Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Ndugu Mkandara,

Si kweli kwamba sera ya majimbo ilichangia CCM kuzoa kura au kupata " matokeo walioyapata". Kama ungekuwa unakumbuka vizuri mapambano ya hoja wakati wa kampeni, basi CHADEMA walikuwa wawaburuza vibaya CCM, propaganda zote za CCM zilijibiwa kwa ufundi sana na Freeman kwenye mikutano yake ya kampeni.

Hoja ya kwamba Sera ya majimbo italigwa taifa ilijibiwa vizuri kabisa na CHADEMA.Mbowe alohoji kwa kutengeneza jimbo mfano la kanda ya ziwa, ambapo ataonganisha mikoa ya Mara, Mwanza na Kagera anaonganisha makabila mangapi? Akajibu kwa kusema wanaoligawa taifa ni CCM kwa kuendelea kugawa wilaya kwa misingi ya kisisa na kikabilia! Mfano jimbo la hai waligawa kwa misingi ya CCM na CHADEMA, jimbo la Tarime hivyo hivyo na pia sasa wameweka mstari upande wa wajaluo na wakurya! Nani analigwa taifa?

Taifa linaendelea kugawanyika kwa ubinafsi wa viongozi, maamuzi mabaya ambayo yanaongeza nyufa kati ya maskini na tajiri hapa ndio yanaligawa taifa! Angal;ia Zanzibar walipunguza majimbo ya pemba na kuongeza ya unguja kwa misingi ya kunufaika kisiasa!Kwa hiyo mfumo wa sasa ndio unaligwa taifa. CCM walishindwa kujibu hoja, walizidiwa, wakaanza kushambulia helkopta na baadae Mzee kingunge akaja na kituko kwamba Mbowe asimnukuu Nyerere, eti kwa hoja kwamba Nyerere ni mali ya CCM! Hivyo Mbowe na Nyerere ni vitu viwili tofauti!

Kama tungekuwa tunaamua kwa kutumia hoja,CCM walipaswa kuwa wanne! Nyuma ya CHADEMA,CUF na NCCR! Propaganda zote dhidi ya sera ya majimbo zilijibiwa kwa ufasaha kabisa kwenye mikutano yake.CCM walizidiwa na kujawa na hofo.

Hata UDSM ilionekana kumkubali na kumuelewa mno Mbowe, ikumbukwe Mbowe alikwenda Nkurumah kwenye maazimisho ya siku ya mwalimu Nyererena na kuteka wanaafunzi kutokana hoja zake nzito, pia uwepo na mvuto wa Mnyika alie kuwa anaogombea jimbo la ubungo uliasiadia kuleta hamasa kubwa chuo kikuu.

Kouna hivyo, CCM ilizidi kuwa na hofu, ndipo wakaandaa mkutano wao pale Diamond, wakahonga wanafunzi na waliwaletea mabasi kuja kuawachukua wanafunzi kuwapeleka Diamond, JK hakuwa na ujasiri wa kusimama Nkurumah kama ambavyo walikimbia mdahalo wa wagombea uraisi ulioandaliwa na channel TEN. Ni katika mkutano ule wa diamond ndipo JK alipo ahidi kuongeza mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu na kuongeza idadi yawanaopata mikopo, aliropoka kwamba wangetoa mikopo kwa wanafunzi 30,000, hii alilenga tu kuwateka wanafunzi, kwa maana sasa hivi ameshindwa kabisa kutekeleza ahadi yake hii kwa kupunguza idadi ya watu wanao pata mikopo kwa kuongeza kigezo cha Daraja la kwanza kwa wavulana na daraja la kwanza na la pili kwa wasischana, haya yanafanyika wakati takwamu zinaonyesha jumla ya wanafunzi waliopata Daraja la kwanza mpaka la tatu kwa mwaka jana ni 21,000 tu! Hivyo kama angeishi ahadi yake ya 30,000 wanafunzi wote waliofaulu wangepata mikopo!

Na katika kipindiki hiki hata Profesa Rweitama alijenga hoja kuunga mkono hoja ya majimbo katika maadhimisho ya siku ya uhuru.Watu walielewa hoja ya majimbo, propaganda za CCM hazikufanya kazi, ndio maana wameyapika matokeo ili kumkatisha tamaa Mbowe ambao kwa vyovyote vile wanamhofia sana!

Turudi kwenye suala Uchumi, umesema kwamba tatizo letu sasa hivi ni uchumi ni kweli lakini linasababishwa na nini? Uongozi mbovu usiowajibika wala kuwajibishwa.Katiaka Mikutano ya Kampeni, Mbowe alijenga hoja kwa kumnuku ya Nyerere kwamba ili nchi iendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Alifafanua kwamba watu tanao, wengi tu na tuna arhi nzuri na yenye utajiri mkubwa tatizo kuu ni siasa safi na uongozi bora ambao umeshindwa kutumia vyema rasilimali watu na ardhi yenye utajiri mkubwa kuleta maendeleo!

Sera ya majimbo inasisitiza mgawanyo wa rasilimali na kuwapa mamalaka zaidi wananchi kwa kuchagua viongozi na kupunguza idadi ya viongozi wakuteuliwa, kwa kufanya hivyo tutakuwa na uongozi unawajibikla zaidi na kuchochea maendeleo.

Kuhusu wilayani, hoja ya majimbo haisemi tutakuwa na wabunge wenye nguvu zaidi ya wakuu wa wilaya. Nilipo andika nilitaka kuonyesha utitiri wa viongozi wilayani amabo wanagongana kimajukumu,na kuwa mzigo kwa taifa na pia nilionyesha nguvu ya viongozi wa kuteuliwa dhidi ya wale wa kuchaguliwa.

Sera ya majimbo itafuta mikoa, wilaya zitabaki. Ila viongozi wote wa kuteuliwa wataondoka! Kuanzia mkuu wa wilaya, kiongozi wa juu atakuwa ni meya ambae anachaguliwa na kuwajibika moja kwa moja kwa wanachi, badada ya wilaya ni serakali ya jimbo chini ya gavana(au kwa jina lolote litakalo pendekezwa) ambae atakuwa anachaguliwa. Sera ya .majimbo inaainisha mabo yatakayo kuwa chini ya serekali kuu na sekali za majimbo!

Kwa kufanya hivi tutakuwa tumeondokana na miungu watu wanaoteuliwa, ambao hawana mipanago yoyote ya mandeleo kwa maneo husika wala hawajibiki kwa wananchi, pia vyeo vya kuteuliwa vimekuwa vikitumika vibaya,marafiki, nyumba ndogo za viongozi na wapinzani wanaonunuliwa wamekuwa wakizawadiwa vyeo hivi pasipo kuanagalia uwezo wao au wana mipanago na maono gani ya kimandeleo kwenye maeneo husika.

Siamini kama sera hii inagezwa, imesema itaendana mazingira ya Tanzania. Watu wanababaika na jina jimbo, tunaweza kutumia neno kanda. Ikumbukwe hata mahakama na taasisi nyingine kama TRA zinafanya kazi kikanda! Haya ndio majimbo yenyewe!

Na isitoshe, CHADEMA wanaendelea kusema kwamba, sera ya majimbo haitachomekwa tu watakapo chukua nchi, hapana. Moja wataitisha mjadala wa kitaifa juu ya mabadiliko ya kikatiba pili mabadiliko ya kimfumo wa utawala amabapo serekali ya CHADEMA itapendekeza sera ya majimbo na hoja zake.

wananchi watajadili na kuamua na pia wanaweza kuikarabati watakavyo ona inafaa kukidhi mahitaji ya nchi na kuondoa hofu za watu. Na kuonyeaha kuwa wana maanisha wanachosema, mwaka jana CHADEMA wamefanya mabadiliko ya katiba yao ambapo wameamua kuishi sera ya majimbo! Imingizwa kwenye muundo wa chama, wanaifanyia kazi sera yao baada ya mika mitano watakuwa na uzoefu na sera wanayoisimamia hivi ndivyo chama mbadala kinavyopaswa kuwa.

Kwenye mgawanyo wa rasilimali, nimeeleza mantiki ya kubakiza sehemu ya rasilimali kwenye maeneo husika, katika mchango wangu wa mwisho, rejea suala la gharama za kuwa karibu na rasilimali na pia umuhimu wa wananchi wa maeneo husika kufaidika na rasiliamali, pia rejea mfano wa manispaa za wilaya za kinondoni na Ilala. CHADEMA inasema sehemu ya mapato ya railsimali ndio yatabakishwa na sehemu nyingine kupelekwa serekali kuu.

Naomba ulete hapa hoja zako za kijiwe cha zamani mlizo muhoji Mnyika kwa manufaa ya mjadala huu na kwetu sisi ambao hatukubahatika kuwepo huko.

Tujadili
 
Ogah.

Ukabila na udini Tanzania umeshika hatamu, sikubaliani nawe kwa hili tizama chadema utakuta vyote viwili.

suala la chadema kulilia majimbo ni kutokana na wao chadema kutanguliza ubinafsi na ukaskazini. wanaamini kuwa kaskazini kumepiga hatua ya kimaendeleo kama elimu(shule) kuliko sehemu nyingine za nchi. wanachotaka hizo neema wale wao tu na kitendo cha watu wa sehemu nyingine kama wa Mtwara au Lindi kwenda huko kufuata elimu hawakifurahii.

kifupi ni suala la uchoyo ndio linalowasukuma kuja na sera hii ya majimbo.
 
Mswahili,
You seem to know so much about the underlying motives of Chadema. Were you a founding member?
 
Ogah.

Ukabila na udini Tanzania umeshika hatamu, sikubaliani nawe kwa hili tizama chadema utakuta vyote viwili.

suala la chadema kulilia majimbo ni kutokana na wao chadema kutanguliza ubinafsi na ukaskazini. wanaamini kuwa kaskazini kumepiga hatua ya kimaendeleo kama elimu(shule) kuliko sehemu nyingine za nchi. wanachotaka hizo neema wale wao tu na kitendo cha watu wa sehemu nyingine kama wa Mtwara au Lindi kwenda huko kufuata elimu hawakifurahii. kifupi ni suala la uchoyo ndio linalowasukuma kuja na sera hii ya majimbo.

Mswahili, kama lilivyo jina lake, amechoka kufikiri. Ameridhika na yaliyopo. Anamlaumu Mungu kwa kumpa kichwa! Vinginevyo, asingeandika hayo hapo juu, hasa baada ya kumsoma Ongara hapo juu.

Miaka 45 baada ya uhuru tunazidi kurudi nyuma katika kila kitu. Tuna kila kitu, hatuendelei, tunajivuna kuitwa maskini, huku wananchi wakiahidiwa maisha bora. Lazima tutafute ufumbuzi.

Waliowaza majimbo walizingatia tatizo moja kubwa linalotufanya tusiendelee. Ukubwa wa nchi. Tanzania yenye kilometa za mraba zaidi ya 946,000, haiwezi kuendelea kwa kutegemea maamuzi yanayofanyikia Dar es Salaam tu.

Mtu ye yote aliyetembelea mikoa yote ya Tanzania anajua ninachosema. Nchi ni kubwa mno, na vipaumbele vya wananchi havifanani, wala havilingani. Lakini kila mkoa una raslimali zinazosubiri maamuzi kuhusu matumizi kutoka Dar es Salaam. Karibu kila mkoa Tanzania una madini fulani. Misitu kibao. Ardhi yenye rutuba. Mito, maziwa au mbuga za wanyama. Mazao yanayolimwa....ni ivingi. Vyote vinasubiri JK na EL waamue wakiwa Dar.

Laiti wananchi wangekuwa wanaamua wenyewe huko huko mikoani, mambo yangekuwa tofauti. Ungekuwapo ushindani wa kimaendeleo. Na kwa kuwa viongozi wangekuwa wote ni wa kuchaguliwa, si kuteuliwa na rais kama ilivyo sasa, uwajibikaji ungekuwapo.

Masuala ya kitaifa ndiyo yangekuwa yanaletwa katika Bunge kujadiliwa na kufanyiwa uamuzi.

Ukabila? Ukabila hauwezi kuchomoza kwenye jimbo lenye makabila 10 tofauti, kama hauchomozi leo kwenye wilaya moja moja yenye kabila moja! Kama iliwezekana kuunda wilaya na mikoa kwa nini isiwezekane kuunda jimbo. Fikra zetu zinachekesha. CCM wanapozungumzia ukanda tuna sawa. Chadema wakisema majimbo tunaona nongwa!

Naona Mswahili anasubiri ruhusa ya CCM. Mwache aendelee...

Udini? Sioni uhusiano kati ya majimbo na udini. Hivi kuna dini ya makabila ya katikati mwa Tanzania, au Mashariki, au Magharibi? Inaongozwa na nani? Kwa mwavuli upi? Kwanii hata tungekwenda wenye hizo wilaya za CCM hakuna watu na imani zao?

Hebu tukue jamani...Let's be mature!
 
Lowasa wa Chama cha Mapinduzi si mkabila na mbaguzi ambaye sasa mashule na kila maendeleo yana elekea kwake bila ya aibu ? Na anakaribiwa hata kuweka ofisi ya waziri Mkuu Monduli bila hata ya aibu.

Je naye huyu ni Chadema ? Ama Tanzania ni Monduli pekee ?
 
Kichwamaji na Ongara,
Good points. Kinachowasumbua Wadanganyika wengi ni mwamko finyu na kwa wenye uelewa mpana ni UOGA WA MABADILIKO.

Hivi inakuwaje mtu anafikiria Ukabila na Udini katika Tanzania ya leo? Ni wapi huko ambako leo kuna watu wa kabila moja tu na na dini moja? Kama ni huo ukabila nini kinazuia mikoa na wila kuendekeza ukabila?

Na washukuru wachangiaji wa hapo juu walivyoonyesha kwa kina jinsi utaratibu wetu wa sasa unavyoendekeza huo utaratibu wa kugawa wilaya, majimbo na mikoa kwa kuangalia makabila.

Ongara umepigilia msumari kwa kusema tayari tunao utaratibu wa kanda (majimbo) mahakama kuu, benki kuu, TRA na hata elimu mitihani ya kidato cha pili inafanyika ki-kanda haya yote mbona hayajaleta ukabila na udini?

Mkandara,
Nafikiri wengi hapo juu wamekueleza, hakuna mkoa au kanda Tanzania ambayo haina raslimali, hiyo mikoa ya Singida na Dodoma ina utajiri wa kutupwa. Singida kuna madini ni balaa. Mifugo ya Dodoma na Singida inaweza kulipatia taifa pato la ajabu kuzidi hata hiyo dhahabu tunayoibiwa.

Dodoma inaweza kabisa kuwa Calfornia yetu kwa mvinyo na list ni ndefu.
 
Mavidonge haya lazima wayameze tu .Ni mavidonge yenye akili .CCM bwana wana ujanja ujanja wao basi kia kona wana ueneza .

Ukabila kaja nao JK nakuliza mnieleze nina Mkristo kambaye ni Mkuu wa Wilaya ama Mikoa ya Pwani ama maeneo yenye kuaminika kuwa na waislam wengi.

Angalieni hizo na mseme wenyewe kama ukabila unaanzia upinzani ama ?
 
Ndugu Mkandara,

Si kweli kwamba sera ya majimbo ilichangia CCM kuzoa kura au kupata matokeo walioyapata. Kama ungekuwa unakumbuka vizuri mapambano ya hoja wakati wa kampeni, basi CHADEMA walikuwa wawaburuza vibaya CCM, propaganda zote za CCM zilijibiwa kwa ufundi sana na Freeman kwenye mikutano yake ya kampeni.

Hoja ya kwamba Sera ya majimbo italigwa taifa ilijibiwa vizuri kabisa na CHADEMA.Mbowe alohoji kwa kutengeneza jimbo mfano la kanda ya ziwa, ambapo ataonganisha mikoa ya Mara, Mwanza na Kagera anaonganisha makabila mangapi? Akajibu kwa kusema wanaoligawa taifa ni CCM kwa kuendelea kugawa wilaya kwa misingi ya kisisa na kikabilia! Mfano jimbo la hai waligawa kwa misingi ya CCM na CHADEMA, jimbo la Tarime hivyo hivyo na pia sasa wameweka mstari upande wa wajaluo na wakurya! Nani analigwa taifa?

Taifa linaendelea kugawanyika kwa ubinafsi wa viongozi, maamuzi mabaya ambayo yanaongeza nyufa kati ya maskini na tajiri hapa ndio yanaligawa taifa! Angal;ia Zanzibar walipunguza majimbo ya pemba na kuongeza ya unguja kwa misingi ya kunufaika kisiasa!Kwa hiyo mfumo wa sasa ndio unaligwa taifa. CCM walishindwa kujibu hoja, walizidiwa, wakaanza kushambulia helkopta na baadae Mzee kingunge akaja na kituko kwamba Mbowe asimnukuu Nyerere, eti kwa hoja kwamba Nyerere ni mali ya CCM! Hivyo Mbowe na Nyerere ni vitu viwili tofauti!

Kama tungekuwa tunaamua kwa kutumia hoja,CCM walipaswa kuwa wanne! Nyuma ya CHADEMA,CUF na NCCR! Propaganda zote dhidi ya sera ya majimbo zilijibiwa kwa ufasaha kabisa kwenye mikutano yake.CCM walizidiwa na kujawa na hofo.

Hata UDSM ilionekana kumkubali na kumuelewa mno Mbowe, ikumbukwe Mbowe alikwenda Nkurumah kwenye maazimisho ya siku ya mwalimu Nyererena na kuteka wanaafunzi kutokana hoja zake nzito, pia uwepo na mvuto wa Mnyika alie kuwa anaogombea jimbo la ubungo uliasiadia kuleta hamasa kubwa chuo kikuu.

Kouna hivyo, CCM ilizidi kuwa na hofu, ndipo wakaandaa mkutano wao pale Diamond, wakahonga wanafunzi na waliwaletea mabasi kuja kuawachukua wanafunzi kuwapeleka Diamond, JK hakuwa na ujasiri wa kusimama Nkurumah kama ambavyo walikimbia mdahalo wa wagombea uraisi ulioandaliwa na channel TEN. Ni katika mkutano ule wa diamond ndipo JK alipo ahidi kuongeza mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu na kuongeza idadi yawanaopata mikopo, aliropoka kwamba wangetoa mikopo kwa wanafunzi 30,000, hii alilenga tu kuwateka wanafunzi, kwa maana sasa hivi ameshindwa kabisa kutekeleza ahadi yake hii kwa kupunguza idadi ya watu wanao pata mikopo kwa kuongeza kigezo cha Daraja la kwanza kwa wavulana na daraja la kwanza na la pili kwa wasischana, haya yanafanyika wakati takwamu zinaonyesha jumla ya wanafunzi waliopata Daraja la kwanza mpaka la tatu kwa mwaka jana ni 21,000 tu! Hivyo kama angeishi ahadi yake ya 30,000 wanafunzi wote waliofaulu wangepata mikopo!

Na katika kipindiki hiki hata Profesa Rweitama alijenga hoja kuunga mkono hoja ya majimbo katika maadhimisho ya siku ya uhuru.Watu walielewa hoja ya majimbo, propaganda za CCM hazikufanya kazi, ndio maana wameyapika matokeo ili kumkatisha tamaa Mbowe ambao kwa vyovyote vile wanamhofia sana!

Turudi kwenye suala Uchumi, umesema kwamba tatizo letu sasa hivi ni uchumi ni kweli lakini linasababishwa na nini? Uongozi mbovu usiowajibika wala kuwajibishwa.Katiaka Mikutano ya Kampeni, Mbowe alijenga hoja kwa kumnuku ya Nyerere kwamba ili nchi iendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Alifafanua kwamba watu tanao, wengi tu na tuna arhi nzuri na yenye utajiri mkubwa tatizo kuu ni siasa safi na uongozi bora ambao umeshindwa kutumia vyema rasilimali watu na ardhi yenye utajiri mkubwa kuleta maendeleo!

Sera ya majimbo inasisitiza mgawanyo wa rasilimali na kuwapa mamalaka zaidi wananchi kwa kuchagua viongozi na kupunguza idadi ya viongozi wakuteuliwa, kwa kufanya hivyo tutakuwa na uongozi unawajibikla zaidi na kuchochea maendeleo.

Kuhusu wilayani, hoja ya majimbo haisemi tutakuwa na wabunge wenye nguvu zaidi ya wakuu wa wilaya. Nilipo andika nilitaka kuonyesha utitiri wa viongozi wilayani amabo wanagongana kimajukumu,na kuwa mzigo kwa taifa na pia nilionyesha nguvu ya viongozi wa kuteuliwa dhidi ya wale wa kuchaguliwa.

Sera ya majimbo itafuta mikoa, wilaya zitabaki. Ila viongozi wote wa kuteuliwa wataondoka! Kuanzia mkuu wa wilaya, kiongozi wa juu atakuwa ni meya ambae anachaguliwa na kuwajibika moja kwa moja kwa wanachi, badada ya wilaya ni serakali ya jimbo chini ya gavana(au kwa jina lolote litakalo pendekezwa) ambae atakuwa anachaguliwa. Sera ya .majimbo inaainisha mabo yatakayo kuwa chini ya serekali kuu na sekali za majimbo!

Kwa kufanya hivi tutakuwa tumeondokana na miungu watu wanaoteuliwa, ambao hawana mipanago yoyote ya mandeleo kwa maneo husika wala hawajibiki kwa wananchi, pia vyeo vya kuteuliwa vimekuwa vikitumika vibaya,marafiki, nyumba ndogo za viongozi na wapinzani wanaonunuliwa wamekuwa wakizawadiwa vyeo hivi pasipo kuanagalia uwezo wao au wana mipanago na maono gani ya kimandeleo kwenye maeneo husika.

Siamini kama sera hii inagezwa, imesema itaendana mazingira ya Tanzania. Watu wanababaika na jina jimbo, tunaweza kutumia neno kanda. Ikumbukwe hata mahakama na taasisi nyingine kama TRA zinafanya kazi kikanda! Haya ndio majimbo yenyewe!

Na isitoshe, CHADEMA wanaendelea kusema kwamba, sera ya majimbo haitachomekwa tu watakapo chukua nchi, hapana. Moja wataitisha mjadala wa kitaifa juu ya mabadiliko ya kikatiba pili mabadiliko ya kimfumo wa utawala amabapo serekali ya CHADEMA itapendekeza sera ya majimbo na hoja zake.

wananchi watajadili na kuamua na pia wanaweza kuikarabati watakavyo ona inafaa kukidhi mahitaji ya nchi na kuondoa hofu za watu. Na kuonyeaha kuwa wana maanisha wanachosema, mwaka jana CHADEMA wamefanya mabadiliko ya katiba yao ambapo wameamua kuishi sera ya majimbo! Imingizwa kwenye muundo wa chama, wanaifanyia kazi sera yao baada ya mika mitano watakuwa na uzoefu na sera wanayoisimamia hivi ndivyo chama mbadala kinavyopaswa kuwa.

Kwenye mgawanyo wa rasilimali, nimeeleza mantiki ya kubakiza sehemu ya rasilimali kwenye maeneo husika, katika mchango wangu wa mwisho, rejea suala la gharama za kuwa karibu na rasilimali na pia umuhimu wa wananchi wa maeneo husika kufaidika na rasiliamali, pia rejea mfano wa manispaa za wilaya za kinondoni na Ilala. CHADEMA inasema sehemu ya mapato ya railsimali ndio yatabakishwa na sehemu nyingine kupelekwa serekali kuu.

Naomba ulete hapa hoja zako za kijiwe cha zamani mlizo muhoji Mnyika kwa manufaa ya mjadala huu na kwetu sisi ambao hatukubahatika kuwepo huko.

Tujadili
Eric Ongara: Umenifanya nisome hoja zako tena na tena; hongera sana. Hilo ni darasa zito ndugu yangu. Ingekuwa sio ushabiki ningesema hii mada ya majimbo imekwisha, tuendelee na mengine.

Lakini acha watu waendelee kulumbana ndio raha ya hii forum. Ahsante sana. Umenikuna!
 
Ongara safi sana .

Ukabila na udini umejaa ndani ya CCM kama Chama na Viongozi wake hulioni hilo unalia na Chadema tuu
 
Kichwa & Eric,

well said,
ili tu-move ahead, tusimuache mswahili akiwa na maswali mengi kichwani mwake, kwani mswahili akija kuelewa nini maana ya Majimbo/Kanda, itakuwa bomba zaidi.
 
EO
Kichwamaji
Lunyungu
Tabasamu
Jasusi

Mswahili, kama lilivyo jina lake, amechoka kufikiri. Ameridhika na yaliyopo. Anamlaumu Mungu kwa kumpa kichwa! Vinginevyo, asingeandika hayo hapo juu, hasa baada ya kumsoma Ongara hapo juu.
Miaka 45 baada ya uhuru tunazidi kurudi nyuma katika kila kitu. Tuna kila kitu, hatuendelei, tunajivuna kuitwa maskini, huku wananchi wakiahidiwa maisha bora. Lazima tutafute ufumbuzi.

Nafikiri hapa ni wewe ambaye unashindwa kufikiria hakuna binadamu anayeridhika na kile ambacho anakipata kama ameridhika basi huyo ni punguani. Unaongelea miaka 45 tunarudi nyuma wewe binafsi kumbuka kisomo hicho ambacho kimekuwezesha kuandika haya unayoandika kimetokana na policy zilizowekwa na serikali hiyo ambayo ni ya CCM.

Waliowaza majimbo walizingatia tatizo moja kubwa linalotufanya tusiendelee. Ukubwa wa nchi. Tanzania yenye kilometa za mraba zaidi ya 946,000, haiwezi kuendelea kwa kutegemea maamuzi yanayofanyikia Dar es Salaam tu. Mtu ye yote aliyetembelea mikoa yote ya Tanzania anajua ninachosema. Nchi ni kubwa mno, na vipaumbele vya wananchi havifanani, wala havilingani. Lakini kila mkoa una raslimali zinazosubiri maamuzi kuhusu matumizi kutoka Dar es Salaam. Karibu kila mkoa Tanzania una madini fulani. Misitu kibao. Ardhi yenye rutuba. Mito, maziwa au mbuga za wanyama. Mazao yanayolimwa....ni ivingi. Vyote vinasubiri JK na EL waamue wakiwa Dar.


Hivi ni nani alikudanganya kwamba maamuzi yote yanafanyika Dar Es Salaam? Kutembelea mikoa yote Tanzania ni nyenzo ya uelewaji? Wewe unaiga mkumbo wa majimbo kama yalivyo kule Marekani unafikiri ukishafanya hivyo utakuwa umeendelea kama Marekani huo ni ulimbukeni. Endelea tu kulala kwani waswahili walisema usimwamshe aliye lala. Unaongelea vipaumbele vya wananchi havifanani are you serious? Ni mwanachi gani hataki maendeleo? Nani alikwambia maamuzi yote yanatoka kwa JK na EL tu. Hivi ni jinsi ambavyo hufahamu mechanism ya ufanyaji kazi wa serikali.



Laiti wananchi wangekuwa wanaamua wenyewe huko huko mikoani, mambo yangekuwa tofauti. Ungekuwapo ushindani wa kimaendeleo. Na kwa kuwa viongozi wangekuwa wote ni wa kuchaguliwa, si kuteuliwa na rais kama ilivyo sasa, uwajibikaji ungekuwapo. Masuala ya kitaifa ndiyo yangekuwa yanaletwa katika Bunge kujadiliwa na kufanyiwa uamuzi.


Hivi wananchi gani ambao wamezuiwa kufanya ushindani hivi sasa katika maendeleo yao? Unaweza kutoa mfano kwa hili? Hivi unafahamu leadership ladder wewe? Au tunaongea na mtu ambaye ni form VI failure?

Ukabila? Ukabila hauwezi kuchomoza kwenye jimbo lenye makabila 10 tofauti, kama hauchomozi leo kwenye wilaya moja moja yenye kabila moja! Kama iliwezekana kuunda wilaya na mikoa kwa nini isiwezekane kuunda jimbo. Fikra zetu zinachekesha. CCM wanapozungumzia ukanda tuna sawa. Chadema wakisema majimbo tunaona nongwa!
Naona Mswahili anasubiri ruhusa ya CCM. Mwache aendelee...
Udini? Sioni uhusiano kati ya majimbo na udini. Hivi kuna dini ya makabila ya katikati mwa Tanzania, au Mashariki, au Magharibi? Inaongozwa na nani? Kwa mwavuli upi? Kwanii hata tungekwenda wenye hizo wilaya za CCM hakuna watu na imani zao?
Hebu tukue jamani...Let's be mature!


Ukabila unaozungumziwa hapa ni Chadema tangu kianze wenyeviti wake wote ni wakaskazini na ni uchaga tu hakuna cha zaidi, wabunge wa kuchaguliwa ni wana ndugu tu sio mtu mwingine. Chadema ndio mnatakiwa mkue na muache utoto.


Good points. Kinachowasumbua Wadanganyika wengi ni mwamko finyu na kwa wenye uelewa mpana ni UOGA WA MABADILIKO.


Watanzania hao ambao mnawadharau eti wana mawazo finyu ndio wamewashitukia jaribuni kukaa chini na kujiuliza kulikoni? Huwezi kumdharau mtu ambaye unamtegemea akupe ujiko.


Hivi inakuwaje mtu anafikiria Ukabila na Udini katika Tanzania ya leo? Ni wapi huko ambako leo kuna watu wa kabila moja tu na na dini moja? Kama ni huo ukabila nini kinazuia mikoa na wila kuendekeza ukabila?


Ukabila unaoongelewa hapa ni wa Chadema toeni mboni zilizo machoni mwenu.



Ongara umepigilia msumari kwa kusema tayari tunao utaratibu wa kanda (majimbo) mahakama kuu, benki kuu, TRA na hata elimu mitihani ya kidato cha pili inafanyika ki-kanda haya yote mbona hayajaleta ukabila na udini?
Mavidonge haya lazima wayameze tu .Ni mavidonge yenye akili .CCM bwana wana ujanja ujanja wao basi kia kona wana ueneza . Ukabila kaja nao JK nakuliza mnieleze nina Mkristo kambaye ni Mkuu wa Wilaya ama Mikoa ya Pwani ama maeneo yenye kuaminika kuwa na waislam wengi .Angalieni hizo na mseme wenyewe kama ukabila unaanzia upinzani ama ?



Hakuna vidonge hapa ni upupu tu umejaa na ushabiki wa yanga na simba.

kazi kwenu
 
Wacha/Mswahili/chinga and now jadilithentafiti,
Kunahaja gani ya wewe kuja na jinatofauti kila wakati ili kutetea uoza ulioifikisha Tanzania hapo ilipo?
 
EO

Hakuna vidonge hapa ni upupu tu umejaa na ushabiki wa yanga na simba.

kazi kwenu

What brought you here kama hapa pamejaa UPUPU?Posting yako ya kwanza na dharau dhidi ya uliotukuta!Leave the forum and us alone,neda huko kusiko na upupu.Shwain!!
 
Tabasamu.

wewe tukuite Mbowe/Mnyika/Mwanasiasa/Lunyungu/Lucy Kiwele?
kwanini nitumie majina tofauti tena kwa wajinga kama chadema?

Lunyungu.

Mkuu wa mkoa wa pwani ni mkristu DR.christina Ishengoma na mhaya.
kamanda wa vijana wa ccm wa wilaya ya mkurunga-Pwani ni mhaya dr.MUTEMBEI na mkristu.

wenyeviti wa mikoa wa ccm wakristu ndio wengi, makatibu wa chama wa wilaya na mikoa bado wakristu wengi.
wakuu wa wilaya wa serikali ya ccm wakristu ni wengi sana tena hata sifa hawana mfano Betty MKWASA,

maofisa tawala wamechaguliwa wakristu wengi tu, JK katika appointment zake toka amekuwa rais wa Tz kawabeba sana wakristu ila tu hambebeki.

Lunyungu.

Huko chadema ndio kama vatican.
 
Tabasamu,
Hiyo Hoja ya Kusema Dodoma na Singida ni matajiri nadhani itakuwa vizuri ukinipa data za mauzo yao kwa mwaka!. Pili, nini LENGO la zoezi zima:- Kugawana Mirathi!:-

Kinachowashinda kuona hatari yake ni kwa sababu mnaipotosha maana ya majimbo ya Utawala ili kugawa mali zilizoko ktk maeneno hayo!

Mshikaji ERIC,
Hii sera ya majimbo inagawa mirathi ya Tanzania (maliasili) na ajabu mnakataa kabisa kuwa kugawa mirathi hata siku moja hakutenganishi familia hali mnataka hata kuwepo na wasimamizi wa mgao wenyewe!

Sijui mnashindwa vipi kuona hili!.. Tofauti na kuyaweka Majimbo ya kiuchumi...wenznetu waliweza kuchuma wao na majimbo yao ni kuweza kuhifadhi walichokuwa nacho pamoja na culture zao!.. why majimbo ya kiutawala kuingia ktk uchumi?.. thats my question!

Labda nikupeni mfano ambao uko nje yenu yaani Chadema!..
Mnakumbuka EAC ilivyoanza?.. na wapi tulikuja kwama! pale kila mtu alipoanza kudai haki ya kumiliki alichokuwa nacho kwa faida ya wananchi wake!.. Kosa kubwa tulokuja lifanya ni pale viongozi wetu wanasiasa walipokuja kutupangia uchumi na maendeleo ya jumuiya hiyo KIUCHUMI.

Politicians wakaingia ktk muundo wa EAC na kuweka sheria za kisiasa ambazo zilifikia kuvunja JUMUIYA!.. Muungano wetu wa kiuchumi ulivunjika kwa sababu ya Politicians ambao walitaka changes za kiuchumi kutokana na tamaa zao binafsi hali wasomi wanaoendesha EAC walifahamu kuwa jumuiya yetu ama (muungano wa nchi hizi Kiuchumi) ulitufanya kuwa very strong kibiashara.

Na utengano wenyewe ulitokana na dhana kuwa Kenya ilipendelewa zaidi yetu, waliweza kutumia maliasili zetu kujitangaza wao n.k ... Well! what happened?... 30 years after EAC tumeshindwa kujitangaza kabisa na sidhani kama tumejiendeleza zaidi nje ya jumuiya hiyo.

ATC ndio hiyooo haya RTC Mungu anajua mwenyewe! lakini bado tunajivuna kwa sababu no one anaweza kutupa mtazamo wa Tanzania leo hii kama jumuiya ile ingeendelea kuwepo!

What I need from Freeman ni future plan ya haya majimbo ktk kujiendeleza kibiashara na sio jinsi ya kupata utajiri tukigawana mirathi!..yale yale ya CCM ingawa wao wanapeana wao kwa wao.
Kisha kuna tatizo gani kuondoa hawa ma DC na RC leo hii na kupendekeza Wabunge, Meya na madiwani kushika uongozi wa serikali hizi!..that is the problem au sio then kwa nini tuondoe kabisa mikoa kuweka majimbo na which city will be makao makuu ya Jimbo?... yaleyale ya Dodoma kuwa makao wakuu.

Guys nataka mkae mfikiri zaidi, umizeni vichwa vyenu na kulitazama hili swala kwa undani zaidi kwani sii dogo kama mnavyofikiria. Nimesema kuwa nchi zote zilizojitenga zilianza kwa matumaini kama yenu.. Kuwa haiwezekani kutokea Ukabila ama Kujitenga!...
trust me, wasukuma na hao wa kanda ya ziwa wakisha ona kuwa wanaweza kabisa kujiendesha wenyewe na majimbo mengine ni mzigo kwao wataomba UHURU wao!...

Utawala wa majimbo ni moja ya kiamsho cha yule aliyelala!..kuweza kujitazama yeye na sio taifa zima kwa ujumla.

Changes ktk katiba ni lazima lakini hili la majimbo bado kabisa!...
Kibaya zaidi hakuna kati yenu ambaye anaweza kunipa hata nchi MOJA iliyokuwa haina majimbo ya kiutawala kisha wakajigawa kwa majimbo na leo wameweza kufanikiwa.

Zaidi ya hapo sote tunajua kuwa nchi zote zenye majimbo ya Utawala hawaishi vita!... Problem ya nchi zetu ni UTAWALA..ile title kila mtu anataka awe mungu mtu na kuweza kuiba zaidi!...Otherwise, kama tungekuwa kama wenzetu wa nchi za Ulaya ningekubaliana na hoja yenu longtime!.

We are different..might be created different when it comes to leadership!...Kwanza sijawahi kuwaona toka wale waliotuletea Uhuru!
 
Tabasamu.

wewe tukuite Mbowe/Mnyika/Mwanasiasa/Lunyungu/Lucy Kiwele?
kwanini nitumie majina tofauti tena kwa wajinga kama chadema?

Lunyungu.

Mkuu wa mkoa wa pwani ni mkristu DR.christina Ishengoma na mhaya.
kamanda wa vijana wa ccm wa wilaya ya mkurunga-Pwani ni mhaya dr.MUTEMBEI na mkristu.
wenyeviti wa mikoa wa ccm wakristu ndio wengi, makatibu wa chama wa wilaya na mikoa bado wakristu wengi.
wakuu wa wilaya wa serikali ya ccm wakristu ni wengi sana tena hata sifa hawana mfano Betty MKWASA,

maofisa tawala wamechaguliwa wakristu wengi tu, JK katika appointment zake toka amekuwa rais wa Tz kawabeba sana wakristu ila tu hambebeki.

Lunyungu.

Huko chadema ndio kama vatican.

Ukisikia Islamic fundamentalism ndio hii.Distorted view of everything including dini yenyewe.Huyu mujahidina nilipoweka wild guess kuwa next minister for foreign affairs atakuwa Muslim akaniita MDINI.

What crap is he talking about here kama sio udini. May be more than udini bali UJAHIDINA.
 
Mlalahoi.
nilikuwa najibu hoja ya udini aliyokuja nayo Lunyungu. lakini kama kawaida yako ya kuvamia wanaume umeanza kamchezo kako nitakushughulikia.

Tunajua umekuja kuuvuruga huu mjadala wa Mbowe ili ufutwe kama wa Mengi.

hilo nimekushtukia mtu haumwi na nyoka mara mbili.na wengine kuweni macho na huyu Mgalatia (bishop mlalahoi). kama mnakumbuka amesoma chuo kisicho na wahadhiri wenye sifa cha Iringa.
 
Tafiti,
Umeniunganishaje kwenye mada hii? Mimi bado sijajibizana na wewe. Au ndiyo mambo ya guilt by assosiation?
 
Mwanasias, Lunyungu, Ogah, kichwamaji asanteni, Majimbo ni sera murua

Ndugu yangu Mkandara,
Nafurahia sana unavyojadili umesimamia hoja, inanifanya niheshimu michango yako na muda wote kuwa na shauku kujibu hoja zako. Asante kwa hili naamini uwepo wako kwenye forum hii utamsaidia na kumfunda sana ndugu yetu Mswahili.

Turudi kwenye hoja zako baada ya mchango wangu wa mwisho juu ya sera ya majimbo.

1. Juu ya suala la mirathi: Tumesema kwamba sehemu ya mapato ya rasilimali ndio yatabakishwa na mengine yatapelekwa serekali kuu. Kwanini iwe hivyo? Tafadhali rejea michango yangu iliyopita juu ya gharama ya kuwa na rasilimali na pia umuhimu wa wananchi waliopo kwenye maneo ya rasilimali kufaidika na rasilimali. Naomba nisirudie kujibu hili.

2. Kuhusu Kujitenga: Ukitafakari vizuri, sasa hivi ndio kuna hatari ya kujitenga kuliko wakati mwingine wowote, huoni kwamba watu kutofaidika na rasilimali ni hatari zaidi? Watu watasema tungekuwa na mamalaka na maamuzi juu ya rasilimali zetu tungefaidika zaidi kuliko hivi sasa hatufaidiki kabisa badala yake tuaachiwa mashimo tu!

Kuendelewa kuripotiwa habari kama za Buhemba, mgodi umekauka na maeneo kubaki na umaskini inaweza kuchochea kabisa watu kutaka kujitenga! Sera ya majimbo ndio suluhisho, wataweza kufaidika na rasilimali zao.

3.Future Plan ya Majimbo: Si vyema kumtaka Mbowe atoe future plan za majimbo kujiuza, ukiangalia vizuri sera yenyewe inakutaka wewe na mimi tutengeneze hizo future plan, kwamba tofauti na sasa kuchomeka watu kwa kuwateu katika wilaya na mikoa kwenye sera ya majimbo,watu wenye maono watashindana na kuwasilisha mikakati yao, wenye mikakati bora, ndio watakuwa magavana na mameya, mikakati yao itahakikiwa na kuamuliwa na wanachi wa maeneo husika,tuanze basi kutengeneza hizo plans sasa.

Huu ndio uzuri mwingine wa sera ya majimbo inawataka watu wajadili wafikiri hatma ya maeneo husika, kwenye mfumo wa sasa uhuru wa fikra unakuwa umebanwa sana, na kusubiri maagizo toka serekali kuu. Ni kupitia sera majimbo watu wenye mawazo mazito na mbadala ya kuindeleza nchi wataibuka na mawazo yao kuthaminiwa na kufanyiwa kazi. Kumtaka Freeman atoe future plan ni kurudi kwenye utamaduni wa zidumu fikra za mwenyekiti jambo ambalo sera ya majimbo inajitahidi kuondokana nalo.Kwenye majimbo mjadala au ushiriki wa wananchi kuamua hatma yao unaongezeka zaidi!

4. Umekubaliana na sera ya majimbo: Nafurahi umeelewa na kukubaliana na baadhi ya maeneo katika sera hii murua. Kwenye mchango wako wa mwisho umekubaliana na suala kuondoa viongozi wa kuteuliwa na kwamba tuingize kwenye mfumo wa sasa. Pia mwisho unasema ingekuwa ulaya ungekubaliana na hoja zetu, kwa hiyo tatizo hapa ni kwamba huamini watu wako, hili linahitaji mjadala mwingine wa kina, ila kukubali baadhi ya hoja ni mwanzo mzuri na hii inaonyesha ukomavu wako.

5.Unataka ishara: Mimi sipendi utamaduni wa kudesa nje wanafanya nini na sisi ndio tufanye, unasema tukutajie ni maeneo gani wametumia sera hii na wakafanikiwa! Ikumbukwe hapo mwanzo ulisema sera hii CHADEMA imegezwa na ukapinga. Nikakukutalia nikisema sera imetengenezwa kukidhi mazingira ya Tanzania. Turudi kwenye mstari huu huu, mjadali uwe ni kwa kiasi gani sera hii inafaa na sio nani wanafanya nini mazingira ya Tanzania ni tofauti na sehemu nyingine na kama kuna kitu kinalila taifa ni kugeza, sasa hivi wameliundia jina " best practice" sera ya majimbo haipaswai kwenda huko, hii ni sera mbadala, sera ya wanachi!

Naendelea kusema kwamba, CHADEMA wamesema wakichukua nchi wataitisha mjadala wa kitaifa, sasa maadam umekubaliani na baadhi ya hoja si vibaya tukaanza kujadili kuikarabati sasa kama itakavyofanywa wakati huo CHADEMA itakapo shika dola maana CCM nao wanonekana kukubali baadhi ya hoja za sera ya majimbo(Nitaeleza), kwa hiyo ni suala la muda to sera ya majimbo kukubaliwa na Tanzania nzima, mwanzoni kuna hofu.

Ni kweli majimbo yataleta ushindani, itakumbukwa kwamba Raisi mstaafu (MKAPA),kiserakali, aliwaaga wananchi Kikanda(Majimbo) hakunzunguka mkoa hadi mkoa,nchi kubwa hii! Unakumbuka ilivyokuwa? Kanda zilishindana kwenye kumpa zawadi kumuaga, huyu akitoa magunia mia mwingine anatoa magunia miambili. Na kwenye mkutano mkuu pia wa CCM mikoa ilishindana kugawa zawadi kwa kiongozi. Sasa sera ya majimbo itahamisha mashindano toka kwenye zawadi mpaka kwenye maendeleo, huyu anajenga madaraja kumi mwingine thelathini, kwa mtindo huu kitaeleweka!

Turudi kwa CCM kukubali sera ya majimbo! Bada ya uchaguzi kuisha, hapo mwanzo serekali ya awamu ya nne ilifanya mazungumzo na wamiliki wa migodi kwamba wawe wanatoa dola laki mbili(kama nakumbuka vizuri) kwa halamashauri ambapo mogodi ipo! Pamoja na kwamba wametekeleza vibaya, hii ni sehemu ya hoja za sera ya majimbo, kwamba sehemu ya rasilimali ibaki na wanachi wa meneo husika wanafuake na rasilimali. Ni katika mkutano huu ndio Mkono alisusia. Kwamba hela wanazotoa ni kidogo na haijafafanuliwa ni kiasi gani hawa jamaa wanavuna!

Ukiangalia mradi wa maji wa ziwa Victoria,lengo ni kufanya watu wafaidike na rasilimali walizo karibu nazo,sera ya majimbo!

Rejea mjadala wa mapanki ujumbe ulikuwa ni nini? Wananchi wa kanda ya ziwa hawafaidiki na rasilimali(Ziwa Victoria)

Tujadili
 
Wacha/Mswahili/chinga and now jadilithentafiti,
Kunahaja gani ya wewe kuja na jinatofauti kila wakati ili kutetea uoza ulioifikisha Tanzania hapo ilipo?

Mbaazi zikikosa jua ..........................
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom