Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

UKAWA hakuna nafasi ya mafisadi aende zake huko. UKAWA hawawezi kufanya makosa ya kipumbavu ya kumkaribisha huyu fisadi.

Najua ulipata ugumu sana kuelewa tunamaanisha nini tukisema Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai. Kila siku kinabuni mbinu mpya za kuwalaghai watu.
Werevu kama Dr. Slaa wameshashtuka...
 
Mtoa mada umeongelea Lowassa 'kugawa pesa kama njugu' ili awe rais. Nakukumbusha kuwa UKAWA haihitaji mgombea mwenye sifa kama hiyo! Na siyo mgombea tu, bali haihitaji hata mwanachama wa kawaida tu kuwa na hiyo sifa ya kutoa rushwa.

LOWASSA hawezi bila CCM, Acheni kujidanganya!

Mkuu hawa BAVICHA wengi ni walevi wa mirungi! Lowassa sio mjinga kama wanavyodhani!

UKAWA wasimkatae akija kama mwanachama au kugombea jimbo la Munduli lakini si cheo cha uraisi. Kwa nini aje mwisho kisha apewe ugombeaji wa uraisi? Maana yake shida yake ni urais walasi upinzani! Alikuwa na nafasi nzuri sana muda wote kuingia upinzania hawezi tena. Pili hana jipwa Lowasa, alisha zeeka apumzike huyu.

Dah! ni sawa na kubeba sufuria la moto

sisi hatupokei watu wachafu

Nashangaa watu wanavyomnadi EL huyu hawezi kuwa rais wa Tanzania pamoja na njugu zote anazomwaga, watakula na kuvimbiwa kama JK alivyovimbiwa wizi kwa miaka 10 iliyopita. Hana jipya. wakuu endeleeni kufaidi hizo njugu kutoka Voda phone hazina mwenyewe. Kiini cha kuvuruga shirika la simu Tanzania.

UKAWA hatuwezi kumpokea mtu mchafu kama Lowassa

Lowassa ndo huyu hawezi hata kukimbia mitaa 100

Baadhi ya posts kutoka kwa newly found mashabiki wa Lowassa walivyosema 2014
Kuna kudhalilishwa na kujidhalilisha
Maskini Ukawa mnakula matapishi yenu
Mungu amzidishie nguvu Dr Slaa na Prof Lipumba kwa hekima waliyo nayo ya kukaa pembeni.
Cha kusikitisha ni kuwa tulikuwa tunachangia harakati tulizodhani ni za dhati kumbe ni backroom deal ya Mbowe.
Sasa kuamua kujivua ufahamu ni dhambi kubwa sana!
 
kukwagua gwaride hataweza .Lowasa akishinda uraisi ntatembea uchi dar-moro

Wenye kuwania urais kupitia sisiemu na wanaokubalika wapo kimya, nashangaa nyie mapovu kila siku. Huyo ni mwizi, na silaha ambayo upinzani wataitumia dhidi yake ni Richmond. Tambua watz si wajinga kama wewe na team yako mnavyodhani.

Kuna jitihada zozote amezifanya za kuwahakikishia wananchi kuwa alionewa? Au anavyogawa pesa kama njugu ndo kuwaonyesha kuwa alionewa? Sijapandikizwa chuki. Ni kwamba hana sifa na ana skendo.

hata akijisafisha na magadi bado ataendelea kuwa mchafu

ninyi ndio mbulala mnaotusumbua hapa tz. kwa mtindo huu tutakuwa na lundo la wezi wanaojisafisha halafu nyie mnapewa ela . ni afadhari ya kuishi na mbuzi lakini sio na watu kama nyie .

Mmmh ata kuja kuharibu chama yule

Ataingia ACT au TLP kwa Mrema ili apate kugombea urais

Jamani Ikulu ni pahali patakatifu sio kwa kuhonga kunakofanywa wazi wazi hivyo...tuwe wakweli CCM IWE MAKINI NA IMSAIDIE MUNGU SIO KUBEBA WALA RUSHWA NA KUHONGA KUINGIA IKULU.

Yani huyo Lowasa yeye ni spacial kiasigani, hata atoke ccm asubuhi, jioni aingie Ukawa nakupewa nafasi ya juu kiasihicho!!.

Ivi huko UKAWA ndo wanapokea mafisadi

Naendelea kusoma maoni ya wadau ya 2014..
Dah! Nasubiri waje kulamba matapishi yao wana Ukawa.
Hivi arguments hizi ndo zinabadilika overnight? Sasa tukiwapa nchi mkihongwa na Pablo Escobar si mtauza nchi?
Aibu sana!
 
Kama UKAWA lengo lao kuu ni kushinda uRais tu (kiasi cha hata kumtumia mtu kama Lowasa), basi HAWATUFAI! Nchi inahitaji marekebisho makubwa sana kisiasa. Watu kama Lowasa (na wenzake huko CCM) wanawakilisha uozo unaolitesa taifa letu leo hii.

Mkuu upo bado?
Umeongea kile ambacho leo mashabiki wa Ukawa na Chadema hawataki kusikia eti tunataka kuing'oa CCM
Sasa hebu waeleze loud and clear kama ulivyofanya miezi kadhaa iliyopita:
LOWASA ANAWAKILISHA UOZO UNAOLITESA TAIFA LETU LEO
Na akina Mnyika, Lissu, Baregu wote wanajua hili!

Ukawa shame on you! You sold us for 30 pieces of silver!
 
Acha sitaki - nataka!Lowasa hafai hafai basi oo sijui awe mwanachama wa kawaida wa kazi gani?Kama ni mwanachama ana haki ya kugombea urais!

Ukawa hauijui wewe!

ukawa hatutaki mapepo!! huko huko

Kwa7bu hzo bora CCM ife kuliko kumweka huyu mtumwa wawahindi. Inaniuma sn kuona watu timamu mnamsafisha mtu alie tuingza kwenye hasara kubwa wakati wapo watu wasio fungamana na makundi jaman huyu mzee hafai

EL ni kielelezo cha vyote ambavyo ukawa wanapinga. Haitawezekana kumpokea kwa vyovyote vile. Labda kama ukawa watakuwa wamerukwa na akili.

Haya tuendelee na mjadala!
Sibonike Ukawa wamerukwa na akili kama ulivyotabiri!
Babu Chodo mapepo yamehamia Ukawa!
 
duuh kweli kuna watu wa ajabu hapa JF ukiwasoma wote hao tena waliapa leo ndiyo watetezi wa wa Lowasa wengine walidrilki kueuelza wanaachana na siasa wengine waliandika jambo lisilo wezekana leo wanamwona Lowasa hero nimewadharau kwa kweli
 
Ule msemo usemao " hifadhini maneno yenu" umeonyesha maana kubwa leo. Nyeti zao ziko wazi baada ya upepo kuvuma. Members wote warudie kusoma walichosema hapo nyuma kupitia huu uzi.....ahsante mods kwa kututunzia huu uzi. ....lets wait...loading....
 
Back
Top Bottom