1. Kwa nini Werema alisema ati ''nimeshaisoma hukumu na nimeufunga uu mjadala, DOWANS walipwe tu''?
2. Kwa nini JK haipeleki issue hii kwenye baraza la Mawaziri ili ijadiliwe na kutolewa maamuzi?
3. Kwanini wanaharakisha process ya kuwalipa DOWANS wakati hata suala lenyewe halijaandikishwa mahakama kuu?
4. Kwanini Ngeleja amekumbuka kuwatafuta ''wamiliki halali'' wa DOWANS kutoka BRELA juzi juzi tu? alikuwa wapi muda wote huu? au alikuwa anavuta time ili documents zitengenezwe?
5. Kwanini Werema hakuupita ushauri uliotolewa na REX Attorneys kwa TANESCO kuupiga chini mkataba?
6. Kwa nini JK yu KIMYA?? hivi aliigusia issue hii wakati akitoa salamu zake fake za kuufunga mwaka 2010??
7. .............
MY TAKE: Wadanganyika wote tulishaonekana mazuzu tu. Longolongo nyiiiiiiiiiiingi na hatuwezi kufanya lolote. JK analijua hili, Karamagi analijua hili, Lowasa, Chenge, Rostam, Werema, Msabaha etc wanajua kwamba watamlipa DOWANS (watajilipa wenyewe na kuwakatia 10% maswahiba walioshiriki kufanikisha mpango mzima) na issue itafukiwa kama kawaida na life litaendelea kama kawa.
Kuna mtu mmoja alishauri japo wadanganyika waonyeshwe picha za wamiliki hao - ili tujue wanaotudai ni akina nani!
God help us!