Mjumbe wa kamati kuu ya CCM amuomba Askofu Mwamakula kumfikishia ujumbe wake kwa Wananchi kuhusu mkataba wa bandari Ili asifukuzwe uanachama

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Feb 26, 2021
949
2,865
Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Kwenye vikao vilivyoisha (Kamati Kuu ya CCM na Halmashauru Kuu ya CCM) imeelezwa kuwa Wajumbe wamebariki mkataba tata wa Bandari. Ninajiuliza maswali kadhaa: Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao hivyo ni wanasheria au wachumi walioweza kuingia katika vikao na nakala ya mkataba na kuanza kujenga hoja ya kujadili kifungu kwa kifungu kuwa kifungu hiki hakiko sawa na hiki kiko sawa?

Je, Mwenyekiti wa kikao alitangaza maslahi yake katika jambo husika kuona busara kuwa jambo hilo lijadiliwa kwa uwazi bila yeye kuwa Mwenyekiti wa kikao kwa kuwa limepigiwa kelele sana na hivyo kujenga neutrality kwake? Je, isingekuwa ni busara kumuachia Makamu Mwenyekiti ili asimamie vikao husika?

Mpendwa Baba Askofu! Unajua kwenye Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ili mtu aweze kuingia katika Political Committee ama Kamati ya Siasa na ngazi zingine kubwa za maamuzi ni lazima awe na uelewa wa mambo hususani katika masuala ya fedha, sheria, mazingira na pia lazima awe na elimu au uwezo wa kuweza kujenga hoja.

Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao vyetu ambao ni wanasheria na wachumi walio na uwezo wa kujenga hoja katika vikao ambavyo tumeambiwa kuwa wameridhia kwa kishindo?

Ninaomba ikikupendeza Baba Askofu unisaidie kuyafikisha haya kwa Watanzania kwani sio wote ndani ya CCM tunaounga mkono mkataba huo wa Bandari. Mazingira yetu ni magumu na hivyo tunaogopa kufukuzwa uanachama ndio maana hatutoki hadharani kupinga au kukosoa.

Ndimi .....
Dar es Salaam, 10 Julai 2023
 
Baba Askofu,

Hawa jamaa ndio walio muuza Yesu Mtoto Wa Bikira Maria kwa vipande vya fedha, kwa kujali matumbo yao. Hata kwa hili la mkataba wameshakiri kujali matumbo yao bado, hawajatubu...!!! Sasa, kama walimuuza Yesu Mwana Wa Israel, wewe ni nani wasikuuze huko mbele ya safari hata kwa kipande cha muhogo, kitumbua, fungu la dagaa, au chipsi kavu sahani moja???

Baba Askofu, CCM hawana heri! Shauri yako! Usiseme wana tuliku kaushia uingie cha kike, wana tushakupa mtonyo!

Wako mtiifu,
Alexander The Great
 
I
Baba Askofu,

Hawa jamaa ndio walio muuza Yesu kwa vipande vya fedha, kwa kujali matumbo yao. Hata kwa hili la mkataba wamekiri kujali matumbo yao bado. Sasa, kama walimuuza Yesu, wewe ni nani wasikuuze huko mbele ya safari hata kwa kipande cha muhogo, kitumbua, fungu la dagaa, au chipsi kavu sahani moja??? Baba Askofu, CCM hawana heri! Shauri yako!

Wako mtiifu,
Alexander The Great
Ila ccm wako tayari kufanya chochote ili wapate pesa.
 
Bwana "NDIMI"
Usiogope kufa!

Kufa kumepangwa na Muumba....Kuuza na kuwaweka binadamu wenzako rehani, haujapangwa na Muumba!

Hakuna atakaye kugusa...tembea kichwa juu.
 
Madini yalienda,
Gesi ikaenda ,
Mbuga za wanyama zinaondoka ivo,
Bandari plus bahari na ndio hiyo inaenda,
Ardhi soon inaenda baada ya bunge kuridhia.
HII SAFISHA SAFISHA MALI ZA WATANZANIA sijui tutajikuta tumebaki na nini..
Na tukiendelea kuwachekea na mlima kiliimanjaro utawekwa sokoni....
 
Madini yalienda,
Gesi ikaenda ,
Mbuga za wanyama zinaondoka ivo,
Bandari plus bahari na ndio hiyo inaenda,
Ardhi soon inaenda baada ya bunge kuridhia.
HII SAFISHA SAFISHA MALI ZA WATANZANIA sijui tutajikuta tumebaki na nini..
Tutakuwa kama SA wakati WA Makaburu
 
Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Dar es Salaam, 10 Julai 2023
Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao vyetu ambao ni wanasheria na wachumi walio na uwezo wa kujenga hoja katika vikao ambavyo tumeambiwa kuwa wameridhia kwa kishindo?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!


Ndimi .....
Dar es Salaam, 10 Julai 2023
Mazingira yetu ni magumu na hivyo tunaogopa kufukuzwa uanachama ndio maana hatutoki hadharani kupinga au kukosoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu atadhani andiko hilo ni la utani, lakini hakuna utani hapo.

Hawa watu wa CCM wamelifikisha taifa pabaya sana.

Huyu mjumbe wa CCM hata kumwonea huruma inakuwa vigumu sana kwa sababu hawa hawa ndio wameruhusu hali iwe mbaya kiasi hiki. Kwa hiyo kumwonea huruma mtu kama huyu haifai, wote ni samaki waliooza ndani ya tenga.

Ukiona wanavyotoa rushwa wakati wa uchaguzi wa wajumbe hawa ndipo utakapoelewa kuwa CCM hakuna aliyebaki na akili zake timamu.
 
Madini yalienda,
Gesi ikaenda ,
Mbuga za wanyama zinaondoka ivo,
Bandari plus bahari na ndio hiyo inaenda,
Ardhi soon inaenda baada ya bunge kuridhia.
HII SAFISHA SAFISHA MALI ZA WATANZANIA sijui tutajikuta tumebaki na nini..
Na tukiendelea kuwachekea na mlima kiliimanjaro utawekwa sokoni....
Mimi ninatumaini waTanzania wamepata funzo la kutosha hapa, kama bado walikuwa na matumaini juu ya hiki chama cha CCM.

Kwenda kupiga kura kuchagua yeyote ndani ya CCM ni kuliumiza taifa letu.

Ni wakati sasa watu watambue kwamba CCM ipo si kwa maslahi ya nchi na wananchi wake, bali ni kwa hawa viongozi na wanachama wanaofaidika na uwepo wa chama hiki.
 
Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Kwenye vikao vilivyoisha (Kamati Kuu ya CCM na Halmashauru Kuu ya CCM) imeelezwa kuwa Wajumbe wamebariki mkataba tata wa Bandari. Ninajiuliza maswali kadhaa: Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao hivyo ni wanasheria au wachumi walioweza kuingia katika vikao na nakala ya mkataba na kuanza kujenga hoja ya kujadili kifungu kwa kifungu kuwa kifungu hiki hakiko sawa na hiki kiko sawa?

Je, Mwenyekiti wa kikao alitangaza maslahi yake katika jambo husika kuona busara kuwa jambo hilo lijadiliwa kwa uwazi bila yeye kuwa Mwenyekiti wa kikao kwa kuwa limepigiwa kelele sana na hivyo kujenga neutrality kwake? Je, isingekuwa ni busara kumuachia Makamu Mwenyekiti ili asimamie vikao husika?

Mpendwa Baba Askofu! Unajua kwenye Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ili mtu aweze kuingia katika Political Committee ama Kamati ya Siasa na ngazi zingine kubwa za maamuzi ni lazima awe na uelewa wa mambo hususani katika masuala ya fedha, sheria, mazingira na pia lazima awe na elimu au uwezo wa kuweza kujenga hoja.

Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao vyetu ambao ni wanasheria na wachumi walio na uwezo wa kujenga hoja katika vikao ambavyo tumeambiwa kuwa wameridhia kwa kishindo?

Ninaomba ikikupendeza Baba Askofu unisaidie kuyafikisha haya kwa Watanzania kwani sio wote ndani ya CCM tunaounga mkono mkataba huo wa Bandari. Mazingira yetu ni magumu na hivyo tunaogopa kufukuzwa uanachama ndio maana hatutoki hadharani kupinga au kukosoa.

Ndimi .....
Dar es Salaam, 10 Julai 2023
Uongo mtupu.
 
Ujumbe ufuatao umetoka kwa mwanachama wa CCM ambaye amekuwa Mteule wa Rais wa muda mrefu. Kwa kuogopa kufukuzwa CCM, ameomba afikishe ujumbe kupitia kwa Askofu.

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Kwenye vikao vilivyoisha (Kamati Kuu ya CCM na Halmashauru Kuu ya CCM) imeelezwa kuwa Wajumbe wamebariki mkataba tata wa Bandari. Ninajiuliza maswali kadhaa: Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao hivyo ni wanasheria au wachumi walioweza kuingia katika vikao na nakala ya mkataba na kuanza kujenga hoja ya kujadili kifungu kwa kifungu kuwa kifungu hiki hakiko sawa na hiki kiko sawa?

Je, Mwenyekiti wa kikao alitangaza maslahi yake katika jambo husika kuona busara kuwa jambo hilo lijadiliwa kwa uwazi bila yeye kuwa Mwenyekiti wa kikao kwa kuwa limepigiwa kelele sana na hivyo kujenga neutrality kwake? Je, isingekuwa ni busara kumuachia Makamu Mwenyekiti ili asimamie vikao husika?

Mpendwa Baba Askofu! Unajua kwenye Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ili mtu aweze kuingia katika Political Committee ama Kamati ya Siasa na ngazi zingine kubwa za maamuzi ni lazima awe na uelewa wa mambo hususani katika masuala ya fedha, sheria, mazingira na pia lazima awe na elimu au uwezo wa kuweza kujenga hoja.

Je, ni Wajumbe wangapi katika vikao vyetu ambao ni wanasheria na wachumi walio na uwezo wa kujenga hoja katika vikao ambavyo tumeambiwa kuwa wameridhia kwa kishindo?

Ninaomba ikikupendeza Baba Askofu unisaidie kuyafikisha haya kwa Watanzania kwani sio wote ndani ya CCM tunaounga mkono mkataba huo wa Bandari. Mazingira yetu ni magumu na hivyo tunaogopa kufukuzwa uanachama ndio maana hatutoki hadharani kupinga au kukosoa.

Ndimi .....
Dar es Salaam, 10 Julai 202
Mjumbe yuko sahihi, conflict of interest ni kanuni ya kimaadili, kwa viongozi waadilifu kimsingi ni katazo la kimaadili, ambalo linamtaka mhusika yeyote kutojihusisha na jambo lolote ambalo ana mslai nalo binafsi, au kueleza maslai yake binafsi katika majadiliao ili kuepuka kuathiri au kuweka maslai binafsi katika uamuzi wowote.

( katika sakata la Bandari, rais samia ana maslai binafsi kwa sababu zifuatazo:
1.ametajwa kwa nafasi yake kama rais kuridhia waziri wake kusaini mkataba,
2.ametajwa anauza mali za watanganyika kwa makusudi,
3. ametajwa kama anagawa mali hizo kwa maslai binafsi kwa wajomba zake.
) hivyi vyote ni maslai binafsi, kwa nafasi yake kama mwenyekiti kanuni za kimaadili za conflict of interest kama kiongozi ni mwadilifu na wajumbe wengine wote ama waliohusika au kutajwa kwa namna yeyote ile kugawa mali, au waliotajwa kwa namna yoyote ile. walipaswa kudeclare conflict of interest ili wawaachie wengine wajadili na kutoa uamuzi bila ya kuegemea upande wowote.

ila upande wa pili wanaccm yeyote anayeoogopa kusema ukweli kwa kisingizio cha kuogopa kufukuzwa pia ni usaliti kwa taifa, kwani ni wazi maslai yao wameweka mbele kwa rasilimali za taifa
 
Back
Top Bottom