Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

UKAWA haihitaji Sub-dakika ya 90, timu imeshakamilika, tunachosubiriwa ni KIPENGA tu ili mshuhudie timbwili.
 
ukawa wana mipango yao mtu anayetaka kujiunga akiwa na sababu zake ajitafakari mara mbili ,ukawa haiwezi kuwa kivuko ina watu wake wa kuvuka nao wenye ajenda za vyeo na mambo mengine binafsi naona pagumu.
 
Hapa lazima iwe UGOMVI wa wanandugu..... :sorry:mie naenda shamba.................Maana:rain:yaja........
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Raia mwema wameuliza , wewe mleta mada umeuliza kwani Lowassa si yupo ? Ingefaa akaulizwa yeye hili swali .

Mwaka 2005 Jakaya alimtisha Mkapa kwa stail kama hii kuwa atajiunga na CHADEMA na akina Emmanuel Nchimbi waliifanya hiyo kazi sawaswa kwa kutishia hata kuifanya UVCCM kuwa ya CHADEMA ..........msiwe wasahaulifu sana ......
 
Ingekuwa mimi ni UKAWA,ningemkaribisha kwa masharti.
1.Sharti la kwanza,atoke hadharani na kueleza kinagaubaga jinsi alivyohusika na kashfa ya Richmondi,AICC n.k
2.Aseme alimaanisha nini wakati wa kuijuzulu aliposema ameamua kung'atuka ili kuiokoa serikali ilhali yeye ndio alikuwa kiongozi mkuu wa serikali na kujiuzulu kwake maana yake serikali ilianguka.
3.Aeleze fedha zote alizogawa misikitini,makanisani,kwenye saccos mbalimbali alikuwa anazitoa wapi na lengo lake lilikuwa nini maana kabla ya kujiuzulu hakufanya hivyo.
4.Akane kutamani nafasi yeyote kisiasa kupitia UKAWA kinyume na utaratibu ulipo wa UKAWA.
5.Aeleze sababu zinazomfanya ahame ccm ambazo hizo sababu hazipo kwenye hichi chama kwenye UKAWA.
Akijibu haya yoote kiufasaha mbele ya waandishi wa habari,NINGEMPATIA kadi ya uanachama wa chama na ningemtumia kwa kadiri nitakavyomhitaji.
 
Teh teh teh hiki chama bhana teh teh....Ama kweli jamaa kawashika vibaya kila siku Lowasa

Chama gani kimeshikwa vibaya? Ila team lowassa wanamuhangahikia mzee wa richmond lakini watambue hawezi kuwa Rais JMT.
 
UKAWA hakuna nafasi ya mafisadi aende zake huko. UKAWA hawawezi kufanya makosa ya kipumbavu ya kumkaribisha huyu fisadi.

ukawa tambueni wapiga kura ni zaidi ya hao mnaokuwa nao katika mikutano na maandamano tena hao si wapiga kura wanakuja kupitisha muda siku ipite, Watu wengi sana hawana muda wa maandamano wala mikutano, wao ni peni na karatasi katika kituo cha kupigia kura. Mnajipa matumani yasiyokuwepo, mtajishangaa kwenye matokeo yakitangazwa.Ushauri wa bure mpokeeni haraka huyo baba wa monduli anayetaka urais kwa nguvu zote. Ila angegombea irais wa wapiga madeal siyo wa kuongoza taifa la Tanzania.
 
ukawa tambueni wapiga kura ni zaidi ya hao mnaokuwa nao katika mikutano na maandamano tena hao si wapiga kura wanakuja kupitisha muda siku ipite, Watu wengi sana hawana muda wa maandamano wala mikutano, wao ni peni na karatasi katika kituo cha kupigia kura. Mnajipa matumani yasiyokuwepo, mtajishangaa kwenye matokeo yakitangazwa.Ushauri wa bure mpokeeni haraka huyo baba wa monduli anayetaka urais kwa nguvu zote. Ila angegombea irais wa wapiga madeal siyo wa kuongoza taifa la Tanzania.

Wezi wabakie huko huko kwenu ccm...ukawa tuko kamili
 
ukawa wana mipango yao mtu anayetaka kujiunga akiwa na sababu zake ajitafakari mara mbili ,ukawa haiwezi kuwa kivuko ina watu wake wa kuvuka nao wenye ajenda za vyeo na mambo mengine binafsi naona pagumu.
umeandika kizembe sana .
 
Raia mwema wameuliza , wewe mleta mada umeuliza kwani Lowassa si yupo ? Ingefaa akaulizwa yeye hili swali .

Mwaka 2005 Jakaya alimtisha Mkapa kwa stail kama hii kuwa atajiunga na CHADEMA na akina Emmanuel Nchimbi waliifanya hiyo kazi sawaswa kwa kutishia hata kuifanya UVCCM kuwa ya CHADEMA ..........msiwe wasahaulifu sana ......

Ujakosea kaka lowasa anawapasua vichwa saaana
 
El haweze kujiunga kwenye chama kilichoporwa ambacho wakati wowote Mahakama itaamua kirudishwe kwa wenyewe na katiba, jina, nembo na kadi za chama zitumike zile za awali
 
Aende mapema kabisa kabisa akaungane na mafiadi wenzake.
 
Wapiga kura wanaojitambua na wenye mapenzi ya kweli na Tanzania kamwe hawawezi kupoteza kura zao kwa huyu fisadi mgawa rushwa katika nyumba za ibada.

ukawa tambueni wapiga kura ni zaidi ya hao mnaokuwa nao katika mikutano na maandamano tena hao si wapiga kura wanakuja kupitisha muda siku ipite, Watu wengi sana hawana muda wa maandamano wala mikutano, wao ni peni na karatasi katika kituo cha kupigia kura. Mnajipa matumani yasiyokuwepo, mtajishangaa kwenye matokeo yakitangazwa.Ushauri wa bure mpokeeni haraka huyo baba wa monduli anayetaka urais kwa nguvu zote. Ila angegombea irais wa wapiga madeal siyo wa kuongoza taifa la Tanzania.
 
Back
Top Bottom