Kwa Tanzania hairuhusiwi lakini pia haipigwi vita. Wengi katika safu ya uongozi wamenunua vyeti au wamenunua ufaulu. Na hao ndio wengi walioishia kwenye uongozi wa nchi hii. Ndio sababu kila kitu ni hewa , roho mbaya na unafiki ndio vimetawala bongo land kwa miongo mingi.Kwahiyo kufoji vyeti inaruhusiwa?
Yupo viongozi wamemaliza daraja zote za elimu, kuanzia chekechea mpaka udokta na uprofesa tena wametumia kiingereza kusoma lakini nimesikia wamekisahau kiingereza au kiingereza kiliyeyuka baada ya kumaliza masomo na wengine kiingereza kimawasahau wao.
Waliosoma na wenye taaluma za kweli wanaonekana ni takataka tu au wenyewe kutokana mfumo wa kinafiki inawabidi waziweke mfukoni taaluma zao wajiingize kwenye unafiki ili wapate mgao kutoka shamba la bibi.
Mimi nina imani tukileta wachunguzi huru kutoka nje ya Tanzania kuja kuhakiki elimu au vyeti vya watanzania, tunaweza kulazimika kuwaomba wachungaji, mapadre, makasisi na masheikh watuombee dua kwa siku arobaini kwanza kabla ya hao wachunguzi kuanza kazi kwa sababu hatutaamini matokeo ya uchunguzi/uhakiki wao.