Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

ngoja nitafute uraia halafu mniite coward!

Yaani siku zote hizi?? ulikuwa unasubiri nini?? Watasema ati huna ballz, utafikiri kuwa raia wa nchi ambayo bado ipo kwenye "stone age" ni ujasiri wenye maana.......laana iliingia bongo pale mkandamizaji alipoonekana ndio mwokovu wa nchi ile!!. Watu wanataka kutoka shimoni kwa kuchimba shimo zaidi!! sasa sijui wanataka kutokea kwenye earth core au wapi......mie sijui!.

Hata wamarekani hawamwiti George wa Mount Vernon "baba wa taifa".......halafu kuna mtu anashangaaa ati "maendeleo walipata wapi??? Genious uuunh!!.
 
Nadhani alikuwa anamaanisha kuwa Kamati haina nguvu za kisheria kama ile ya bunge. Na kuna mambo ambayo amayekiri ambayo binafsi yamenifanya nisikie kizunguzungu. Alijibu maswali yangu kwa kikamilifu lakini akanipa suprise moja...
 
Mkjj, malizia hiyo suprise basi, au ndiyo hiyo imesemwa hapo juu kuwa umekuwa mzee wa "ma - suspense"
 
Hivi kweli bado kuna watanzania wanaoamini kuwa JK atachukua hatua kwa hawa wabadhirifu?? hiyo kamati ni danganya toto tu ili kuvuta muda kupoza hiyo issue ipite kama issues nyingine za madawa ya kulevya na kadhalika.
 
Ina maana we are doomed Milele?? Ina maana kubadilisha hata sheria zilizopo hawawezi?

Very sad, lakini usishangae Mazee huu kuwa ndio ukweli wenyewe mkuu!

huu ni uzandiki, na hii ni dalili ya kuumizwa tena hivi karibuni kwa mkataba mwingine mpya....

jamani ni budi tukatae kudhalilishwa na hawa tunaowapa dhamana, hawawafikirii wananchi bali matumbo yao. kwa nini sheria zisibadilike?? sasa tme ni yanini?? au ndo funika kombe....?

sielewe
 
na wataendelea kujenga mahotel nk. maana wao si wavivu kama sisi.
So wanatengeneza mazingira mazuri zaidi ili na sisi tuweze kuchangia maendeleo ya Nchi. Kwenyewe wanasema tajiri na maskini/ au wasio na uwezo mnakuwa na nafasi sawa za kimaendeleo iwe shule, nafasi za kazi na uongozi etc
 
hayo maneno,

will be standbay there at Bongo radio, itakuwa saa ngapi??
 
Rais anaweza kufuta sheria yoyote au kuliagiza bunge kubadili sheria with immediate effect sioni shida hapo. Kama hafanyi hivyo anakuwa na sababu ambazo sio za kitaifa.
 
Kinacho uma sana ni pale serikali pamoja na kuona haya mambo na kujua fika kuwa hakuna changes kuendelea kusaini mikataba kama Buzwagi.

Kama mulivyo ona kwenye muziki wa jana tatizo la kamati pamoja na finds zote ilitoa conclussion ambayo ni poor sana. Iliyosababisha tuendelee kuumia
 
Niliyasema haya miaka iliyopita wengi waliniona Mjamaa aliyekunywa maji ya Uhuru - MBISHI na kadhalika, leo ndio kwanza mnafunguka macho?..
Ukisoma mikataba yote ya Mkapa imesema wazi kuwa hao jamaa wamepewa kumiliki ardhi na madini hayo kwa muda wa MAISHA ya migodi hiyo!..
Tulizungumzia hili kwa kina na nakumbuka tulikubaliana kuwa JK hana solution isipokuwa kuweka makubaliano mapya mezani kama vile mikataba ilisainiwa dhahabu ikiwa dollar 200 kwa Ounce tofauti na hali iliyopo sasa hivi, other than we are doomed for life unless one thing ONLY.. mapinduzi ya serikali na kumpata Chavez!

Tunaweza kuzua deal wenyewe la mapinduzi ya kiushikaji ambayo sidhani kama JK yupo tayari yaani serikai inapinduliwa kwa mission zetu wenyewe against mafisadi wa nje kulinda maslahi ya Taifa. Still tutarudishwa miaka 20 nyuma kwa kuwekewa vikwazo.. Are we ready for that?... sidhani!
Mkandara napomchukia Mkapa mnafikiri labda nina langu jambo lakini uchafu alotuachia wala sii wa kuzungumziwa!..
 
mtakachosikia siyo tu kitawakata maini, bali kitawafanya muelewe kwanini wengine tumeona mazingaombwe tangu Kamati hii kuundwa. Mnachokidhania ndiyo kumbe siyo....
 
Ina maana we are doomed Milele?? Ina maana kubadilisha hata sheria zilizopo hawawezi? Ngoja tutasikiliza mahojiano yako Mwanakijiji tujue zaidi.

OUCH!!,
Unajua uzuri wa JF ni kupata habari nyeti ambazo huwezi kuzipata mahali popote, labda tu uwe kwenye corridors of power au, uwe mtoto, mke au mume wa vigogo au pia uwe mfanyabiashara unayewalisha au unaokula nao rushwa hao vigogo. Ubaya wa JF ni kuwa ukishafahamu hayo mazingaombwe, viini macho, sungura watolewao kwenye kofia na pia jinsi hao viongozi wa kudumu wasivyokuwa na akili (mbumbumbu), na pia wanavyoiuza nchi unaishia kutamani kuwa more "millitant", na uingie msituni na watanzania wengine ili muanze kurudisha hadhi ya nchi yetu tena. Tatizo kubwa ni kuwa unapoanza kufikiria mambo ya kwenda msituni unakumbuka zaidi damu za watu wa kawaida zitakavyomwagika na pia wingi wa hao victims wa mapinduzi, hapo unabaki umeduwaa, hujui ufikie nini, uendelee kuwa mwanamapinduzi au ukae kimya kama kondoo aliyenyeshewa na nchi inaliwa na hao wenye meno.

Kwa kifupi ni kuwa hiyo biashara ya kusema ati hatuna nguvu kisheria mimi sikubaliani nayo na nipo tayari kuingia msituni, kama mtanzania mwenye uchungu na nchi yangi hiyo mimi nasema siikubali, potelea mbali!
 
choveki, hivi mmewahi kuona Kamati inayoangalia Kamati ambayo iliangalia Kamati nyingine!? Hivi mapendekezo ya Kamati ya Bomani yakitolewa na yakaonekana yote yametoka kwenye kamati nne za nyuma mtapiga makofi, mtashangaa, au mtalia kwa vile mmeliwa?
 
Ina maana we are doomed Milele?? Ina maana kubadilisha hata sheria zilizopo hawawezi? Ngoja tutasikiliza mahojiano yako Mwanakijiji tujue zaidi.

Wanabadilisha kwani wao ni Bunge? vipi waheshimiwa???
 
Mwanakijiji ndo maana nimekuambia nageuka kuwa more militant!, sitegemei kuona jipya wala kuona intellectual arguments kwenye hayo mapendekezo, natamani tu kulia kwa kuonea huruma watanzania wenzangu.
 
choveki, even with militancy at the end you have to be able to make an intellectual argument why you chose militancy. Fortunately, the modern world is not as tolerant to militancy as it was in the 70s or early 80s. Africa as a continent knows more about the gravity, destruction and devastation that armed conflicts have caused to its sons and daughters.

Tanzania in particular, tunajua zaidi ubaya wa mapambano ya silaha na jinsi ambavyo sisi tumekuwa waathirika pia. Tuliyoyaona Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya, DRC, Mozambique na kwingineko vimetufundisha jambo moja kubwa; militancy is no joke! Kama kweli you are inclined to consider or even persue military solutions to political problems, I declare myself your enemy numero uno!

Tutawashinda kwa kufungua fikra za watu, kuwaonesha kuwa hoja zetu na mawazo yetu ya utatuzi wa matatizo ya nchi yetu ni bora zaidi kuliko ya wale walioko madarakani. Hadi pale tutakapoweza kuwashawishi wanakijiji kama mimi kuwa Tanzania bila CCM inaweza kutawalika na inaweza kunufaika ndipo hapo tutakapoweza kuleta mabadiliko tunayoyataka. Vinginevyo, hata umshikie mtu mtutu wa bunduki na kumuambia CCM haifai, anaweza kukubali kufa akikuonesha kidolee kwenye Bunduki yako kuwa kwa wewe kumshikia bunduki, ndio maana amechagua CCM!
the devastation that armed conflicts
 
Back
Top Bottom