The Invincible
JF-Expert Member
- May 6, 2006
- 6,006
- 3,280
RIP J SUMARI. Poleni wafiwa wote.
Ni MBUNGE. Ibara ya 68 ya KATIBA ya JMT inasema hivo. Anaishia tu kumchagua Spika. Ili aendelee na kazi zingine za kibunge inabidi aape kwanza. Ibara ya 71(1) inaainisha mambo yatakayomfanya mtu asiendelee kuwa mbunge. La kuapa halimo.
Swali langu ni kifungu 71(1)(e) kinavyotumiwa sasa na vyama vyetu vya SIASA ni sahihi? Kinachosemwa hapa ni Mbunge kuacha uanachama sio kuachishwa au kufukuzwa kama inavyofanyika. Mahakama zetu zitupatie tafsiri sahihi ya kifungu hiki.Nawapa pole wale wote walioguswa na msiba huu kwa njia moja au nyingine, watoto wake, serikali, majirani na wakazi wa jimbo lake.
lakini msiba huu pia nadhani utufumbue macho katika mchakato wa katiba mpya (sio huu feki) utakapoanza, kuna mambo mengi sana ya kurekebishwa na kuwekwa
..............
SEHEMU YA PILI YA KATIBA, INAYOZUNGUMZIA WABUNGE, WILAYA YA UCHAGUZI NA UCHAGUZI HEBU NINUKUU MACHACHE:-
Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge:-
66.1.b) Ikiwa kwa mujibu wa sheria inayotumika katika JM imethibitika rasmi kwamba mtu huyo ana UGIONJWA WA AKILI; au;
68. kila Mbunge atatakiwa kuapishwa ktk bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki ktk shughuli za bunge; lkn mbunge aweza kushiriki uchaguzi wa spika hata kabla hajaapishwa
69.(1) kila mbunge atatakiwa, kabla ya kumalizika siku 30 tangu aapishwe kushika madaraka kama mbunge kuwasilisha kwa spika nakala 2 za tamko rasmi kwamba hajapoteza sifa za uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya aya (d) ya ibara ndogo ya (2) ya ibara ya 67.
71.(1) Mbunge atakoma kuwa mbunge na ataacha kiti chake ktk bunge litakapotekea lolote ktk mambo yafuatayo:-
a) ikiwa litatokea jambo lolote ambalo, km asingekuwa mbunge lingemfanya asiwe na sifa za uchaguzi au apoteze sifa za uchaguzi au asiweze kuchaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu wa masharti ya katiba hii;
b) ikiwa mbunge huyo atachaguliwa kuwa Rais;
c) ikiwa mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano ya bunge 3 mfululizo bila ruhusa ya spika;
d) ikiwa amethibitika kwamba amevunja masharti ya sheria ya maadili ya viongozi wa uma;
e) ikiwa Mbunge Ataacha kuwa Mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa mbunge;
f) iwapo mbunge anachaguliwa au anateuliwa kuwa makamu wa rais;
g) kwa Mbunge ambaye anatakiwa kutoa taarifa rtasmi ya mali kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 70, ikiwa atashindwa kutoa hilo tamko kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 70 katika muda uliowekwa mahususi kwa ajili hiyo kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na bunge
Lakini iwapo mbunge hatakoma kuwa mbunge kwa mujibu wa jambo lolote kati ya mambo yaliyotajwa na kama hatajiuzulu au KUFARIKI mapema zaidi; basi mbunge ataendelea kushika madaraka yake kama mbunge mpaka wakati wa bunge litakapovunjwa kwa mujibu wa ibara ya 90, BILA KUATHIRI HAKI NA STAHILI ZINAZOTOKANA NA UBUNGE WAKE.
.........
Kama alitenda MEMA atalipwa MEMA kama alitenda Mabaya atalipwa Mabaya! Amen
@ Duble Chris
Samahani Nje ya mada kidogo:
frustration is given by expectation divide by
outcome
ie frustration = expectation/outcome
R.I.P. Mzee Sumari
Tunatarajia upendo ulioonyeshwa na wana ccm kwenye mazishi ya dada Regia tutauona kwa wanachedema pia kwenye msiba huu!