Ndio shida ya Body za kisasa ambazo asilimia kubwa ni Fiberglass.Mti umetulia ila gari limechakaa daah!!
Poleni sana wahanga. Kumbe ndio maana watu hung'ang'ania seat za upande wa dereva.
@Mshana jr.Dah ....Poleni abiria..... Kongole nyingi kwa mtuma mpicha....umetuma picha za ajali bila kuonyesha tone la damu...ila hujatutendea haki tunaopenda kuona damu.....Nadhani Profesa Mchana Junia atakuwa ananung'unika huko aliko....
Hahaaa, nauona unafaa kutibu nguvu za kiume..! Umebaki umesimama dede na michubuko kidogo licha ya gari kuharibika vibaya na abiria kuvuja damu.Huo mti utatoweka kama yule fisi wa Tabora kufikia kesho utachimbwa hadi mizizi.
Mkuu umechefukwa!iyo takataka nilsishawahi kuipanda, inanuka hadi kunuka ndani humo. ni basi 3rd class kabisa na wanachelewaga kuondoka na njiani wanakimbia, waliturush akwenye matuta sitasahau.
Kwakweli.Ndio shida ya Body za kisasa ambazo asilimia kubwa ni Fiberglass.
Upendo/Standard inabidi wajitathimini kwenye ubora wa mabasi yao. Mabasi mazuri yamekuwa ya kubahatisha. Abiria unakata tiketi kwa nauli ya semi luxury lakini unakuta gari halina hadhi hiyo isipokuwa viti tu ndiyo 2x2.iyo takataka nilsishawahi kuipanda, inanuka hadi kunuka ndani humo. ni basi 3rd class kabisa na wanachelewaga kuondoka na njiani wanakimbia, waliturush akwenye matuta sitasahau.
Umefika wakati ambapo mtu kabla hajapewa leseni ya kuendesha magari apimwe akili. Haiwezekani kila siku wataalamu wa masuala ya barabarani wanaongelea jambo hilohilo lakini watu hawaelewi. Hakuna tofauti na kumpigia mbuzi gitaa.Ajali ya basi la Standard Coach kutokea Iringa kwenda Dar.
Saa tatu asubuhi hii imetokea ajali ya basi la Standard Coach lenye namba za usajili T543 CSF lililokuwa likitokea mkoani Iringa kwenda Dar es Salaam. Ajali imetokea maeneo ya Mikumi wilayani Kilosa eneo maarufu kama kona za Iyovi.
Ajali hiyo imehusisha magari mawili, basi na lori ambalo halikupata madhara yoyote.
Chanzo cha ajali kulingana na mashuhuda ni uzembe wa dereva wa lori kukosa umakini barabarani, dereva wa basi alijaribu kukwepa lori lililoingia upande wa basi na kusababisha basi kwenda kugonga mti uliopo pembezoni mwa barabara.
Nimeshuhudia majeruhi kadhaa kwa kuwasaidia kuwatoa kwenye basi na kuwakimbiza hospitali ndogo ya Mikumi na majeruhi wengine wamebebwa na madereva wa malori kwenda zahanati ya Ruaha Mbuyuni kwa ajili ya matibabu. Mpaka natoka eneo la tukio hakuna kifo chochote ila majeruhi watano hali zao si nzuri. Mmoja kavunjika mguu (mwanaume), mwingine kapasuka kichwani (mwanaume) na wengine wamepata majeraha sehemu mbalimbali za mwili.
Mpaka natoka eneo la ajali bado jeshi la Polisi lilikuwa halijafika eneo la tukio kutokana na ukosefu wa mtandao eneo la ajali hivyo taarifa kuchelewa kufika lakini tumewapa taarifa kwa kuwafuata hapo Ruaha Mbuyuni.
Nawaombea majeruhi wapate nafuu haraka.
View attachment 1872532
View attachment 1872535
View attachment 1872541
View attachment 1872542
View attachment 1872545