Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Si kila jipu ni la kutumbua hadharani kwa mbwembwe kaa kutaja majina ya wauza unga feki
Jipu hili BASHITE linahitaji kutumbuliwa Surgery room katika mazingira controlled.
Bila hivyo linaweza anzisha donda ndugu kiasi cha kuhatarisha hata uhai wa mtumbuaji.
Alitumbuliwa shwahiba wa misungwi sembuse huyu ambayo hamna uswahiba ni uhusiano wa kinyalugusu tu?
 
Ngoma ikivuma sana inakaribia kupasuka. Kama naiona tabia ya baba Mchungaji wa kanisa lile inasadifu ngoma inayovuma!
 
bashite anastahili kufunguliwa mashitaka na ameiaibisha sana serikali hiyo ya baba yake.

Shida ni mkuu wa nchi alimuamini mno mno mno Bashite! Kumbe waliofanya vetting walimdanganya labda purposely!
 
ngwajima huwa simuamini sijui kwanini . kabla ya yote aanze na stori ya Mbasha hapo nitamwelewa

Umesema hujui kwa nini?
Kwa sababu
Unasoma mno magazeti ya udaku.
Sijasema uache punguza.
Sasa unaletewa viztu halisi na mtu halisi kwa mazoea uliyonayo unasubiri kukonfemu kwenye magazeti ya udaku.
ha ha ha ha ha
 
Shida ni mkuu wa nchi alimuamini mno mno mno Bashite! Kumbe waliofanya vetting walimdanganya labda purposely!

Serikali yote imejaa MABASHITE.
Tatizo si ubashite tatizo ni kuanzisha mashambulio ya aibu kwa watu makini kama Askofu Gwajima.
Kama umefoji vyeti ili kupenya upate elimu ya juu fanya kazi huku ukijua iko siku la kuvunda kibindoni mwako halitasikiliza moshi wa ubani
 
Inaweza kuwa ni kweli lakini sioni mantiki kwa anayejiita mtumishi tena wa Mungu kuendeleza vita. Siku zote watumishi wa kweli humkabidhi Mungu vita vyao. Daudi akasema Mungu pigana na wanaopigana nami...zaburi 35:1b

ukome kabisa kusimama nyuma ya neno kujaribu kumsema mtumishi wa Mungu.
Unaongea kitu usichokijua kabisa.
Unaleta nukuu kwa kukariri.
Biblia ninayoisoma mimi haina upuuzi huo unaouongelea.
Askofu Gwajima anaeleza ukweli wa Biography ya mtu ambaye jina lake halisi ni Daudi Bashite.
Hapo vita iko wapi?
Daudi alisema pigana nao wanao pigana nami lakini unajua Daudi aliua watu wangapi kwa upanga wake mwenye katika maisha yake?
Hadi Mungu alimnyima nafasi ya kujenga Hekalu kwani mikono yake ilijaa damu.
Mbona hakusubiri Mungu aje awaue adui zake?
Lete mstari mwingine kwa mstari huo umekwama
 
It takes a village to rise a child. Kuna watu/wanakijiji wanamfahamu. Kama haya yote yaliyowekwa hapa ni uongo, Makonda anashindwa nini kumshitaki makonda?
 
Daudi atuoneshe cheti malumbano yaishe.
Daudi Bashite anapenda soo hii iishe si kwa kuweka mambo sawa.
Anataka soo hii iishe kwa kumnyamazisha Askofu Gwajima na ushahidi wake ili aendelee kudunda.
Angetajwa mbunge wa jimbo lolote la Dar Meya au Diwani kwamba ana vyeti vya kufoji Daudi angeagiza polisi wakamleta kaputula yake na chupi zikiwa zimwekwidwa kwa staili ya Tanganyika Jeki,
Sasa kwa vile ametajwa yeye mwenyewe Bashite hawezi kujipiga Tanganyika jeki badala yake amepeleka polisi nyumbani kwa Askofu Gwajima wakamsachi tena ikiwezekana waue ushahidi.
Akiamini kwamba kumtishia mtumishi wa Mungu kutamwondolea kosa lake la jinai la kutumia cheti cha mtu mwingine kupenyeza chuo kikuu.
Rais naye anamung'unya jiwe juu ya vita aliyoianzisha mwenyewe.
Sasa aliianzisha ili atubane sisi Malumpeni proletarieti na kuwaacha wao akina Lyanda wakipeta?
Ya Lugumi ilimshinda na hii ya Bashite nayo imeota mbingiri.
Nyani hakai kwenye jiwe la moto na makalio matupu.
 
Nilimsikia Mchungaji Gwajima kwenye video akisema ana vyeti vya mtu anayeitwa Daudi Bashite na Paul Christian Muyenge akimlenga Paul Makonda pamoja na kwamba alitumia umakini mkubwa katika maelezo yote kutolitaja jina la Paul Makonda ili asiingie kwenye mkono wa sheria.

Gwajima alifahamu kama angesema ana vyeti vya Paul Makonda basi angejikuta kwenye kosa la kuhodhi cheti/vyeti vya Paul Makonda bila idhini yake.

Haya ni maelezo mazuri sana kisiasa lakini kwa watu wanaofahamu sheria wataanza kujiuliza maswali mengi kwa sababu madai ya Gwajima yanamuingiza kwenye makosa ya jinai ambayo yameorodheshwa kwenye Kanuni ya adhabu Sura ya 16 katika sehemu ya 258-259 inayohusu wizi na pia sheria ya Usalama wa Taifa namba 3 ya mwaka 1970, Sheria ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa namba 3 ya mwaka 2002, Sheria ya Utumishi wa Umma namba 8 ya mwaka 2002 na Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma.

Sheria hazina siasa pamoja na kwamba siasa wakati mwingine hazina sheria lakini pia hoja zangu hazimtetei Paul Makonda kama kweli ametumia vyeti vya mtu mwingine kitaaluma.

Kuhodhi cheti cha mtu mwingine bila idhini yake ni kosa la jinai kama ilivyo kutumia cheti cha mtu mwingine kwa idhini yake.

Ifahamike kuwa, hata kama ukiokota cheti/vyeti vya mtu mwingine lazima utoe taarifa mapema kwenye vyombo vya serikali na kushindwa kufanya hivyo utakuwa unahesabiwa ni mwizi kama ilivyoainishwa katika kanuni ya adhabu Sura ya 16.

Ninaamini Gwajima hawezi kutoa vyeti vya Paul Makonda bila idhini yake pamoja na kwamba amesema atavitoa.

Nimesikia anasema ameleta watu waliokuwa watumishi wa umma watoe ushuhuda kuhusu ukweli wa Daudi Bashite na Paul Christian Muyenge lakini hao watu lazima waelewe wanaweza kujikuta katika mikono ya sheria kama hawatapata wanasheria wazuri wa kuwaeleza jinsi ya kuruka mitego ya kisheria.

Nimalizie kwa kusema, watoa ushuhuda wa Mchugaji Gwajima lazima waelewe kuwa wakoloni walipoondoka katika makoloni yao hawakufuta sheria walizozitunga na kikubwa zaidi, serikali zilizorithi utawala wa kikoloni ziliongeza zaidi sheria zinazoweza kuwaingiza matatani kama watawala wakiamua kuzisimamia kikamilifu.

Nimalizie kwa kuwatakia ushuhuda mwema !

My Friend, Chuki zako Binafsi na Gwajima usizilete hapa, Ni nyaraka gani za serikali alizonazo?
 
Sifuri kabisaa..yani hakuna alicho kua anakijua yeye. Saivi ndo kapewa manukumu yooote ya kusimia jiji....kudhiirisha elimu yake ushahidi nadhani mnayo
Hii ni moja ya sababu kubwa za MH huyu Bashite kutumia msuli zaidi badala ya akili.
Amekwisha haribu maisha ya wengi kwa unafiki mkubwa wa kujipendekeza kwa mkuu.
Kumtaja Askofu Gwajima kwamba ni muuza unga huku akijua wazi hauzi wala hatumii ilikuwa ni moja ya hatua zake muhimu za kulitia ganzi kanisa na watumishi wote wa Mungu na kuwafanya wamwabudu yeye tu.
Juhudi zake zimeshindwa,watu sasa wanajiuliza huyu kweli ni Mungu wa Dar es salaam?
Jiwe hili ni jiwe la kutweza naye amekwisha livaa shingoni litampeleka hadi kilindini.
 
Sheria hii nzuri sana, kwanini serikali haifuatilii kujua ukweli wa sakata hili la vyeti fake. Makonda kwa kutumia wanasheria wake (kama wewe mtoa mada) anashindwa nini kumshitaki Mchungaji Gwajima. Kuna ukweli unafichwa katika suala hili la jinai, No body is above the law. Serikali na vyombo vya sheria amkeni toka usingizini
Ninaamini serikali haiwezi kufuatilia suala kama hili kama hakuna official complain with solid evidence.

Hata kwenye nchi zinazotufundisha utawala wa sheria, huwezi kuona serikali zao zinaanza kufanya uchunguzi kwa sababu kuna baadhi ya watu wanasema maneno fulani. bila solid evidence.

Ninaamini kama wanaotoa madai watatoa solid evidence basi hata serikali itabidi iyafanyie kazi malalamiko yao.
 
Wewe umejuaje kama alikuwa akimaanisha ni makonda... Si alikuwa anamzungumzia MTU yule anaetumia cheti cha Paul Makonda
 
Ninaamini serikali haiwezi kufuatilia suala kama hili kama hakuna official complain with solid evidence.

Hata kwenye nchi zinazotufundisha utawala wa sheria, huwezi kuona serikali zao zinaanza kufanya uchunguzi kwa sababu kuna baadhi ya watu wanasema maneno fulani. bila solid evidence.

Ninaamini kama wanaotoa madai watatoa solid evidence basi hata serikali itabidi iyafanyie kazi malalamiko yao.
Mkuu hapo "official complain with solid evidence"
Ko kipind gwajima anaitwa central na kuhojiwa suala la madawa ya kulevya ilikuwepo hyo bac hata mh.makonda kama ni rumours bac aitwe na mamlaka husika ahojiwe
.
.
.
Kyenekyaka mkighanile une
 
Back
Top Bottom