Mene mene tekeli na peresi - Lema

Mene mene tekeli na peresi - Lema

not necessarily, Waisrael ni taifa la Mungu, na walikaa utumwani Misri kwa miaka 400!.
Paskali
So what brother. Tunaongea habari za Nebkadneza hapa ; pharaoh na Kaisari zilikuwa just tittle kama ilivyo Rais na gavana na kati ya wenye hizo tittle kuna waliofanya uovu na Mungu akawashughulikia
 
Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.
Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa hari, Na viwe fungu la kikombe chao.
Hapa hawakupati tena kwa uchochezi kwani una nukuu maandiko Mh. ambayo ni kama unabii kwa nchi yetu
 
Hapa hawakupati tena kwa uchochezi kwani una nukuu maandiko Mh. ambayo ni kama unabii kwa nchi yetu

Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda; Midomo yetu ni yetu wenyewe, Ni nani aliye bwana juu yetu?
Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema Bwana, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
 
Matamshi ya namna hii yanetengeneza chuki kubwa sana ndo maana mpaka sasa kuna watu wanaona kama kafa panya tu..hawashtuki...Jamani msitegemee kupanda chuki mkavuna upendo.
 
Matamshi ya namna hii yanetengeneza chuki kubwa sana ndo maana mpaka sasa kuna watu wanaona kama kafa panya tu..hawashtuki...Jamani msitegemee kupanda chuki mkavuna upendo.View attachment 1728722
Duh kwa kweli haya masuala ndio yalimchafua sana Hayati JPM. Kama angechapa kazi huku anajenga harmony kma anavyofanya Mwinyi Jr nadhani angekua Rais bora wa awamu zote (bar Nyerere).

Mungu amlaze mahali panapostahili I hope kamanda Mawazo na Ben Saa8 wanampokea huko.
 
sote tunapita njia moja. hatupaswi kufurahia kifo cha binadamu mwenzetu maana Mungu anaweza kumchukua yeyote yule amtakaye. Lema acha kuhalalisha chuki zako kwa kulinganisha maandiko
 
Back
Top Bottom