Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

sisi hatutaki

SUPU YA MAWE: Huko kwetu supu ya mawe ni pombe haramu ya chang'aa!

On a serious note, tafuta thread yangu yenye title "Ndoto ya matumaini ya Lowassa kuishia CC ya CCM"

Mpaka sasa hivi mikakati ya CCM ni kukata jina la Lowassa kwenye CC ya CCM. Vigunge wa CCM na hasa Mwenyekiti wao hawataki kabisa Lowassa awe next Rais wa JMT, kwasababu hawajui Lowassa atamfanya nini JK na Ridhwani baada ya kumtosa kwenye sakata la Richmond.

Mkulu alikwisha mwambia Lowassa aachane na ndoto ya Urais, lakini Lowassa akamwambia kwamba ni haki yake ya kikatiba hivyo amuache demokrasia ichukue mkondo wake ndani ya CCM, halafu Watanzania tutaamua.

Lakini pia baada ya muungano wa UKAWA kwa wale wachache wanaoipenda CCM, wanaona itakuwa ni mlima mkubwa kumnadi Lowassa mbele ya UKAWA kutokana na kashifa za ufisadi zinazo mzunguka. Zile zama ambapo mgombea wa CCM alipokuwa anapitishwa na mkutano mkuu wa CCM tayari ni Rais wa JMT zimepita.

Aidha pia kuna swala la afya ya Lowassa. It is un deniable true, kwamba afya ya Lowassa sio "NZURI" sana. Je, kama Lowassa atachaguliwa kupeperusha bendera ya CCM ataweza about four months grueling za kampeni? Na hasa wana CCM hao wakirejea matukio ya kuanguka kwa JK, ambaye relatively ana afya "nzuri" kulinganisha na Lowassa, tena mbaya zaidi kwenye kampeni zenye ushindani mkubwa katika historia ya nchi hii, ambapo sasa vyama vya upinzani vyenye nguvu vimeungana kuunda UKAWA.

CCM is now on DILEMA, wanataka kum contain Lowassa kwani akitoka CCM is a double edged sword to CCM, hata kama hatagombea URAIS kupitia UKAWA, lakini Lowassa akitoka CCM ndiyo hivyo CCM wanakipa a kiss good bye kiti cha URAIS wa JMT. Lowassa anafahamu hilo, CCM wanafahamu hivyo.

Mpaka sasa CCM wametegeneza mkakati mmoja, watapandikiza wagombea mamuluki wa nafasi ya rais, ili CC ya CCM itakapokata majina, yawe mengi including jina la Lowassa. Ili kama baadaye Lowassa atalalamika, ionekane hoja yake haina mashiko bali uroho wa madaraka, kwani CCM watakuja na propaganda mbona majina yaliyokatwa ni mengi tu, kwanini yeye Lowassa tu ndiye alalamike kama sio uroho wa madaraka. Akina Nape tayari wameshaandaliwa kwa kazi hiyo.

Kulingana na Katiba ya CCM, CC ya CCM itapendekeza majina yasiyozidi matano kwenda NEC ya CCM kupigiwa kura kwa waombaji wa nafasi ya URAIS. Majina matatu ya kwanza yatakayoshika nafasi ya juu kwenye kura za NEC yatapelekwa mkutano mkuu kupigiwa kura, kumpata mgombea mmoja atakaye peperusha bendera ya CCM.

Hakuna vigezo vya wazi vinavyofahamika ambavyo CC ya CCM hutumia kupendekeza majina yasiyo zidi matano kwenda NEC kupigiwa kura. CC ya CCM ndiyo litakuwa the last nail on the coffin of Lowassa, kwani jina lake na majina mengine ya wana CCM wengi wao wakiwa waliopandikizwa yatapokatwa.

Mpaka sasa hivi majina yatakayopendekezwa na CC ya CCM ili priority order ni kama ifuatavyo
  1. Mizengo Kayanza Pinda (sitting PM)
  2. Prof Mark Mwandosya (alifanya Vizuri nyuma ya JK kwenye uchaguzi wa 2005)
  3. Jina moja la Mzanzibari (kudumisha muungano, bado jina hilo halijakubaliwa yapo 3 yanayotajwa)
  4. Dr. Asha Rose Migiro (gender balance, Prof Tibaijuka alikuwa awe mmojawapo lakini nafikiri sasa sakata la escrow limemtupa nje)
  5. ........................... (??) Hili bado ni kitendawili linajumuisha wana CCM wengi eg, Mwakyembe, Sitta, Membe, Magufuri, Nahodha, Karume Jnr,Wassira, Makamba Jnr etc lakini Lowassa si miongoni mwao. Hili jina litachaguliwa kutokana na upepo wa kisiasa wakati huo.

Naomba kuwasilisha

ndio tunataka

Lowasa hafai urais(tuwe waungwana na wakweli tu).
Na muarobaini wake ni huyu Mzee! Nasikia amekonga nyoyo za watu na amebomoa karibuni kambi zote!




Sio Lowasa ambaye hafai bali CCM haifai kuendelea kutawala.
Kama mnabisha basi endeleeni kuishabikia CCM na kumpata rais wa awamu ya Tano toka CCM muone kama amani ya hii nchi itadumu chini ya Katiba pendekezwa na waroho na walafi wa CCM.

Kikwete alijitahidi kuwa rais wa watanzania wote na kutaka kuwaletea watanzania katiba bora na usawa bila kujali udini ,ukanda na ukabila lakini hofu ya Chama cha Lusifa CCM ikaibuka na kuvuruga nia njema ya Kikwete na kumgeuka Jaji Warioba pamoja na watanzania waliotaka kuweka misingi bora ya Taifa hili kwa vizazi vijavyo.

CCM wameua misingi ya uwazi na Uwajibikaji na hakuna yeyote ndani ya CCM anayeamini katka uwajibikaji na sheria ya maadili. Kiongozi bora toka CCM ni yule anayeweza kuwagawa watanzania kulingana na dini zao.

Leo umaarufu wa Pinda ni kwa kuwa ni Mkatoliki na sio utendaji wala uadilifu.Lengo ni kupunguza kura za Dr.Slaa kwa kuwahadaa watu kuwa Slaa ni Padri hivyo waislam wasimchague.
Tumeona jinsi Pinda alivyomshawishi Mkurugenzi wa Benki ya Mkombozi ili kutakatisha fedha haram na kutoa sadaka ya fedha haram kwa kiongozi wa dini.
Mpaka sasa hatujasikia tamko lolote toka Baraza la maaskofu Katoliki kuhusiana na uchafu ulioasisiwa na Pinda akishirikiana na Kilaini kupaka matope Kanisa na taasisi yake ya kifedha iliyoonyesha jinsi kanisa hilo linavyotumia ukubwa wake kuhujumu uchumi wa taifa hili na kuwatumia BAKWATA kama chambo cha kuwapooza waislam huku mfumo mbaya ukiendelea kutawala.
Raisi wa nchi anachaguliwa na kakamati ka watu wachache ndani ya CCM.Fomula inayotumika ni ile ile ya zamu ya Wakatoliki na zamu ya waislam watakaoikumbatia BAKWATA.

Wakati umefika sasa kwa UKAWA kuja na sera bora zitakazoimarisha utaifa wetu na kupata viongozi bora wenye maono mapana zaidi. Tuwajenge watanzania kwenye misingi bora ya kuwapata viongozi kwa sera na uwezo.
 
Kwani wee ni ccm!!
Mzee ni ccm damu na jina lake alilopewa la fisadi limeanza kutoweka mawazo mwa ccm wengi
napenda apitishwe kugombea akichaguliwa tu six na washrika wake ajiandae kutoswa rasmi na kusulubiwa!!!
Mimi ni mwananchi wa kawaida
 
Jamani Ikulu ni pahali patakatifu sio kwa kuhonga kunakofanywa wazi wazi hivyo...tuwe wakweli CCM IWE MAKINI NA IMSAIDIE MUNGU SIO KUBEBA WALA RUSHWA NA KUHONGA KUINGIA IKULU.
 
Siasa hutumia sana mtaji wa muda, kama kuna mifumo imara ya kinidhamu ndani ya UKAWA Lowasa anaweza kuwa kiongozi mzuri kwani mifumo hiyo inaweza kumshape, wasiwasi wangu ni historia yake na uwezo wake mkubwa wa KIFEDHA na IMANI yake kwamba yeye tu ndie anafaa kuwa rais.Pia naogopa falsafa waliyonayo viongozi wengi waliopo CCM ya kuingia madarakani ili kulinda historia yao mbaya ya nyuma,lakini pia uwezekano wa CCM kutumia nafasi ya kumjua vizuri Lowasa kuuchafua upinzani.
Ni hayo tu niyaogopayo Mr SUPU YA MAWE
 
Yani huyo Lowasa yeye ni spacial kiasigani, hata atoke ccm asubuhi, jioni aingie Ukawa nakupewa nafasi ya juu kiasihicho!!.
 
mjomba supu ya mawe .sina imani na wewe .friends for lowassa . au ndio msaka tonge kwa muheshimiwa
 
Lowasa naye sijui anachokitafuta japo na wewe mleta mada ni mzushi wa kutupa kabisa.
2005 uchaguzi mkuu kazi yake mliiona na mkaitukuza, 2010 kazi yake ya kumngoa mzee wa Urambo aliyejifanya kuikaanga Serikali kupitia Bunge mkaiona mkaibariki - iweje leo 2015 mnamkana??? haiwezekani kabisa.
 
hatutaki viongozi waliowahi kuliingizia taifa hasara ndo waje huku never on earth, labda awe mwanachama wa kawaida tu na sio kugombea nafasi yoyote ya uongozi vinginevyo arudi huko huko kwa chama chake cha mashetani

Acha sitaki - nataka!Lowasa hafai hafai basi oo sijui awe mwanachama wa kawaida wa kazi gani?Kama ni mwanachama ana haki ya kugombea urais!
 
Japo ambalo si la siri kwamba kambi zote za wagombea uraisi CCM zinamuogopa sana Lowassa, hivyo kuna kila aina ya jitihada ya kuhakikisha jina la Lowassa halipitishwi kugombea nafasi ya uraisi.

Huku wapinzani wakijipanga kukata jina lake lakini Lowassa yeye anaendelea na mikakati yake ikiwa ni pamoja na kugawa fedha kama njugu kwani anaamini yeye ni raisi wa Tanzania 2015-2025 "PIGA UA"

Lowassa anatishia kukiua chama (CCM) endapo hata pitishwa kugombea uraisi.

Wakati huo huo, endapo jina la Lowassa halitapitishwa CCM wanyetishaji wetu wanasema mkakati wa Lowassa kugombea kupitia UKAWA kwakuwa tayari ana mtaji wa wanaCCM wengi hivyo ni rahisi kwake kushinda nafasi ya uraisi.

Inasemekana kuwa tayari Lowassa ameshaanza mazungumzo ya chini chini na viongozi wa UKAWA lakini bado hawajafikia makubaliano rasmi.

By: SUPU YA MAWE

Ukawa hauijui wewe!
 
Last edited by a moderator:
Japo ambalo si la siri kwamba kambi zote za wagombea uraisi CCM zinamuogopa sana Lowassa, hivyo kuna kila aina ya jitihada ya kuhakikisha jina la Lowassa halipitishwi kugombea nafasi ya uraisi.

Huku wapinzani wakijipanga kukata jina lake lakini Lowassa yeye anaendelea na mikakati yake ikiwa ni pamoja na kugawa fedha kama njugu kwani anaamini yeye ni raisi wa Tanzania 2015-2025 "PIGA UA"

Lowassa anatishia kukiua chama (CCM) endapo hata pitishwa kugombea uraisi.

Wakati huo huo, endapo jina la Lowassa halitapitishwa CCM wanyetishaji wetu wanasema mkakati wa Lowassa kugombea kupitia UKAWA kwakuwa tayari ana mtaji wa wanaCCM wengi hivyo ni rahisi kwake kushinda nafasi ya uraisi.

Inasemekana kuwa tayari Lowassa ameshaanza mazungumzo ya chini chini na viongozi wa UKAWA lakini bado hawajafikia makubaliano rasmi.

By: SUPU YA MAWE

Aende hata leo! Atakula cha moto, askari wale wale waliokuwa wanamlinda ndo watamchapa mpaka chupi ilowe uhalo. CCM si chama cha kutishiwa. Kazi ya kupata mgombea urais pale kizota basi huyo ndo atakuwa rais wa nchi hizi nyingine unaweka mbwembwe ambazo haziingiii maskioni.
 
Back
Top Bottom