Mi sijaona Tatizo la Mleta mada ingawa watu wanamshambulia sanaa... Kuna watu wakifikisha 25 wameshafanikiwa kuliko anayesema 30 ...
Sisi wengine mbn tumesoma shule za Kupeleka mbolea na majembe ... Ila Wazazi baadae ndo maisha yamekuwa mazuri tunasoma Vyuo vya Private.. na Mdogo wangu ambaye nimemzidi miaka 10 ndo Anafaidi Kuliko hata Sie Wawili ...
Ila Kuna Msemo Mmoja Alishaniambia Mtoto wa Ba Mkubwa.. Ukiwa na Familia Baraka Mungu Ndo Anazinwaga... Ingawa Si wote Tutaweza Pata Watoto ila Kwa Uweza Wake Mungu
Suala la Majaliwa lipo, yaani hapo nakubali bila kipingamizi.
Na suala hilo inaweza kuwa matatizo ya Kizazi, au hata pia matatizo ya Kiafya.
Yote yanawezekana.
Tukirudi kwenye mada husika,
Wewe mwenyewe umeona mfano hai kupitia Familia yenu.
Mleta Mada yuko sawa sana.
Wengi wanakuambia wanajipanga, na hao wanaojipanga wanaenda kufunga Vizazi, kitu ambacho ni hatari na baadae kama ni Mtu wa bahati mbaya, hapo inaweza ikawa chanzo cha kujitia ubovu.
Hebu wewe mwenyewe fikiria, kuna baadhi ya Wasichana kuna sindano wanadungwa, na wakishadungwa hizo sindano basi ujue huyo haingii mwezini miezi mitatu au zaidi.
Sasa hujui hapo unauharibia mfumo wa mwili kutokufanya kazi kama inavyostahili?
Je, kama yakitokea matatizo ya kutokuwa na Kizazi utatafuta Mchawi?
Na wale wengine wenye tabia ya kucholopoa Mimba eti kwasababu bado hawajajipanga, sasa kama hujajipanga! Kwanini ufanye tendo la Ndoa?
Wewe kama imeshatokea, kubali matokeo na wala usiogope kushutumiwa Mtoto wa Zinaa, mara sijui hivi, mara sijui vile.
Mtoto hana kosa hata kidogo, wenye makosa ni Wazazi.
Sasa hebu jiulize, kucholopoa Mimba si sawa na kuua?
Jibu ndio, ule ni Uuaji.
Je wewe unaedai unajipanga kufikia mpaka kukiua Kiumbe, hebu jiulize?!
Kama Mzazi wako angediriki kucholopoa Mimba ya wewe,
Je wewe ungelikuwepo hapa Ulimwenguni hadi hivi sasa tunavyozungumza?
Jibu, hapana.
Kwahiyo tutafakari