 
Hivi mnajua machafuko yanavyotokea nyie au huwa mnajiwehusha tu kudhani watu wakiandika kwenye mitandao ndio kutokea kwa machafuko?

Tokea lini mtu apange machafuko na aandike mahali ambapo polisi na vyombo vya dola vinaona?
Hahaha watu wanasema tu machafuko machafuko.
 
Huo mkakati upo na umesukwa kwa kukitumia Chadema ili kuvunja au kuvuruga uchaguzi wa nchi.
Vyombo vya ulinzi na usalama fuatilieni watu hao hadi chooni.
Mjinga kabisa wewe. Mtu kukuambia anataka UCHAGUZI HURU, WA HAKI na wenye kuaminika ndo kuvuruga amani ya nchi?
Imlisoma shule gani nyie MACHAWA!
Amani ya nchi wanavuruga CCM, TISS, POLISI NA TUME YA UCHAGU!I
 
Jambo hili sio jepesi kulisema lakini hakuna budi lisemwe bila kupindisha maneno. Viongozi wa CHADEMA wanataka vurugu na machafuko yaliyotokea Kenya na maeneo mengine duniani yatokee nchini kwetu kama njia ya kuzuia au kuvuruga uchaguzi.

Baada ya Fr Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu (TEC) kujeruhiwa, jana Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Ndugu Godbless Lema, ameandika kuwataka Maaskofu watoe tamko ili waumini wao wasusie uchaguzi.

Pia, Ndugu Godlisen Malisa ambaye ni mwanachama wa CHADEMA ameandika kwenye ukurasa wake wa instagram akimtaka Askofu Mkuu wa KKKT atoe tamko. Wafuasi wake wamemshambulia sana Askofu Malasusa kwa kila aina ya matusi bila yeye kuchukua hatua zozote.

Naye Bi. Maria Sarungi, shabiki na mshirika wa karibu wa Tundu Lissu aliyeko nchini Kenya akiratibu na kuhamasisha matukio haya kwa msaada wa mataifa ambayo hayana nia njema na nchi yetu, ameandika kwamba aliyekamatwa na Polisi hausiki!! Amejuaje hausiki? Aliyepigwa yuko hospitalini. Je anamjua aliyempiga? Alimuona na kumtambua usiku saa nne?

Maria anasema aliyekamatwa alikuwa anakula tu Kanteen ya TEC. Sasa mtu akiwa anakula hawezi kuwa mshirika wa tukio? Maria anajuaje mtu huyo hakuwa anakula kama sehemu ya mpango wa kutekeleza uhalifu? Anajuaje hakuwa pale akiwaambia aliopanga nao muda Fr Kitima akinyanyuka wakae tayari kumshambulia?

Hii sio bahati mbaya hata kidogo. Ni mkakati maalumu wa kuchochea vurugu za kisiasa kwa kutumia dini.

Suala la kupigwa na kujeruhiwa kwa Fr Kitima ni muendelezo wa mpango wa makusudi kuigombanisha Serikali na wananchi, haswa wa dini ya kikristo.

Ni lazima watanzania tuwe makini sana. Amani na utulivu wa nchi yetu ni lazima tuvilinde. Niwahakikishie, hapa kinachotafutwa na CHADEMA ni ‘trigger point’ (jambo litakalosababisha chuki isiyomithilika kwa kundi fulani aidha vijana au waumini wa dini) ili kuanzisha vurugu na machafuko kuzuia uchaguzi.

Viongozi wa CHADEMA wanatafuta kila namna nchi yetu ionekane inakiuka haki za binadamu iwekewe vikwazo! Wanawaaminisha wafuasi wao kwamba wanakubalika ila wanaonewa na sasa wanaumizwa!

Hii ndio nia yao! Hakuna namna wataweza kushinda uchaguzi sasa wameamua kutekeleza mkakati huu ovu. Wanachi wenzangu, tusikubali kuingizwa mtegoni. TUSIKUBALI. Tuilinde nchi yetu. Tuelimishane. Tuhimizane upendo na kuthaminiana. Tupingane kwa hoja. Tuhakikishe hakugawanyiki 🙏🏿
Wakisaidiwa na Hawa hapa 👇 👇

View: https://x.com/stats_feed/status/1920530641575121176?t=oOge8KhbRSjgOQxLhSh3hg&s=19
 
Wenye akili timamu wanajua kuwa uchaguzi mkuu ni mchakato wa kuja na kuondoka, huwa wanatazama kitu gani chenye kutazamika na kushikika kinachoachwa na huo uchaguzi.

SGR inakamalika muda huu limebakia eneo dogo tu kuelekea Mwanza.

Viwanja vya ndege vinakamilika muda huu nchi nzima.

Maji yanapatikana karibu kila mahali Tanzania. Umeme umesambazwa mikoa karibu yote.

Hayo ni masuala yenye kuwapa heshima CCM mbele ya mpiga kura. Hizi siasa za kina Lissu na uanaharakati huwa ni habari ya muda mfupi inayokuwepo haswa miaka hii ya uchaguzi.
Wewe sasa nakuweka kwenye kundi stahiki; pamoja na yule ndugu yako MAITI Tlaatlaah.
Nyote mlikuja hapa kwa kazi moja tu, ya kutetea kila anachofanya Samia, kiwe kizuri, kibaya kazi yenu ni kusifu tu.

Zaidi ya hivyo, inavyoonekana sasa wewe na huyo Tlaatlaah na wengineo mtakuwa ni sehemu ya genge linalowatendea maovu waTanzania kwa huu utekaji na mauaji. Hata siku moja hujathubutu kuandika chochote kuhusu uovu huu, maana yake ni kuwa wewe ni mshiriki.

Kila unacho andika humu hakina maana yoyote bali kuwadharau waTanzania. Sasa kama wewe ni sehemu ya waOman mliopo hapa kututawala na kutudhalilisha kupitia kwa mpwa wenu, elewa hilo haliwezekani tena.

Unahangaika hapa ukidhani mtalazimisha Samia aendelee kuvuruga nchi hii. Kumbakisha madarakani kwa nguvu safari hii hapana.
 
Jambo hili sio jepesi kulisema lakini hakuna budi lisemwe bila kupindisha maneno. Viongozi wa CHADEMA wanataka vurugu na machafuko yaliyotokea Kenya na maeneo mengine duniani yatokee nchini kwetu kama njia ya kuzuia au kuvuruga uchaguzi.

Baada ya Fr Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu (TEC) kujeruhiwa, jana Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Ndugu Godbless Lema, ameandika kuwataka Maaskofu watoe tamko ili waumini wao wasusie uchaguzi.

Pia, Ndugu Godlisen Malisa ambaye ni mwanachama wa CHADEMA ameandika kwenye ukurasa wake wa instagram akimtaka Askofu Mkuu wa KKKT atoe tamko. Wafuasi wake wamemshambulia sana Askofu Malasusa kwa kila aina ya matusi bila yeye kuchukua hatua zozote.

Naye Bi. Maria Sarungi, shabiki na mshirika wa karibu wa Tundu Lissu aliyeko nchini Kenya akiratibu na kuhamasisha matukio haya kwa msaada wa mataifa ambayo hayana nia njema na nchi yetu, ameandika kwamba aliyekamatwa na Polisi hausiki!! Amejuaje hausiki? Aliyepigwa yuko hospitalini. Je anamjua aliyempiga? Alimuona na kumtambua usiku saa nne?

Maria anasema aliyekamatwa alikuwa anakula tu Kanteen ya TEC. Sasa mtu akiwa anakula hawezi kuwa mshirika wa tukio? Maria anajuaje mtu huyo hakuwa anakula kama sehemu ya mpango wa kutekeleza uhalifu? Anajuaje hakuwa pale akiwaambia aliopanga nao muda Fr Kitima akinyanyuka wakae tayari kumshambulia?

Hii sio bahati mbaya hata kidogo. Ni mkakati maalumu wa kuchochea vurugu za kisiasa kwa kutumia dini.

Suala la kupigwa na kujeruhiwa kwa Fr Kitima ni muendelezo wa mpango wa makusudi kuigombanisha Serikali na wananchi, haswa wa dini ya kikristo.

Ni lazima watanzania tuwe makini sana. Amani na utulivu wa nchi yetu ni lazima tuvilinde. Niwahakikishie, hapa kinachotafutwa na CHADEMA ni ‘trigger point’ (jambo litakalosababisha chuki isiyomithilika kwa kundi fulani aidha vijana au waumini wa dini) ili kuanzisha vurugu na machafuko kuzuia uchaguzi.

Viongozi wa CHADEMA wanatafuta kila namna nchi yetu ionekane inakiuka haki za binadamu iwekewe vikwazo! Wanawaaminisha wafuasi wao kwamba wanakubalika ila wanaonewa na sasa wanaumizwa!

Hii ndio nia yao! Hakuna namna wataweza kushinda uchaguzi sasa wameamua kutekeleza mkakati huu ovu. Wanachi wenzangu, tusikubali kuingizwa mtegoni. TUSIKUBALI. Tuilinde nchi yetu. Tuelimishane. Tuhimizane upendo na kuthaminiana. Tupingane kwa hoja. Tuhakikishe hakugawanyiki 🙏🏿
WANATAKA WAKINUKISHE KISHA WAKIMBILIE CANADA NA UBELIGIJ.UROHO WA MADARAKA UTAWATOKEA PUANI
 
Wewe sasa nakuweka kwenye kundi stahiki; pamoja na yule ndugu yako MAITI Tlaatlaah.
Nyote mlikuja hapa kwa kazi moja tu, ya kutetea kila anachofanya Samia, kiwe kizuri, kibaya kazi yenu ni kusifu tu.

Zaidi ya hivyo, inavyoonekana sasa wewe na huyo Tlaatlaah na wengineo mtakuwa ni sehemu ya genge linalowatendea maovu waTanzania kwa huu utekaji na mauaji. Hata siku moja hujathubutu kuandika chochote kuhusu uovu huu, maana yake ni kuwa wewe ni mshiriki.

Kila unacho andika humu hakina maana yoyote bali kuwadharau waTanzania. Sasa kama wewe ni sehemu ya waOman mliopo hapa kututawala na kutudhalilisha kupitia kwa mpwa wenu, elewa hilo haliwezekani tena.

Unahangaika hapa ukidhani mtalazimisha Samia aendelee kuvuruga nchi hii. Kumbakisha madarakani kwa nguvu safari hii hapana.
Mungu ndiye mwenye mipango mikubwa na yenye kustahili kuheshimiwa siku zote. JPM alipoaga dunia mrithi wake akachukua madaraka. Hakuna aliyetegemea kuwa ufikapo mwaka 2025 Mwezi May JPM awe tayari ameshaaga dunia miaka minne iliyopita.

Tuwe wapole tu, kulialia kukizidi inageuka kuwa kufuru kwa Mungu.
 
Mungu ndiye mwenye mipango mikubwa na yenye kustahili kuheshimiwa siku zote. JPM alipoaga dunia mrithi wake akachukua madaraka. Hakuna aliyetegemea kuwa ufikapo mwaka 2025 Mwezi May JPM awe tayari ameshaaga dunia miaka minne iliyopita.

Tuwe wapole tu, kulialia kukizidi inageuka kuwa kufuru kwa Mungu.
Huyo mungu wenu mnayemtanguliza mbele wakati mkifanya maovu ni mungu wa namna gani huyo, kama siyo shetani. mwenyewe. Nyote, katika kundi lenu, na huyo maiti Tlaatlaah; kila siku ni kutanguliza mungu katika maandishi humu wakati mkitimiza mipango ovu. Mnamdanganya nani, kama hamjidanganyi wenyewe.

Nilisha kwambia siku nyingi, safari hii hamponi. Maovu haya mnayowafanyia waTanzania italazimu mfikishwe mbele ya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili. Hamtaachwa tu muendele kufaidi matunda ya uovu wenu baada ya kuondolewa madarakani.
Subiri, utatambua nani analialia.
 
Huyo mungu wenu mnayemtanguliza mbele wakati mkifanya maovu ni mungu wa namna gani huyo, kama siyo shetani. mwenyewe. Nyote, katika kundi lenu, na huyo maiti Tlaatlaah; kila siku ni kutanguliza mungu katika maandishi humu wakati mkitimiza mipango ovu. Mnamdanganya nani, kama hamjidanganyi wenyewe.

Nilisha kwambia siku nyingi, safari hii hamponi. Maovu haya mnayowafanyia waTanzania italazimu mfikishwe mbele ya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili. Hamtaachwa tu muendele kufaidi matunda ya uovu wenu baada ya kuondolewa madarakani.
Subiri, utatambua nani analialia.
Wewe unayaona maovu lakini wengi sana wanayaona ni mema sana.

Unapoilaani CCM kwa kufanya maovu wale kinamama vijijini wanaopata matibabu kwenye zahanati mpya wanaiombea mema serikali hiyo hiyo.

Unapoilaani CCM kwa maovu kuna wafanyabiashara wanaofikisha bidhaa zao huko Ulaya na kwingineko ndani ya muda huu huu hao wanaibariki kwa fursa kufunguliwa.

Kuna wale wadau wa sekta nzima ya madini, wanapowezeshwa kupata zana za kisasa za uchimbaji wanaibariki serikali hii hii na ilani zake.

Kila sehemu ambapo ipo miundo mbinu ya usafiri na umeme maana yake pameshafunguliwa tayari kwa ajili ya fursa nyingi tu za kimaendeleo.

Na kote huko wapo mamilioni ya watu wanaoibariki serikali ambayo wewe Kalamu unailaani!. Tatizo la wanaharakati ni kudhania kuwa maisha ya TZ yanaanzia na kuishia humu humu Dar huwa hamna vichwani mwenu ile picha pana ya maana halisi ya taifa lenye watu milioni 64.
 
Jambo hili sio jepesi kulisema lakini hakuna budi lisemwe bila kupindisha maneno. Viongozi wa CHADEMA wanataka vurugu na machafuko yaliyotokea Kenya na maeneo mengine duniani yatokee nchini kwetu kama njia ya kuzuia au kuvuruga uchaguzi.

Baada ya Fr Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu (TEC) kujeruhiwa, jana Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Ndugu Godbless Lema, ameandika kuwataka Maaskofu watoe tamko ili waumini wao wasusie uchaguzi.

Pia, Ndugu Godlisen Malisa ambaye ni mwanachama wa CHADEMA ameandika kwenye ukurasa wake wa instagram akimtaka Askofu Mkuu wa KKKT atoe tamko. Wafuasi wake wamemshambulia sana Askofu Malasusa kwa kila aina ya matusi bila yeye kuchukua hatua zozote.

Naye Bi. Maria Sarungi, shabiki na mshirika wa karibu wa Tundu Lissu aliyeko nchini Kenya akiratibu na kuhamasisha matukio haya kwa msaada wa mataifa ambayo hayana nia njema na nchi yetu, ameandika kwamba aliyekamatwa na Polisi hausiki!! Amejuaje hausiki? Aliyepigwa yuko hospitalini. Je anamjua aliyempiga? Alimuona na kumtambua usiku saa nne?

Maria anasema aliyekamatwa alikuwa anakula tu Kanteen ya TEC. Sasa mtu akiwa anakula hawezi kuwa mshirika wa tukio? Maria anajuaje mtu huyo hakuwa anakula kama sehemu ya mpango wa kutekeleza uhalifu? Anajuaje hakuwa pale akiwaambia aliopanga nao muda Fr Kitima akinyanyuka wakae tayari kumshambulia?

Hii sio bahati mbaya hata kidogo. Ni mkakati maalumu wa kuchochea vurugu za kisiasa kwa kutumia dini.

Suala la kupigwa na kujeruhiwa kwa Fr Kitima ni muendelezo wa mpango wa makusudi kuigombanisha Serikali na wananchi, haswa wa dini ya kikristo.

Ni lazima watanzania tuwe makini sana. Amani na utulivu wa nchi yetu ni lazima tuvilinde. Niwahakikishie, hapa kinachotafutwa na CHADEMA ni ‘trigger point’ (jambo litakalosababisha chuki isiyomithilika kwa kundi fulani aidha vijana au waumini wa dini) ili kuanzisha vurugu na machafuko kuzuia uchaguzi.

Viongozi wa CHADEMA wanatafuta kila namna nchi yetu ionekane inakiuka haki za binadamu iwekewe vikwazo! Wanawaaminisha wafuasi wao kwamba wanakubalika ila wanaonewa na sasa wanaumizwa!

Hii ndio nia yao! Hakuna namna wataweza kushinda uchaguzi sasa wameamua kutekeleza mkakati huu ovu. Wanachi wenzangu, tusikubali kuingizwa mtegoni. TUSIKUBALI. Tuilinde nchi yetu. Tuelimishane. Tuhimizane upendo na kuthaminiana. Tupingane kwa hoja. Tuhakikishe hakugawanyiki 🙏🏿
HAKI ina gharama kiduchu sana kuliko DHULUMA. Moyo wangu unatetemeka.Ee Mungu nakuomba uingilie Kati🙏
 
Wewe unayaona maovu lakini wengi sana wanayaona ni mema sana.

Unapoilaani CCM kwa kufanya maovu wale kinamama vijijini wanaopata matibabu kwenye zahanati mpya wanaiombea mema serikali hiyo hiyo.

Unapoilaani CCM kwa maovu kuna wafanyabiashara wanaofikisha bidhaa zao huko Ulaya na kwingineko ndani ya muda huu huu hao wanaibariki kwa fursa kufunguliwa.

Kuna wale wadau wa sekta nzima ya madini, wanapowezeshwa kupata zana za kisasa za uchimbaji wanaibariki serikali hii hii na ilani zake.

Kila sehemu ambapo ipo miundo mbinu ya usafiri na umeme maana yake pameshafunguliwa tayari kwa ajili ya fursa nyingi tu za kimaendeleo.

Na kote huko wapo mamilioni ya watu wanaoibariki serikali ambayo wewe Kalamu unailaani!. Tatizo la wanaharakati ni kudhania kuwa maisha ya TZ yanaanzia na kuishia humu humu Dar huwa hamna vichwani mwenu ile picha pana ya maana halisi ya taifa lenye watu milioni 64.
Ndio mfanye reforms sasa ili mshinde kwa kishindo!
 
Mimi CDM nawashangaa huku kwetu matawi yote ya CDM yamekufa kimebakia kuwa Chama Cha mitandaoni tu Sasa huo uchaguzi watashinda vipi
 
Back
Top Bottom