Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Hao Intern hawana akili kabisa, au njaa imeyeyusha ubongo wao. Kwani walivyoshawishiwa na MAT, hawakufikiria kabla ya kujiunga? Sasa kama wanajuta, how about the lives of innocent people who are died during huo mgomo wanaojutia? Kama wamesalitiana, M/Mungu atawahukumu kwa mazambi yenu.
 
17 September 2012




Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari walioathirika na mgomo Dr. Paul Swakala (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Na Datus Boniface

Wanaodaiwa kuwa ni Madaktari wanaofanyakazi chini ya usimamizi wa madakatari bingwa (Intern Doctors), wamemwangukia Rais Jakaya Kikwete huku wakimwomba radhi kwa ushiriki wao katika mgomo wa madaktari uliosababisha maafa kwa baadhi ya wagonjwa.

Kwa upande mwingine wamekijua juu Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT) kuwa kimewasaliti katika kutatua matatizo yao kwa sasa.
Hata hivyo, wameomba radhi kwa Wananchi walioathirika na mgomo huo kwa usumbufu uliyosababishwa na mgomo huo.

Hadi sasa Madaktari 364, wako mtaani baada ya kusimamishwa kazi kutokana na kushiriki katika mgomo ambao umeisha hivi karibuni, baada ya kushawishiwa na wenzao wakiwemo viongozi wa MAT.


Akitoa tamko kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari hao, Paul Swakala alisema “Tulikaa na MAT kuzun gumza juu ya kutusaidia kutatua kero zetu lakini wameshindwa kutusikiliza na baadala yake tumeamua kufika hapa na kutoa kilio chetu”


Kutokana na kusalitiwa huko, alitoa onyo kwa Madaktari wengine kuwa wanaweza kupima kama wataendelea kujiunga na MAT au la.

Alienda mbali zaidi na kusema, hawako tayari tena kushiriki kwa namna yoyote katika migomo inayoweka rehani maisha ya Watanzania.
Alisema, kwa hakika wanajutia kosa lao la kushiriki mgomo na wako tayari kurejea kazini ili kuendelea na kazi ya kuwahudumia Wananchi kwa moyo mweupe.


Na ninyi mmekuwa wanasiasa kweli kweli, Laiti mngesema ukweli. Mnasema kuwa mnaomba radhi kwa kusababisha vifo.....Je ni watu wangapi wanakufa kila siku kwa kukosa vifaa muhimu katika hospitali zetu??? Ni wanawake wangapi hufa kwa kujifungua kwa kukosa dawa ndogo tu ya kuzuia bleeding?? Serikali iombe msamaha kwa nani kwa kusababisha maafa haya. Mungu Ibariki Tanzania.
 
17 September 2012




Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari walioathirika na mgomo Dr. Paul Swakala (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Na Datus Boniface

Wanaodaiwa kuwa ni Madaktari wanaofanyakazi chini ya usimamizi wa madakatari bingwa (Intern Doctors), wamemwangukia Rais Jakaya Kikwete huku wakimwomba radhi kwa ushiriki wao katika mgomo wa madaktari uliosababisha maafa kwa baadhi ya wagonjwa.

Kwa upande mwingine wamekijua juu Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT) kuwa kimewasaliti katika kutatua matatizo yao kwa sasa.
Hata hivyo, wameomba radhi kwa Wananchi walioathirika na mgomo huo kwa usumbufu uliyosababishwa na mgomo huo.

Hadi sasa Madaktari 364, wako mtaani baada ya kusimamishwa kazi kutokana na kushiriki katika mgomo ambao umeisha hivi karibuni, baada ya kushawishiwa na wenzao wakiwemo viongozi wa MAT.


Akitoa tamko kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari hao, Paul Swakala alisema “Tulikaa na MAT kuzun gumza juu ya kutusaidia kutatua kero zetu lakini wameshindwa kutusikiliza na baadala yake tumeamua kufika hapa na kutoa kilio chetu”


Kutokana na kusalitiwa huko, alitoa onyo kwa Madaktari wengine kuwa wanaweza kupima kama wataendelea kujiunga na MAT au la.

Alienda mbali zaidi na kusema, hawako tayari tena kushiriki kwa namna yoyote katika migomo inayoweka rehani maisha ya Watanzania.
Alisema, kwa hakika wanajutia kosa lao la kushiriki mgomo na wako tayari kurejea kazini ili kuendelea na kazi ya kuwahudumia Wananchi kwa moyo mweupe.



Wameka-taaaaaaaaaaa!
 
Walimpiga mchingaji kondoo wakatawanyika. Hayo ni maneno toka kitabu kitakatifu na sasa yametimia.
 
Mkuu Mohamedi tantawi, Just because SOME have protested doesnt mean MAT "imesambaratika" ... ican yell you hawa intern 160 waliikuta MAT walipokuja mwaka jana, na MAT itaendelea kuwepo..

Saying MAT imeaambaratika? as kukumbushana tu ..Just because YOU SEE it that way, doesnt meant it LOOKS that way!

mkuu hipo,kinachoangaliwa hapa ni uwezo wa kusaidia wanachama hasa wakati wa matatizo na ndio kipimo cha ukomavu wa chama.sasa kama wanachama wanafika mahali wanaona kuwa wametelekezwa na wamebaki wenyewe bila msaada manake ni nini hapo?
 
Junior doctors siku zote ni chachu ya vuguvugu sasa hawa wakiwa consultants kweli tutafikia hali ya ubora wa huduma na vitendea kazi ktk mahospitali.

Kweli Vyuo Vyetu Vikuu sasa vinazalisha wasomi muflisi hawawezi kutambua kuwa wagonjwa hawapatiwi huduma bora na wao pia hawana vitendea-kazi na mishahara duni!
 
mkuu hipo,kinachoangaliwa hapa ni uwezo wa kusaidia wanachama hasa wakati wa matatizo na ndio kipimo cha ukomavu wa chama.sasa kama wanachama wanafika mahali wanaona kuwa wametelekezwa na wamebaki wenyewe bila msaada manake ni nini hapo?

Mkuu Moh'd , taarifa ilitoka kuwa since suala liko mahakamani, and with that NOTHING can be done till uamuzi huo, lakini during the same time MAT President Dr.Namala Mkopi alishtakiwa, je out of those 160 Interns nani alikwenda hata mahakamani?!

The same time, MAT ilikuwa inaandaa Mkutano(MAT Conference) i believe you know that... ni kweli unaweza kuweka matumaini kwa uongozi, lakini ni vizuri KUUAMINI uongozi,...

Mkuu remember when tulipokuwa Med school, being busy all the time, the truth is med student to loose a day at school he thinks has lost alot(evn if he'l spend the same day doing nothing vut being around books without studying) ...same scenario applies here, kukaa without doing anything while ushazoea heka heka za round, theatre, call nk ni NGUMU and I ADMIT IT, but 160 Intern doctors they had impatience...imagine what is their next move? i liked one of comments someone said Nchi haiendeshwi ka misamaha bali sheria... anyway tusubiri what is next Mkuu Moh'd tantawi.
 
Nina Coke classic na Popcorn pembeni naitazama picha hii.....Tarariraaaa tara!
 
Hawafai kuwa madaktari hawa serikali iwafutilie mbali maana thinking capacity yao ndogo sana! maana walipaswa kujua kuwa hawajahitimu na je wanachokisimamia ni sawa kama ni sawa wangeelea nacho hadi mwisho, hii inareflect kwenye tiba wanatotoa unampa mgonjwa dawa huna uhakika katikakati unabadilishabadilisha anakufa!

Umenena vyema sana mkuu, ukutafakari kwa makini uanaona hawa hawafai hata kuwa wasaidizi wa madaktari (manaesi)
manake hawafikiri kabla ya kutenda, ndo utakuja kusikia wamesahau mkasi tumboni kwa mgonjwa.
 
MAT kama CWT,tatizo la kuwa na viongoz mapoyoyo,igeni yanayotokea merikana kwa zuma
 
Wasaliti wakubwa hawa na vibaraka watiifu wa Magamba

Na Dr Paul aliyeongea ni kada Wa chama twamjua sana, UVCCM hongera sana mmefanikiwa kuwasambaratisha madaktari... Movie ndo imeaanza. Where is my popcorn bag!!!
 
Na Dr Paul aliyeongea ni kada Wa chama twamjua sana, UVCCM hongera sana mmefanikiwa kuwasambaratisha madaktari... Movie ndo imeaanza. Where is my popcorn bag!!!

Mkuu measkron, si ndiye huyu aliyesema wamemhaidi ukuu wa wilaya?!..this was expected..i like your last statment mkuu.
 
Siku zote nyimbo walizokuwa wanaimba madaktari ni solidarity forever. Sasa solidarity hiyo imeonekana iko midomoni tu.

Solidarity gani wakati wengine wanaendelea na maisha yao kama kawaida kazini wakati wenzao wamepoteza hata fursa ya kupata kibali cha kupractice udaktari?

Mgomo umeleta madhara tupu na hakuna faida. Katika kujali uwajibikaji ilipaswa viongozi wote wa madaktari wajiuzuru kwa kushidnwa kupima madhara yanayoweza kuletwa na mgomo waliouitisha na kwa kukataa usahuri wa watu wema wa kusitisha mgomo na kutafuta suluhu na serikali mapema.
 
Unajua hapa jamii forum watu huwa hawaangalii mambo critically. Serikali imekuwa inatafuta namna ya kuwarudisha madaktari kazini. Na wamekuwa wanatoa matamko mbali2 kuwa nia yao ssio kuwafukuza madaktari. ili kujisafisha mbele ya wahisani. Kutokana na hilo wamekuwa wakitaka madaktari waombe msamaha ili serikali isionekane kwamba imebow down kwenye madai yao au isionekane dhaifu, kwamba walitishia nyau sasa wamewarudisha wenyewe! Actually hawa walioomba radhi ni vibaraka ambao wameandaliwa na CCM ili ionekane madaktari walikuwa hawana mantiki katika mgomo wao. Na wameweza kuwapata kwa sababu ya njaa. Mwisho niseme hao interns kwa level yao ya education ni aibu kusema kuwa walipotoshwa au walidanganywa! Ndugu yangu njaa mbaya sana unaweza hata kuikana familia!!
 
Ina maana wamekubali kulipwa chochote ilimradi warudi kazini? Mi na wasiwasi watapewa sharti la kufanya kazi miezi 6 bila malipo kama adhabu ya mgomo waliofanya. Ina maana hata zile tuhuma za Joyce Nyoni, mama Nkya, Dr. Mpondo zilikuwa feki? Kama ndivyo wakawaombe msamaha Lucy Nkya na Dr. haji Mponda kwa kuwaharibia kazi
 
Mkuu mcfm40, can you really imagine eti baba wa familia yake au mama wa familia anadiriki kusema "alipotoshwa/alidanganywa" ... seriously? if they meant that sincerely, i then sincerely doubt the way they run their families...No offence.
 
Ina maana wamekubali kulipwa chochote ilimradi warudi kazini? Mi na wasiwasi watapewa sharti la kufanya kazi miezi 6 bila malipo kama adhabu ya mgomo waliofanya. Ina maana hata zile tuhuma za Joyce Nyoni, mama Nkya, Dr. Mpondo zilikuwa feki? Kama ndivyo wakawaombe msamaha Lucy Nkya na Dr. haji Mponda kwa kuwaharibia kazi

Mkuu MVUNBUZI, I salute to that...absolutely right.
 
Back
Top Bottom