Mbunge Jeremiah Sumari afariki dunia

Mbunge Jeremiah Sumari afariki dunia

Haya tena!!!
Mungu anajua mahali sahihi pa kumlaza huyu mtu;na amekwisha mlaza huko!Poleni wafiwa!!!
 
Kuna habari zimenifikia sasa havi kwamba Mbunge huyu amefariki!.

Mbunge huyu alikuwa mgonjwa na hakuapishwa 2010.

Alipelekwa India na iliandikwa hapa jukwaani, hali ilikuwa mbaya sana!

Baada ya kupata matibabu ya uvimbe kwenye ubongo, alirudishwa kimyakimya na sasa nimesikia amefariki.

UPDATE:

Naibu Spika kathibitisha habari hizi na marehemu alifariki saa 8 usiku wa kuamkia leo akiwa hospitali ya taifa - Muhimbili

Kama alikuwa hajaapishwa basi hakuwa mbunge kamili...au sheria zinasemaje.Hivi ndio baba yao akina nancy na Nakaaya?
Poleni wafiwa..
 
RIP Mh. Sumari Mungu amekupumzisha na aipiganie familia yako. Mama sumari pole sana mama Mungu atakutia nguvu kuanza masiha ya ujane kwa kumkosa uliyemzoea. watoto wa sumari poleni kwani mtakuwa na majonzi makubwa kwani baba hamtomwona tena. mungu awatie nguvu
 
Huyu Sumari kama nae alichakachua, basi mtu aliemchakachua mzizi wake kiboko.....yaani mtu hata kuapishwa ilishindikana!!
Jamani mgombea waq CHADEMA awe yuleyule.....wakimchakachua tena...anakaba koo mtu!

RIP Sumari
 
Tunamwomba Mungu ampe pumnziko la milele na kuifariji familia yake.
 
kapumzike kwa amani ndugu yetu kipenzi. Tanzania tunazidi kugubikwa na majonzi ee Mwenyezi Mungu mwingi wat rehema tua kutie nguvu kuyakubali na kuyapokea mapenzi yako.
 
chadema naona wanafurahia sana vifo vya wenziwao, hata hii michango inaonyesha jinsi gani chadema walivyokaa kitumbo tumbo tu
Una matatizo ya akili nani aliyechangia hapa halafu akajitambulisha kama chadema? Upupu mtupu!!
 
Sawa ahsante kwa taarifa ya kifo. Familia yake iiendelee na mazishi.
Sisi Tujipange Upya na Maendeleo yaliocheleweshwa na kiburi cha kukataa kujiudhulu japo alijua Kuwa ni mgonjwa na hangeshindwa kuwahudumia wananchi.
 
maxence Melo yupo, ngoja tusubiri athibitishe.

Hivi imeandikwa wapi kuwa Maxence Melo ndi anatakiwa ku-cofirm vifo vya watu vinapotokea? Tuache mawazo majitaka wakuu,hii nchi ina issue nyingi kuzisemea na sio kuja na umbea na uzabizabina hapa.Kwa mtu mwenye akili amekwisha kusoma mawazo yako,na kwa kweli umepotoka sana.
 
Pumzika kwa amani Mheshimiwa Sumari. Mungu amekupenda zaidi
 
RIP Sumari. Samahani natoka nje ya mada kidogo kwenye katiba mpya kuwe na muda maalum ambapo mbunge akichaguliwa na wakati wa kuapishwa akawa mgonjwa basi hiyo nafasi iwe wazi. Kuliko mbunge anakuwa mgonjwa na zaidi ya mwaka hajaapishwa
Inajulikana kuwa mfanyakazi wa serikali anapaswa kulipwa nusu mshahara endapo atapata likizo ya ugonjwa zaidi ya miezi 6 na ataachishwa kazi baada ya mwaka 1 endapo atakuwa hajapona kuweza kurudi kazini. Kama hili halikutekelezwa basi hiyo ni aina ya ufisadi inayopaswa kupigwa vita bila kujali inamgusa nani! Kuna wanafanyakazi wengi wa umma waliofanyiwa kama sheria inavyotaka kwanini ni tofauti kwa wabunge? Sheria ni msumeno!!!!!
 
Jana tumemzika shujaa wetu Regia Mtema, wengi tulimwona shujaa wetu. Je huyu Jere100 ni shujaa?
Shujaa wa kutuibia watanzania hana hadhi ya kufananishwa na Bi Regia hata kidogo, ni CCM ndo watamlilia kama shujaa maana wao ushujaa una tafsiri tofauti na tafsiri tuijuayo sisi
kwa CCM
Kwiba pesa za Serikali = Ushujaa
Kudhulumu haki za wanyonge = Ushujaa
Kuchakachua matokeo ya uchaguzi = Ushujaa

Na huyu alikuwa navyo vyote, si ajabu ukaona wanaCCM wakimwita shujaa!!
 
Back
Top Bottom