Mbunge Jeremiah Sumari afariki dunia

Mbunge Jeremiah Sumari afariki dunia

Poleni kwa msiba wapiga kura wake huko Arumeru.Nasakia EL alimsaidia kupata ubunge nusura apingwe chini na kijana wa CDM
 
Poleni wana Arumeru japo kwenye red pana kaukweli. Nafikiri mbunge akikosa vikao vitatu mfululizo anakuwa amepoteza sifa ya kuwa mbunge. Sasa Marehemu alikosa kikao kile cha kuapishwa, kakosa cha january, mwezi wa nne, mwezi wa sita (cha bajeti) na mwezi wa kumi. Bunge na Tume ya Uchaguzi vilikaa kimya.

Je, Pamoja na kutokuapishwa, Hata kama alikuwa kaapishwa bado alikuwa na uhalali wa kuitwa mbunge? Naomba wanasheria
mnisaidie

Wakuu hata mimi sijapata picha juu ya hilo suala la kutokuhudhuria vikao mfululizo na kutokuapishwa.mtueleweshe kwa wale mnaojua
 
Tangu mda sana wanaJF walianza kutabiri kifo hiki kama cha MH Dr sasa imekuwa kweli?

ee mungu mlaze mahali panapo stahili Mh Sana

Tupo pamoja wana CCM ktk wakati huu mgumu
 
Natoa pole za dhati jwa familia ya Sumari, ndugu jamaa na marafiki kwa msiba huu mkubwa. Pia kwa wale wote waliouguswa na msiba huun Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi amen._
 
Mkuu kwani Mwigulu Hana famila mpaka Anavizia za wenzake? Hebu nijuze zaidi kamanda

Anayo mkuu ila hilo ndo sharti alilopewa na sangoma wake kuwa napokuwa kampeni meneja kwenye byelection lazima abanjue mke wakada eti ndiyo ushindi utapatikana,kwetu usukumani kwa wenyekuamini ushirikina masharti ya aina hii huitwa NDAGU kwa hiyo hiyo ndiyo NDAGU ya jamaa
 
Alex Kaaya si nasikia amestafu DAWASCO ama nilipotoshwa?

Prof. Pallangyo anaweza kumudu siasa kweli MUHAS imemuelemea, tangu mwanzoni mwa miaka ya 2000 nasikia wanafunzi wanamlalamikia lakini bado wamo tu. Kujuana na wakubwa wa nchi raha sana, hata ukiboronga wanakupa 😛oa
Hakustaafu. Alirudishwa wizarani alikokuwa kabla ya kuja kuanzisha DAWASCO ambayo ilichukua nafasi ya CityWater. Aliondoka kwa aibu kule ambako alikuwa amepelekwa na Lowasa.
 
Wadau bado wimbi la vifo vya wanasiasa na watu mashuhuri linaendelea kutanda katika wingu wa Tanzania.

Mungu aiweke roho ya marehemu Jeremiah Sumari mahali pema peponi
 
Ee bwana ee, mtoa roho kapiga kambi Bongo?

R.I.P. Mh. Sumari.
 
Natoa pole za dhati jwa familia ya Sumari, ndugu jamaa na marafiki kwa msiba huu mkubwa. Pia kwa wale wote waliouguswa na msiba huun Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi amen._

Mwanakijiji tujulishe kama unafahamu kuhusu mbunge kutokuapishwa mara baada ya uchaguzi na kutokuhudhuria vikao mfululizo,sheria zinasemaje?
 
I'm ant-CCM but with this statement you have crossed the line.

RIP Mh. Sumari. Poleni sana wafiwa, Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Bwana alitoa na sasa ametwaa.

chadema jimbo lenu hilo'wote walioiba kura zetu hawatanusa 2015 akiwemo jk
 
Kulikuwa na ile thread ya majimbo yanayoelekea kuwa wazi. Mh naona inaanza kuwa kweli japo bado hukumu ya kafulila na hamad. Kwenye list pia alikuwepo EL na Shibuda. Ngoja tusubiri
 
Thanks mkuu: cdm Igunga 0-26,000 kwa Arumeru Mashariki cdm kutoka 19,000-50,000 ni kama kumsukuma mlevi.ccm record yao imekuwa ni ya kura kushuka sababu ya kukoswa mvuto
"Mmiliki" halisi wa Jimbo hili ni Lowasa akisaidiwa na Mzee Jackson Kaaya. Unaiona shughuli ilivyo pevu. Hapa kumsukuma mlevi hakupo. CHADEMA ilipata kura hizi Igunga baada ya "mmiliki" wa Jimbo lile, RA, kususa.
 
Mwanakijiji tujulishe kama unafahamu kuhusu mbunge kutokuapishwa mara baada ya uchaguzi na kutokuhudhuria vikao mfululizo,sheria zinasemaje?
Ni MBUNGE. Ibara ya 68 ya KATIBA ya JMT inasema hivo. Anaishia tu kumchagua Spika. Ili aendelee na kazi zingine za kibunge inabidi aape kwanza. Ibara ya 71(1) inaainisha mambo yatakayomfanya mtu asiendelee kuwa mbunge. La kuapa halimo.
 
Back
Top Bottom