Hakuna kilichowekwa wazi.
Kilichopo ni maneno tu.
Hata huyo anayedaiwa kuwa ndo Paul Makonda mwenyewe sura yake haijulikani.
Hayo majina ya watu unaodai walisoma naye hayajathibitishwa na mwingine yeyote zaidi ya wapinzani wake ambao hawawezi kuaminika kivile.
Hata huyo Gwajima wenu licha ya kudai anavyo vyeti vya Makonda huko ofisini kwake bado hajatuonyesha kama kweli anavyo. Na anaweza kabisa kuwa anatudanganya tu.
Na yeye Makonda kutokukanusha chochote mpaka sasa hivi [kama unavodai] si ushahidi wa chochote wala lolote lile.
Bado kabisa sijaiona hiyo jinai unayodai kaitenda. Sisemi kuwa hajatenda jinai. La hasha. Nasema kuwa sijaona ushahidi wowote ule wa kunishawishi kuwa katenda jinai. Maneno yenu pekee si ushahidi wa kunishawishi mtu kama mimi.
Na hii mada yako wala haina jipya zaidi tu ya kujaribu kuipa uhai habari ambayo inaelekea kaburini.
Mwambieni Gwajima wenu atuonyeshe hivo vyeti alivyonavyo ofisini kwake maana Makonda mwenyewe hataki.