Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

unacheza na njaa ya mtaani wamekumbuka fedha waliokataa kuwa ni ujira mdogo.... maneno mengi ya kuomba msamaha lakini sababu kuu ni hiyo.
 
chezea serikali uone cha mtema kuni wote walifaa kunyongwa ingekuwa china kwani wamekiri kuua
 
waache wakome, wakinyooka ndo tutawafikiria kama tuwasamehe au la...kwasasa waacheni tu wanyookeee hadi wajiuze kama kameruni.
 
chezea serikali uone cha mtema kuni wote walifaa kunyongwa ingekuwa china kwani wamekiri kuua
 
unacheza na njaa ya mtaani wamekumbuka fedha waliokataa kuwa ni ujira mdogo.... maneno mengi ya kuomba msamaha lakini sababu kuu ni hiyo.

Njaa mbaya sana. Sii tu kuwa wanakosa vijimshahara vidogo ambavyo wafanyakazi wengi wa serikali tunapata ila kwa sehemu kubwa hii ni kutokana na kuwa wanakosa nafasi ya kupokea virushwa mshenzi wanavyopata kwa wagonjwa wakiwa kazini. Kama kweli ni uzalendo watueleze kama kweli dai la kudai vitendea kazi lilikuwa ni la kizushi au la!
 
Hakuna mtu asiyeaminika kama mtanzania. umasikini ni kitu kibaya sana. mwingine atauza hadi utu wake


Kamanda futa usemi huo. Siyo watanzania wote wasioaminika. Jivunie asili yako hata kama utokako kuna nyumba mbavu za mbwa au makuti. Sina uhakika na alama yako kama wewe ni gamba kinyonga kwa kusema "Hakuna mtu asiyeaminika kama Mtanzania." Ajabu sana!

Labda utujuze asili yako wewe wapi? Mbinguni kunakosemekana Malaika na watakatifu wote ni waaminifu na wasio na dhambi? Nina wasiwasi sana na mtu asiye na fahari ya atokako kama wewe. Ni nani anayeliibia Taifa hili na Afrika kwa ujumla kwa kuwatumia viongozi wezi na wala rushwa kupitia mikataba isiyo na tija?

Unapaswa kukemea hao madaktari kuwa umasikini wao kama watanzania wengine, usiwafanye wauze utu wao. Wasiangalie wanakosa au wamekosa nini kwa sasa (kazi na matokeo ya kufanya kazi). Mahitaji yao au yetu kama Taifa yawe ya muda mrefu zaidi na yenye manufaa kwetu wote.
 
Taarifa za ndani ya jamii ya madaktari zinamuelezea intern doctor aliyejitokeza na kuomba msamaha leo hii ni kada mtiifu wa ccm.toka mwanzo wa mgomo alihusishwa na kukwamisha mipango ya madaktari.alikuwa kiongozi wa interns mwananyamala hosp ambayo ktk kipindi cha mgomo haikisikika sana kuunga mkono mgomo wa madaktari.
More profile to come!
 
Poleni sana Madaktari wetu wameomba msamaha na JK serikali yake ni wasikivu watasamehewa...hawakujua masikini Chadema wakawaingiza mkenge wakiwadanganya kuwa kama wakifukuzwa wataenda Marekani kuna kazi.
 
Badala ya kupigia kura hifadhi ya serengeti kuingua katika maajabu ya dunia MIMI NAPIGA KURA HII SCENARIO YA MADAKTARI KULA MATAPISHI, NDIO IINGIE MAAJABU YA DUNIA!
 
Inanikumbusha siasa za udsm kutoa matamko afu kesho yake umoja wa vyuo vikuu TAHLISO unakuja na tamko lake kubatilisha maazimio ya udsm.

Hii style is just the same! Serikali inaunda kikundi cha kipuuzi kinaenda kuomba msamaha kwa rais! upuuzi mtupu. Nikiwakumbuka hawa TAHLISO napata hasira sana.
 
CCM oyeeee!!! tumewashinda Chademaaaaaa!!!!!!......kwa wanaCCM wenye upeo mdogo watadhani wameshinda, wanajidanganya tatizo bado lipo pale pale wawarudishe wasiwarudishe,

hizo ni propaganda za muda tu.wanaodhani wameshinda hakika ndo watakuwa wahanga wa kwanza wa huduma duni katika Hosipitali zetu.... amini nawaambieni acheni ushabiki katika swala hili.

CCM na serikali yake wanadhani wandhaani propganda za kijinga za vyombo vya habari zitasaidia bila kutimiza wajibu. huko ni kujilisha upepo

hata hiyo coverage ya vyombo vya habari haizidi 5% ya watanzania wote ambao wanataabika.

kwa wanaoitakia mema nchi yetu hili sio jambo la kushabikia kisiasa linamuumiza kila mtanzania.

hata wewe unayejifanya huyaoni matatizo ya vijana wetu na huduma duni za hospitali zetu ipo siku yakikufika na ukapelekwa hosipital au ndugu, yako utakubaliana na mimi
 
Miongoni mwa madai yao ilikuwa nipamoja na vitendea kazi,kwa tamko ili inanifanya niamini yakwa madai yao yametekelezwa na vitendea kazi wamepewa.
 
"WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.."
sitaki kuamini ndio upeo wa kufikiri umeshia hapa ..
hivi tunakwenda shule kufanya nini..?
 
si mmesaini wote 160 na kuomba radhi, endeleeni kuangukia magamba mtawaliwe milele au wote 160 ni makada?
 
Nakubaliana na wewe kabisa kwa uzalendo huo huo basi hakuna haja ya kuanzisha migomo na usipopata mshahara piga kazi tuu ukisubiri kuliko kuitisha mgomo ambao unatueleza objective zako za mgomo then unarudi kupiga magoti kuomba ulikosea means ulikurupuka kugoma na hii inatoana na akili ndogo ambayo ndio hiyo inaua wagonjwa!Daktari mwenye akili sawa na weledi alipaswa asome objective za mgomo ajiridhishe ndio agome sio kugoma leo kesho umerudi kupiga magoti kwa mwajiri!

Uzuri wa nchi yetu ni kuwa watawala CCM wana upeo mkubwa kuliko watawaliwa. Kuna gap kubwa sana ya uelewa kati ya watawala na watawaliwa, iliyopelekea kuwepo Gap ya Kipato then elimu kutofautiana kati ya haya matabaka mawili ipelkeayo fikra kuwa tofauti then kuendelea kutawaliwa mpaka vitukuu. Mligoma ili huduma kwa maskini iwe bora akinamaama wajawazito wannee waachekulala kitanda kimoja, gloves ziwepo, wazee watibiwe bure, watoto watibiwe bure, dawa usiambiwe kanunue pharamarcy safari za india zipungue, heshima yenu irudi mtaani nk. Iwapo mnaona mlifanya kosa basi tuhakikishieni kuwa huduma za mwananyamala zitakuwa sawa na Regency, Agakhani, Hindu Mandal,mtaacha kufungua viosiki mtaani. Sisi ambao hata 1% ya popn ya watanzania tupo kwenye keyboard wengi wetu tuna uwezo wa kulipia au makampuni yetu yanatugharamia. Tuhakikishieni kuwa, huduma itakuwa poa no visingizio, maana dawa nk, laaa mligoma kwa maslahi yenu tu. Ila mjue iwapo mmegeuka na kusema mlikosa hamatasamehewa kamwe katika maisha yenu kwa ujinga mliofanya. For that reason hamjui mfanyalo mfutwe tu kazi moja kwa moja, hamna maana nyie.Isitoshe mwaendeleza rushwa kwa kuwa huduma itaendelea kuwa bora kwa wenye pesa ambao watajaza ndugu zao kutoka vijijini nyumbani mwao walipiwe hospitali nzuri na mwisho ni kuendeleza rushwamaofisi mwao waweze lipia ndugu zao na nchi kuwa ya kishenzi kila sehemu rushwa tu.
 
Back
Top Bottom