Mchezo: 'Niongezee Sentensi' – Hadithi Hai ya Mtaa na Taifa

Mchezo: 'Niongezee Sentensi' – Hadithi Hai ya Mtaa na Taifa

HenrysoN

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2017
Posts
230
Reaction score
222
Habari wanaJF,

Leo tunakuja na mchezo mpya unaoitwa “Niongezee Sentensi” – huu ni mchezo wa fikra, ubunifu na mantiki, ambao wa mwisho kabisa tutamtumia mkono wa pongezi. Unaburudisha, unachokoza akili na pia unaweza kuibua hadithi ya ajabu au tafakari ya kina juu ya maisha yetu ya kila siku.

📌 Kanuni ni rahisi sana:

  • Mtu anaandika sentensi moja tu ya kuanzisha au kuendeleza hoja/hadithi.
  • Mchango wako unapaswa kuunganisha na aliyemaliza kabla yako.
  • Usihitimishe hadithi au hoja – acha nafasi kwa mwingine kuendeleza.
  • Unaruhusiwa kutumia ubunifu, ucheshi, falsafa au maisha ya kawaida.

🔰 Twende na mfano huu hapa kuanzia:

Nilipofika kijiji cha Kifaru, nilimkuta diwani wa zamani akila mihogo chini ya kivuli cha mninga.
Mtu anayefuata ataandika,
Aliniangalia kwa macho yaliyobeba historia ndefu, kisha akasema, “Hawa walinipigia kura, lakini wakasahau kuwa mimi pia ni binadamu.”
Mtu anayefuata ataandika,
Pembeni yake kulikuwa na kijana aliyebeba mabango ya uchaguzi yaliyopigwa jua hadi yamegeuka vumbi.
Mtu anayefuata ataandika,
Kwenye mbao ya matangazo bado limebandikwa tangazo la “Mkutano wa Mbunge: Tutashusha Bei ya Mbolea na Mafuta!”
Mtu anayefuata ataandika,
Wazee wanne walikuwa wanacheza drafti huku wakilalamikia jinsi ahadi za umeme zimekuwa kama ndoto za mchana.
Mtu anayefuata ataandika,
Mmoja wao akasema, “Miaka mitano imepita, transformer bado ipo kwenye kiwanja cha fundi aliyehamia Kenya.”
(Sasa mtu anayefuata anaendeleza kwa kuandika sentensi moja tu)

Kumbuka:
  • Mshindi ni wa mwisho, lakini kila mchango wako ni wa maana.
  • Hii ni nafasi ya kuandika bila kizuizi – andika kwa ubunifu, kwa tahadhari, au hata kwa mzaha.
🔥 Karibuni sana wanaJF! Tuoneshe uwezo wetu wa kufikiri nje ya boksi – uzi huu ni wa wote!
 
Tena alizua tabia mpya yakujifanya nunda mpiganaji!, alikuwa akipigana na kila rika, ngumi na mateke yake yalimpiga yoyote aliekuwa kikwazo mbele yake!..
Aliamini kuwa kila kipigo kilikuwa ishara ya nguvu, lakini hakujua kuwa alijichimbia kaburi la huzuni na machungu yake mwenyewe.
Vijana walimwita "Haduri wa matusi," na kila mapigano yaliongeza ukimya wa umoja wa kijiji kilichokuwa kimechoka na vurugu zake.
 
Aliamini kuwa kila kipigo kilikuwa ishara ya nguvu, lakini hakujua kuwa alijichimbia kaburi la huzuni na machungu yake mwenyewe.
Vijana walimwita "Haduri wa matusi," na kila mapigano yaliongeza ukimya wa umoja wa kijiji kilichokuwa kimechoka na vurugu zake.
Kila siku, wazazi wake hasa baba, walitafuta mbinu zote ili mtoto wao Haduri aache ulevi na ukorofi lakini ilishindikana, hivyo wakaamua wahamie upande wa pili...yaani kwa waganga wa kienyeji ili mtoto wao aweze kupona hiyo hali ya ulevi na matusi, wakiamini mtoto wao amerogwa na mtu mbaya pale kijijini...
 
Kila siku, wazazi wake hasa baba, walitafuta mbinu zote ili mtoto wao Haduri aache ulevi na ukorofi lakini ilishindikana, hivyo wakaamua wahamie upande wa pili...yaani kwa waganga wa kienyeji ili mtoto wao aweze kupona hiyo hali ya ulevi na matusi, wakiamini mtoto wao amerogwa na mtu mbaya pale kijijini...
licha ya kwenda kwa waganga lakini bado waligonga mwamba!, ulevi wa haduri ulikuwa ni sugu!.
kila dawa ilidunda mbele yake!, ulikuwa ni mti mkavu usiosikia dawa waweza sema ule usemi wa "sikio la kufa halisikii dawa" ulianzia kwake!.
si mvua si jua haduri chapombe nae alikuwa ni kama kiungo kwenye pombe yenyewe!, hata umpulizie manukato ya malaika lakini bado harufu yake ya pombe ilizidi manukato!..
 
licha ya kwenda kwa waganga lakini bado waligonga mwamba!, ulevi wa haduri ulikuwa ni sugu!.
kila dawa ilidunda mbele yake!, ulikuwa ni mti mkavu usiosikia dawa waweza sema ule usemi wa "sikio la kufa halisikii dawa" ulianzia kwake!.
si mvua si jua haduri chapombe nae alikuwa ni kama kiungo kwenye pombe yenyewe!, hata umpulizie manukato ya malaika lakini bado harufu yake ya pombe ilizidi manukato!..
Hakupenda kunywa pombe ila mawazo ya majukumu aliyonayo akiwa ni mtoto mkubwa kwenye familia akitegemewa na wazazi na wadogo zake aikomboe familia kwenye umasikini ila akiangalia umri unaenda hana kazi, mke wala nyumba na msichana pekee aliyempenda aitwaye rose alimuacha, kichwa kinajaa mawazo na njia pekee aliyoiona kupunguza mawazo ilikuwa ni pombe
 
Hakupenda kunywa pombe ila mawazo ya majukumu aliyonayo akiwa ni mtoto mkubwa kwenye familia akitegemewa na wazazi na wadogo zake aikomboe familia kwenye umasikini ila akiangalia umri unaenda hana kazi, mke wala nyumba na msichana pekee aliyempenda aitwaye rose alimuacha, kichwa kinajaa mawazo na njia pekee aliyoiona kupunguza mawazo ilikuwa ni pombe
Huku akisindikizia na Ule wimbo wa ''mawazo'' wa msanii Diamond, Ipo siku pia aliwambia marafiki zake kwamba yeye pia anaweza kuimba.
 
Huku akisindikizia na Ule wimbo wa ''mawazo'' wa msanii Diamond, Ipo siku pia aliwambia marafiki zake kwamba yeye pia anaweza kuimba.
Familia yake na Ndoto ya kuwa muimba mziki ndio vitu pekee vilivyomfanya aendelee kuishi kwenye dunia ingawa kichwani kuna sauti ilimwambia kuwa haiwezi kuimba...
 
Familia yake na Ndoto ya kuwa muimba mziki ndio vitu pekee vilivyomfanya aendelee kuishi kwenye dunia ingawa kichwani kuna sauti ilimwambia kuwa haiwezi kuimba...
Miaka ilizidi kwenda, na umri wa Haduri ukawa mkubwa zaidi, hana kazi, hana mke, hana mtoto na mbaya zaidi ni mlevi kupindukia.
Aliamini ndoto zake za kuwa mwanamuziki atazitimiza siku moja.....
 
Miaka ilizidi kwenda, na umri wa Haduri ukawa mkubwa zaidi, hana kazi, hana mke, hana mtoto na mbaya zaidi ni mlevi kupindukia.
Aliamini ndoto zake za kuwa mwanamuziki atazitimiza siku moja.....
Kila aliposhika chupa, aliiona kama kipaza sauti, na kila lalamiko lake liligeuka kuwa beti ya wimbo wa huzuni.
Usiku kucha alikuwa akipiga magitaa ya plastiki kwenye magunia, akiimba kwa sauti iliyochanganyika na kilio kisicho na mshabaha.
 
Miaka ilizidi kwenda, na umri wa Haduri ukawa mkubwa zaidi, hana kazi, hana mke, hana mtoto na mbaya zaidi ni mlevi kupindukia.
Aliamini ndoto zake za kuwa mwanamuziki atazitimiza siku moja.....
Siku moja alilewa kichwa kikawa kizito kuliko makalio hivyo akaangula kichwa chini makalio juu
 
Kila aliposhika chupa, aliiona kama kipaza sauti, na kila lalamiko lake liligeuka kuwa beti ya wimbo wa huzuni.
Usiku kucha alikuwa akipiga magitaa ya plastiki kwenye magunia, akiimba kwa sauti iliyochanganyika na kilio kisicho na mshabaha.
Hali iliendelea hivyo hivyo kwa Haduri mpaka watoto walimdharau.

Siku moja aliamka asubuhi na kuwaza safari ya kuelekea Msamvu stendi kupanda basi la BM Coach linalokwenda jijini Dar es Salaam.
Aliamini akienda jijini humo, maisha yake yanaweza kumuendea sawia licha ya kuwa hana kipaji wala ujuzi wowote.

Siku ya safari ilifika na akaelekea Msamvu stendi kutafuta basi la kwenda jijini Dar es Salaam ili kutafuta maisha....
 
Siku moja alilewa kichwa kikawa kizito kuliko makalio hivyo akaangula kichwa chini makalio juu
Watu wakijiji kile wakamkuta asubuhi, akiwa ameanguka katika kongoro la mto lupaso.

Alisikikaa Mashauri akisema "loh huyu si Haduru, ameanguka, kichwa chini makalio juu"

Bibi yake, akasema jina ndio linamfanya awe mlevi maana ni la urithi, hivyo wakambalisha jina kutoka kuwa Haduru na kumpa jina jipya la Amada!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom