Halafu hawajui kuwa vitendo hivi vinazidi kuitenga Zbar na jumuiya ya kimataifa.
Milipuko hii kama kweli ni mabomu basi wenye makosa ni serikali kutokuwa makini na matatizo hayo toka mwanzo.Sijaona kilichofanyika ili kuwapata wahalifu,na sijui wanaona furaha gani watanzania wakirumbana kwa mihemuko ya udini wakati huo ni uhalifu na auhusiani na dini yoyote.Sipendi na sitaki kuaminishwa kwamba ni usilamu bali huyo aliyeweka mabomu hayo ni mhalifu tu na wala si kuweka dini mahali penye uhalifu ambao unaweza kutolewa majibu sahihi na wakosaji wakaadhibiwa.Rai yangu kwa Wanzanzibar bila kujali dini zao inabidi wafanye doria wenyewe ili kuwakamata wahalifu hawa.Kwa kweli wanaudhi.
...mkuu' ni wahuni tu, kama wale walio haribu, kuvunja na kuchoma Makanisa mbalimbali hapa Tanzania (hasa kama wale wa Mbagala, baada ya kukojolewa kitabu)
Hivi hii nchi inaeleke wapi lakini!
Tunaweza tusikuelewe kwa sasa lakini kwa wajuzi wa mambo ya nchi hii basi wakupe japo 50/50.
Watu wanataka kujitenga na wameonyesha dhahir kutuchukia, sasa sijui tunawang'ang'ania wa nini?
Mkuu unastuka leo kwani kwenye safu za viongozi wa serikali ya Zanzibar wakristo ni wangapi?Duh!! Kanisani tena kumbe ndio maana katika wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka Zanzibar kati ya 67 Wakristo ni 2 na wote wametoka katika kipengere cha vikundi vya Kidini. inamaanisha kama kungekuwa hakuna kipengere cha dini Kutoka Zanzibar kusingekuwepo na Mkristo.
Umeandika mwenyewe hii au umeandikiwa?Wewe mupunguwani hao watu wanajiripua wenyewe kwa uroho wa sadaka
Aliyemuua yule padri si alipatikana,ulishasikia habari zake tena? hizi ni move za kuchonga,msimamo wa CDM wa kujilinda uigwe na makanisa kule Zanzibar.Nitapingana na wewe viongozi wetu wanapenda kutumia lugha nyepesi hivi muhuni anapata wapi mabomu?Hawa ni wahalifu wanaoharibu amani na upendo tulionao watanzania.Serikali inatakiwa iwatafute ili tuapate amani.
TBC1 bado wanaifanyia utafiti habari hii na kusubiri tamko la polisi.Wasubiri watakujulisha.itakuwa ni mazoezi ya kijeshi tu, mbona mimi naangalia TBC1 sasa hivi sijaona breaking news na TBC1 ndiyo tv ya umma, lazima kwa jambo kama hili wasingeachia vyombo vingine pekee ndiyo vitoe habari. ikiwa hivyo nitaamini kweli TBC1 sio ya umma.