Karibu sana Zitto, na pole na majukumu.
MwanaKijiji,
Inabidi tu leo niseme kuhusu suala hili la Kamati. Maana naona wenye misimamo ya kupinga kamati bado wapo pale pale na hasa wewe ambae ninakuheshimu kweli kweli na critics zako huzipa umuhimu mkubwa kama ilivyo kwa wengi tu hapa JF akiwemo Field Marshal ES.
Ninaamini kamati hii ya sasa itafanya kazi vizuri kutokana na matokeo ya kazi za kamati nyingine. Kamati hii haichunguzi kamati nyingine. Kamati hii inajifunza kutoka kamati nyingine, inaangalaia hali ya sasa na kisha si tu kutoa mapandekezo bali kuweka ratiba ya utekelezaji (action plan).
Kamati ya mwisho kupitia suala hili ni mwaka mmoja uliopita tu; nini kitakuwa kimebadilika kwa kiasi kikubwa kulazimisha kuunda kamati nyingine? Katika mapendekezo mtakayotoa ambayo ni ushauri na si lazima na Rais hafungwi kuyafuata kitatokea nini kama Rais hatayafuata? Je, mtayaweka mapendekezo yenu hadharani kabla hamjamkabidhi ripoti Rais?
Inawezekana mapendezo yasiwe tofauti sana na ya kamati nyingine, lakini hatutatoa blank cheque. Tutaweka nini kifanyike lini na kwa nini?
Kaka Zitto, kusema nini kifanyike na lini kifanyike ni rahisi mno. Tatizo hamuwezi kulazimisha kifanyike kwa sababu hamna nguvu za kufanya hivyo. Mapendekezo mtakayoweka ni ushauri tu ambao haumlazimishi mtu yeyote kuufuata; sivyo?
Pia kumbuka kamati hii ya sasa ipo katika public scrutiny kuliko kamati nyingine zote. Hivyo, pale ambapo serikali itashindwa kutekeleza itakuwa ni jukumu la jamii nzima kuishinikiza serikali kufanya. Ripoti ya kamati hii itakuwa ni reference point kama ilivyo sasa kwa ripoti ya Nyalali kuhusu vyama vingi. Ndipo tunapolenga.
Ripoti ya Nyalali ililetwa na Tume ya Nyalali. Kwanini basi Rais hakuamua hata kuifanya Kamati yenu iwe Tume na kuipa nguvu fulani fulani. Sasa hivi kwa jinsi nilivyomuelewa Jaji Makani, nyinyi ni Kamati ya Ushauri tu na ushauri unaweza kusikilizwa, kujadiliwa, kufuatwa au kupuuzwa na kutupwa. Kwanini basi mapendekezo ya Kamati zilizopita yasiwekwe hadharani ili tuone ya kwenu itakuwa na tofauti kiasi gani? Kama mnachoangalia ni kile kile kilichoangaliwa na waliotangulia kuna uwezekano gani mkubwa wa tofauti kubwa ya mapendekezo?
Sasa hii tabia ya kulalama tu haitatusaidia. Maana those who were against kamati, have continued to be so even if they now see nyaraka from kamati which they wouldnt have seen kama si kamati hii. Badala ya kutumia nyaraka hizi to push for radical changes, nyaraka hizo zatumika kuonesha kamati hii haina kazi.
Sidhani kama ni kulalama kimsingi bali kuweka hiyo pressure ambayo mnaitaka kwenye Kamati. Endapo wote tungepokea na kufurahia kamati hii bila kuhoji basi kuna mambo ambayo yangepita kiurahisi tu. Kuweza kupata baadhi ya nyaraka inatusaidia kuona ni kwanini Kamati hii jinsi ilivyo sasa haikuhitajika.
Lazima mkumbuke kuwa mpaka sasa kiasi cha madini tunayochimba ni asilimia 0.5 tu ya hazina ya madini inayojulikana nchini. kuna mikataba 6 ya madini ya dhahabu mpaka sasa. Hivyo wakati inabidi kuchukua hatua madhubuti kurekebisha makosa ya nyuma,
Hili ni kweli, upande mmoja linatisha (kwamba kidogo tulichofanya tumeboronga kiasi hiki, kikubwa sijui itakuwaje hasa kama mafuta yatapatikana) na upande mwinginee inatia moyo (makosa tuliyoyafanya yanakuwa somo kwa yale makubwa zaidi ya yanayokuja)
to shame those waliotuingiza katika mikataba ya kipumbavu kabisa licha ya mapendekezo ya kamati mbalimbali na kuwachukulia hatua za kisiasa na kisheria,
Nafikiri huo ndio ulikuwa msingi wa hoja yako Bungeni. Sidhani kama Kamati hii jinsi ilivyo sasa ndicho ulichokitaka Bungeni na kama ndiyo hicho basi miye nitakuwa nimekosea tafsiri yangu kuhusu hoja yako. Sidhani ulitaka iundwe kamati ya rais kupitia mikataba na kutoa mapendekezo. Nilivyoelewa ni kuwa wewe ulitaka kamati teule yenye uwezo wa kuchunguza hata waliotuingiza huko badala ya kutaka waaibike tu kwa "upumbavu wao".
ni lazima pia tuangalie mbele ili kulinda hazina ya 99.5% ambayo haijaingia katika mkataba wowote na ile ambayo bado hatujaijua ni kiasi gani kama Uranium, Coltan na Platinum.
Very good point kaka, muanze kwa kukupendekeza wasitishe uingaji wa mikataba mipya hadi sheria mpya itungwe na mechanisms zimewekwa kusimamia sekta ya madini; nna kuingiwa upya kwa mikataba iliyokwisha pita, hata ikibidi makampuni kufunga virago! Ni suala la maisha ya taifa letu. Na zaidi ya yote chondechonde mshaurini Rais ipigwe marufuku mawaziri kuwa na hisa kwenye makampuni ambayo wanayatolea maamuzi kama alivyofanya Yona!
Nkrumah alisema, forward ever, backward never! Ni lazima tuangalie mbele huku tukisafisha nyuma. Vinginevyo tutakalia kusafisha tu ilhali mbele kunaharibika. Sisi tumesema katika kamati yetu, this should be the last kamati on Madini kama ilivyo kuwa kwa Nyalali on vyama vingi. Ripoti iwe wazi ili itumike kushinikiza viongozi kuitekeleza.
Kamati inahitaji zaidi msaada more than ever, critics zimeshatoka nyingi. Isiwe kuna watu wanataka kamati ishindwe kazi ili waseme 'si tulisema, yako wapi sasa'. Hatutatenda mema kwa Taifa hili.
Endeleeni kufurahia music, na mingi naamini itakuja!
Asante sana, sidhani kama Kamati ikishindwa kuna mtu atafurahi; kwani itakuwa ni kushindwa kwa mojawapo ya Kamati muhimu sana katika historia yetu. Binafsi naamini kuwa liwalo na liwe, ndiyo watu washayavulia nguo maji, hawana budi kuyaoga. Tatizo langu ni kuwa ingawa naamini waliopo wanaweza kufanya walichoaminiwa na taifa lao, sidhani kama matarajio ya wananchi yatakuwa yametimizwa kwa sababu kile kilichosababisha wewe ufungiwe vikao vya Bunge hakiguswi na Kamati hii, so mkimaliza we will be back to square one!