Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya madini inazidi kuchachafya wananchi, naona ndiyo kabisaa kumekuchwa tu...

Mkataba wa EPAs hauna maslahi kwa wananchi

Na Kizitto Noya
Gazeti la Mwananchi


HOFU ya ufisadi na ubovu wa mikataba katika sekta ya madini, vimewatisha viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu ambao sasa wameazimia kuishinikiza serikali kutosaini mkataba wa Mpango wa Makubaliano ya Kibiashara na Uchumi kati yake na nchi za Jumuiya ya Ulaya (EPAs).

Viongozi hao walifikia uamuzi huo jana katika hitimisho la warsha yao ya siku mbili ya mashauriano ya EPAs iliyoandaliwa na Kikundi cha Majadiliano cha Makanisa ya TEC na CCT (TEDG) na kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Baraza la Maaskofu Tanzania, jijini Dar es Salaam kwa siku mbili.

Wakizungumza katika warsha hiyo iliyoandaliwa kwa ajili ya kutathmini faida na hasara ya mkataba huo, viongozi hao walisema kama ilivyo kwa mikataba mingine, mkataba wa EPAs hautaisaidia Tanzania zaidi ya kuliongozea taifa umaskini.

Mpango wa EPAs unalenga kupunguza masharti ya kibiashara baina ya nchi zinazoendelea na za Jumuiya ya Ulaya kwa bidhaa zinazozalishwa katika nchi hizo.

Mratibu wa Shirika la Madeni na Maendeleo nchini (TCDD), Chamba Kejege, alisema kuwa mikataba mingi nchini imekuwa chanzo cha umaskini kwa kuwanufaisha wageni na kuwasahau wazawa.

Alisema pamoja na sababu nyingine, umaskini nchini umechangiwa na mikataba mibovu iliyosainiwa kuwanufaisha wageni na kikundi fulani cha watu badala ya wananchi wa kawaida.

Alisema Tanzania ni ya tatu barani Afrika kwa umaskini ambao kwa kiasi kikubwa unatokana na madeni haramu yaliyopatikana kwa hulka za baadhi ya watu kujiongezea utajiri.


"Wakati mwingine huwa tunaomba mikopo wakati hatuna ulazima na matokeo yake fedha hiyo zinaingia katika matumizi ambazo hayakuainishwa," alisema Kajege.

Alisema historia inaonyesha kuwa nchi za Ulaya hazijawahi kufanya biashara yenye lengo la kuzinufaisha nchi maskini na mpango wa EPA hauna maana yoyote zaidi ya kuendelea kuziibia nchi hizo.

Alisema Tanzania haina budi kuanza kujifunza kukuza uchumi kwa kudhibiti matumizi ya rasilimali zake, badala ya kutegemea mikopo na mikataba ambayo kwa kiasi kikubwa inaliongezea taifa umaskini.

Kwa mujibu wa Kajege ni hatari kwa Tanzania kuingia katika mpango wa EPA kwa kuwa masharti yake yameonekana dhahiri kutaka kuua soko la bidhaa za ndani na kupalilia soko la bidhaa za nje.

Mwakilishi wa Shirika la Misaada la Makanisa la Norway nchini, Fredrik Glad-Gjernes aliwataka viongozi wa dini kuwa mstari wa mbele kupinga mpango huo kwa kuwa nchi inaweza kujiendesha kwa rasilimali zake.

"Utasemaje kuna uwiano wa uhuru wa kibiashara wakati kuna masharti ya ubora wa bidhaa na mengine mengi?" alihoji.

Alidai kuwa mpango wa EPA ni maalum kwa ajili ya kuzinyonya nchi maskini kwani masharti yanayoambatana nao hayatoi fursa kwa nchi maskini kufanya biashara yenye uwiano kati yake na Ulaya.

Kwa mujibu wa mwakilishi huyo, Tanzania inapaswa kuacha tabia ya kukimblia mikataba bila kufanya tafiti za faida na hasara zake, kwani kufanya hivyo ni kulipeleka taifa pabaya.

Aliwataka viongozi wa dini kusimamia hatima ya nchi yao kwa kuishinikiza serikali isitishe mpango wake wa kusaini mkataba huo ufikapo Desemba 31 mwaka huu kwa maslahi ya wazawa.

Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Dismas Shekalaghe aliitaka serikali kupitisha sheria ya wabunge kushirikishwa katika kuidhinisha madeni ya nje ili kuziba mianya ya rushwa na ufisadi

Alisema moja ya sababu za umaskini nchini ni rushwa na ufisadi unaofumbiwa macho na wabunge ambao ndio wawakilishi wa wananchi.

"Mimi nina mashaka na Bunge kwamba linachangia ufisadi kwa kuwakilisha maoni yao na matakwa ya vyama badala ya wananchi. Kwa nini lisishirikishwe katika kuidhinisha madeni ya nje ili kuziba mianya ya rushwa?" alihoji Shekalaghe.

Awali, Kajege alitaja sababu za bunge kushindwa kudhibiti mianya ya rushwa kuwa ni pamoja na tabia ya kulindana.

"Bunge lilitakiwa kuidhinisha madeni ya nje likiwawakilisha wananchi, lakini hapa nchini hili haliwezekani kwa sababu nyingi ikiwamo kulindana na takrima.

Alitaja tatizo lingine kuwa ni udhaifu wa katiba ya nchi ambayo mpaka sasa hairuhusu wananchi kuwafukuza kazi wabunge waliowachagua.

Askofu Dk Peter Mwamasika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma alisema Tanzania haihitaji kuendelea kuwanufaisha watu wachache kwa kusaini mikataba isiyokuwa na tija kwa taifa.

Alibainisha kuwa umaskini wa Tanzania ni matokeo ya ufisadi na kubebana kwa baadhi ya viongozi katika kuendesha nchi.

Juzi mtaalam wa masuala ya mikataba ya biashara za Kimataifa, Profesa Francis Matambalya alisema katika mada zake kuwa mpango wa EPA ni hatari kwa kuwa hauruhusu ushindani wa kibiashara baina ya pande hizo mbili.

Alisema kimsingi Tanzania inatakiwa kuingia katika mpango huo baada ya kuwashirikisha wananchi wake na watalaam ili kubaini faida na hasara zake, kuondoa matatizo yasiyo ya lazima.

"Serikali peke yake haitoshi kuingia katika mkataba huo bila kuwashirikisha watalaam kuuchambua na kujua athari zake," alisema Matambalya.


SteveD.
 
Ukishaona viongozi wa Ibada wanazungumza ujue idadi kubwa ya wananchi watapata taarifa ya nini kinaendelea na hii mikataba feki

Time will tell............siku hiyo HAKI ya mwananchi itakapokuwa HAKI

Inshaallah
 
kwawale waliyo wengi na wachangiaji wa JF mimi ninawapa pongezi sana kwa kila jambo, muendelee hivyo hivyo ujumbe umefika makanisani na misikitini basi sauti za wengi ni sauti ya mungu, kilio chetu kimesikika tena kwa kishindo asilimia 80%
ameni
 
Mwalimu Nyerere hakuwa mjinga. Yeye alisema yaacheni hayo madini ardhini mpaka Watanzania watakapokuwa na uwezo wa kuyachimba wenyewe. Waliomfuata wakaona eti amepitwa na wakati. Guess nani kapitwa na wakati? Angalia sasa tunaambulia kitu gani?
 
Ukishaona viongozi wa Ibada wanazungumza ujue idadi kubwa ya wananchi watapata taarifa ya nini kinaendelea na hii mikataba feki

Time will tell............siku hiyo HAKI ya mwananchi itakapokuwa HAKI

Inshaallah

Very positive comment.......i hope kila mtu anaona umbali huo!!!. Kuna some mvts ambazo bado nazichungulia,conspirancies ambazo ni no brainer....but let's see. Kama ulivyosema inshallah kila mtu ataelewa nini kipo at stakes hapa!!.
 
Hapa walau viongozi hawa wa dini wameanza kuzungumzia ukombozi wa taifa hili.

Naamini sasa wale watu waliokuwa wamezoea kubeza kuwa hizi ni kelele za wapinzani sasa watakosa la kusema kwani hawa viongozi wa dini nao ni watu walioshindwa uchaguzi?

Mapambano yaendelee naamini kuwa kilaq siku yanachukua sura mpya kila kukicha,

Osama wetu sisi ni ufisadi tumsakame hadi torabora.
 
Serikali yazinduka

*Yaanza kukagua makapuni ya madini
*Lengo ni kujua mapato na faida halisi
*Chakula cha maafisa kutozwa kodi
* Kufuatilia Safari za ndege migodini


Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
15/10/2007


HATIMAYE serikali imezinduka na kuanza ukaguzi wa kina wa mapato na matumizi kwa makampuni yote ya madini yaliyowekeza nchini.

Habari zilizopatikana kutoka Wizara ya Nishati na Madini, zinasema kuwa ukaguzi huo unalenga kubaini faida halisi au hasara yanayopata makampuni ya madini nchini ili kuzuia udanganyifu.

Mkurugenzi wa Elimu kwa Walipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Protas Mmanda aliiambia Mwananchi kuwa ukaguzi huo ulianza mwishoni mwa Septemba na kwamba mpaka sasa unaoendelea.

Hatua hiyo imchukuliwa huku kukiwa na taarifa kwamba baadhi ya makampuni ya madini yamekuwa yakifaidika na utajiri huo na kuacha mashimo bila ya kuwanufaisha Watanzania kwa kushindwa kulipa kodi kwa kisingizio cha kutopata faida.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, serikali imeamua kufanya ukaguzi huo ambao utahusisha pia mambo mbalimbali ikiwamo chakula cha maafisa wa makampuni hayo kinachoagizwa kutoka nje, safari za ndege, nchi kavu, mawasiliano ya simu na mambo mengine.

"Lengo la serikali ni kutaka kujua kila kampuni ya madini inapata kiasi gani, inatumia na inalipa nini, ndiyo maana imeamua kufanya Intensive Auditing (ukaguzi wa mahesabu wa kina)," alisema Afisa mmoja wa serikali ambaye hakupenda kutajwa jina lake.

Katika mpango huo serikali imeamua kuangalia kwa karibu sekta ya madini ili kuondoa malalamiko ya makampuni ya madini kuiba rasilimali hiyo na kuifanya nchi kunufaika kidogo.

Kuhusu kodi ya chakula, TRA imesema kodi itakatwa kiwango ambacho hutolewa kwa maafisa chini ya mpango maalum ambao hauhusu wafanyakazi wengine ambao unatumika pia katika kuangalia mwenendo wa safari za maafisa na wafanyakazi wengine.

Akifafanua kuhusu suala hilo, Mmanda alisema linatekelezwa chini ya Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka 2004.

Taarifa kutoka serikalini zinaonyesha kuwa mwaka 2005/06 hadi kufikia kabla ya Juni mwaka huu, jumla ya kodi zilizolipwa na makampuni yote ya madini nchini ni Sh126.17 bilioni.

Kodi hizo ni pamoja na kodi ya makampuni (corporate tax ), asilimia 30, inayolipwa baada ya kampuni kupata faida ambayo ni Sh 7,847,650,428, kodi inayotokana na mishahara ya wafanyakazi (Paye) Sh78,976,589,223, kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) Sh9,101,611,204, ushuru wa maendeleo ikiwamo ya Elimu ya Ufundi (Skills Development Levy-SDL) ambayo hulipwa asilimia nne kiasi cha Sh12,268,926,877.

Kodi nyingine ni kodi ya utaalam (Withholding Tax) Sh17,615,967,890, Gharama za Nyaraka (Stamp Duty) Sh352,804,651na kodi za viwanja vya ndege (Airport Charges) Sh6,530,000.

Kwa mujibu wa kumbukumbu hizo zilizopo TRA, ambazo gazeti hili ilifanikiwa kupata nakala yake, makampuni yote ya madini yaliyolipa fedha hizo ni pamoja na Stanley Mining Service (T) Ltd, Geita Gold Mining Ltd, Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu (Barrick).

Makampuni mengine ni Resolute Tanzania Ltd, Williamson Diamonds, North Mara Gold Mine Ltd (Barrick), East African Mines Ltd, Pangea Minerals Ltd, (Barrick) Kabanga Nickel, Barrick Exploration, Meremeta Ltd (Buhemba Mining), Tanzanite One Ltd ( Mererani), LTA Construction (T) Ltd, Consolidated African Diamonds, Bulk Mining Explosives (T) Ltd na Kagera Mining Company Ltd.

Hata hivyo, hadi wakati takwimu hizo zinaandaliwa kabla ya Bunge la Bajeti la mwaka huu, baadhi ya makampuni hayakuwa yameanza kulipa baadhi ya kodi kama VAT, Stamp Duty, gharama za usafiri katika viwanja vya ndege na kodi za makampuni ambayo huanza kulipwa baada ya kampuni kuanza kupata faida.

Mmanda alisema Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, hajawahi kulidanganya Bunge kwani taarifa alizotoa ni sahihi kuhusu kodi zilizokuwa zimelipwa na makampuni ya madini.

Alifafanua kwamba, wakati Meghji anaeleza bungeni baadhi ya makampuni yalikuwa yamelipa kodi na kuwashangaa baadhi ya watendaji wa makampuni ambao hawajui kodi zinazolipwa ndani ya makampuni yao.

Mmanda alitaja makampuni hayo na kodi zao kuwa ni Bulyanhulu ambayo katika kipindi cha mwaka 2005/06 hadi kabla ya Bunge la Bajeti ilikuwa imelipa kodi ya makampuni Sh1.37 bilioni na kwamba hata kama Waziri alitaja Sh1.12 bilioni hakukuwa na kosa kwani hakuwa ametaja zilizoongezeka mapema mwaka huu.

Alipoulizwa vipi kuhusu kodi ya makampuni kwa North Mara Gold Mining, alisema kulikuwa na kasoro ndogo, lakini kampuni hiyo ililipa Sh9 bilioni kama Vat na kodi ya makampuni.

"Hapa inawezekana sijui kulitokea tatizo dogo, lakini kweli kodi iliyolipwa hadi kipindi hicho ilikuwa ni Vat na ya makampuni jumla sh 9 bilioni," alisema.

Alisema ni kweli pia Geita Gold Mining ilikuwa imelipa kodi ya makampuni Sh1 bilioni hadi kipindi hicho wakati waziri anawasilisha taarifa hizo.

Kuhusu taarifa ya kwamba baadhi ya makampuni yamekana na kusema yataanza kulipa kodi ifikapo mwaka 2011, Mmanda alisema kwa mujibu wa Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka 2004, kampuni haiwezi kusema lini itaanza kulipa kodi na kutaja kipindi kirefu cha namna hiyo.

Hivi karibuni kumeibuka utata kuhusu kodi ambayo Waziri Meghji alisema ililipwa kwa makampuni ya madini, kwani baadhi ya wahusika walisema hawajaanza kulipa na hivyo wataanza kulipa kodi ifikapo mwaka 2011, lakini TRA walisema waziri alikuwa sahihi kwani kodi ilishaanza kulipwa.
 
kushakuchwa tayari ndugu yangu yaani ndo wanagutuka leo wakati giza lishaganda watu washapata faida washajenga na kununua mahekalu ya kifahari ndo wao wanashtuka leo
kwani ndege zimeanza kutua leo mgodini au ile mali inayotoka kule mgodini hao maafisa wa TRA wanajua ni kiasi gani au wanapima tuu uzito na urefu wa container
inashangaza watu washafaidika na kula kuku kwa mrija wao ndo leo wanashtuka wakati watu wamebakisha vimiguu
wabongo kweli ni wazuri sana kwenye kufanya mambo na wanasahau maana wangekuwa wanakumbuka angefanya haya mapema sana wakati wanaingia kwenye hii mikataba na sio muda huu wakati yanakatibia kubaki mashimo tuu kwenye maeneo ya migodi na nchi kadhaa zishatajirika kwa kuuza madini yanayozalishwa hapa bongo
 
Jamaa wa TRA anaonekana kujing'ta ng'ata... bado mapambano yanaendelea tukitoka huku tunakuja TRA. Maana tunawajua maudiotor wao wenye maekalu karibu na mbuga huko.
 
yaani anaonekana hajajua kuwa anataka nini kwa wakati huu na ni nini anatarajia kupata kuk\tokana na uchunguzi wake
 
walikuwa wapi wasichukue hatua kama hizi, wakati walikuwa wanaambiwa what is going on na mapungufu ya hii mikataba. au kwa sababu helkopta zinapigwa mawe, viongozi wanazomewa, watu wanalilia hela ya rada, na gulf5 stream, na baada ya wengine kujenga mahoteli, na watoto wao kwenda kuishi merekani etc
 
walikuwa wapi wasichukue hatua kama hizi, wakati walikuwa wanaambiwa what is going on na mapungufu ya hii mikataba. au kwa sababu helkopta zinapigwa mawe, viongozi wanazomewa, watu wanalilia hela ya rada, na gulf5 stream, na baada ya wengine kujenga mahoteli, na watoto wao kwenda kuishi merekani etc



ndo hapo wanaponyanyuka muda huu kuangalia kimefanyka nini wakati it is already too late to catch the bus

wangojee kuachiwa mashimo tooo kama yatakuwepo maana kwenye hii mikataba yao wameweka na kipengele kuwa ardhi inaweza kuwa mali yao wakitaka watakapomaliza issue ya uchimbaji wa madini

wabongo kweli tupo maana kuna siku itauzwa hata ikulu huku tunaona
 
Swala la upitiaji wa mikataba ya madini si jambo geni kwetu; kama mnakumbuka hiyo ndiyo iliyokuwa moja ya key policy pillars za Bwana Mbowe wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005. Hata hivyo baada ya ushindi wake wa tsunami, Bwana Kikwete akawahidi wananchi kupitia inaugural speech yake pale Bungeni kuwa mikataba yote ya madini itapitiwa tena upya. Kufuatia ahadi hiyo, rais akaagiza kuwa serikali haitaingia mikataba mingine ya madini mpaka baada ya mapitio ya mikataba ya sasa na kuboresha kwa sheria zetu za madini. Ni wazi kuwa mikataba yote ya madini iliyoingiwa wakati wa utawala wa Mkapa ilikuwa na dosari kubwa sana kiasi kuwa hata wananchi wa kijijini wasiojua biashara ya kimataifa wanajua kabisa kuwa madini yetu yanachukuliwa bure. Hivi Majuzi tu Waziri Mkuu wa Kanada naye ametukandia kuwa sisi wewenyewe ndio tunaoachia mali zetu kuchukuliwa bure kwa kuwa na sheria mbovu. Kwa hiyo agizo la kuboresha sheria zetu za madini na kupitia upya mikataba ya madini iliyopo kabla ya kuingia mikataba mingine lilikuwa na nia njema kabisa.


Hata hivyo, wakati wananchi bado wanasubiri upitiwaji wa mikataba hiyo, mnamo mwanzoni mwa mwaka huu serikali yetu iligundulika kuingia mkataba mwingine wa madini tena mkataba wenyewe ukasainiwa hotelini nje ya nchi. Jambo hilo lilimfanya Mheshimiwa Zitto Mbunge wa kigoma kuuliza kwa nini serikali iliingia mkataba huu wa madini ilihali zoezi la kupitia mikataba ya madini kama alivyoagiza Rais halijafanyika. Swali hilo lilijibiwa na Waziri kama ifuatavyo:

"
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kabwe Zitto anazungumzia eti maagizo ya Rais yalikiukwa, kauli anayoitoa bila ya kutafakari maagizo hayo yalikuwa ya aina gani. Mheshimiwa Rais aliagiza mikataba yote ya madini kufanyiwa mapitio ili kubaini maeneo yanayoweza kurekebishwa kwa faida ya pande zote mbili – faida ya Nchi na faida kwa Mwekezaji (win-win situation). Kamati iliundwa kwa ajili hiyo na baada ya kukamilisha kazi iliyopewa, iliwasilisha mapendekezo yake Serikalini tarehe 14 Septemba, 2006. Baadhi ya mapendekezo ya Kamati hiyo yalitumika katika majadiliano na makampuni ya madini yenye mikataba ya zamani. Mafanikio ya majadiliano hayo niliyataja kwenye hotuba yangu wakati nawasilisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ya mwaka 2007/08 kuwa ni:-

• Kuondoa nyongeza ya asilimia 15 kwenye mtaji wa uwekezaji ambao haujarejeshwa (15% additional capital allowance on unredeemed qualifying capital expenditure). Hatua hii itawezesha kampuni hizi kukomboa gharama zao za uwekezaji mapema na hivyo kuweza kulipa kodi ya mapato (corporation tax). Kwa hili, ningependa kumsahihisha Mheshimiwa Kabwe Z. Zitto kwamba kuondolewa kipengele hicho siyo automatic kwamba kampuni inaanza kulipa kodi, isipokuwa inaharakisha muda wa kampuni kulipa kodi.

• Kulipa kiasi cha Dola za Marekani 200,000 kwa mwaka kwa Halmashauri zinazohusika na migodi hiyo. Kampuni ya Barrick Gold Corporation imekubali na imeanza kulipa Dola za Marekani milioni 7 kila mwaka kama malipo ya awali ya kodi ya mapato ya kampuni hadi migodi yake itakapoanza kulipa kodi stahili.

• Kampuni ya Resolute (Tanzania) Limited imeondoa kipengele kwenye mkataba wake kilichokuwa kinairuhusu kutokulipa kodi ya mapato kwa wafanyakazi wake wa kigeni. Kuondolewa kwa kipengele hiki kutailazimu kampuni hii kulipa takriban Dola za Marekani milioni 2.2 kila mwaka kama malipo ya kodi ya mapato. Katika mwaka 2006/07 kampuni hiyo imelipa Dola za Marekani milioni 2.3.

• Kampuni ya AngloGold Ashanti inayomiliki mgodi wa Geita imekubali kulipa kiasi cha Dola za Marekani 200,000 kwa mwaka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Aidha, majadiliano katika maeneo mengine ya mkataba wake, yanaendelea.

Mheshimiwa Spika, hivyo, si kweli kuwa zoezi la kudurusu mikataba ya madini bado linaendelea.



.............


Mheshimiwa Spika, kwa vielelezo na maelezo ya Serikali niliyoyatoa, sasa naomba kupitia kwako kuliomba Bunge lako tukufu vile vile liangalie vielelezo alivyovitoa mtoa hoja kama vipo ili liweze kupima na kuamua ni nani, mwongo ni nani aliyelidanganya Bunge mimi au Mheshimiwa Kabwe Zuberi Zitto. (Makofi)

Baada ya majadiriano hayo Bunge la Muungano likapitisha adhabu ya kumzuia Mbunge Zitto asiwakilishe wananchi wake bungeni "eti kwa kusema uwongo bungeni." Yaani madai ya kuwa rais aliagiza serikali isiingie mikataba mpaka baada ya kupitiwa mikataba yote ya sasa na kuwekwa sheria mpya ya madini. Bunge lilikubali jibu la Mheshimwa Karamagi kuwa kamati ilishaundwa na kumaliza kazi yake Tarehe 14 Septemba, 2006.

Sasa sote tunajua kuwa ni hivi majuzi tu, ndipo kweli Rais kaunda kamati ya kupitia mikataba ya madini ambayo sote tunaifahamu. Wajumbe wake ni pamoja na Mhesmiwa Iddi Simba, Mheshimwa Zitto na Mheshimiwa Mzee Mapesa.

Swali langu ni kwamba, kufuatia matukio hayo, je ni nani alilidanganya Bunge? Mheshimwa Karamagi alidai kamati ilishaundwa na kutoa mapendekeazo yake Septemba 2006, wakati Rais kateua kamati hiyo majuzi tu na wala haijaanza kazi. Kama Mbunge Zitto alifungiwa miezi sita kwa madai kudanganya bunge, ambayo sasa yamethibitika kuwa yalikuwa ni sahihi, halafu Waziri amethibitika kuwa ndiye aliyedanganya Bunge, na Bunge lilitoa adhabu kwa watu wa Kigoma kimakosa, je ni adhabu gani itolewe kwa Karamagi na kwa Bunge lote lililotoa adhabu ya kimakosa kwa mbunge Zitto?
 
Mzee Kichuguu, nadhani hadi hivi sasa Karamagi yuko Sawa na Zitto amekosea. Kamati iliyoundwa na Rais haipitii mikataba mmoja mmoja bali inaangalia mikataba hiyo na kutoa ushauri kwa serikali bla bla bla; at least that is what Chiligati na Makalla wamesema. Kuwa wale wanaodhania kuwa Kamati hii inapitia mikataba kama ya Buzwagi wamekosea.

Akinukuliwa na gazeti la Tanzania Daima la leo Bw. Chiligati alisema:
"Tunapenda wananchi waelewe kuwa, alichounda rais ni kamati ya kuangalia upya sera, sheria na mikataba ya uchimbaji madini na si tume ya kuchunguza mikataba ya uchimbaji madini"

Sasa kina Zitto wanapofikiria kuwa wameingia kwenye Kamati yenye nguvu fulani ukweli ni kuwa kamati hiyo si lolote isipokuwa vikao vya ushauri na kukusanya mawazo tu, siyo vya kutafuta makosa na kuangalia nani kakosea na nani awajibike. Kilichofungwa siyo goli la maradona tu bali ni mtu kapigwa ndoo ya Zinedine Zidane!! Sisi wengine tumebakia kubonyeza "replay" tena kwa slow motion
 
Kwa kipindi cha miaka mitano ama sita iliyopita ni kuwa serikali imeunda kamati sita za kufanya kazi hiyo hiyo.

Kamati ya DR.Kipokola ilifanya kazi nzuri na pia ile ya General Mboma ilifanya vizuri sana .

Ila la kusikitisha na kutisha ni kuwa pamoja na DR. Kipokola kuwa alikuwa mwenyekiti wa kuangalia sheria na mikataba sasa yeye ni Public Relations Officer wa Barric Gold Tanzania.

Ukiangalia hapo unawweza kuona na kujua aina ya watanzania tuliokuwa nao hawana hata huruma na nchi yao hata kidogo.

Zitto alionewa na kama bunge letu likiwa na busara nzuri sa spika wanapaswa kumwomba radhi na pia kuwahakikishia watanzania kuwa hawatarudia tena kosa kama hilo na pia kama kuna posho n.k za Zitto wamrudishie kwani Karamagi ndio mwongo na hata rais kaonyesha hivyo.

Kama JK angekuwa serious na kuunda hii kamati yake wale mafisadi walioko kwenye kamati angewatoa nje na pia wote wenye mgongano wa kimasilahi ili kuweza kutoka na kitu chenye maslahi kwa taifa kwa ujumla.
 
Hapa Mwanakijiji nami nitaendelea ku-replay huo muziki wako mpaka kieleweke. Kamati hii inapitia mikataba na sheria za madini kutambua udhaifu na ku-recommend remedies. Mapendekezo yatakayotoka ni juu ya Rais mwenyewe na vyombo vingine kama vile bunge kujua namna ya kuyatekeleza yote, kiasi au kuyatupilia mbali yote. Mpaka hapo sijaona tatizo liko wapi hasa.

Zitto as a politician, yeye hana cha kupoteza hapa. Maana wakitoa mapendekezo mazuri na JK akayakubali na kuyafanyia kazi anaingia kwenye rekodi kuwa aliwahi kufanya kazi nzuri katika kuokoa madini yetu. JK akiyatupilia mbali mapendekezo haya, yeye (Zitto) na CHADEMA watayabeba baadhi au yote na kuya-integrate kwenye sera za chama chetu kuhusu raslimali, he, CHADEMA and the nation still win. Haya mzee wangu endelea ku-replay hiyo cd nami na-replay ya kwako mpaka kitakapoeleweka kwa Zitto kutuletea yaliyojiri kwenye kamati!
 
Hapa Mwanakijiji nami nitaendelea ku-replay huo muziki wako mpaka kieleweke. Kamati hii inapitia mikataba na sheria za madini kutambua udhaifu na ku-recommend remedies. Mapendekezo yatakayotoka ni juu ya Rais mwenyewe na vyombo vingine kama vile bunge kujua namna ya kuyatekeleza yote, kiasi au kuyatupilia mbali yote. Mpaka hapo sijaona tatizo liko wapi hasa.

Hapa ndipo tatizo; kama wanataka kuangalia mapungufu mbona tume nyingine zilishafanya hivyo? Hivi kama watu wanaangalia kitu kile kile kwa kutumia ujuzi ule ule what are the chances that watafikia mtazamo tofauti? Kama Kamati zilizofanya kazi kabla yake ziliangalia matatizo ya sheria ya madini na mikataba, hii nyingine inafanya nini tofauti?

Zitto as a politician, yeye hana cha kupoteza hapa. Maana wakitoa mapendekezo mazuri na JK akayakubali na kuyafanyia kazi anaingia kwenye rekodi kuwa aliwahi kufanya kazi nzuri katika kuokoa madini yetu. JK akiyatupilia mbali mapendekezo haya, yeye (Zitto) na CHADEMA watayabeba baadhi au yote na kuya-integrate kwenye sera za chama chetu kuhusu raslimali, he, CHADEMA and the nation still win. Haya mzee wangu endelea ku-replay hiyo cd nami na-replay ya kwako mpaka kitakapoeleweka kwa Zitto kutuletea yaliyojiri kwenye kamati!

as a politician hana cha kupoteza isipokuwa misjudgement. Zitto anaingia kwenye Kamati akiwa na matumaini kuwa kamati hii itaweza kufanya jambo fulani kwa "maslahi ya Taifa" na yeye atatumia nafasi yake kufanya hivyo. Anaingia akiwa na imani kuwa Kamati hii inayo nguvu ya kuangalia kinachotakiwa kuangalia. Hadi hivi sasa tunafahamu wazi kuwa kamati hiyo haina nguvu hiyo isipokuwa ya kutoa ushauri tu. Haina nguvu ya kuhoji, haina nguvu ya kuita nyaraka, haina nguvu ya kuita mashahidi n.k Inayo nguvu moja tu nayo ni kusikiliza maoni na kutafuta maoni. Kama hilo ndilo alilolitaka Bungeni basi amelipata. Lakini kama Bungeni alitaka kitu zaidi ya hicho, ukweli ni kuwa Kamati hii sicho hicho. Itakuwa ni jambo la kuchekesha kwenye kikao kingine Zitto asimame na kusema tunataka Kamati Teule ya Bunge ipitie mikataba mikubwa kwani ile ya Rais haikufanya hivyo; watu watamcheka.. unajua watamwambia nini?..... anybody's guess..?
 
Hapa Mwanakijiji nami nitaendelea ku-replay huo muziki wako mpaka kieleweke. Kamati hii inapitia mikataba na sheria za madini kutambua udhaifu na ku-recommend remedies. Mapendekezo yatakayotoka ni juu ya Rais mwenyewe na vyombo vingine kama vile bunge kujua namna ya kuyatekeleza yote, kiasi au kuyatupilia mbali yote. Mpaka hapo sijaona tatizo liko wapi hasa.

Zitto as a politician, yeye hana cha kupoteza hapa. Maana wakitoa mapendekezo mazuri na JK akayakubali na kuyafanyia kazi anaingia kwenye rekodi kuwa aliwahi kufanya kazi nzuri katika kuokoa madini yetu. JK akiyatupilia mbali mapendekezo haya, yeye (Zitto) na CHADEMA watayabeba baadhi au yote na kuya-integrate kwenye sera za chama chetu kuhusu raslimali, he, CHADEMA and the nation still win. Haya mzee wangu endelea ku-replay hiyo cd nami na-replay ya kwako mpaka kitakapoeleweka kwa Zitto kutuletea yaliyojiri kwenye kamati!

Mkuu Mkumbo alichokisema Kiligati watu wengi hata ukienda ktk janvi hili hawakukielewa kabisa. Wengi walijua Zitto anakwenda kuchambua mkataba hadi mkataba lakini hili halipo kabisa.

Ndio maana hata baadhi ya watu walizungumzia kuwa sheria ndio ina mapungufu. Lakini kikubwa hapa ni kwamba hawakujua kazi ya kamati hii. Watu waliojua hili vizuri walipendekeza kuwa kwa nini watu kama Shivji waliokwisha bainisha mapunguvu wasiweze kuwekwa ktk kamati. Anyway kamati ktk hili nafikiri watamtumia shivji vizuri awape nyanga za kuweza kucompliment report yao.

lakini ukiangalia mbali sana hizi kamati hazitakuwa na kipya sana maana zimeisha kuwa nyingi sana. Ningependa ktk ripoti zao kuwe na majumuisho ya finds za kamati zilizopita na wao watuonyeshe kipya (originality yao iko wapi). na pia finds tofauti na za mtaalamu wa sheria prof. Shivji.
 
HIla mpaka sasa nafikiri tuna bunge la watu waoga sana kuna mambo mengi sana ambayo Mzee Karamagi kadanganya nafikiri ktk story nzima ya Buzwagi ina ulakini wa kutosha ambayo wabunge wenye uchungu na Tanzania wanaweza kumtoa kwa kusema uongo hila ninacho ona hapa ni uoga.

Uongo uliosemwa na karamagi kuhusu Buzwaji umedhalilisha Bunge hata kuliko sentensi ndogo alizosema Zitto. Nafikiri kuna haja ya kuwaandikia wabunge makala ya kusoma Bungeni hili waweze kumuodoa Karamagi hili na yeye apate adhabu ya kutoshiriki bunge angalau siku moja tu kwa kudanganya bunge.
 
Huenda nimeachwa nyuma kidogo kihabari. Mimi nadhani kuwa uundwaji wa kamati hii ni kutokana na haja ya kutimiza ahadi yake ya kupitia upya sheria za madini na mikataba yote. Sasa kama Rais anatudanganya kwa kuunda kamati inayoonekana heavyweight lakini kumbe ni danganya toto basi nimevunjika nguvu kabisa. Siamini kuwa kiongozi wa nchi anaweza kuwa mwongo na mnafiki kiasi hichio, nadhani Makala na Chiligati hawajui wasemalo.

Kwa vyovyote vile, uundaji wa kamati hii unaonyesha kuwa Karamagi alipuuza lile agizo lake la kutoingia mikataba mingine hadi baada ya kupitia upya sera ya madini na mikataba yote.
 
Back
Top Bottom