Salamu Watanzani naomba tusome andiko hili kutoka katika Biblia . Daniel 5 : 19-21 na mstari wa 25 hadi 28.
Na kwa sababu ya ule ukuu aliompa , watu wa kabila zote , na mataifa , na lugha , wakatetemeka na kuogopa mbele yake ; aliyetaka kumwua alimwua ; na aliyetaka kumwacha hai , alimwacha hai ; aliyetaka kumtukuza , alimtukuza ; na aliyetaka kumshusha , alimshusha . Lakini moyo wake ulipoinuliwa , na roho yake ilipokuwa ngumu akatenda kwa kiburi , aliuzuliwa katika kiti chake cha enzi , nao wakamwondolea utukufu wake . Akafukuzwa mbali na wanadamu moyo wake ukafanywa kuwa kama moyo wa mnyama , na makao yake yalikuwa pamoja na punda - mwitu ; akalishwa majani kama ng'ombe , mwili wake ukalowa maji kwa umande wa mbinguni ; hata alipojua ya kuwa Mungu aliye juu ndiye anayewatawala katika ufalme wa wanadamu , na yakuwa umweka juu yake yeye amtakaye , awaye yote.
Na maandiko yaliyoandikwa ni haya ; MENE , MENE , TEKELI NA PERESI . Na tafsiri ya maneno haya ni hii ; MENE , Mungu ameuhesabu Ufalme wako na kuokomesha . TEKELI , umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka . PERESI , ufalme wako umegawanyika , na wamepewa Wamedi na Waajemi .