S. S. Phares
JF-Expert Member
- Nov 27, 2006
- 2,138
- 88
siku zote alikuwa wapi huyu!? 😕
Mbunge wa CCM naye akerwa na wawekezaji katika migodi
* Awakoromea mbele ya Waziri Mkuu Lowassa
Na Mkinga Mkinga, Mara
Kutoka Gazeti la Mwananchi
Mbunge huyo aliwahi kususia makabidhiano ya Sh240 milioni kutoka kwa wawekezaji, akidai kuwa hataki kuona uchafu ukifanyika mbele yake kwa sababu hajui umiliki wa migodi hiyo pamoja na uliokuwa jimboni lake la Buhemba.
Sitaki kuona uchafu huo unafanyika mbele yangu. Maana hiyo mikataba mimi siijui, hata ule wa mgodi wa Buhemba, ambao uko jimboni kwangu sijui unamilikiwa na nani,? alinukuliwa Mkono wakati akisusia kushuhudia makabidhiano hayo kati ya Kampuni ya Barrick Gold Tanzania na halmashauri za wilaya ambako kuna migodi yake.
Nilipata kichefuchefu saba ninaposoma
Huyu Mkono ni mtu wa ajabu sana; msimamo wake kuhusu wawekezaji haueleweki na sijui kama hapa anafanya unafiki au ndiyo msimamo wake kweli kweli. Kumekuwa na tetesi zisizothibitishwa kuwa yeye alikuwa msitali wa mbele katika kutayarisha mikataba ile na hivyo kujipatia mapesa mengi sana. Makampuni mengi ya nje yaliyoingia Tanzania yameptia kwake, na kuna siku aliwahi kusema kuwa yeye ndiye aliuza MNB. Sasa imekuwaje? hata mimi sielewi, nadshani huu utakuwa unafiki tu.
Katika maneno yake hapo juu na hizi tetesi za Kichuguu; ni mtazamo wangu kuwa huenda kweli hata yeye ameachwa gizani.