Nimekuwa nikifuatilia kwa kina madai mbalimbali ya Mchungaji Gwajima, akidai vyeti vya Rc Makonda kuwa ni feki nakuwa hata Elimu yake nayo ni feki. Yafuatayo hapa ni mashaka yangu juu ya madai hayo;
1.Gwajima anadai kuwa Rc Makonda mwaka 1996 aihitimu darasa La 7 nakufeli mtihani wa kuingia kidato cha kwanza, lakini mwaka 1997 akajiunga kidato cha I Shule ya Secondary Pamba, hapa napata mashaka, aliwezaje kujiunga kidato cha Kwanza bila kuwa na TSM9?, kwani haupo utaratibu wa mwanafunzi kujiunga kidato cha kwanza bila kuwa na TSM9, hapa moja kwa moja madai haya yana mashaka na kwa kifupi ni ya uongo.
2. Gwajima anaendelea kudai kuwa Makonda alipofika kidato cha IV pia aliferi nakupata division zero.
Gwajima hapa pia anadai kuwa anao ushahidi wa vyeti vya Gwajima ambavyo vinathibitisha kuwa Makonda alipata Zero.
Mashaka yangu hapa nikuwa, inawezekanaje mtu apate Division Zero halafu apewe cheti? Na wakati huo huo cheti hicho original awe nacho Gwajima badala ya Makonda? Au Bashite kama yeye anavyodai?
Gwajima pia anadai kuwa Rc Makonda alibadili jina na kutumia la mtoto wa Mzee Sitta baada ya kuwa yeye alifeli nakupata Zero. Sasa vyeti original vya mtoto wa Sitta navyo anavyo Gwajima?je kila moja wao yeye anachukua vyeti vyao tena original kwa sababu zipi?
> Gwajima atueleze yeye kwavile kimsingi yeye ndiye anayetuhumu, na mtu akikutuhumu yeye ndiye wajibu wake kuthibitisha tuhuma badala ya kusubili mtuhumiwa athibitishe. Shida siyo ya Makonda, shida ni ya Gwajima na wote wanaodhani hoja ya Gwajima inamashiko. Makonda yeye tayari anaamini amesoma na vyeti vyake ni sahihi, na tayari ni Mkuu wa Mkoa wa Dsm, na Rais kamuamini vya kutosha na amethibitisha wazi kuwa nafasi aliyopewa anaiweza ndiyo maana kaanzia ukuu wa Wilaya hadi ukuu wa Mkoa na huenda akaenda zaidi ya hapo. Sasa nani mwenye shida? Gwajima au Makonda?
Kimsingi hapa ndugu zangu, kilichopo hapa ni chuki binafsi, mtu anapost nakudai kuwa eti watu wengine wameondolewa kazini chini ya usimamizi wa Makonda wakati wa zoezi La watumishi wasiokuwa na sifa. Sasa tujiulize kama ndugu yako alithibitika kuwa hana cheti sahihi, na akaondolewa bila hata kudaiwa fedha aliyokuwa akilipwa huoni kuwa ni nafuu? Kama unahakika kuwa Makonda anavyeti feki, kwanini usitumie mamlaka sahihi kumshitaki? Kuna haja gani kumtaka yeye ndiye athibitishe? Narudia yeye ana shida gani hadi ahangaike kuthibitisha?
Watu wooote wanaohangaika na kumtaka Makonda athibitishe, wanapoteza mda, haitakaa itokee, ikumbukwe kuwa Makonda ni mtu mstaarabu, mwelewa,anajiheshimu, ni kiongozi wa Mkoa, anayeifahamu kazi yake, asiyetishwa, jasiri, mpambanaji, na kuwa Vita dhidi ya Mihadarati itaendelezwa kwa kiwango cha juu na pengine kuzidi hapa. Wanaojaribu kuipunguza kasi hii humu wakivunga kuunga mkono, watashindwa bila kutarajia. Mungu mbariki Makonda, Mbariki Waziri Mkuu, Ibariki Serikali, Ibariki Tanzania.