Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Kichuguu,
Mimi naamini kabisa kuwa Zitto hakutendewa haki hata kidogo. Na rais mwenyewe ndiye shuhuda wa yote yaliyotokea na hasa alipofanya unafiki wa Kumpa support Karamagi kuwa mabadiliko yalishafanyika hivyo kutuwezesha kupokea corporate tax mwaka 2010.

Kama zilikuwepo kamati za mwanzo nadhani ipo haja yetu sisi kukubali kwamba hazikufanya kazi yao vizuri kutokana na sheria tulizoziona ktk mikataba iliyofuata na hasa ule wa Buzwagi.

Tukumbuke tu kuwa hizi ni SHERIA za nchi ktk madini ambazo zinafanyiwa mapendekezo na sidhani kama ipo sheria ya kitaifa ambayo imepitishwa bila kupitia Bunge. Kwa hiyo alichosema Karamagi bungeni kilikuwa ni kamba moja safi sana.

Ukimsoma vizuri Karamagi (hapo juu ulipomnukuu) utagundua kuwa alichouliza Zitto kilihusiana na SHERIA ya madini lakini jibu la Karamagi na kamati aloitaja haikuwa ikihusiana na sheria ama mapendekezo ya kamati ktk sheria ya madini isipokuwa kazi ya kamati ile ilikuwa kufanya mapitio ya mikataba ilokwisha sainiwa kubaini maeneo yanayoweza kurekebishwakwa faida ya pande zote mbili. Hapa utakuta ni vitu viwili tofauti kabisa vilivyozungumzwa kama maelezo ya Chiligati hapo juu, lakini wabunge wetu kwa Umbumbumbu wao na hasa Karamagi aliposherehesha na kifungu cha sheria ya kodi wakamwona yeye mkweli zaidi wakati kalikimbia swali.

Agizo la rais toka mwanzo halikuwa kubadilisha ama kupitia sheria za madini na ndipo Zitto alipojengewa uzio na ndio maana Karamagi hakujibu maswali ya Zitto kwa kutazama agizo la rais liliyokuwa na tobo kwa kutoifanya sheria. Ndio maana hata mapendekezo ya kamati ile yalikwenda moja kwa moja wizarani (serikalini) yakawaacha wabunge hawana habari ya kile kilicho kubaliwa.

Kwa hiyo hata kama zipo kamati nyingi ni muhimu tufahamu kwanza nini madhumuni ya kamati hiyo. na sidhani kama huko nyuma ipo kamati ambayo iliteuliwa kuzitazama upya SHERIA za uwekeshaji ktk madini.
 
Mkandara nichukue hiyo sentensi yako ya mwisho. Kamati ya kupitia sheria ya madini tayari ilishaundwa na mapendekezo yake ndiyo hayo yaliyopelekwa serikalini Septemba 14. Kitendo cha Rais kuunda kamati nyingine yenye kuangalia kitu kile kile na tatizo lile ina maana kadhaa.

a. Kamati ya mwanzo haikufanya kazi iliyotakiwa. Hoja hii inakuwa ngumu kwa sababu Kamati ile iliwakilisha ripoti yake Septemba 14, 2006. Kama kilichofanywa na Kamati ile hakikuwa sawasawa wao wamejuaje? Kwanini wasiweke hiyo ripoti ili wataalamu waone kama kilichofanywa ni upuuzi hadi tuunde Kamati nyingine.

b. Kamati iliyopita haikuwa na uwezo na utaalamu wa kufanya hivyo (kupitia mikataba). Sasa je Kamati iliyoundwa sasa ina uwezo na utaalamu huo?

Hivi ukiwachukua watu wakaenda kumuangalia Tembo halafu waje na ripoti yao, itachukua mara ngapi na makundi mangapi tofauti kuja na ripoti tofauti kabisa kuhusu huyo Tembo. There comes a point when looking at the same problem, using the same data, will lead to the same conclusions. Tofauti pekee ni mapendekezo ya kufanya tufanye nini.

Sasa kama Kamati hii ya RAis lengo lake ni "tufanye nini" kwa msingi wa ripoti zilizopita basi ina maana; lakini kuanza moja kuangalia kitu kile kile halatu tutegemee majibu tofauti ni mazingaombwe ya hali ya juu.
 
No Comment... Tusubiri tuone kama tume hii itakuja na majibu ya kuwaridhisha watanzania
 
Swali langu ni kwamba, kufuatia matukio hayo, je ni nani alilidanganya Bunge? Mheshimwa Karamagi alidai kamati ilishaundwa na kutoa mapendekeazo yake Septemba 2006, wakati Rais kateua kamati hiyo majuzi tu na wala haijaanza kazi. Kama Mbunge Zitto alifungiwa miezi sita kwa madai kudanganya bunge, ambayo sasa yamethibitika kuwa yalikuwa ni sahihi, halafu Waziri amethibitika kuwa ndiye aliyedanganya Bunge, na Bunge lilitoa adhabu kwa watu wa Kigoma kimakosa, je ni adhabu gani itolewe kwa Karamagi na kwa Bunge lote lililotoa adhabu ya kimakosa kwa mbunge Zitto?



Dawa ya hao wabunge wasiojali maslahi ya nchi yao, na wasiofuata kile walichotumwa na waliowachagua ni ndogo sana; Kutowapigia kura 2010, wananchi wakifahamu vizuri ni lini inatakiwa kukiadhibu chama na wabunge wake wote wasio makini kazi itakuwa rahisi sana 2010.
 
Tanzania hainufaiki na madini - Mzungu

Yohanes Mbelege na Flora Temba, Moshi

TANZANIA imekuwa ikipata faida kidogo kutokana na madini ikilinganishwa na nchi zingine zenye madini, imeelezwa.

Hayo yalisemwa jana mjini hapa na Mwakilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la Norwei la Norwegian Church Aid, Bw. Fredrick Glad-Gjernes, wakati akitoa salamu kwenye mkutano wa wachungaji na wajumbe wa Bodi za SACCOS zilizo chini ya Benki ya Uchumi inayomilikiwa na Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT).

Alisema kimsingi si Tanzania pekee yenye tatizo hilo, kwani Afrika imekuwa ikifadhili mataifa tajiri, ambayo yamekuwa yakichukua raslimali nyingi kutoka Afrika.

Bw. Glad-Gjernes alisema ipo haja kwa mataifa ya Afrika kuweka juhudi za pamoja kwa ajili ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi, ambapo alimnukuu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kuwa alikuwa akihubiri mapinduzi hayo.

Akizungumzia uhusiano wa kibiashara, Bw.Glad-Gjernes, alisema kutokana na bidhaa za nchi za nje kuwekewa ruzuku na mataifa hayo, bidhaa za Tanzania zimekuwa haziwezi kushindana nazo.

Aidha, alisema wakulima wa mazao mbalimbali wamekuwa hawanufaiki na kilimo na akatolea mfano wa kahawa, kuwa wakulima huambulia asilimia mbili tu ya bei ya madukani Ulaya.

Katika hatua nyingine, mwakilishi huyo alipigwa na butwaa kuona maduka makubwa nchini, yakiuza matunda ya nje na kuwataka Watanzania kujenga tabia ya kupenda bidhaa zao.

“Nilikuwa na mke wangu natafuta juisi Dar es Salaam, nikawa kila nikipita nakuta juisi imetengenezwa kwa matunda ya Ulaya au maziwa yametoka nchi za nje, huku vitu hivyo vikioza Tanzania kwa kukosa soko!,” alisisitiza Bw. Glad-Gjernes.

Alisema tatizo kubwa ni uhusiano wenye mifumo ya kiunyonyaji katika sekta za biashara na uwekezaji, zilizopo baina ya Tanzania na mataifa makubwa.

Aliongeza kuwa hali hiyo ikiachwa ilivyo, itaifanya Tanzania iendelee daima kuwa maskini.

Alisema uhusiano wa aina hiyo umekuwapo kwa muda mrefu, huku matajiri kutoka mataifa makubwa yakijitajirisha kutokana na raslimali za Tanzania.

“Hii ni changamoto kwa Kanisa, kwani bila hivyo Watanzania wataendelea kubaki maskini, iwapo hakutakuwa na nguvu ya pamoja kukomesha uhusiano ya aina hiyo,” alisema.
 
Leo mchana nimepata nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Ushauri kuhusu Sekta ya Madini Mhe. Jaji Mark Bomani. Mahojiano kamili yatarushwa siku ya Jumapili kupitia Bongo Radio ambayo yatafuatiwa na mjadala kuhusu "Tanzania miaka 46 Baadaye". Wote mnakaribishwa!
 
Hatuna nguvu za kisheria kubadilisha mikataba ya madini tuliyoingizwa mkenge ndiyo siyo?!

SteveD.
 
Ina maana we are doomed Milele?? Ina maana kubadilisha hata sheria zilizopo hawawezi? Ngoja tutasikiliza mahojiano yako Mwanakijiji tujue zaidi.
 
Ina maana we are doomed Milele?? Ina maana kubadilisha hata sheria zilizopo hawawezi?

Very sad, lakini usishangae Mazee huu kuwa ndio ukweli wenyewe mkuu!
 
Kwa wenzetu ukiingiza serikali hasara, unapoteza kazi. Wacha tusubiri hiyo kamati itasema nini juu ya hao waliosaini mikataba mibovu.
 
mikataba sawa, ila mi nauliza hata huu utumbo wa pembeni wa kusamehe kodi ya mafuta yanayo tumika katika migodi, yaani nayo haiwezi batilishwa?
 
Leo mchana nimepata nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Ushauri kuhusu Sekta ya Madini Mhe. Jaji Mark Bomani. Mahojiano kamili yatarushwa siku ya Jumapili kupitia Bongo Radio ambayo yatafuatiwa na mjadala kuhusu "Tanzania miaka 46 Baadaye". Wote mnakaribishwa!

Tulishasema hapa JF, hii kamati ni usanii tu hakutakuwa na lolote jipya la kuikwamua Tanzania katika mikataba ambayo inawanufaisha makampuni ya nje na haina maslahi yoyote kwa Watanzania. Na cha kusikitisha zaidi wale wote waliohusika na kusaini mikataba hiyo bado wamo kwenye siri kali na hakuna wa kuwagusa! Wanaendelea kupeta kama vile hawajawakosea chochote Watanzania!
 
From the pace we are going, and the decisions we are making......I believe Tanzania is digging itself into a very unstable country.
 
"Hatuna nguvu za Kisheria"......labda mwenyekiti alikuwa na maana ya kwamba 'Kamati yake haina nguvu ya Kisheria!' .....maanake siku hizi Mkjj amekuwa hodari sana wa 'suspense.'

In any case, hiyo kamati ilikuwa ni udanganyifu mkubwa tokea mwanzo wa kuundwa kwake. Na maskini wananchi tuna tabia za kusahau mambo haraka mno, ndio matatizo yetu. Hadidu za rejea za kamati hii zilizuunguuuuuushwa, hakuna tena anayezikumbuka! Kamati haikupewa jukumu la kutafuta sababu za kutengua mikataba iliyokwisha wekwa sahihi; lakini wananchi tupo, na tunadhani hiyo ndio kazi ya hiyo kamati!

........"Na cha kusikitisha zaidi wale wote waliohusika na kusaini mikataba hiyo bado wamo kwenye siri kali na hakuna wa kuwagusa! Wanaendelea kupeta kama vile HAWAJAWAKOSEA chochote waTanzania"(Bubu Ataka Kusema).

Hao ni akina nani? Hawastahili kuonewa aibu hawa, tuwataje tu:

1. Mramba
2. Andrew Chenge, Former Attorney General, waziri wa miundo mbinu sasa.
3. Kikwete; aliyajua yote haya akiwa katika baraza la mawaziri, na bado akaendelea kuwateua hao hao
3.
Endeleza orodha tuwafahamu vizuri hawa.
 
ngoja nitafute uraia halafu mniite coward!
 
Mambo ya Profesa Singira, kuchezesha mayai gwaride........kaazi kweli ipo!!.
 
ngoja nitafute uraia halafu mniite coward!

Koba:
Na wale ndugu zako pale mahali........; bibi na babu pia utawafanyaje; au ndio kwa vile utakuwa umejitoa na wao utawatelekeza?
 
Back
Top Bottom