BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Ajali hiyo imetokea leo Jumapili Machi 24, 2024 katika Kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera wakati wanafunzi 35 wa shule hiyo wakisafiri kwenda Kata ya Katoro wilayani Chato mkoani Geita kwenye mapumzikoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa Kagera, Bracius Chatanda amethibitisha kutokea ajali hiyo na kuwa bado uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo chake.
Mkuu wa Wilaya Muleba, Dk Abel Nyamahanga amesema ajali hiyo imetokea Saa 8 usiku wa kuamkia leo.
"Basi lilikuwa limebeba wanafunzi limepata ajali usiku wa kuamkia leo majira ya saa nane na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja na wenzake sita wamepata majeruhi," amesema DC Nyamahanga.
Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera, Asheri Mpango amethibitisha kupokea mwili wa mwanafunzi huyo na majeruhi sita, wakiwamo wanafunzi na watumishi wa shule hiyo.
"Umepokelewa mwili wa mwanafunzi mmoja, majeruhi sita ambao mmoja kati ya hao, amevunjika mkono ambaye ni matroni wa shule, jina lake ni Anitha Frederick, mfanyakazi mmoja aitwaye Ashraf Athman (21) na Magdalena Muhage (16) ambaye ni mwanafunzi," amesema Mpango.