Medecin
JF-Expert Member
- Nov 29, 2011
- 7,896
- 21,305
Ajali ya basi la Standard Coach kutokea Iringa kwenda Dar.
Saa tatu asubuhi hii imetokea ajali ya basi la Standard Coach lenye namba za usajili T543 CSF lililokuwa likitokea mkoani Iringa kwenda Dar es Salaam. Ajali imetokea maeneo ya Mikumi wilayani Kilosa eneo maarufu kama kona za Iyovi.
Ajali hiyo imehusisha magari mawili, basi na lori ambalo halikupata madhara yoyote.
Chanzo cha ajali kulingana na mashuhuda ni uzembe wa dereva wa lori kukosa umakini barabarani, dereva wa basi alijaribu kukwepa lori lililoingia upande wa basi na kusababisha basi kwenda kugonga mti uliopo pembezoni mwa barabara.
Nimeshuhudia majeruhi kadhaa kwa kuwasaidia kuwatoa kwenye basi na kuwakimbiza hospitali ndogo ya Mikumi na majeruhi wengine wamebebwa na madereva wa malori kwenda zahanati ya Ruaha Mbuyuni kwa ajili ya matibabu. Mpaka natoka eneo la tukio hakuna kifo chochote ila majeruhi watano hali zao si nzuri. Mmoja kavunjika mguu (mwanaume), mwingine kapasuka kichwani (mwanaume) na wengine wamepata majeraha sehemu mbalimbali za mwili.
Mpaka natoka eneo la ajali bado jeshi la Polisi lilikuwa halijafika eneo la tukio kutokana na ukosefu wa mtandao eneo la ajali hivyo taarifa kuchelewa kufika lakini tumewapa taarifa kwa kuwafuata hapo Ruaha Mbuyuni.
Nawaombea majeruhi wapate nafuu haraka.
Saa tatu asubuhi hii imetokea ajali ya basi la Standard Coach lenye namba za usajili T543 CSF lililokuwa likitokea mkoani Iringa kwenda Dar es Salaam. Ajali imetokea maeneo ya Mikumi wilayani Kilosa eneo maarufu kama kona za Iyovi.
Ajali hiyo imehusisha magari mawili, basi na lori ambalo halikupata madhara yoyote.
Chanzo cha ajali kulingana na mashuhuda ni uzembe wa dereva wa lori kukosa umakini barabarani, dereva wa basi alijaribu kukwepa lori lililoingia upande wa basi na kusababisha basi kwenda kugonga mti uliopo pembezoni mwa barabara.
Nimeshuhudia majeruhi kadhaa kwa kuwasaidia kuwatoa kwenye basi na kuwakimbiza hospitali ndogo ya Mikumi na majeruhi wengine wamebebwa na madereva wa malori kwenda zahanati ya Ruaha Mbuyuni kwa ajili ya matibabu. Mpaka natoka eneo la tukio hakuna kifo chochote ila majeruhi watano hali zao si nzuri. Mmoja kavunjika mguu (mwanaume), mwingine kapasuka kichwani (mwanaume) na wengine wamepata majeraha sehemu mbalimbali za mwili.
Mpaka natoka eneo la ajali bado jeshi la Polisi lilikuwa halijafika eneo la tukio kutokana na ukosefu wa mtandao eneo la ajali hivyo taarifa kuchelewa kufika lakini tumewapa taarifa kwa kuwafuata hapo Ruaha Mbuyuni.
Nawaombea majeruhi wapate nafuu haraka.