Mikumi: Basi Standard Coach lililokuwa likitokea Iringa kwenda Dar es Salaam lapata ajali

Poleni sana wote mliopata ajari lakini ili BUS ni bovu jamani nilivyoliona pale Mbezi stendi ,nilishangaa kuona mamlaka husika wakishindwa kulizuia ili Bus lisiendelee kutoa huduma kutokana na uchakavu na ubovu.
 
Mti umetulia ila gari limechakaa daah!!
Poleni sana wahanga. Kumbe ndio maana watu hung'ang'ania seat za upande wa dereva.
Ndio shida ya Body za kisasa ambazo asilimia kubwa ni Fiberglass.
 
Huo mti utatoweka kama yule fisi wa Tabora kufikia kesho utachimbwa hadi mizizi.
Hahaaa, nauona unafaa kutibu nguvu za kiume..! Umebaki umesimama dede na michubuko kidogo licha ya gari kuharibika vibaya na abiria kuvuja damu.
 
Aisee,

Nimeona taarifa STANDARD bus ikitokea Iringa kwenda Dar imepata ajali Iyovi leo saa 3 asubuhi ikihusisha lori lililoingia site ya basi bila tahadhari na basi likakwepa na kwenda kugonga mti.

Kwa mujibu wa shuhuda hakuna vifo bali kuna majeruhi. Taarifa rasmi nadhani tapatikana kwa mamlaka husika.

Wenye ndugu na jamaa waliosafiri na basi hilo au kutoka Iringa kuelekea Dsm siku ya leo wanashauriwa kufuatilia kujua hali ya ndugu zao huko barabarani.

E7c1zL2XMAAaYQn.jpg
 
iyo takataka nilsishawahi kuipanda, inanuka hadi kunuka ndani humo. ni basi 3rd class kabisa na wanachelewaga kuondoka na njiani wanakimbia, waliturush akwenye matuta sitasahau.
 
iyo takataka nilsishawahi kuipanda, inanuka hadi kunuka ndani humo. ni basi 3rd class kabisa na wanachelewaga kuondoka na njiani wanakimbia, waliturush akwenye matuta sitasahau.
Mkuu umechefukwa!
 
iyo takataka nilsishawahi kuipanda, inanuka hadi kunuka ndani humo. ni basi 3rd class kabisa na wanachelewaga kuondoka na njiani wanakimbia, waliturush akwenye matuta sitasahau.
Upendo/Standard inabidi wajitathimini kwenye ubora wa mabasi yao. Mabasi mazuri yamekuwa ya kubahatisha. Abiria unakata tiketi kwa nauli ya semi luxury lakini unakuta gari halina hadhi hiyo isipokuwa viti tu ndiyo 2x2.
 
Ajali ya basi la Standard Coach kutokea Iringa kwenda Dar.

Saa tatu asubuhi hii imetokea ajali ya basi la Standard Coach lenye namba za usajili T543 CSF lililokuwa likitokea mkoani Iringa kwenda Dar es Salaam. Ajali imetokea maeneo ya Mikumi wilayani Kilosa eneo maarufu kama kona za Iyovi.
Ajali hiyo imehusisha magari mawili, basi na lori ambalo halikupata madhara yoyote.

Chanzo cha ajali kulingana na mashuhuda ni uzembe wa dereva wa lori kukosa umakini barabarani, dereva wa basi alijaribu kukwepa lori lililoingia upande wa basi na kusababisha basi kwenda kugonga mti uliopo pembezoni mwa barabara.

Nimeshuhudia majeruhi kadhaa kwa kuwasaidia kuwatoa kwenye basi na kuwakimbiza hospitali ndogo ya Mikumi na majeruhi wengine wamebebwa na madereva wa malori kwenda zahanati ya Ruaha Mbuyuni kwa ajili ya matibabu. Mpaka natoka eneo la tukio hakuna kifo chochote ila majeruhi watano hali zao si nzuri. Mmoja kavunjika mguu (mwanaume), mwingine kapasuka kichwani (mwanaume) na wengine wamepata majeraha sehemu mbalimbali za mwili.

Mpaka natoka eneo la ajali bado jeshi la Polisi lilikuwa halijafika eneo la tukio kutokana na ukosefu wa mtandao eneo la ajali hivyo taarifa kuchelewa kufika lakini tumewapa taarifa kwa kuwafuata hapo Ruaha Mbuyuni.

Nawaombea majeruhi wapate nafuu haraka.

View attachment 1872532
View attachment 1872535
View attachment 1872541
View attachment 1872542
View attachment 1872545
Umefika wakati ambapo mtu kabla hajapewa leseni ya kuendesha magari apimwe akili. Haiwezekani kila siku wataalamu wa masuala ya barabarani wanaongelea jambo hilohilo lakini watu hawaelewi. Hakuna tofauti na kumpigia mbuzi gitaa.

Mbaya zaidi, watu wanaona kazi ya udereva ni ya kukimbilia kila mtu; labda wanaona kuwa ni kazi rahisi kuliko kazi zingine, lakini ukweli ni kwamba kazi ya udereva sio rahisi kama watu wanavyofikiria, na ndio maana wanashindwa kuelewa sheria za barabarani.

Vyombo vinavyohusika na usalama barabarani, wapelekeni watu wanaohitaji leseni kwenye mamlaka husika ku-test uwezo wao wa kufikiri, vinginevyo ajali hazitaisha. Msiishie kuwaangalia viwango vya pombe tu, kwani ni dhahiri wengine hawapaswi kuendesha vyombo vya moto.
 
Back
Top Bottom