Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Hii ni political diversion,naona sasa serikali imeweza kutuhamisha kwenye mjadala wa Mwangosi.
 
Ukombozi wa nchi hii uko mbali sana wasomi wenye uelewa hawana msimamo sijuwi tufanyaje
 
uzuri wa medical field ni mmoja tu.
Kosa la kusaliti medical fratenity ni baya kuliko yote.serikali ikiwasemehe hawa vilaza specialists ambao ndio waalimu wao professionally hawatawasamehe na matokeo yake hawatamaliza internship and ultimately they will never qualify to practise medicine in Tz.kamwe kikwete hana uwezo wa kusema hawa ni madaktari kamili,so they have to choose kama watapiga magoti kwa serikali au walimu wa madaktari.this is a big battle!

No comment!
 
Mimi nawashauri waende huko Rwanda, Botswana na SA.

Si nilisikia walikuwa wengi sana kwenye ubalozi wanaomba VISA kuna shuhuda alisema aliwaona.

teh teh teh
 
Tatizo la kufuata MOB.

Haya mambo ya migomo hata huko vyuoni watoto wa wavuja jasho huwa wanakuwa victim.

Wewe wenzako kula kulala wapo hapa hapa DSM wanakuhamasisha ugome upate milioni 3.5 halafu unafukuzwa unarudi kwenu Kipatimu kuokota korosho wao wapo mjini tu wanakula bata!
 
Ni jambo la kusikitisha sana kusikia Madaktari wetu wanakuwa Vigeugeu wakijua maisha ya Watanzania yanawategemea wao.

swala la madaktari kugoma sio kwamba lilikuwa linawafurahisha wananchi wanaoishi katika nchi hii bali ni kutokana na muda mrefu wananchi tukifika katika Hospitali zetu tunakuta karaha nyingi sana kama kukosa dawa, tunaanza kuilaumu Serikali yetu kumbe matatizo mengine yalikuwa yanatengenezwa na yanaletwa na hao ndugu zetu.

Madaktari waliposema hawana vifaa katika shughuli zao za utendaji wa kila siku, dawa hakuna Hospitali na baadhi ya vifaa, mimi na wtz wenzangu nilidhani ni kweli kumbe sasa yaonyesha ni mipango inayopangwa na wasomi hao,Kitendo cha kupanga Mgomo halali ambao Serikali kwa muda mrefu haikusikiliza kilio chao.

Watanzania ilitufanya tuamini yasemwayo ni ya kweli maana mgonjwa akienda hospitali huduma muhimu zilikosekana hadi kufikia Madaktari kugoma na kumfanya mwenzao mmoja kutekwa kupigwa karibia kufa, yote wtz tuliyapokea kwa vile walikuwa wanadai kitu kinachowagusa ndugu zao.

Lakini usaliti wa kwanza umeonyeshwa na Ndugu yetu Stephen Ulimboka ambaye kila Mtazania alimlilia kwa kipigo alichokipata na watu ambao hadi leo hawajajulikana kwa vile hata yeye mwenye kufahamu siri ya kupigwa kwake ameamua kukaa KIMYA eti amemwachia Mwenyezi Mungu, najiuliza bila majibu Ulimboka wakati anatekwa huyu Mungu hakumuona ya kwamba alikuwa anawakilisha kilio cha Madaktari pamoja na Watanzania wengine masikini?

Naye akaamua kutusaliti kwa hiyo watanzania tutambue Mgomo wa Ma Dr, umeisha kiaina katika mafungu (3) kundi moja bado wanaendelea na msimamo wao wa kuishinikiza serikali yetu kuboresha huduma za Hospitali kitu ambacho hata mimi mtz wa kawaida bado nasisitiza na naliunga mkono kundi hili kwani hadi leo huduma nzuri hospitali hakuna.

2.wengine wameamua kuomba msamaha kana kwamba walipoanza mgomo hawakujua wanachokifanya ,

3. wengine wameshitakiwa na serikali kwa kufanya mgomo wakati serikali hiyo ikijua inawakosea Watanzania kwa mamilioni baadhi ya Wtz walipoteza maisha kutokana na mgomo huo.

Ombi langu naanzia kwa Dr,S.Ulimboka na wale walioamua kwenda kumuomba msamaha Rais kutokana na kushiriki mgomo ambao hao sasa sijui mgomo huo wanaupa jina gani naomba wajihukumu wenyewe kama wanavyo ficha sura zao wakati wakiyatamka haya mbele ya watanzania.

Walikuwa huru kutwambia ukweli wakati huo wagonjwa waliteseka wengine walipoteza maisha kumbe hapakuwa na sababu za msingi.

Kwa maoni yangu Kikosi hiki nashauri kiwe cha kwanza kuburuzwa Mahakamani kusababisha usumbufu na vifo kwa Wahanga wa MGOMO wao.
 
Kwa hiyo vile vifaa kaMA GLOVES,madawa vitanda walivyogomea vimeboreshwa?
 
Wewe kiongozi wa CHADEMA unavyosema hivyo unaleta maswali mengi kuhusu uhusiano wa chama chako na mgomo usio na tija wa madaktari...

Sijaona pahala ktk tamko hilo la madaktari walipokitaja au kukigusia CHADEMA..Iweje wewe uanze kukitaja chama hata pasipohusika?Wasiwasi wangu ni kuwa,ipo siku mkeo atashindwa kupata ujauzito na utakit upia lawama CHADEMA..
 
Sioni source ya hii information lakinin kama ni kweli wameomba radhi, wamefanya vyema ila waelewe kuwa machozi yao na haki zao hazitakuja kwa atitude hii ya njaa. Kama walijua wana haki wakati ule, haki ile imekwenda wapi sasa. Je maslahi yameboreshwa, mazingira ya kazi (vikiwemo vitendea kazi kama Citiscan machine); yaani yali waliokuwa wakilalamikia wamepatiwa? kama jibu ni hapana na sasa wao ndo wakuomba radhi wamekwisha. Kama jibu ni ndiyo basi tuko pamoja nao! wasisingizie MAT!
 
Siamini kama madaktari hawa waligoma kwa influence ya MAT tu.,wao hawakuona upungufu ktk field yao?sababu za migomo hazikuwekwa wazi?Hazikuwa za msingi??Na kama zilikua za msingi,zimefanyiwa kazi kwa kiasi gani?La ikiwa hazkuwa za msingi,wao waligoma kwa misingi gani?
 
Zengwe la Magamba, wameona wakiwarudisha hao Jamaa watakuwa wame dhalilishwa, so wameamua kupika hiyo issue.
 
Tatizo la kufuata MOB.

Haya mambo ya migomo hata huko vyuoni watoto wa wavuja jasho huwa wanakuwa victim.

Wewe wenzako kula kulala wapo hapa hapa DSM wanakuhamasisha ugome upate milioni 3.5 halafu unafukuzwa unarudi kwenu Kipatimu kuokota korosho wao wapo mjini tu wanakula bata!

Mkuu issue sio kufata tu mob,hawa interns hawakujipanga kwenye madai yao,waliongozwa na jazba,utoto,na siasa zaidi badala ya uhalisia. Waliamua kudhalilisha taaluma yao na kukubali kufuata siasa majitaka,za wapinzani na wanaojiita wanaharakati. Mgomo wao haukuwa na mashiko wala tija,wali-behave kama wanafunzi wa form-two. Walionyesha unyama wa hali ya juu kwa ndugu zetu mahospitalini.

Msamaha wanaoomba ni unafiki. Watarudisha roho za Watanzania waliopoteza maisha kwa ajili ya mgomo wao? Mawaziri waliwasihi wasigome,wakakataa,Waziri mkuu akawaomba wasigome wakakataa,Rais akawaomba wasigome wakakataa! Na hata mawaziri waliachishwa nyadhifa nyadhifa zao,bado wakakataa. Madaktari wa jeshi walijitolea kwenda kusaidia pale walipogoma,lakini bado waliwafanyia vurugu na hata kuwatishia maisha. Lakini pia hata wale Madaktari wenzao waliowasihi wasigome,waliwafukuza uanachama wa MAT.

Sasa wajiulize kama wapinzani,au wanaharakati kina Bisimba,Ananilea Nkya au shujaa Ulimboka wanaweza kuwapa leseni za udaktari za kufanya kazi. Kwa mtazamo wangu,hawa madaktari wasisamehewe ili wapate fundisho,na iwe mfano kwa wengine.
 
Hapa kuna kesi ya msingi kabisa. Hawa madaktari wanafikiri ignorance of the law is an excuse to break the law.....La hasha sio hivyo. Umegoma na mgomo ulisababisha vifo una kesi ya msingi9 kabisa ya kujibu.

On a very serious note naomba contacts za mwanasheria atakayesoma taarifa hii niandikie kaziyangu@gmail.com nataka unipe quote za kufungua kesi kuwashtaki madaktari wote 200 waliokiri na kuomba msamaha kwa kosa la mauaji. Nataka kuwaburuza wote kotini ili nijue kama Watanzania tunatibiwa na watu mbumbumbu namna hiyo basi acha waende sero wakajifunze.

I am damn serious. Wanasheria kazi hii hapa.

Mkuu Mchapakazi, i salute to this post.
 
Mimi nawashauri waende huko Rwanda, Botswana na SA.

Si nilisikia walikuwa wengi sana kwenye ubalozi wanaomba VISA kuna shuhuda alisema aliwaona.

teh teh teh

Walioungana kuomba msamaha ni 200 out of 364,ukishirikisha akili lazima ujiulize hawa wengine 164 vp??
 
Nijuavyo mimi, mgomo haukuwa na SHURUTI, ila HIARI..then if so, iweje leo wajitokeze na kusema "walidanganywa", hoping that we are great thinkers, does it ring a bell anyhow with their reason?..i dont think so...na hapa ndio walipokosea, kuchanganya kati ya SUBIRA na UKIMYA!!




Nadhani;

WIVU na KUTOJIAMINI:
Mkuu, takribani madaktari 400ambao watahitimu mwaka huu wamepangwa katika hospitali tayari, "wakichukua" nafasi yao, sasa nashindwa kuelewa kwanini baada ya kuona jambo hili likitokea ndio wakumbuke "msamaha" unapaswa kutoka...nisingependa kutoa maneno ya kashfa kwa madaktari wenzangu kwa kiwa ni wanafamilia(kitaaluma), lakini nina uhakika msamaha si wa DHATI ila kurudishwa.


SUBIRA:
Kwa daktari wa kitanzania akaaye masaa 30 macho kabla ya kukabidhi shift nyingine akiwa sehemu mbali mbali (wodini,chumba cha upasuaji,kliniki nk) ambaye amekwishazoea "kutingwa" na utitiri wa kazi, kusubiri bila kufanya kazi, ni MATESO, na hasa inapokuja suala la kimahakama...tofauti na hospitali, mahakama hutaja kesi kwa mpango wake, na huitaji SUBIRA ya hali ya juu kupata kusikilizwa kwa kesi yako..hii imetafsiriwa kuwa ni UKIMYA wa MAT hata mara baada ya MAT kutamka "tusubiri jambo hili lipo kisheria" katika mtandao wao kutokana na wengi(madaktari WALIOFUKUZWA kuwa nje ya jiji na hivyo kuwa ngumu katika kuitisha mkutano physically)


KIBURI:
Ilikuwa ni shida kwao(madaktari "WALIOATHIRIWA" na mgomo kuendelea kusubiri mtaani baada ya kushindwa kwenda nje au kuwa katika ajira binafsi but above all nielewavyo mimi...madaktari wa kitanzania "tuna viburi" at times..na ninasema hivi kwasababu ANTICIPATION before war/battle or any crisis for that matter it's not questionable, lakini kwa baadhi ya madaktari wakitambua kuwa mgomo unaweza kuwatoa kazini.

Kuna msemo unasema "usichague nguo ya kujisitiri ikiwa uko uchi" ..kama mtu aliondoshwa kazini, nijuavyo mimi katika kujisitiri angekuwa na vijikazi vidogo vidogo vimtunze kwa muda hadi pale maamuzi ya mahakama yatapotoka...lakini jambo hili lilikuwa next to impossible kwa baadhi ya madaktari..wakijifariji kwa maneno, "utaua fani", lakini ninachoshindwa kuelewa je fani hiyo ilikuwa "haifi" wakati ukiwa idle??!...but this was used as scapegoat, the truth being Kujishusha ili kufanya kazi hata kama ina kipato kidogo kuliko ulichokuwa unapata ni shida!! wengi walitaka kipato sawa au zaidi..na hicho ndio ninachoita KIBURI.

-lakini mtu anaweza kutafsiri ninawahukumu/kulaumu bure na kuwa sasa ndio "wamejishusha"..ofcourse they have, but is it genuine?..
ingekuwa ni jambo rahisi kuomba msamaha kama suala halipo mahakamani, na takribani wiki mbili zilizopita Mh. Hussein Mwinyi(Waziri wa Afya) alipokuwa pale MNH na MOI alisema "serikali haijawafukuza intern doctors, bali MCT itawaita mmoja mmoja kuwahoji".. sasa swali ni kwamba msamaha huu utabatilisha maamuzi ya Serikali? vipi mahakama na MCT?
 
I used to know that they are SMART persons in the world? So disapointed by u guys, nimebakiza Wakaguzi wa mahesabu tu katika list yangu.
 
Hii ni hatari Dr. anapokuwa msanii na hili linasababishwa na serikali yenyewe. Serikali inafanya isichokijua, hapa madaktari wanachofanya ni kusoma kwa hela ya serikali wakimaliza wanaondoka wanaenda nje, J.K n' Co wanalilia kuombwa msamaha, haya tumekosa. Bwanyenye jinga linafurahia kumbe watu wanapata elimu wanasepa
 
Back
Top Bottom