OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,238
- 103,907
Jana nilibahatika kuhudhuria harusi ya kijana wa jirani yangu. Ile harusi ilihudhuriwa zaidi na watu wa mtaani maana ndio kampani.
Kitu cha kushangaza ni kukutana na midada yenye maumbo mazuri yakiwa yamejiachia na vimini. Wale madada walikuwa na vibe hatari kila nyimbo wanacheza. Nikajaribu kufuatulia kama ni watu wa pale kitaa ikaonekana sura ngeni. Kila mtu nayemuuliza anasema hawajui kwamba pale mtaani hakuna micharuko wa hivi.
Nikaona niongee na mwana kamati kama wamekodiwa au vipi. Akasema yeye pia hajui.
Nikabaki na maswali, hii midada yenye amsha amsha harusini huwa inatokea wapi?