Mdahalo: Kids Vs Spouses

Mdahalo: Kids Vs Spouses

Ohhh alafu Kloro leo nilikua naangalia DR PHIL kulikua na wadada wawili (watu wazima na watoto kabisa) ila walikua wanamlaumua mama yao kwa yaliyowatokea wakiwa wadogo kwasababu alimpa mwanaume wake kipaumbele badala yao. Huyo mwanaume aliwaMOLEST hao mabinti na walipomwambia mama yao hakujali/hakuwaamini wala hakuhangaika kutafuta ukweli. Mambo mengi tu walikua wanamuuliza iweje ukatuweka sisi watoto wako nyuma na kumjali mwanaume wako bila kujali aliyokua anatufanyia???
Leo hii mama hayupo na mwanaume tena....alibaki analia na kusema sikujua angeweza kufanya hivyo...sikuwahi hata kufikiria.Kabaki na majuto.

Ndo nimekumbuka hii sasa hivi na imenifanya nishawishike zaidi na zaidi zaidi kwamba ni muhimu mzazi akawapa watoto kipaumbele!!!Haijalishi ni baba au mama..

...ubarikiwe sana kwa hili...kwa mie nilojaaliwa kusikia sana vilio vya watu,
nimeshalisikia mara nyingi sana hili, na naijua athari zake kwa huyo mtoto ambaye ndiye
naye anakuwa mzazi wa kesho..-lower self esteem pia inanzia hapa...!-

Well well

Nakiri kwa mara ya kwanza nimelazimika kuukimbia uzi wangu mwenyewe.

Ni ukweli uumao lakini lazima tukubaliane nao. Huu uzi kwa mara ya kwanza ukanipeleka mpaka kwa my dear wife kumuuliza. Nilichojibiwa, khaa!

Sasa nakubaliana na my dear wife, MwanajamiiOne, Lizzy, klorokwini, The Boss,Mbu, MTM, Nyani Ngabu na wengine wote kuwa upendo kwa spouses hauwezi kulinganishwa na upendo kwa watoto. Ni vitu viwili tofauti kabisa

Pia naungana moja kwa moja na Dark City mzee mwenzangu, AshaDii shem langu la ukweli na Nyumba Kubwa kwamba kwa kina mama, akishajifungua basi huwezi toa mapenzi yake kwa kiumbe kilichokaa tumboni mwake kwa miezi takriban tisa. Japo kuna rare cases za kinamama wanaowachukia watoto wao utadhani hawajawazaa wao. Tunayashuhudia mengi.

Nawashukuru wooooooote mliouchangia huu msredi.

Nilichojifunza ni kuwa: Mapenzi ya mama kwa mtoto hayalinganishwi na kitu chochote. Wanaume ili tupendwe zaidi na wake zetu yatupasa kwanza tuwapende watoto wao/wetu.

Kumbe ni rahisi sana kwa wazazi: Pendeni watoto wenu ili mpate sababu ya kuendelea kupendana zaidi na zaidi!!

Baada ya kusema hayo naomba kuwashukuru kwa michango yenu. Nimegradueti!

dahhh, ulikuwa wapi siku zote?
umeamua na kuhitimisha kabisa thread asubuhi asubuhi?

mkuu, ubarikiwe sana kwa topik hii....
 
Mama Bishanga analalamika anasema mapenzi yako yote umeyaelekeza kwenye hii thread, usisahau kuja na AshaDii na wengineo kwenye hafla yangu ya kutunikiwa Phd ya heshima

na yeye yuko kwenye thread ileeeeeeeee kizungumkuti ya RussianRoulette,sijui anahisi nina nyumba ndogo,maana haishi kusoma na kisha kunitupia jicho.
 
Bishanga..,

Upo uchafu mwingi ambao wanaume pia tunfanya na wake zetu wanabaki na amani kwa vile hawajui...Sioni sababu ya kuwekeza kila senti kuyafuatilia hayo.....Ni kujitafutia ugonjwa wa moyo!



Hilo halina tatizo kabisa..Unaweza kutoa kitu kwenye mkoba bila kuufungua??? Na ili kuufungua kuna mbinu nyingi. Hiyo hapo ni mojawapo. Hata hivyo haina maana kwamba huo mkoba unaupenda sana...may be ni tamaa ya kupata kilicho kwenye huo mkoba basi.....!!!



Kweli ila tatizo langu linakuja pale ambapo kuna ulazima wa kuweka rank...na katika maishi hili haliepukiki...Mama anakuuliza kwamba hivi leo unaniona mimi sifai mbele ya mkeo??? Lazima umpe jibu ambao halina utata.
Kwangu mimi, mama yangu anajua kuwa mke wangu ni NAMBA MOJA! Hata akinitoa usingizini nitamwabia hivyo hivyo bila kumung'unya maneno!!

Mkuu DC,hapo kwenye red,may be...just maybe.....in good times yes.....likitokea anguko litokanalo na kishawishi you will definately run to your mom,au?
 
Bishanga naamini bado mke wako ana nafasi katika maisha yako until proven otherwise. Hapo sasa unaweza kusema hapa hapana acha watoto wachukue usukani. Ila naamini mke bado ana nafasi ya kwanza katika maisha yako mbele ya ulimwengu.
 
na yeye yuko kwenye thread ileeeeeeeee kizungumkuti ya RussianRoulette,sijui anahisi nina nyumba ndogo,maana haishi kusoma na kisha kunitupia jicho.
Aisee Bishanga, hebu saidia kuiambia hiyo c.r.a.p Finest kuwa hii sredi ni ya wakubwa. Watoto wanatakiwa kule Chit Chat.

Baada ya kusema hayo, ngoja nielekee UDSM nimeahidiwa kadigrii ka udaktari ka heshima kwa ajili ya mchango wangu wa kilimo cha matikiti maji na matango kule Mabwe Pande.
 
MJ1, kuna swali moja ambalo naona umejitahidi sana kulikwepa ila halikwepeki..Naamini ndilo ambalo mimi na Babu yako Asprin tumejaribu kulielezea kwa kirefu toka mwanzo wa hii mada.

Hebu assume, uko kwenye boat na sasa ajali imetokea. Una life jackets 2 tu.. Na pia to make the matter worse, unatakiwa moja uvae wewe (no choice) na ile ya pili uamue utampa nani...Kuna mume na mtoto...

Utampa nani???

Mbona rahisi sana....Just give me your answer...Mine is clear...my life jacket will go to my soulmate, PERIOD!

kwenye red hapo,mimi naona ni bora life jackets wewe umpe mkeo na mwanao, afterall kila siku si tunaimbiwa humu mmu kuwa love ni pamoja na sacrifice? that will be the ultimate sacrifice,kutoa maisha yako kwa hao uwapendao.
 
'hutokaa urudi moyoni mwangu',hilo ni apizo MJ1,usiapize,nshawahi kumpa mimba mwanamke,tukagombana,tukaachana,akaapiza kama wewe,akazaa, akaapiza tena kama wewe ulivyoapiza,leo ni best wangu,tunalea, pamoja na kwamba hatuna ndoa.La kwake ni la kwangu iwe la kheri au la furaha

Umenichoma au we ndio baba nanilihu nini hatujuani tu humu kwa sababu ya hizi ID
 
Dah! Lizzy hapo red umekwenda deep sana aisee! na trust me umeongea kitu platinum kabisa. Na sasa nimeanza kuwaangalia wale wanaopenda wenza wao kwa jicho jipya.
Yaani hii post yako hii dah! acha nikuvulie kofia tu.
Will u marry me?

Lizzy kaniambia nikwambie yes! hongera kaka!
 
Bishanga naamini bado mke wako ana nafasi katika maisha yako until proven otherwise. Hapo sasa unaweza kusema hapa hapana acha watoto wachukue usukani. Ila naamini mke bado ana nafasi ya kwanza katika maisha yako mbele ya ulimwengu.

i keep on saying ..may be ...just may be.....
 
i keep on saying ..may be ...just may be.....
Why may be ......may be...... Huna uhakika mkuu. Jiamini na say it before the whole world kuwa she is the one you love till death do you apart.
 
Aisee Bishanga, hebu saidia kuiambia hiyo c.r.a.p Finest kuwa hii sredi ni ya wakubwa. Watoto wanatakiwa kule Chit Chat.

Baada ya kusema hayo, ngoja nielekee UDSM nimeahidiwa kadigrii ka udaktari ka heshima kwa ajili ya mchango wangu wa kilimo cha matikiti maji na matango kule Mabwe Pande.

usimwonee TF bana,kijeba huyo sema tu kachelewa kupata my wife wake,sijui tumpe Darlingtone,au unaonaje? (though roho itaniuma sana)
 
usimwonee TF bana,kijeba huyo sema tu kachelewa kupata my wife wake,sijui tumpe Darlingtone,au unaonaje? (though roho itaniuma sana)

Mkuu kuhusu TF umepatia sana sana maana jamaa ni kijeba mbaya kachelewa tuu kuingia kwenye hii institution ya marriage
 
Umenichoma au we ndio baba nanilihu nini hatujuani tu humu kwa sababu ya hizi ID

Maty bana,siku moja wana mmu wote tutoe azimio la kujilipua,kila mtu abadili avatar yake iwe picha na jina lake halisi,hakika siku hiyo tutatafutana humu ndani,ukute mke asham PM mmewe kilavidavi na vice versa!
 
Why may be ......may be...... Huna uhakika mkuu. Jiamini na say it before the whole world kuwa she is the one you love till death do you apart.
ah wapi.tumekutana wote tuna meno 32!
 
Why may be ......may be...... Huna uhakika mkuu. Jiamini na say it before the whole world kuwa she is the one you love till death do you apart.

Mapenzi ya till deth hayapo nowdays!
 
Mkuu kuhusu TF umepatia sana sana maana jamaa ni kijeba mbaya kachelewa tuu kuingia kwenye hii institution ya marriage
ana sababu za msingi? eti TF una sababu za msingi za kutooa hadi leo hii?
-hujampata wa kukupenda?
_unasubiri umalizie mansion yako bahari beach?
_unamalizia Phd yako ng'ambo?
_huna hela ya harusi?
_rafiki uliyenaye hajakata shauri?
-unaogopa?
.......twambie bana.
 
..........kila mmoja ana nafasi yake linapokuja swala la kupenda, kabla ya kuolewa nilikuwa nasema siwezi penda mtu yoyote kama ninavyowapenda wazazi wangu. Lakini nikaja kumpenda mume wangu na nikaona na wazazi wangu bado nawapenda sana tu.

Baada ya kupata mimba nilikuwa nasema nitakuja kumpenda mtoto wangu kuliko mtu yoyote mwingine........... baada ya kupata mtoto nikagundua nampenda sana mwanangu lakini bado baba yake pia anapendwa sana tu. Hivyo kila mtu ana nafasi yake, ila sasa kwa namna moja au nyingine mtoto 1st kwa sababu...............!!!

Pretty your right! Mimi wazazi wangu walishafariki lakini bado ninawapenda hadi leo, mume nilikuwa nampenda sana bt alivyonitibua my kids ni number one
 
Maty bana,siku moja wana mmu wote tutoe azimio la kujilipua,kila mtu abadili avatar yake iwe picha na jina lake halisi,hakika siku hiyo tutatafutana humu ndani,ukute mke asham PM mmewe kilavidavi na vice versa!

Teh,teh,teh,teh,vipi ma aliem PM dada yake kimalavidavi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom