Mdahalo: Kids Vs Spouses

hilo nalo neno,mmeachana and stll in love? Acha kuchakachua thread ya Aspirin!
Mama Bishanga analalamika anasema mapenzi yako yote umeyaelekeza kwenye hii thread, usisahau kuja na AshaDii na wengineo kwenye hafla yangu ya kutunikiwa Phd ya heshima
 
Ni kweli lakini tabia pia inaweza kubadilika kutokana na kujifunza. Hata kupenda kwa maana ya mtu ku-treat wengine ni natural yes lakini kuna uwezekano wa ku learn ndo maana kuna washauri wa mambo ya mapenzi; ndoa etc.

Nina imani mwanamke anayechukua muda wake kusoma mambo ya mapenzi au malezi kwa nia ya kujua weakness alizonazo ana better chance ya ku bahave in a manner ambayo itakuwa acceptable na mwenza wake au watoto au jamii kuliko asotaka kujifunza na kuacha nature ichukue mkondo wake.

We always learn by reading or through life experience. Kuna watu wameteswa sana na mama wa kambo kiasi kwamba walishahapa kama nao watakuwa mama wa kambo they will behave in a way that will show society kuwa ni possible kuwa mama wa kambo na still kuwa mwema.

Mfano baba yangu alikuwa na shelf limejaa vitabu vya malezi; mama alikuwa anamponda anasema unalea watoto in a western way. Lakini nina imani alikuwa ana gain something ndio maana we always consider him as a good daddy; alikuwa na muda na sie; anatusikiliza hata tukiwa tunaongea nonsense; anatupa moyo; hachapi mtoto; kwa hiyo hatukuwa tunamuogopa hata kidogo; he was a friend.

Nilikuwa na kaka yangu mkorofi hajabu toka utotoni; lakini baba alikuwa anasema my son you are so bright ndo maana una tabia hiyo ulonayo; kweli bwana alishawahi mpaka kuzamia; but now ana degree na ametulia.

Kuna siku akiwa secondary alifanya kosa kubwa akaambiwa amuite mzazi; akaenda kukodi muuni mmoja na kusema ndiye mzazi wake. Baadae akagundulika; Baba alivyoitwa shule akaenda kumtetea akasema kweli nilikuwa safarini nje ya nchi.
 

Eti nini...??? Kwamba NN ndiey ADii???? Duuuu....basi mie nitakuwa nimeuvaa mkenge!!

Wasamehe bure brother...Siku tukivunja codes na kutoka kwenye magamba yetu ya haya majina ya JF wataujua ukweli....!!
 
Eti nini...??? Kwamba NN ndiey ADii???? Duuuu....basi mie nitakuwa nimeuvaa mkenge!!

Wasamehe bure brother...Siku tukivunja codes na kutoka kwenye magamba yetu ya haya majina ya JF wataujua ukweli....!!

Labda ukisema wewe babu watakusikiliza!! Angalau you know who NN is!
 

Uko sahihi kabisa dada yangu,

Hiyo obsession ya mama kwa mtoto wake wa kiume ndiyo mara nyingi imekuwa ikichangia ndoa kuyumba...Huwa namcheka sana wife. Hapendi kuingiliwa na mama yangu mzazi ila utamsikia akiapia kuwa hatakubali wakwe zake wawe wa hovyo kwa watoto wake!

Ni kawaida sana kwa wanawake. Ndiyo maana wale ambao ni real husbands tunajitahidi kumwacha mama kando ili tujenge ndoa zetu. Ukimwendekeza mama mzazi anaweza kuingia hata bedroom kwako kimzaha mzaha!
 
There is no comparison between the two. Kila mmoja ana nafasi yake and that what brings Happy Family ambayo inazaa Health Marriage.
 

Hii imetulia.. philosophy iko juu hapa!!


Umepima au na wewe umeamini kuwa kitanda hakizai haramu??

Mapenzi kwa mtoto/watoto ni tofauti kabisa na mapenzi kwa mke/mume/ au mwenza.

Nimelisema sana hili....Kwa mke lazima mwisho wa siku mambo yake ki mtindo wa piston za gari...you give and take...ila kwa watoto hakuna expectations zozote za kutoa au kupata badala yake ni tulizo la roho tu!



Tatizo ni kwamba, hakuna anayependa kuwe second best ila ni wachache wanakuwa tayari kuwapa nafasi ya kwanza wenzi wao!

Binafsi, my wife ni number moja hata mama yangu analijua hilo....Nitalisema kwa yeyote hata ikimaanisha kutopumua tena! Yeya kama hanipi nafasi ya kwanza ni juu yake mwenyewe!
 
Mama Bishanga analalamika anasema mapenzi yako yote umeyaelekeza kwenye hii thread, usisahau kuja na AshaDii na wengineo kwenye hafla yangu ya kutunikiwa Phd ya heshima

naanza kupata hisia thread hii just like ya RussianRoulette na The Boss kuhusu ..'nyumba ndogo'..nayo inaelekea kwenye page zaidi ya hamsini....wiki hii naona itatoa thread of the year.
 

thanks Mama

umeongea mengi lakini sijui kama umeaddress hoja ya msingi.... love haina practice, love in straight, what you are talking about ni nafasi katika mapenzi na related issues, mie nazungumia mapenzi regardless ya mafasi

mwanangu akituna mtu ntamkanya au hata kumchapa, will end there.... mke wangu akituka ntamkanya sintamchapa bati it will stick to my mind

TUNACHANGANYA MAMBO.............. LOVE LOVE OH LOVE

Lionel Richie - Love, Oh Love - YouTube

THIS IS THE GREATEST LOVE OF ALL............... HAYA MENGINE YA SIKU HIZI NI MUHIMU NA NI MATAMU, BUT SOMEHOW THEY ARE QUALIFIED
 

Bishanga..,

Upo uchafu mwingi ambao wanaume pia tunfanya na wake zetu wanabaki na amani kwa vile hawajui...Sioni sababu ya kuwekeza kila senti kuyafuatilia hayo.....Ni kujitafutia ugonjwa wa moyo!


Hilo halina tatizo kabisa..Unaweza kutoa kitu kwenye mkoba bila kuufungua??? Na ili kuufungua kuna mbinu nyingi. Hiyo hapo ni mojawapo. Hata hivyo haina maana kwamba huo mkoba unaupenda sana...may be ni tamaa ya kupata kilicho kwenye huo mkoba basi.....!!!


Kweli ila tatizo langu linakuja pale ambapo kuna ulazima wa kuweka rank...na katika maishi hili haliepukiki...Mama anakuuliza kwamba hivi leo unaniona mimi sifai mbele ya mkeo??? Lazima umpe jibu ambao halina utata.

Kwangu mimi, mama yangu anajua kuwa mke wangu ni NAMBA MOJA! Hata akinitoa usingizini nitamwabia hivyo hivyo bila kumung'unya maneno!!
 
naanza kupata hisia thread hii just like ya RussianRoulette na The Boss kuhusu ..'nyumba ndogo'..nayo inaelekea kwenye page zaidi ya hamsini....wiki hii naona itatoa thread of the year.
Umenikumbusha thread moja mwaka jana ilikuwa na views karibia 20,000 na page karibia 30
 
Dah huu mjadala naona unakwenda deep sana bana, mie mtu wa shallow so nakimbiza bawa. Ila tu
Nitawapenda wenetu (wake + wangu+ wetu) lakini naye nafasi yake itabaki yake. Nitawapenda watoto na Baba/Uncle wao nitampenda pia.

Ewe Mwenyezi MUNGU nisaidie.
 

Issue yako naweza kuielewa ila si kama mdau bali kama mtu wa pembeni....Just making an assumption kwamba imenitokea nikaachana na Mama DC, nahisi kizunguzungu!

Ndiyo maana najitahidi kuelezea hisia zangu katika perspective ya couple ambayo bado imesimama na wahusika wanaamini wanapendana kama alivyosema Asprin...Inakuwa ngumu sana kumeza ukija kusikia kwamba kwenye list ya watu ambao mkeo anawependa wewe uko kwenye rank ya chini sana ukitanguliwa na watoto uliowazaa na unawalea mwenyewe!
 
Love ni hisia (feelings) ambazo anayezijua uhalisia wake ni mtu mwenyewe anayependa; na mpendwaji atabaki kukisia. Love ni covert.

That is why ili mtu ajue unampenda ni lazima ufanye matendo (au umwambie kwa maneno) ambayo huyo mtu atatafsiri kuwa unampenda; otherwise bila kushow overt behavior hamna atakayejua hisia zako.

Tatizo ni kuwa watu wengi hawajuhi ni jinsi gani wa behave ili wenza wao wajue wanawapenda; sasa mimi kama mwamnamke nikisoma vitabu na kupitia mijadala naweza kujua wanaume wengi wanapenda kitu fulani; and naweza kujaribu kwa wangu ili nione kama na yeye anapenda. Hence we always learn how to communicate our love.

Unaweza kuta mdada ni full nyodo kwa mpenzi wake kichwani mwake anaona ana show love; baada ya muda si muda anapigwa chini. Kumbe masikini ya Mungu hajuhi jinsi ya ku show love.

 
Labda ukisema wewe babu watakusikiliza!! Angalau you know who NN is!

Pole sana ndugu yangu....Ila kwa vile unaijua JF zaidi ya wengi wetu basi utaelewa kwa nini watu wanakuwa na hang over wakati mwingine.

Ngoja nijaribu kufanya homework yangu halafu nitakuja na kiapo cha mwanasheria kuwatoa hawa watu wasi wasi!
 
..........kila mmoja ana nafasi yake linapokuja swala la kupenda, kabla ya kuolewa nilikuwa nasema siwezi penda mtu yoyote kama ninavyowapenda wazazi wangu. Lakini nikaja kumpenda mume wangu na nikaona na wazazi wangu bado nawapenda sana tu.

Baada ya kupata mimba nilikuwa nasema nitakuja kumpenda mtoto wangu kuliko mtu yoyote mwingine........... baada ya kupata mtoto nikagundua nampenda sana mwanangu lakini bado baba yake pia anapendwa sana tu. Hivyo kila mtu ana nafasi yake, ila sasa kwa namna moja au nyingine mtoto 1st kwa sababu...............!!!
 

Hiyo record (indelible) unatunza ya nini???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…